Enyi mliooa, mlipataje wake?

Habari wakuu.

Poleni sana kwa majukumu, Hoja yangu ni kwamba imefika wakati nataka kuoa sasa, ila sasa imebidi niulize kwa mliooa. Mmepataje wake wakuoa? Maana toka nipate wazo la kuoa nimekua nazurula sana maeneo mbalimbali nikiamini nitakutana na anayenifaa, hii hali imenifanya hata nikiwa nyumba ya ibada nisiwe makini na ibada bali nakagua mke, hata nikiwa kwenye daladala yaani akipanda Dada nakuwa makini sana nikiamini labda ndo huyu..!
MSAADA WENU TAFADHARI...
mwanamke wa kuoa sio kama pesa ya kuokota ni una mjenga kwa mikono yako yako mweneywe ni kam kukamata paka unajaribu kumfuga atakaye kubali kuendana na wewe na kufugwa kwa style unayotaka wewe ndio huyo huyo unaweka ndani...ina maana jaribu hilo wazo la kuoa inatakiwa uwe nalo miaka ya nyuma kabla hujawa tayari maana yake unakua katika mahusiano na wanawake wa ligi yako uanyekupenda, kukuheshimu na mostly kutaka kujena maisha na wewe...note this process can take very long time than actual marriage could take
 
Habari wakuu.

Poleni sana kwa majukumu, Hoja yangu ni kwamba imefika wakati nataka kuoa sasa, ila sasa imebidi niulize kwa mliooa. Mmepataje wake wakuoa? Maana toka nipate wazo la kuoa nimekua nazurula sana maeneo mbalimbali nikiamini nitakutana na anayenifaa, hii hali imenifanya hata nikiwa nyumba ya ibada nisiwe makini na ibada bali nakagua mke, hata nikiwa kwenye daladala yaani akipanda Dada nakuwa makini sana nikiamini labda ndo huyu..!
MSAADA WENU TAFADHARI...
mwanamke wa kuoa sio kama pesa ya kuokota ni una mjenga kwa mikono yako yako mweneywe ni kam kukamata paka unajaribu kumfuga atakaye kubali kuendana na wewe na kufugwa kwa style unayotaka wewe ndio huyo huyo unaweka ndani...ina maana jaribu hilo wazo la kuoa inatakiwa uwe nalo miaka ya nyuma kabla hujawa tayari maana yake unakua katika mahusiano na wanawake wa ligi yako uanyekupenda, kukuheshimu na mostly kutaka kujena maisha na wewe...note this process can take very long time than actual marriage could take
 
Aiseee kuwa makini sana mkuu katika hiyo sekta.
Unamuona mwenzio gwajima na skendo zake zote bado anatetewa na mkewe,si umemuona mkewe alivyokuwa na msimamo thaibiti Ndugu?

Alafu chonde chonde usiyafite mke wakati una genye zimekupanda,kila mke utamuona mzuri sana kwa sababu ya tamaa za mwili.

Mke ambae unaweza kudumu nae ni yule ambae ukimuona tu yanakujia mawqzo ya kumuoa zaidi ya kufanya nae mapenzi tu.maana yake ni kwamba kuna wanawake ukiwatazama tu mavazi yao basi wanakuvutia upate hamu ya kuzini nao.sasa mke akiwa hivyo tahadhari sana.

Nakumbuka wakati nipo kijana nasoma kabla sijaoa kulikuwa na dada falani anavaa hijabu vizuri sana ikawa namzimia sana kwa kweli mpaka nikimuona napata picha ameshakuwa mke wangu tayari na tunaishi vizuri sana,lakini kuna wadada wengine nikiwaona nawaza uchafu tu moja kwa moja.sasa wewe angalia sana sana sana.

Alafu angalia dini yako mkuu,kama ni mkristo basi pahala safi pa kupata mke ni kanisani.sasa kanisani NAKO UCHAGUE,SIO KWA KUWA NI KANISA BASI UNACHUKUA YEYOTE.utajuta na kuleta uzi hapa.kuwa makini kanisani uangalie na kuwashirikisha wazoefu wa sehemu hiyo.

Lakini pia naomba kama una mama basi mtumie kumuulizia akutafutie binti mwenye tabia njema sana anayemjua,wanamama wanajuana sana mtaani wanajua kabisa kwamba nyumba flani yule binti ametulia au hajatulia.kwa hiyo wanajua sehemu sahihi.
Alafu badala ya hapo sasa umwambie akutafutie mke,mama hawezi kukuimgiza chaka hata siku moja,ataeatumia wenzie wamtafutiee nyumba gni kuna binti mzuri.

Akipatikana unawaambie wasiambiwe hapo kwa binti kama una lengo fulani,wewe ufanye mipango kumuona huyo binti na kumtafakari nama alivyo,huku na wewe ukiulizia wadau mbali mbali juu ya mwenendo wake,ukiona umempenda namna alivyo na tabia ziko fressh basi hapo anza kutupa ndoana na kupeleka taarifa rasmi kwa huyo dada mdogo mdogo ili naye tuone kama atakuwa amekukubali.

Ila tu mkuu...

Ukitaka mke mwema basi kuwa wewe mwema kwanza.anza kutengenea mda huu tulie na kutuliza akili sio useme utatulia ukioowa shauri yako
Mkuu umesaidia wengi ,tuanze mchakato wa kupiga simu kwa Bibi mzaa Bibi huko.
 
Kiongozi! Wanawake wanaumiza sana vichwa. Nilimtongoza halafu hakuniambia kama ana mwanaume mwengine. Naye alinijibu ananipenda.... Mama weee! Baadae ananiambia namuweka kwenye wakati mgumu kumbe ana mchumba na kama asingewahiwa basi angelikubali niwe wake wa maisha... Blah! Blah! Kibao zikaendelea.


Nikamwambia rudi kwa bwana wako. Sasa hivi moyo unaniuma! Nakomaa kiubishi tu najua yana mwisho.
 
Habari wakuu.

Poleni sana kwa majukumu, Hoja yangu ni kwamba imefika wakati nataka kuoa sasa, ila sasa imebidi niulize kwa mliooa. Mmepataje wake wakuoa? Maana toka nipate wazo la kuoa nimekua nazurula sana maeneo mbalimbali nikiamini nitakutana na anayenifaa, hii hali imenifanya hata nikiwa nyumba ya ibada nisiwe makini na ibada bali nakagua mke, hata nikiwa kwenye daladala yaani akipanda Dada nakuwa makini sana nikiamini labda ndo huyu..!
MSAADA WENU TAFADHARI...
kwa muda kama ukiweza tafuta movie moja inaitwa 500 days of summer ina mengi ya kujifunza
 
Kiongozi! Wanawake wanaumiza sana vichwa. Nilimtongoza halafu hakuniambia kama ana mwanaume mwengine. Naye alinijibu ananipenda.... Mama weee! Baadae ananiambia namuweka kwenye wakati mgumu kumbe ana mchumba na kama asingewahiwa basi angelikubali niwe wake wa maisha... Blah! Blah! Kibao zikaendelea.


Nikamwambia rudi kwa bwana wako. Sasa hivi moyo unaniuma! Nakomaa kiubishi tu najua yana mwisho.
Huyo mwanamke hafai daima.
 
Habari wakuu.

Poleni sana kwa majukumu, Hoja yangu ni kwamba imefika wakati nataka kuoa sasa, ila sasa imebidi niulize kwa mliooa. Mmepataje wake wakuoa? Maana toka nipate wazo la kuoa nimekua nazurula sana maeneo mbalimbali nikiamini nitakutana na anayenifaa, hii hali imenifanya hata nikiwa nyumba ya ibada nisiwe makini na ibada bali nakagua mke, hata nikiwa kwenye daladala yaani akipanda Dada nakuwa makini sana nikiamini labda ndo huyu..!
MSAADA WENU TAFADHARI...
MKUU KUOA NIKUTOKA SHIMONI KWENDA KABURINI ...
 
Habari wakuu.

Poleni sana kwa majukumu, Hoja yangu ni kwamba imefika wakati nataka kuoa sasa, ila sasa imebidi niulize kwa mliooa. Mmepataje wake wakuoa? Maana toka nipate wazo la kuoa nimekua nazurula sana maeneo mbalimbali nikiamini nitakutana na anayenifaa, hii hali imenifanya hata nikiwa nyumba ya ibada nisiwe makini na ibada bali nakagua mke, hata nikiwa kwenye daladala yaani akipanda Dada nakuwa makini sana nikiamini labda ndo huyu..!
MSAADA WENU TAFADHARI...
Huo ni mchakato mgumu na mara nyingi ni kama kuna hali ya kubahatisha hasa pale mwanzo. Ila cha msingi hakikisha unakuwa na VIGEZO vyako mwenyewe binafsi vya mtu unayetaka awe mama wa watoto wako weka vigezo bila kushinikizwa na mtu yoyote. Mimi niliangalia vitu hivi-

Mosi, kwa kuwa kipindi hicho nilibahatika kufika kidato cha nne lengo langu la kwanza kabisa ni mtu walau aliyefika elimu hiyo, niliona mtu mwenye elimu chini ya hapo tungesumbuana. Na kweli nilikuwa sihangaiki kabisa na mtu wa chini ya elimu hiyo.

Pili, nikasema piga ua mke wangu hawezi kuwa wa makabila dulani. Ni hivi. Kwetu kutokana na uzoefu wa miaka mingi kuna makabila 'hayakubaliki' kirahisi kwa wazazi. Kwa wao kuna makabila yanahesabika kama ni watu wakorofi, wasio na ubinadam n.k. Hukatazwi moja kwa moja kuleta watu hawa ila kwa hakika ujiandae kupata mapokezi hasi. Kwetu mke hasa wa kwanza anahesabika kuwa sio tu wa kukutunza wewe peke yako bali anatunza familia yenu nzima.

Tatu, mke lazima awe wa kuvutia machoni KWAKO. Najua kwa wengine wanaweza kuipuuza hii pointi lakini ni muhimu sana. Usizoe tu mtu huko mtaani. Mke ni mtu maalum sana. Sio kila mwanamke anafaa kuwa mke. Kumbuka huyu ni mtu wa karibu sana utakula nae, utalala nae utashea naye karibia kila kitu lakini kubwa zaidi utaishi naye maisha yako yote hapa duniani. Na kwa baadhi ya imani mke huwa mmoja tu. So ni lazima auzike vizuri kwa vigezo vyote, usijekujuta baadae.

Nne, pata mke kutoka kwenye mazingira sahihi. Kuna hatari zake kuoa mwanamke tu maadam mmekutana tu huko mtaani. Mazingira mazuri ni maeneo ya ibada (makanisa, misikiti), makazini, mashuleni. Hawa mara nyingi wanakuwa kwenye mwelekeo fulani 'kutazama' maisha ya baadae. Kama ni lazima uchukue mtaani hakikisha unaifahamu vema familia yao!!

Hayo ni msingi kwangu, lakini kiujumla hakuna mtu mkamilifu kwa 100% mapungufu yanakuwepo la msingi ni kuvumiliana na kurekebishana.


==KILA LAKHERI KUSAKA MWALI==
 
Mke hatafutwi hivyo kama unatafuta hela!
Cha msingi wewe una sifa na vigezo na sifa za mtu unayetaka awe mke wako. Kwa hiyo huna haja ya kumwangalia kila mwanamke anayepita machoni pako,na kumfanyia usaili.....umakini wako uwe kwenye vigezo vyako...then endelea na maisha ya kawaida.
Utakuja kushangaa unakutana na mwanamke ambaye hata hukuwa na hayo mawazo ya mke...then kuna kitu kitawaka moyoni mwako na kukuambia "this is her"
Na ukigeukia terms and conditions zako utakuta amekidhi kila kitu.
Acha kutafuta mke kama shilingi Mia iliyopotea mchangani mkuu!
Hii ni kweli kabisa mimi ilinitokea. nilimuona mara ya kwanza moyo ukasema 'Yes' hlf tukapotezana kitambo tu. Kumbuka hatukuwa tunafahamiana kabisa.

Nikaja kumuona mara ya pili, lakini sehemu nyingine tofauti kabisa (na sikuwa nakumbuka kama ni yuleyule niliyeonana naye siku ile ya kwanza), 'Yes' ikaja tena. Sasa ni wahenga tuna watoto kadhaa.
 
Hii ni kweli kabisa mimi ilinitokea. nilimuona mara ya kwanza moyo ukasema 'Yes' hlf tukapotezana kitambo tu. Kumbuka hatukuwa tunafahamiana kabisa.

Nikaja kumuona mara ya pili, lakini sehemu nyingine tofauti kabisa (na sikuwa nakumbuka kama ni yuleyule niliyeonana naye siku ile ya kwanza), 'Yes' ikaja tena. Sasa ni wahenga tuna watoto kadhaa.
Inakuaga hivo mkuu japo me sio muhenga kihivo. Mara ya kwanza namuona mke wangu (hadi kale kasauti ka- 'yes this is her' kakanisemesha) walikuja kunitembelea chuoni akiwa na dadake ambaye ni class mate wangu...so nilipomuona tu mdogo mtu nikasema huyu ndo mke wangu. From there hata washkaji nikawa nawaambia mke nitakayemuoa mimi tayari yupo ila yeye hajui lolote...kuna mwanangu mmoja akanicheka sana...kwamba inawwzekanaje useme ni mke wako wakati hata hujarusha mistari? Nikawaambia ndo hivo huyo lazima awe mke wangu.2017 nmefunga naye ndoa na akiwa chuo 2nd year na sasa tunategemea mtoto wetu wa 1
 
Habari wakuu.

Poleni sana kwa majukumu, Hoja yangu ni kwamba imefika wakati nataka kuoa sasa, ila sasa imebidi niulize kwa mliooa. Mmepataje wake wakuoa? Maana toka nipate wazo la kuoa nimekua nazurula sana maeneo mbalimbali nikiamini nitakutana na anayenifaa, hii hali imenifanya hata nikiwa nyumba ya ibada nisiwe makini na ibada bali nakagua mke, hata nikiwa kwenye daladala yaani akipanda Dada nakuwa makini sana nikiamini labda ndo huyu..!
MSAADA WENU TAFADHARI...
KWA NJIA HII UTABUHI AISEE...ILA NO FORMULA WE HIYO NJIA INAWEZA KUKUTOA KIMASOMASO...ILA UVOANGALIA ANGALIA USIJE INGIA PASIPO
 
Habari wakuu.

Poleni sana kwa majukumu, Hoja yangu ni kwamba imefika wakati nataka kuoa sasa, ila sasa imebidi niulize kwa mliooa. Mmepataje wake wakuoa? Maana toka nipate wazo la kuoa nimekua nazurula sana maeneo mbalimbali nikiamini nitakutana na anayenifaa, hii hali imenifanya hata nikiwa nyumba ya ibada nisiwe makini na ibada bali nakagua mke, hata nikiwa kwenye daladala yaani akipanda Dada nakuwa makini sana nikiamini labda ndo huyu..!
MSAADA WENU TAFADHARI...
Njoo nikupatie mke
Mie nina bahati aisee wanakuja tu
 
Mfano me nna mademu kama 6 hivi
Mfano kesho ikitokea ulazima wa kuoa najua nimuoe nani kati yao
Siyo kuzunguka mtaani kutafuta wa kumuoa
HII NDIO INATAKIWA...SI CHINI YA 5 IKITOKEA DHARURA UNAOA KESHO UNACHUKUA HUYU AKIZINGUA CHUKUA YULE
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom