Enjoy this! Dhana asili ya kuchoma UDI na kuvukiza mavumba

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,606
696,720
Niwatakie weekend njema! Najua hizi ndio zile tarehe pendwa... Tarehe za kuitwa majina yote matamu

Nina hakika wengi wetu tumeshawahi kuchoma udi ama kuvukiza mavumba... Wakati mwingine ni taratibu za kiimani kimila ama hata masharti ya mganga
Nimevutika kuandika mada hii kutokana na reply ya mdau Ray 4 real kwenye moja ya mada zangu...

Nitaandika kwa mtazamo wa kijamii zaidi kuliko kiimani kwa maana ya dini
565ea205e3f32a51668f1dac799c3ed4.jpg

Kwanza ni lazima utambue kuwa kuchoma UDI na kuvukiza mavumba kunajumuisha mambo mane makuu

1. Moshi wake ni alama ya hewa na pumzi yaani uhai.. Ukiashiria nguvu zisizoonekana kwa kusambaa na kutoweka milele
2. Moshi husika unatokana na moto, moto ni alama ya jua yaani mwanga
3. Kinachotoa moshi kinatokana na ardhi, ardhi ni msingi, ni mhimili wa dunia... Miti hupandwa ardhini
4. Moshi wake ni zao la maji, bila maji wala unyevu mti hauwezi kumea na kukua ukastawi na kutoa mazao yanayotumika kutengeneza udi
Hivi vinne vinakamilisha uumbaji katika misingi yake.
1b2841365f236761cd38bdb2d48c829b.jpg

Sasa matumizi makubwa ya UDI na kuvukiza mavumba ni yapi?
-kutoa gesi asili ambayo
:italeta harufu anuwai zitakazotumika kwenye mambo ya kiroho, manuizi, matambiko na maagano
:kualika mizimu na mapepo na majini kwa nia ya kutengeneza ama kuharibu
:kuvuta ama kufukuza ukitakacho ama usichokitaka... Maranyingi hapa ni ishu za mahusiano na mapenzi
Lakini kumbuka kwamba si kila mti unaweza kutoa malighafi ifaayo kwa kutengeneza UDI na mavumba.. Miti ama malighafi zifaazo ni kama hizi

(A)Miti ya ubani, yaani miti itoayo malighafi ya ubani... Hii hutumika kutakasa, shughuli za kiroho na kiimani... Maana ya ubani kiroho ni jua na jua ni mwanga ambao unatafsiriwa kama NGUVU ya kiroho

(B) Mti utoao manemane... Mane mane kiroho ni alama ya uponyaji, ulinzi mvuto, na tunu.... Inahusishwa na mwezi ambao kiroho ni nguvu ya mwanamke

(C) Msandali/sandalwood, hutumika kwenye shughuli za kiroho na utakaso

(D) Msandarusi, hutumika kutakasa na mambo ya kiroho pia zana zake kuu ni rangi nyeupe nyeusi na dhahabu... Utakaso wake si wa kiroho tu bali hata kwenye vitu vinavyoonekana.. Huu ndio hutengeneza vanish ya kung'arisha fenicha

(E)Mwerezi/ pine tree kutakasa na kinga dhidi ya nguvu hasi zote

(F) Joka mti damu. Hii hutumika kuimarisha mahusiano, kuleta uthubutu na kujiamini lakini mbaya zaidi ikitumika kinyume kwa kunuia husababisha uhanithi wa jinsia zote mbili

Kwahiyo ndugu zangu tunapoenda kutafuta tiba mbadala jihadharini sana na kupewa mavumba na nyudi... Kwakuwa sometimes mganga hukupa malighafi isiyo sahihi na yenye madhara makubwa
667acc3eee2e573fb3f0027ef4d90423.jpg

Alamsiki

Jr
 
232948-incense-prayers-revelation-throne.jpg
Incenselonghua.jpg

Hapa ni kwa nukuu na kwa mtazamo wa kiimani katika ukristo na ubudha
 
Niwatakie weekend njema! Najua hizi ndio zile tarehe pendwa... Tarehe za kuitwa majina yote matamu
Nina hakika wengi wetu tumeshawahi kuchoma udi ama kuvukiza mavumba... Wakati mwingine ni taratibu za kiimani kimila ama hata masharti ya mganga
Nimevutika kuandika mada hii kutokana na reply ya mdau Ray 4 real kwenye moja ya mada zangu...
Nitaandika kwa mtazamo wa kijamii zaidi kuliko kiimani kwa maana ya dini
565ea205e3f32a51668f1dac799c3ed4.jpg

Kwanza ni lazima utambue kuwa kuchoma UDI na kuvukiza mavumba kunajumuisha mambo mane makuu

1. Moshi wake ni alama ya hewa na pumzi yaani uhai.. Ukiashiria nguvu zisizoonekana kwa kusambaa na kutoweka milele
2. Moshi husika unatokana na moto, moto ni alama ya jua yaani mwanga
3. Kinachotoa moshi kinatokana na ardhi, ardhi ni msingi, ni mhimili wa dunia... Miti hupandwa ardhini
4. Moshi wake ni zao la maji, bila maji wala unyevu mti hauwezi kumea na kukua ukastawi na kutoa mazao yanayotumika kutengeneza udi
Hivi vinne vinakamilisha uumbaji katika misingi yake.
1b2841365f236761cd38bdb2d48c829b.jpg

Sasa matumizi makubwa ya UDI na kuvukiza mavumba ni yapi?
-kutoa gesi asili ambayo
:italeta harufu anuwai zitakazotumika kwenye mambo ya kiroho, manuizi, matambiko na maagano
:kualika mizimu na mapepo na majini kwa nia ya kutengeneza ama kuharibu
:kuvuta ama kufukuza ukitakacho ama usichokitaka... Maranyingi hapa ni ishu za mahusiano na mapenzi
Lakini kumbuka kwamba si kila mti unaweza kutoa malighafi ifaayo kwa kutengeneza UDI na mavumba.. Miti ama malighafi zifaazo ni kama hizi

(A)Miti ya ubani, yaani miti itoayo malighafi ya ubani... Hii hutumika kutakasa, shughuli za kiroho na kiimani... Maana ya ubani kiroho ni jua na jua ni mwanga ambao unatafsiriwa kama NGUVU ya kiroho

(B) Mti utoao manemane... Mane mane kiroho ni alama ya uponyaji, ulinzi mvuto, na tunu.... Inahusishwa na mwezi ambao kiroho ni nguvu ya mwanamke

(C) Msandali/sandalwood, hutumika kwenye shughuli za kiroho na utakaso

(D) Msandarusi, hutumika kutakasa na mambo ya kiroho pia zana zake kuu ni rangi nyeupe nyeusi na dhahabu... Utakaso wake si wa kiroho tu bali hata kwenye vitu vinavyoonekana.. Huu ndio hutengeneza vanish ya kung'arisha fenicha

(E)Mwerezi/ pine tree kutakasa na kinga dhidi ya nguvu hasi zote

(F) Joka mti damu. Hii hutumika kuimarisha mahusiano, kuleta uthubutu na kujiamini lakini mbaya zaidi ikitumika kinyume kwa kunuia husababisha uhanithi wa jinsia zote mbili

Kwahiyo ndugu zangu tunapoenda kutafuta tiba mbadala jihadharini sana na kupewa mavumba na nyudi... Kwakuwa sometimes mganga hukupa malighafi isiyo sahihi na yenye madhara makubwa
667acc3eee2e573fb3f0027ef4d90423.jpg

Alamsiki

Jr
Elimu hii ina udhaifu mkubwa juu ya ubani na udi zichomwacho Leo kwenye majumba au maeneo ya biashara kheri kuulizia ulete kitu kilichosimama ktk dhana nzima ya matumizi ya vitu hivyo.
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom