Eneo la Stend kuu ya Mabasi Tabora, ni chafu Sana.

mdudu

JF-Expert Member
Feb 6, 2014
6,953
9,855
Ndugu wana jamvi salaam kwenu
RC, DC, afisa afya mkoa na wilaya ,licha ya jitihada za Rais Magufuli kuhimiza usafi, lakini uongozi wa mkoa wa Tabora,umeshindwa kusimamia zoezi la usafi, kitu cha kushangaza maafisa afya mkoa na wilaya kazi zao wanafanyia wapi au wako likizo? Jalibuni kutembelea Choo cha kulipia stand, nyuma ya Loliondo bar,nyuma ya SAFI Grocery ni pachafu na niaibu kwa taswila ya mji ,na kunaweza kutokea mlipuko wa magonjwa, Kama uongozi wa mkoa wameshindwa,serikali iingilie kati kupitia wizara inayohusika na usafi,
Nawasilisha.
 
Uongozi wa mkoa ndio Serikali yenyewe, wananchi hapo ndio wanatakiwa waingilie kati wafanye usafi wa kutosha na wahakikishe wanasimamiana wenyewe kwa wenyewe mtu asimwage taka eneo ambalo sio rasmi
 
Uongozi wa mkoa ndio Serikali yenyewe, wananchi hapo ndio wanatakiwa waingilie kati wafanye usafi wa kutosha na wahakikishe wanasimamiana wenyewe kwa wenyewe mtu asimwage taka eneo ambalo sio rasmi
Ok ... kama ni hivyo sasa ule ushuru tunawalipa kwa nini ... bc waturudishie pesa zetu ili usafi tufanye wenyewe ...
 
Back
Top Bottom