Wadau wa JF,
Napenda kuwaletea tahadhari hii,juzi rafiki yangu alikuwa anatoka mjini saa tatu usiku, akirudi nyumbani kwake Sinza akipitia Bagamoyo Road.
alipokuwa anapita daraja la salander, mbele kidogo pale kwenye vichaka vya miti miti mingi opposite na bahari,ghafla gari yake ikazima akampigia simu rafiki yake aje amsaidie. Yule rafiki yake akamwambia usishuke kwenye gari,asubiri kidogo anakuja.
yule rafiki yangu alipoona,yule mtu aliyemwita amsaidie anachelewa akasema ngoja nishuke nifunue boneti inawezekana ni kitu kidogo kinachosumbua.
Akafungua mlango aliposhuka tu,mara likaja kundi la vijana kama kumi wakamzunguka wakampiga sana, wakamyanganya laptop.hand bags,simu,na vitu vingine vilivyokuwa kwenye gari.
moja wa wale wezi akampiga na nyundo mguuni kwenye kisigino,kikaninginia kinatoa damu,baadaye wale jamaa wakakimbia wakamwacha anavuja damu.
ikapita gari moja, kutoka mjini ndio ikambeba kumpeleka Agakhan ambapo amelazwa hadi hii leo. Damu inasemekana ilimwagika sana kama asingewahiwa kuongezewa damu huenda angepoteza maisha.
jamani habari ndiyo hiyo.ya msitu wa salander bridge.
Napenda kuwaletea tahadhari hii,juzi rafiki yangu alikuwa anatoka mjini saa tatu usiku, akirudi nyumbani kwake Sinza akipitia Bagamoyo Road.
alipokuwa anapita daraja la salander, mbele kidogo pale kwenye vichaka vya miti miti mingi opposite na bahari,ghafla gari yake ikazima akampigia simu rafiki yake aje amsaidie. Yule rafiki yake akamwambia usishuke kwenye gari,asubiri kidogo anakuja.
yule rafiki yangu alipoona,yule mtu aliyemwita amsaidie anachelewa akasema ngoja nishuke nifunue boneti inawezekana ni kitu kidogo kinachosumbua.
Akafungua mlango aliposhuka tu,mara likaja kundi la vijana kama kumi wakamzunguka wakampiga sana, wakamyanganya laptop.hand bags,simu,na vitu vingine vilivyokuwa kwenye gari.
moja wa wale wezi akampiga na nyundo mguuni kwenye kisigino,kikaninginia kinatoa damu,baadaye wale jamaa wakakimbia wakamwacha anavuja damu.
ikapita gari moja, kutoka mjini ndio ikambeba kumpeleka Agakhan ambapo amelazwa hadi hii leo. Damu inasemekana ilimwagika sana kama asingewahiwa kuongezewa damu huenda angepoteza maisha.
jamani habari ndiyo hiyo.ya msitu wa salander bridge.