Eneo la kujenga nidhamu ya fedha hasa kwenye utoaji. Hii kitu imekaaje kwenu?

g vizy

JF-Expert Member
Jan 5, 2016
896
977
Ni eneo la muhimu sana la kudhibiti utumiaji kwenye utoaji wa pesa ambazo wakati mwingine unakuta hakuna ulazima wa wewe kufanya hivyo kwa sababu ya kukuza nidhamu yako ya uwekaji wa kipato chako kwa ajili ya kesho yako

Swali ni je linapokuja swala la kutoa fedha kama mtu anakuomba na unafahamu kabisa siwezi kujinyima na mtu amekulilia uwenda ni rafiki,mama mzazi,baba mzazi au ndugu wa kawaida kua anashida anaomba umsaidie na wewe fedha unayo ila unasita kumpa kwa kuofia uwenda nidham yako ya kutunza fedha itapungua uwa unafanyaje kuendelea kua katika nidhamu yako ile ile
 
Pesa yako isikufanye mtumwa kiasi cha kushindwa kujua umuhimu wa pesa. Si pesa ni kwa ajili ya kusolve problems, au unataka ukifa wakuzike nazo!!???
 
Kama imetokea mara chache na unajua fika hali halisi ya muombaji/mhitaji nitampa ila ikishakuwa ni mazoea kwa sababu anaona uwezo ninao hata kwa matumizi yasiyo na ulazima sana sitoi.
 
Pesa yako isikufanye mtumwa kiasi cha kushindwa kujua umuhimu wa pesa. Si pesa ni kwa ajili ya kusolve problems, au unataka ukifa wakuzike nazo!!???
kumbuka inapotumika bila malengo ni sawa na kupoteza mwelekeo wako wa kifedha siku zijazo na hela ni hela haijalish ni kiwango gani
 
Ki ukweli ni bora niwe mtoaji KWA wazazi wangu,yaani muda wote Siwezi sikia nyumbani Wana matatizo nishindwe kuwasaidia.Hapa Mimi Nitakuwa mtoaji.
 
Back
Top Bottom