Eneo la biashara ya baa

magesa77

Senior Member
May 22, 2011
123
15
Natafuta eneo linalofaa kwa biashara ya baa hapa Dar es salaam. Sifa husika: Eneo liwe sehemu za kuwalenga wateja, sehemu ya wazi, jirani na barabara, na pia liwe na parking ya kutosha. Mwenye eneo tajwa ani PM au tuwasiliane kupitia no. 0713 478675. Asanteni!
 
Natafuta eneo linalofaa kwa biashara ya baa hapa Dar es salaam. Sifa husika: Eneo liwe sehemu za kuwalenga wateja, sehemu ya wazi, jirani na barabara, na pia liwe na parking ya kutosha. Mwenye eneo tajwa ani PM au tuwasiliane kupitia no. 0713 478675. Asanteni!

mkuu ukipata mie nipe jiko kea ajili ya chipsi tu!!!
 
Una mtaji wa kiasi gani? Vinywaji na Vyakula vinauzika eneo lolote kwa kuwa kila mahali kuna wanywaji na walaji. Biashara ya Baa siku hizi kwa wenye kauwezo wanaziboresha kidigitali zaidi kwa kuweka muonekano mzuri, vitendea kazi vya kisasa na huduma VIP ili kuweza kuvutia zaidi, mfano unaweza kukodi au kununua nyumba kisha ukafanya ukarabati na maboresho na kuwewa eneo la jiko, kaunta ya nje eneo la kukaa watu nje na ukatenga space ya kuweka VIP Lounge au Night Club ya kisasa, kwa maeneo mengi ya Sinza na Kinondoni siku hizi kuna Baa za aina hii jaribu kutembelea uone. Ndo maana nikakuuliza una mtaji wa kiasi gani ili tujue namna ya kukushauri pa kutafuta eneo na mambo mengine. Biashara ya Baa ni JIKO ZURI, HUDUMA NZURI, MANDHARI NZURI na UONGOZI BORA mengine ni ziada.
 
Una mtaji wa kiasi gani? Vinywaji na Vyakula vinauzika eneo lolote kwa kuwa kila mahali kuna wanywaji na walaji. Biashara ya Baa siku hizi kwa wenye kauwezo wanaziboresha kidigitali zaidi kwa kuweka muonekano mzuri, vitendea kazi vya kisasa na huduma VIP ili kuweza kuvutia zaidi, mfano unaweza kukodi au kununua nyumba kisha ukafanya ukarabati na maboresho na kuwewa eneo la jiko, kaunta ya nje eneo la kukaa watu nje na ukatenga space ya kuweka VIP Lounge au Night Club ya kisasa, kwa maeneo mengi ya Sinza na Kinondoni siku hizi kuna Baa za aina hii jaribu kutembelea uone. Ndo maana nikakuuliza una mtaji wa kiasi gani ili tujue namna ya kukushauri pa kutafuta eneo na mambo mengine. Biashara ya Baa ni JIKO ZURI, HUDUMA NZURI, MANDHARI NZURI na UONGOZI BORA mengine ni ziada.

Biashara ya baa ni wahudumu(barmaid)
 
Una mtaji wa kiasi gani? Vinywaji na Vyakula vinauzika eneo lolote kwa kuwa kila mahali kuna wanywaji na walaji. Biashara ya Baa siku hizi kwa wenye kauwezo wanaziboresha kidigitali zaidi kwa kuweka muonekano mzuri, vitendea kazi vya kisasa na huduma VIP ili kuweza kuvutia zaidi, mfano unaweza kukodi au kununua nyumba kisha ukafanya ukarabati na maboresho na kuwewa eneo la jiko, kaunta ya nje eneo la kukaa watu nje na ukatenga space ya kuweka VIP Lounge au Night Club ya kisasa, kwa maeneo mengi ya Sinza na Kinondoni siku hizi kuna Baa za aina hii jaribu kutembelea uone. Ndo maana nikakuuliza una mtaji wa kiasi gani ili tujue namna ya kukushauri pa kutafuta eneo na mambo mengine. Biashara ya Baa ni JIKO ZURI, HUDUMA NZURI, MANDHARI NZURI na UONGOZI BORA mengine ni ziada.

Yeye anataka eneo wewe unamuuliza mtaji!!!!!....ukiona anatafuta mpaka eneo ujue keshafanya research ya kutosha na keshajipanga.
 
Biashara ya baa ni wahudumu(barmaid)

Wahudumu hawawezi kufanya kufanya kazi wao kama wao pasipo uongozi na usimamizi. Uongozi bora ndo hufanya wahudumu kutoa huduma bora. Ndo maana mteja akiwa Baa na asiporidhika na huduma humwambia muhudumu amuitie meneja.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom