Eneo hatari kwa ajali Mbeya latafutiwa ufumbuzi

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,365
8,097
Siku moja baada ya kifo cha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Igunga, Fatma Omary na watu wengine wawili kwa ajali ya gari, tayari eneo la Inyala mkoani Mbeya sehemu hiyo imeanza kutafutiwa ufumbuzi.

Leo Alhamis, Septemba 15, 2022, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (RC), Juma Homera amezindua barabara ya mchepuko eneo hilo yenye urefu wa kilometa 2.8.

Jana Septemba 14,2022 eneo hilo lilisababisha kifo cha Mkurugenzi wa Igunga, Fatma Omary dereva wake, Alex Mtabika (48) pamoja na Shafih Said.

Homera amesema eneo hilo limekuwa na changamoto kubwa na kusababisha ajali kila wakati jambo ambalo kwa sasa limepatiwa ufumbuzi.

Kwa upande wake, Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mhandisi Matari Masige amesema kwa sasa barabara hiyo itatumika kwaajili ya magari madogo pamoja na yale ya abiria.

"Tutaendelea kuboresha zaidi eneo hili kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama kuhakikisha sehemu hii inakuwa salama zaidi kwa wananchi hasa waendesha vyombo vya moto," amesema Masige.

Mwananchi
 
Wapumbavu hao asipokufa mkurugenzi au mbunge yanakaa kimya limeguswa kundi la walamba asali mara moja tu chini ya masaa 72 wanakuja na suluhisho.

Kabla ya hili tukio miezi minne nyuma walikufa watu 19 eneo hilo hilo majuzi tena wakafa nane mlikaa kimya hao hawakuwa binadamu?leo kidogo tu mnafunguka masikio,jueni hamuwezi kukikimbia kifo kitawafata hata vitandani mwenu kwa dhulma mnazowafanyia Watanzania.
 
Issue ya school busses mbovu ndio ishatoka hio kwasababu hakuna mtoto wa kiongozi anayebebwa kwa school bus mbovu, wanafuatwa na V8 za SERIKALI, anyway Mungu ni wetu sote
 
Haya mawimbi ya Mlandizi to Chalinze siku gari ya kiongozi mwingine ilambwe na Lori nadhani watatoa tamko kwa vitendo
acha kabisa pale alafu huwa wanaovertack kwa fujo sana na mavieite yao pale.
 
Back
Top Bottom