Endapo Serikali itaacha kutumia mabavu kukusanya kodi, wafanyabiashara wapo tayari kulipa kodi bila kudanganya na kofoji "documents"?

winnerian

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
335
530
Wote ni mashahidi kwa namna ambavyo watanzania wengi ni wagumu kufuata utaratibu pamoja na sharia halali zilizowekwa. Wengi wetu tunapenda sana kupata mali kirahisi na kwa njia ya udanganyifu ama rushwa.

Sasa je, serikali ikaamua kutumia upole na njia laini kukusanya kodi Watanzania wangapi watasema wamepata faida kwa halali kabisa bila kudanganya hasara hewa na za uongo?

Hili la kukwepa kulipa kodi linawagusa kuanzia mawaziri waliopo madarakani mpaka mama ntilie, ni nadra sana kumkuta mfanya biashara ameweka vitabu vyake safi na kwa ukweli mtupu bila kudangaya hapa nilipata hasara hapa, imekuwa hivi ilimradi akwepe kutoa ya kaisari.

Tunailaumu sana serikali kwakua ndio inayowajibika kuweka mambo sawa, lakini na sisi wananchi tujiuleze kweli tupo tayari kuwa nchi ambayo wote tutakuwa mstari wa mbele katika kufuata na kuwajibika mbele ya taratibu na sharia halali zilizowekwa.

Tujiulize nasisi: Je tupo tayari kumsaidia Mama Samia Suluhu Hassani kuitibu Tanzania ugonjwa wa unafiki na uongo?
 
Na hiyo kodi yenyewe iwe rafiki! Siyo kodi ya kugawana nusu kwa nusu, huku serikali yenyewe ikiwa haijakusaidia chochote. Yaani mtu atafute juani, halafu kuna watu wako maofisini kwenye viyoyozi wanakusubiria ukawagawie nusu ya kile ulicho kipata juani!

Dawa hapo ni kukwepa tu! Hata ije hiyo task force, itapigwa tu chenga ya mwili.

Lakini pia serikali iachane na matumizi ya hovyo ya kodi zetu. Mfano mwaka wa jana walichezea zaidi ya bilioni 300 kwenye uchaguzi ambao washindi wa huo uchaguzi, walikuwa waulikana hata kabla ya kutangazwa kwa matokeo! Hii inakatisha tamaa walipa kodi! Achilia mbali yale Ma V8, kununua Wabunge na Madiwani wa Upinzani, Ujenzi wa miradi isiyo na tija! Mfano ule uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Chato, nk.
 
Na hiyo kodi yenyewe iwe rafiki! Siyo kodi ya kugawana nusu kwa nusu, huku serikali yenyewe ikiwa haijakusaidia chochote. Yaani mtu atafute juani, halafu kuna watu wako maofisini kwenye viyoyozi wanakusubiria ukawagawie nusu ya kile ulicho kipata juani!..
Naungana na wewe kwa asilimia 100%. Na kwa maana hiyo basi lazima kuwepo na serikali inayowajibika kikamilifu na kwa uwazi bila kificho
 
Hakuna mfanyabiashara anaependa kulipa kodi popote pale ata iwe America! Kama wakina Ronaldo na Messi walikutwa na hatia ya ukwepaji kodi kwa kuto wasilisha taarifa sahihi sembuse huku kwetu?
Pakiwepo mazingira rafiki na yenye kumjali mfanyabiashara kwa asilimia kubwa sana watu watakuwa wazalendo na hata kile wanachobaki nacho kitaisaidia nchi kwa namna moja ama nyingine.
 
Wote ni mashahidi kwa namna ambavyo watanzania wengi ni wagumu kufuata utaratibu pamoja na sharia halali zilizowekwa. Wengi wetu tunapenda sana kupata mali kirahisi na kwa njia ya udanganyifu ama rushwa..
Kama wafanyakazi wa taasisi za umma wangekua wanaamua kuhusu kodi, wengi wasingelipa.

Duniani hakuna anaetaka kulipa kodi kwa hiari, Donald Trump alikwepa kodi ndo marekani.

Marekani wanasema hata hela uliyooiba au kuokota lazima uilipie kodi.

Serikali yetu inacheza, watakuja kufumbua macho hamna walilofanya. Mama anaona uongozi ni kuteua, kutumbua na kuhamisha. Magufuli alikua mzee wa field, alikua anasimamia kila kitu.
 
Wote ni mashahidi kwa namna ambavyo watanzania wengi ni wagumu kufuata utaratibu pamoja na sharia halali zilizowekwa. Wengi wetu tunapenda sana kupata mali kirahisi na kwa njia ya udanganyifu ama rushwa.

Sasa je, serikali ikaamua kutumia upole na njia laini kukusanya kodi Watanzania wangapi watasema wamepata faida kwa halali kabisa bila kudanganya hasara hewa na za uongo?

Hili la kukwepa kulipa kodi linawagusa kuanzia mawaziri waliopo madarakani mpaka mama ntilie, ni nadra sana kumkuta mfanya biashara ameweka vitabu vyake safi na kwa ukweli mtupu bila kudangaya hapa nilipata hasara hapa, imekuwa hivi ilimradi akwepe kutoa ya kaisari.

Tunailaumu sana serikali kwakua ndio inayowajibika kuweka mambo sawa, lakini na sisi wananchi tujiuleze kweli tupo tayari kuwa nchi ambayo wote tutakuwa mstari wa mbele katika kufuata na kuwajibika mbele ya taratibu na sharia halali zilizowekwa.

Tujiulize nasisi: Je tupo tayari kumsaidia Mama Samia Suluhu Hassani kuitibu Tanzania ugonjwa wa unafiki na uongo?
Hivi sasa wafanyabiashara hawataki kutoa risiti za kielektroniki sasa wapi serikali itapata kodi za kufanya maendeleo naona kunasintofahamu kubwa sana , sijui hii serikali itaendeshwa vipi.
 
Hivi sasa wafanyabiashara hawataki kutoa risiti za kielektroniki sasa wapi serikali itapata kodi za kufanya maendeleo naona kunasintofahamu kubwa sana , sijui hii serikali itaendeshwa vipi.
Nadhani serikali italazimika kuzirudia upya sheria za kodi ili ziwe rafiki na pia kuboresha namna ya ukusanyaji kodi uwe bora zaidi na wa kutoa mwanya kwa kila mmoja kushiriki kikamilifu kwenye suala la ulipaji kodi
 
Ninachojiuliza mimi ni kwamba hakuna namna yoyote ya kufanya hao Wafanya biashara walipe hizo kodi au shortcut ni kutumia mabavu tu?.

Sasa mnaenda shule kujifunza nini kama mbinu yenu pekee ni kutumia mabavu kukusanya kodi?.
 
Hakuna mfanyabiashara anaependa kulipa kodi popote pale ata iwe America! Kama wakina Ronaldo na Messi walikutwa na hatia ya ukwepaji kodi kwa kuto wasilisha taarifa sahihi sembuse huku kwetu?
Kwa hiyo njia pekee ni kupora?
 
Ninachojiuliza mimi ni kwamba hakuna namna yoyote ya kufanya hao Wafanya biashara walipe hizo kodi au shortcut ni kutumia mabavu tu?.

Sasa mnaenda shule kujifunza nini kama mbenu yenu pekee ni kutumia mabavu kukusanya kodi?.
viongozi waanze kuwa wenye kuonesha matumaini kwa wanachi wote na wenye kufuata sheria na hata wananchi wenyewe watafuata sheria bila shuriti
 
viongozi waanze kuwa wenye kuonesha matumaini kwa wanachi wote na wenye kufuata sheria na hata wananchi wenyewe watafuata sheria bila shuriti
Na Viongozi wanapotamani tuwe kama wa Sweden kulipa kodi wafuatilie pia namna Serikali ya Sweden inavyowajibika kwa Wananchi wake.
 
Hata hao wanaotumia mabavu, ujue kabisa kutoa kwa hiari imeshindikana. Na hata kama ikiwa kodi ikiwa 5% bado watu watalalamika.

Kingine hakuna mtu anataka kulipa kodi duniani kote ni sawa na mwajiriwa akatwe mshahara wake inauma mno.

Nchi yoyote ile duniani inategemea kodi iweze kujiendesha so kulipa kodi kunahitaji enforcement ya hali ya juu wala sio kwenda kunywa chai na mfanya biashara huku unamchekea ukidhani atakupa hela yake kizembe.

Kizazi hiki cha 197.. kinalalamika sana wao wanataka kila kitu anachokiwaza kichwani mwake basi kiwe hivyo.

Mbona kipindi cha muasisi wa taifa kulikuwa na kodi ya kichwa kama unazaidi ya miaka 18 lazima ulipe kodi. Watu walikuwa mpaka wanatelekeza familia zao wanakimbilia maporini wanakwepa mgambo. Hii ingekuwepo ndio ungesikia mara vijana hawana kazi serikali iwawezeshe vijana ili wapate kodi vizuri.

Tupunguze kulalamika na suala la kodi sio la kuomba ukizengua bora ufie jera huko hayo mazingira rafiki yapo ukishindwa hama nchi nenda ambako hawalipi kodi
 
Mfanya biashara wa Aina hiyo atakuwa siyo mtanzania

Jiulize Kwa nini kina Mbowe hawakuwahi kulipa Kwa hiari?? Je Nani ataweza??
 
Back
Top Bottom