MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Kuna kijana mdogo anamiliki kampuni ya udalali wa nyumba na viwanja, inaitwa Mbaga Real Estate Agency. Yeye mwenyewe anaitwa Emmanuel.
Nilipewa jina lake na rafiki yangu fulani. Nikampigia na kumwambia kuna biashara ya kiwanja kinauzwa, tena mahali penyewe ni pa bei mbaya.
Tukakubaliana, kimsingi, kwamba tungekutana njiani, mahali ambapo ningemsubiri, kisha tungefuatana mpaka kwa mmiliki wa kiwanja, aliyenituma kazi hiyo.
Jamani, hii ni biashara. MIMI ndiye niliyempigia, kumpelekea biashara; kiwanja hiki, uza, upate commission yako, ukifanikiwa na mimi utanipa kitu kidogo. MIMI ndiye niliyemtafuta, kumpelekea biashara.
Wakati niko njiani kwenda kwenye sehemu ya ahadi, nikampigia tena. Nanukuu alichonijibu:
"Sikiliza bwana mdogo, sisi ni real estate agency, hatuna wakati wa kukusubiri wewe umalize shughuli zako mia moja. Ukishamaliza, tupigie, tutakuambia tuko wapi, utatufuata!"
Nikamwambia: Sawa.
Nikakata simu.
Nikaona hii imeshakuwa soo. Kwanza mimi si BWANA MDOGO. Ni mtu mzima mwenye ndevu zangu, familia na watoto. Nimetumwa nimpelekee biashara hiyo na mtu ambaye NINAMHESHIMU SANA, TENA MNO! Sio kawaida yangu kutafuta DEAL za viwanja, n.k. Nina shughuli zangu rasmi. Huyu kijana aniite mie BWANA MDOGO? EBOOOO!
Alinipigia tena baada ya nusu saa, nikamwambia BADO SIJAMALIZA! Nadhani aligundua kosa lake, inaonekana walikuwa kwenye ulabu, kwani leo ni Ijumaa, na vijana HUANZA MAPEMA masuala ya ulabu siku za wikiendi.
Ndio tatizo la vijana. Wakipata vijisenti, wanachofikiria ni pombe na starehe (soma NGONO). Hakuna kupanga mambo ya maana!
Nimemtafuta mtu mwingine, mtu mzima, anayefanya kazi hiyo kama PROFESSION, sio HOBBY! Nitakamilisha biashara.
Emmanuel, YOU NEED TO GO TO CUSTOMER SERVICE SCHOOL! YOU REALLY SUCK!
Nilipewa jina lake na rafiki yangu fulani. Nikampigia na kumwambia kuna biashara ya kiwanja kinauzwa, tena mahali penyewe ni pa bei mbaya.
Tukakubaliana, kimsingi, kwamba tungekutana njiani, mahali ambapo ningemsubiri, kisha tungefuatana mpaka kwa mmiliki wa kiwanja, aliyenituma kazi hiyo.
Jamani, hii ni biashara. MIMI ndiye niliyempigia, kumpelekea biashara; kiwanja hiki, uza, upate commission yako, ukifanikiwa na mimi utanipa kitu kidogo. MIMI ndiye niliyemtafuta, kumpelekea biashara.
Wakati niko njiani kwenda kwenye sehemu ya ahadi, nikampigia tena. Nanukuu alichonijibu:
"Sikiliza bwana mdogo, sisi ni real estate agency, hatuna wakati wa kukusubiri wewe umalize shughuli zako mia moja. Ukishamaliza, tupigie, tutakuambia tuko wapi, utatufuata!"
Nikamwambia: Sawa.
Nikakata simu.
Nikaona hii imeshakuwa soo. Kwanza mimi si BWANA MDOGO. Ni mtu mzima mwenye ndevu zangu, familia na watoto. Nimetumwa nimpelekee biashara hiyo na mtu ambaye NINAMHESHIMU SANA, TENA MNO! Sio kawaida yangu kutafuta DEAL za viwanja, n.k. Nina shughuli zangu rasmi. Huyu kijana aniite mie BWANA MDOGO? EBOOOO!
Alinipigia tena baada ya nusu saa, nikamwambia BADO SIJAMALIZA! Nadhani aligundua kosa lake, inaonekana walikuwa kwenye ulabu, kwani leo ni Ijumaa, na vijana HUANZA MAPEMA masuala ya ulabu siku za wikiendi.
Ndio tatizo la vijana. Wakipata vijisenti, wanachofikiria ni pombe na starehe (soma NGONO). Hakuna kupanga mambo ya maana!
Nimemtafuta mtu mwingine, mtu mzima, anayefanya kazi hiyo kama PROFESSION, sio HOBBY! Nitakamilisha biashara.
Emmanuel, YOU NEED TO GO TO CUSTOMER SERVICE SCHOOL! YOU REALLY SUCK!