Emelda Mwamanga(BANG) aelezea bifu lake na Jacky pamoja na the late Mengi

warumi

R I P
May 6, 2013
16,273
18,378
Wanazengo today is Thursday right ? Sio mbaya tukajikumbusha matukio ya nyuma ambayo yaliyokea Ila hayakuwahi kusikika au kuvuma.

Kama wewe utakua ni mdau mzuri wa entertainment , Jina la Emelda mwamanga halitakua geni kwenye your ear drum , namzungumzia Yule CEO wa BANG MAGAZINE, jarida lililokua likifanya vizuri miaka kadhaa iliyopita, please simzungumzii emelda mtema Yule shilawadu wa global publisher msichanganye Ma file wanazengo, huyu ni boss-lady, owner wa BANG MAGAZINE, lile jarida linalopambwaga na lugha ya malkia, najua wambea wenzangu humu wengi ni standard seven and form four leavers so wengi wenu mnaweza msiwe mnalijua🤣( jokes bhana) .

Basi bwana , turudi kwenye mada yetu hot ya Leo , kama mnavyojua au wacha niwajuze kuwa hilo BANG MAGAZINE, ni jarida lililokua linapambwa na Ma celebrities wazito, yani watu wakubwa wakubwa , yani wale mastaa wenye hadhi zao , please sizungumzii akina amber rutty wala Gigy money .

Basi bwana, nakumbuka ilikua ni kipindi kile da jacky Ndo alikua kwenye uchumba hot na the late mengi ( rest in peace), story Yao Ndo ilikua hot in town , kila mtu alitaka kusikia habari za couple hii ya billionare , wanazengo wengi walionekana kuwa fascinated kusikia chochote kutoka kwenye hii couple , lakini unaaambiwa marehemu alikua hataki kuzungumziwa na chombo chochote cha habari kuhusu mahusiano yao , yani unaambiwa mzee baba alikaza ki kweli kwel na mikwara alitoa kama yote.

Basi bwana, inasemekana huyu Emelda alikua na ukaribu na jacky even before she got engaged to mengi , kama mnavyojua jacky was a musician and a model, so they were kind of friends coz pia yeye aliwahi kupamba kwenye jarida la mwanamama huyo ambaye kimuonekano ni mpole na asiye na makuu.

Basi bwana , unaambiwa engagement ikafika, dada jacky akavalishwa Pete ya uchumba, Ila ikumbukwe mambo yalikua yanaenda kisiri siri tu japokua watu walijua, na bahati nzuri au mbaya emelda akapata picha za tukio zima la engagement , Sasa si mnajua bibie akataka kuwaweka akina mengi kwenye jarida lake kwenye ukurasa wa mbele kabisa yani FENTI FODI( in magufuli's voice🤣) au kwa lugha ya malkia iliyonyooka ni FRONT PAGE.

Basi bwana, bibie nadhani alikua kashaanza process za ku print hiyo habari na picha kabisa alikua kaweka kwenye jarida lake , si unajua Tena mambo ya exclusive? Bila shaka angepata mtonyo wa maana na jarida lake kuuza zaidi ikiwa tu deal lake lingeenda sawa.

Maskini Dada wa watu, alijua kwa kuwa wanafahamiana na jacky ofcourse pia mengi alikua anamfahamu coz wote ni wafanyabiashara, alijua kabisa isingekua issue wala nini kutumia picha za love birds Hao kupamba jarida lake, unaambiwa kabla ya ku publish hiyo habari emelda akawapigia simu akina jakcy kuwaambia kuwa watatokea kwenye jarida la BANG MAGAZINE.

Tofauti na matarajio yake maskini , mengi alimjia juu bi dada huyo , akampiga mikwara mizito na kumwambia endapo angejaribu ku publish picha zao kwenye jarida lake , basi angejuta kuzaliwa, yani unaambiwa issue ilikua nzito , ugomvi mkubwa sana , ikabidi Sasa emelda aongee na jacky hili wayamalize.

Emelda anakwambia hilo jibu alilopewa na jacky hatokuja kusahau maisha yake yote na hapo ndo ushoga ukafa, baada ya mikwara ya mengi mpka kesho sijui BANG MAGAZINE liliishiaga wapi, sijui alifirisika au mzee baba alimnyoosha kama alivyoahidi, hayo siyajui.


Basi bwana , kutokana na huo mkasa wa kusisimua, ebu turudi zama hizi Sasa , maana mzee wetu alikua hapendi kabisa mambo ya media na habari zake zilikua Zikienea tu kwenye mitandao ya kijamii, Sasa wanazengo wanajiuliza, ilikuaje mzee baba akaamua kuweka life yake na jacky in public wakat hata baada ya kuoana mzee alikua hataki media ziandike au yeye kuhojiwa kuhusu mke wake na wala mke wake pia?

Hii interview ya jacky ya juzi naweza kusema ilikua her debut interview Toka aanze Kuwa na mahusiano na mengi, yani nowadays walikua so open , so inlove, they didn't care at all about the public eyes , wanazengo wanauliza je kuna usalama?, jacky Ma nyimbo ya Celin dion I will always love you ilikua kama yote, mzee baba akatoa speech ya hatari kwa mke wake

Jamani huu mkasa unasisimua sana, pumzika kwa amani Reginald mengi

Imendikwa na
WARUMI
IMG_6672.JPG
 
Chezeya Madam boss, jaman huyu dada alikua ananata, kwa wanaomjua karibu watakubaliana na Mimi

Ila mm niwe mkweli..sitaki kuside kwa Mange au Jacky...jaman..nna mume ndyo...sijawah fiwa na mume sawa nakubali kbs...ila jaman Jacky hata kulia??au ndo udhungu huo jaman...tatizo misiba ya matajri bwana...wanaremba na milipstick na misunglass juu...misiba ya wanyaki bwana wee😂😂😂..au ndo wale wenye uchungu rohoni??aisee...Jacky ameniacha na maswali mno jamn
 
Nadhani umechanganya Stori Binamu.... Haikuwa Picha za Engagment. Ni picha za watoto wake na Mengi ambayr watu walitaka kumjua.... kwani Jacy alikuwa anapost picha anawaficha watoto.... Mara anaweka miguu n.k... Imelda akataka kuwaweka kwenye jarida lake la Bang Jacy na Familia yake Akiwepo Mengi.... ile wanasubiria na picha tayari anazo mara anaona Jacy kazipost kwenye Mitandao... Kumuuliza akadai Mzes kagoma... Dili la Imelda likaingia Doa.. ndiyo Beef lao lilipoanzia..
 
Ila mm niwe mkweli..sitaki kuside kwa Mange au Jacky...jaman..nna mume ndyo...sijawah fiwa na mume sawa nakubali kbs...ila jaman Jacky hata kulia??au ndo udhungu huo jaman...tatizo misiba ya matajri bwana...wanaremba na milipstick na misunglass juu...misiba ya wanyaki bwana wee..au ndo wale wenye uchungu rohoni??aisee...Jacky ameniacha na maswali mno jamn

Shost wee, mume kamwachia mimali yote ile anaanza kulia ili iweje? Wajane sie tunaotegemea waume zetu wauza mikaa Ndo watulishe familia nzima mpaka ukoo apo mume akifa utalia kama wanawake wa kinegeria🤣🤣🤣
 
Mwenzangu Tena wakat anasimulia utatamani kulia, akasema wenzangu wana pesa na mtandao mkubwa Mimi sina cha kufanya, yani jamani binadamu mmh

Ww una kumbukumbu nzuri sana..nahis lilikia la august 2014 lile hakuuza .alipata hasara sana..maana alishapublish kbs...na tukawa tunaona Ads...khaa pesa nyoko sana..Emelda kajitilizia na mhehe wake kimyaa...ila yule mdg wake naskia yupo nje..Ritha
 
Shost wee, mume kamwachia mimali yote ile anaanza kulia ili iweje? Wajane sie tunaotegemea waume zetu wauza mikaa Ndo watulishe familia nzima mpaka ukoo apo mume akifa utalia kama wanawake wa kinegeria🤣🤣🤣


Hhahaha au misiba ya kinyakyusa wanalia mwezi..ukimuona mfiwa km huwez vunga utacheka ufe .kapaukaaaa..na litambaa jeusi kichwan na kipara cha kutosha😂😂muda wote ukimkumbuka mumeo unaloanzisha kwa ngv sana sana.. na kweli siye waume zetu wauza mikanda ya kiunoni lazima ulie huna namna
 
Story kamili ilikua. Kupitia ushosti wa imelda na jacky,imelda akafanikiwa kupata nafasi ya kuwainterview Mengi na jacky kuhusu maisha yao etc na pia wakaphotoshoot kabisa kwenye jumba lao,mapicha kama yote huku ime akiwaambia likitoka jarida atawajulisha pia picha hawezi kuwapa mpaka jarida litoke

Siku ya siku Jack akamuuliza imelda kama picha zimetoka akajibiwa ndio akaomba azione kwa makubaliano hatazipost mtandaoni mpaka jarida litoke,imelda akamkubalia kishingo upande(kwa kumuogopa bwana machache) maana ni kukiuka masharti waliyojiwekea(Bang)

Siku kadhaa kabla jarida halijatoka,jack akazipost picha mtandaoni,imelda kumpigia simu azitoe ataharibu biashara maana mzigo tayari ushachapishwa binti akagoma. Imelda akatishia kuwashtaki ee bana Boss akaingilia kati imelda akakosa nguvu na support
 
Ww una kumbukumbu nzuri sana..nahis lilikia la august 2014 lile hakuuza .alipata hasara sana..maana alishapublish kbs...na tukawa tunaona Ads...khaa pesa nyoko sana..Emelda kajitilizia na mhehe wake kimyaa...ila yule mdg wake naskia yupo nje..Ritha

Warumi Niko juu binamu, Sasa Mimi habari za mujini naanza kukosaje? Nimeanza umbea miaka hiyo, nashangaa humu watu wanakurupuka tu wanataka kushindana na Mimi , ahahahaah , mbea mie Nina kumbu kumbu hatari, kichwa kinahifadhi ma file tu kichwani🤣🤣

Ila Mimi nilikua fan mzuri tu wa BANG, Tena nilikua naendaga mpaka pale mikochen kwenye office zao , nilikua napenda sana kufanya kazi kwenye lile jarida, sema nilikuaga nasoma nje nakuja bongo na kurudi

Ila emelda Yule dada hanaga makuu jamani , mpole mwenyew mcheshi, Ila wanadamu mmh Ila Malipo hapa hapa duniani
 
Nadhani umechanganya Stori Binamu.... Haikuwa Picha za Engagment. Ni picha za watoto wake na Mengi ambayr watu walitaka kumjua.... kwani Jacy alikuwa anapost picha anawaficha watoto.... Mara anaweka miguu n.k... Imelda akataka kuwaweka kwenye jarida lake la Bang Jacy na Familia yake Akiwepo Mengi.... ile wanasubiria na picha tayari anazo mara anaona Jacy kazipost kwenye Mitandao... Kumuuliza akadai Mzes kagoma... Dili la Imelda likaingia Doa.. ndiyo Beef lao lilipoanzia..

Haikua engagement binamu ? , I stand corrected kama Sipo sahihi , Ila kipindi kile hata watoto walikua hawana binamu.
 
Hhahaha au misiba ya kinyakyusa wanalia mwezi..ukimuona mfiwa km huwez vunga utacheka ufe .kapaukaaaa..na litambaa jeusi kichwan na kipara cha kutoshamuda wote ukimkumbuka mumeo unaloanzisha kwa ngv sana sana.. na kweli siye waume zetu wauza mikanda ya kiunoni lazima ulie huna namna

Ahahahaah binamu umenivunja mbavu hakyamungu , Ila wanyakyusa kiboko kwa kulia wee

Ndio hivyo unajua mtu ukiwa na mtu unayemtegemea kwa kila kitu halafu ghafla hayupo na mambo hayaeleweki, yan utalia mwaka mzima, watu wanasema Ana uchungu sana na mumewe kumbe anawaza maisha yatakuwaje, lol 🤣🤣🤣
 
Warumi Niko juu binamu, Sasa Mimi habari za mujini naanza kukosaje? Nimeanza umbea miaka hiyo, nashangaa humu watu wanakurupuka tu wanataka kushindana na Mimi , ahahahaah , mbea mie Nina kumbu kumbu hatari, kichwa kinahifadhi ma file tu kichwani🤣🤣

Ila Mimi nilikua fan mzuri tu wa BANG, Tena nilikua naendaga mpaka pale mikochen kwenye office zao , nilikua napenda sana kufanya kazi kwenye lile jarida, sema nilikuaga nasoma nje nakuja bongo na kurudi

Ila emelda Yule dada hanaga makuu jamani , mpole mwenyew mcheshi, Ila wanadamu mmh Ila Malipo hapa hapa duniani



Nazikumbuka mnoo ofisi zao nami niliwah kwenda...yes Emelda ana roho ya upekee mnoo ht ukikutana naye mitaanj ukimsalimka anakichangamkia sana sana na tabasamu juu...alafu sasa Emelda na Jacky ...Emelda katoka familia ya kisomi na kitajiri..kwao wanazp balaa ..yaan khaa..Ila ndo binadamu
 
Story kamili ilikua. Kupitia ushosti wa imelda na jacky,imelda akafanikiwa kupata nafasi ya kuwainterview Mengi na jacky kuhusu maisha yao etc na pia wakaphotoshoot kabisa kwenye jumba lao,mapicha kama yote huku ime akiwaambia likitoka jarida atawajulisha pia picha hawezi kuwapa mpaka jarida litoke

Siku ya siku Jack akamuuliza imelda kama picha zimetoka akajibiwa ndio akaomba azione kwa makubaliano hatazipost mtandaoni mpaka jarida litoke,imelda akamkubalia kishingo upande(kwa kumuogopa bwana machache) maana ni kukiuka masharti waliyojiwekea(Bang)

Siku kadhaa kabla jarida halijatoka,jack akazipost picha mtandaoni,imelda kumpigia simu azitoe ataharibu biashara maana mzigo tayari ushachapishwa binti akagoma. Imelda akatishia kuwashtaki ee bana Boss akaingilia kati imelda akakosa nguvu na support

I stand corrected binamu , yeah ni kweli mwanazengo
 
Back
Top Bottom