Embu tumjadili Rais ajaye wa awamu ya sita 2025

DATAZ

JF-Expert Member
May 25, 2012
2,442
5,955
"Mwisho wa uchaguzi mkuu mmoja ni mwanzo wa uchaguzi mkuu mwingine"
JAKAYA KIKWETE.

Je, Rais wetu 2025 awe mtu wa aina na sifa zipi? Hapa chini natoa baadhi kwa maoni yangu (nawe toa yako):​
  1. Awe na sifa, uzoefu na uwezo wa kusimamia vyema tunu za taifa kwa manufaa ya wote. Mfano amani, haki na usawa, uhuru, umoja, utawala bora na muungano wenye tija.​
  2. Atoke CCM ila asiwe mhafidhina wa U-CCM ule ulioathiri taifa na kutufanya kuendelea kuwa maskini miaka 59 toka tupate uhuru, kwa maoni yangu upinzani kwa mwaka 2025 hautaweza kuaminika kuchukua dola kwani mifumo ya ndani ya vyama bado ni dhaifu na pia mifumo nje ya vyama bado ni hatarishi kuweza kuvipa vyama hivyo smooth operation.​
  3. Awe muislam na mwenye mawazo huru. Hapa sizungumzii udini, nazungumzia life principles. Kwa maoni yangu viongozi wa kiislam wanaonesha sana kusikia na kujali vilio vya watu. Tumeona kwa awamu zake nchi hii. Nina imani kwa maumivu yaliyopo sasa, kiongozi wa aina hiyo atatufaa sana.​
  4. Awe kiongozi atakayependa serikali mseto. Uwakilishi wa vyama kadhaa ndani ya serikali na jinsia pia.​
  5. Awe tayari kurekebisha mfumo wa utawala wa nchi kwa kuridhia upatikanaji wa katiba mpya itakayohakikisha, mihimili ya dola inakuwa huru zaidi, madaraka ya raisi yanapunguzwa zaidi, muungano unakuwa bora zaidi, wananchi wanafurahia uhuru wao na mipaka yake zaidi n.k.​
ENDELEA...
 
Hili sasa ndo la kujadili, yaani tuanze kujiandaa na uchaguzi 2025 badala ya kuendelea kulialia na mambo yaliyokwisha jiishia.Ndo ishatoka iyo....!!
 
kwa nini hamuitaki katiba pendekezwa?
Hatutaki kwasababu iliyatupilia chooni maoni ya wenye nchi/wananchi ikachukua maoni ya wana CCM.

Mfano tulipendekeza matokeo ya Urais yapingwe mahakamani mkakataa kwa sababu ya wizi wenu wa kura.

Tulipendekeza serikali tatu mkakataa kwa sababu mnataka kuendelea kuitawala Zanzibar.

Tulipendekeza mbunge angalau awe na bachelor mkakataa kwa sababu mnawategemea kina kibajaji.

N.k.
 
Tunataka rais atakayekubali katiba mpya, tena ile ya rasimu ya Warioba, aheshimu maoni ya watu, na asijigeuze kuwa Mungu mtu kwa kiburi cha madaraka.
Katiba inatakiwa kabla ya kupata Rais mpya, bila katiba mpya Jiwe ataweka boya lake na ndio litakuwa Rais.

Nadhani wote mmeona kilichotokea, mimi bila tume huru kamwe sipigi tena kura, ni kupoteza muda na maigizo tu.
 
Wadau maendeleo ya Nchi yataletwa na Wananchi wenyewe, yaani sisi watanzania. Sioni kama ni afya kwetu kumaliza uchaguzi wa 2020 juzi na kuanza mijadala ya uchaguzi wa 2025 leo. Tunayo miaka mitano (5) ya kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025 kila mmoja kwa nafasi yake, Mhe.Rais, Makamu, Waziri Mkuu, Mbunge Diwani, Mwenyekiti wa kitongoji. Ndiyo Maana Rais mmoja wa Marekani (nadhani Kenedy J F) aliuliza wewe umeifanyia nini Marekani?

Tuulizane kila mtanzania wewe umeifanyia nini Tanzania kwa nafasi yako, usiseme nikiwa Rais, Mbunge, Diwani au Mwenyekiti wa kitongoji! Kila mmoja kwa nafasi yake anaowajibu na anaweza kuacha alama za uongozi au utendaji. Wenzetu hasa wamarekani uchaguzi ukiisha ,siasa zinaisha tunatekeleza , aliyeshindwa anampongeza mshindi na kumpa mikakati mbadala (plan B) mimi ningeshinda ningefanya moja,mbili nk.

Kwetu unaficha madesa, unaomba usiku na mchana asitekeleze ili safari ijayo ushinde wewe, unakwenda kwa wafadhiri unawambia msitoe msaada, unaanza harakati miaka mitano (5) kukwamisha, kutabiri mabaya na kuzomea utendaji, nadhani hili limepitwa na wakati, tubadirike na mabadiriko yaanze na sisi.
 
"Mwisho wa uchaguzi mkuu mmoja ni mwanzo wa uchaguzi mkuu mwingine" JAKAYA KIKWETE.

Je, Rais wetu 2025, awe mtu wa aina na sifa zipi? Hapa chini natoa baadhi kwa maoni yangu. (nawe toa yako);

1) Awe na sifa, uzoefu na uwezo wa kusimamia vyema tunu za taifa kwa manufaa ya wote. Mfano amani, haki na usawa, uhuru, umoja, utawala bora na muungano wenye tija.

2) Atoke CCM ila asiwe mhafidhina wa U-CCM ule ulioathiri taifa na kutufanya kuendelea kuwa maskini miaka 59 toka tupate uhuru, Kwa maoni yangu upinzani kwa mwaka 2025 hautaweza kuaminika kuchukua dola kwani mifumo ya ndani ya vyama bado ni dhaifu na pia mifumo nje ya vyama bado ni hatarishi kuweza kuvipa vyama hivyo smooth operation.

3) Awe muislam na mwenye mawazo huru. Hapa sizungumzii udini, nazungumzia life principles. Kwa maoni yangu viongozi wa kiislam wanaonesha sana kusikia na kujali vilio vya watu. Tumeona kwa awamu zake nchi hii. Nina imani kwa maumivu yaliyopo sasa, kiongozi wa aina hiyo atatufaa sana.

3) Awe kiongozi atakayependa serikali mseto. Uwakilishi wa vyama kadhaa ndani ya serikali na jinsia pia.

4) Awe tayari kurekebisha mfumo wa utawala wa nchi kwa kuridhia upatikanaji wa katiba mpya itakayohakikisha, mihimili ya dola inakuwa huru zaidi, madaraka ya raisi yanapunguzwa zaidi, muungano unakuwa bora zaidi, wananchi wanafurahia uhuru wao na mipaka yake zaidi n.k

ENDELEA...
Ndugu nakuonea sana huruma juu ya uwezo wako wa kuchambua mambo ya siasa (japo una uhuru huo wa kufanya hivyo).

3) Awe muislam na mwenye mawazo huru. Hapa sizungumzii udini, nazungumzia life principles. Kwa maoni yangu viongozi wa kiislam wanaonesha sana kusikia na kujali vilio vya watu. Tumeona kwa awamu zake nchi hii. Nina imani kwa maumivu yaliyopo sasa, kiongozi wa aina hiyo atatufaa sana.

Naomba utaje hapa jukwaani ni principles zipi za maana ambazo Marais wastaafu wa Tanzanina waislamu wamezionyesha na Marais wastaafu wakristo hawakuzionyesha. Usitake kuleta mada chochezi kwa mslahi yako na upeo wako mdogo wa kushabikia udini katika taifa ambalo lina diversification ya dini na uhuru wa kuabudu.

Tangu lini dini ya mtu ikawa ni sifa ya kuchaguliwa katika nafasi ya uongozi wa serikali (nchi)? Unataka kutuaminisha kwamba marais waliotangulia ambao ni waislam walifanya waliyofanya wakiwa madarakani kwa sababu ni waislamu? Kama ni rushwa kutamalaki katika kipindi cha uongozi wao ina maana dini ya kiislamu ndiyo inayoruhusu rushwa pamoja na maovu mengine ambayo yalitendeka katika awamu zao za urais?.

Hakuna kitu ninachokichukia katika Tanzania kama mtu kuweka udini na ukabila mbele kama kigezo cha kuomba uongozi. Na mwalimu Nyerere alishasema katika moja ya hotuba zake kwamba wanasiasa/watu waliofilisika hoja/sera za kisiasa mara nyingi hukimbilia kwenye udini na ukabila. Maendeleo ya Tanzania hayataletwa na dini ya mtu bali uzalendo toka moyoni mwake kwa nchi yake. Dini ni jambo binafsi la mtu. Hivyo kusema kwamba eti rais akiwa wa dini fulani ndiyo maisha ya watanzania yatakuwa mazuri huo ni ULOFA NA UPUMBAVU (in Benjamin Mkapa's Voice-RIP)
 
Wadau maendeleo ya Nchi yataletwa na Wananchi wenyewe, yaani sisi watanzania. Sioni kama ni afya kwetu kumaliza uchaguzi wa 2020 juzi na kuanza mijadala ya uchaguzi wa 2025 leo. Tunayo miaka mitano (5) ya kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025 kila mmoja kwa nafasi yake, Mhe.Rais, Makamu, Waziri Mkuu, Mbunge Diwani, Mwenyekiti wa kitongoji. Ndiyo Maana Rais mmoja wa Marekani (nadhani Kenedy J F) aliuliza wewe umeifanyia nini Marekani? Tuulizane kila mtanzania wewe umeifanyia nini Tanzania kwa nafasi yako, usiseme nikiwa Rais, Mbunge, Diwani au Mwenyekiti wa kitongoji! Kila mmoja kwa nafasi yake anaowajibu na anaweza kuacha alama za uongozi au utendaji. Wenzetu hasa wamarekani uchaguzi ukiisha ,siasa zinaisha tunatekeleza , aliyeshindwa anampongeza mshindi na kumpa mikakati mbadala (plan B) mimi ningeshinda ningefanya moja,mbili nk. Kwetu unaficha madesa, unaomba usiku na mchana asitekeleze ili safari ijayo ushinde wewe, unakwenda kwa wafadhiri unawambia msitoe msaada, unaanza harakati miaka mitano (5) kukwamisha, kutabiri mabaya na kuzomea utendaji, nadhani hili limepitwa na wakati, tubadirike na mabadiriko yaanze na sisi.

Umeshinda kwa wizi wa kura na kumwaga damu unataka uungwe mkono na nani. Watakuunga mkono waliokupa kura na kukusaidia kuiba kura. Na kama ni wafadhili wasitoe hela zao, maana ndio zinatumika kumwaga damu za wananchi.
 
Nikweli mkuu maana mwislamu ndo alituletea maendeleo kwa kusafiri kila siku kwenda ughaibuni, akatuletea zawadi ya Richmond, Dowans, Epa, Escrow (tena hapa akakazia kuwa fedha za ESCROW hazikuwa za serikali) bila kusahau Meremeta, Malipo hewa na mengine lukuki.

Hatutachagua mkristo asije akatujengea Flyover, Reli, Kupanua bandari, Hospitali na Vituo vya Afya, miradi ya maji, kusambaza umeme nchi nzima, kununua ndege mpya 11 kwa cash na ku order nyingine 5, kujenga shule mpya zaidi ya 3000 nchi nzima, kukarabati za awali, kutumbua wazembe na wala rushwa, kuzuia safari za nje zisizo na tija, kuwafundisha watanzania kulipa kodi na kuipenda nchi yao, Kujenga stand zakisasa kila kona, kujenga miradi mikubwa ya kuzalisha umeme, kudhibiti sekta ya madini, kudhibiti sekta ya uchukuzi hasa bandarini, kujenga madaraja yakihistoria, kununua meli kubwa zaidi ya 5 na ku order 8 nyingine, elimu bure. Hatutaki haya tena.
Hayo yote wazungu wa Afrika kusini walifanya, lakini wakina Mandela waliwapinga. Tunataka utawala bora, na vitu isiwe sababu ya kuonea wasiokukubali.
 
Kwani Yesu amesema hagombei 2025? Si tuliaminishwa na Ndugai atalazimishwa hata kama hataki.
 
Back
Top Bottom