Email au namba ya simu ya afisa usalama wa taifa

Parapanda

Member
May 30, 2010
39
4
Wana JF; mwenye email au namba ya simu ya Afisa Usalama wa Taifa yeyote naomba anitumie sasa hivi sasa hivi hapa.
 
078kisha namba ulizokwangua kwenye vocha utampata live bila chenga ila iwe vocha ya sh elfu10
 
Issue gani wataka ku report? Kama ni deal za watu unataka tia mchanga sikushauri ndugu yangu, utajitia matatizoni. Tanzania saiv hatuna usalama wa Taifa, tuna litaasisi la kulinda interest za mafisadi na chama tawala.
Wewe ni nchi gani umeona takukuru, na usalama wa taifa ndo vinara wa rushwa?
Narudia tena, wacha kabisa ku sniff issues kubwa afu ujifanye we ni mzalendo eti uwa expose! Unachezea kifo!
 
*101*0713698405*namba ya vocha ya sh.10,000/=# nafikiri hapo utakuwa umempata usalama wa Taifa.
 
*101*0713698405*namba ya vocha ya sh.10,000/=# nafikiri hapo utakuwa umempata usalama wa Taifa.
<br />
<br />
bro ni janja ya kupata vocha ya dezo ndo inakufanya utoe no. Yako au ndo no. Inayotajiwa nn?
 
Km kuna ishu waripoti acha kabisa unafiki huo. We kula nao sahan moja upate m zako kadhaa na c kujitia matatani
 
*101*0713698405*namba ya vocha ya sh.10,000/=# nafikiri hapo utakuwa umempata usalama wa taifa.
wewe umenichukiza, sikujua kama humu jf kuna mataaahira! Be serious bana..... Au umezoea kuuza sehemu zako za mwili through airtime..... Stop it... Itakucost
 
Ofisi za Usalama wa Taifa sio kwamba zinafichwa msituni. Tuache mtazamo wa kuona Usalama wa Taifa kama KGB enzi za communist Russia. Mikoani au wilayani mara nyingi zipo jengo la ofisi la Mkuu wa Mkoa au Wilaya. Kwa hapa Dar ukienda pale karibu na Saint Peters njia ya kwenda Oysterbay utawakuta. Nyingine eneo la makuburini Kinondoni. Na makazi ya maofisa wao pale karibu na Victoria njia ya Mwenge. Maofisa wa Usalama wa Wilaya au Mkoa wanajulikana waziwazi.

Jamani, usalama wa Taifa wapo kwa ajili ya usalama wa taifa, ni watu tu wa kawaida kama sisi, wana mapungufu yao (mengi tu) na pia wana mazuri yao.

In fact unapaswa kujua wako wapi ili ukiwa na jambo ambalo unaona ni hatari kwa usalama wa taifa uweze kuwafuata na kutoa taarifa. Ni afadhali uogope kituo cha polisi zaidi ya ofisi ya Usalama wa Taifa!

Achana na mambo ya 007 James Bond na Willy Gamba. Zile ni hadithi tu.
 
Ofisi za Usalama wa Taifa sio kwamba zinafichwa msituni. Tuache mtazamo wa kuona Usalama wa Taifa kama KGB enzi za communist Russia. Mikoani au wilayani mara nyingi zipo jengo la ofisi la Mkuu wa Mkoa au Wilaya. Kwa hapa Dar ukienda pale karibu na Saint Peters njia ya kwenda Oysterbay utawakuta. Nyingine eneo la makuburini Kinondoni. Na makazi ya maofisa wao pale karibu na Victoria njia ya Mwenge. Maofisa wa Usalama wa Wilaya au Mkoa wanajulikana waziwazi.

Jamani, usalama wa Taifa wapo kwa ajili ya usalama wa taifa, ni watu tu wa kawaida kama sisi, wana mapungufu yao (mengi tu) na pia wana mazuri yao.

In fact unapaswa kujua wako wapi ili ukiwa na jambo ambalo unaona ni hatari kwa usalama wa taifa uweze kuwafuata na kutoa taarifa. Ni afadhali uogope kituo cha polisi zaidi ya ofisi ya Usalama wa Taifa!

Achana na mambo ya 007 James Bond na Willy Gamba. Zile ni hadithi tu.
Mweee kwa maelezo yako unaonekana na wwe ni afisa usalama,tehe tehe mtajulikana tu humu JF!
 
Back
Top Bottom