Eliud Kipchoge avunja rekodi yake mwenyewe na kuwa mwanariadha wa kwanza kukimbia KM 42 kwa chini ya saa 2

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,757
48,404
Ni ngumu kumeza hii, huyu Mkenya anataka kufanya kitu ambacho hakiingii akilini, sijui nini anawaza muda huu, neno 'badass' litapata maana na tafsiri mpya leo.

Mbio zenyewe ataanza 09:15am
Kwa watani wetu wa Kusini, ili kuwapa picha ya umbali anaokimbia chini ya masaa mawili, ni kama kutoka Dar hadi Mlandizi, kwa ndugu zangu hapa Kenya hiyo ni kama kutoka Nairobi hadi Lari.

TV nyingi duniani zitapeperusha moja kwa moja mubashara, hata zetu hapa Kenya naona zimeweka live, anajadiliwa kitaani nyumba kwa nyumba. Muhimu sana maana inawapa hamasa vijana wengi kwamba linawezekana na itawezekana.

Pia kampuni ya Youtube inapeperusha mubashara

----UPDATE----

Eliud Kipchoge ran a staggering 1:59:40, shattering the mythical sub-two marathon barrier as he completed the #INEOS Challenge in majestic fashion on the streets of Vienna

--
ELIUD KIPCHOGE: MWANARIADHA WA KWANZA KUKIMBIA KM 42 KWA CHINI YA SAA 2

tapatalk_1570871188726.jpeg

Mwanariadha raia wa Kenya, Eliud Kipchoge ameweka rekodi ya kuwa Mwanariadha wa kwanza Duniani kumaliza mbio za marathon kwa muda wa chini ya saa mbili

Kipchoge mwenye miaka 34, amekimbia Kilometa 42.2 kwa kutumia muda wa saa 1, dakika 59 na sekunde 40 kwenye michuano ya Ineos 1:59 huko Vienna, Australia

Hata hivyo, rekodi hiyo haitatambuliwa kama rekodi rasmi Ulimwenguni kwasababu ameweka rekodi hiyo katika michuano isiyo ya wazi

Aidha, katika jaribio lake la mwisho kutaka kuweka rekodi hiyo mnamo mwaka 2017 alishindwa kwa sekunde 25

 
kippose_pix.jpg
Viena, Austria 09:19 E.African Time, leo asubuhi asubuhi. Eliud Kipchoge atakimbia kwenye INEOS 1:59 Challenge. Marathon ambayo imeandaliwa ili ajaribu kuvunja rekodi yake mwenyewe na kuwa binadamu wa kwanza kumaliza Marathon(kilomita 42.2) chini ya muda wa masaa mawili. Rekodi yenyewe ni ya muda wa 2:01:39 ambayo aliibuka nayo Agosti 18, 2018 kule jijini Berlin kwenye Berlin Marathon. Amedhubutu tena kumaliza marathon chini ya masaa mawili na hakufanikiwa ila aliikosa kwa sekunde 26 baada ya kumaliza kwa muda wa 2:00:25. Msikubali kupitwa wadau hii ndio huwa wanasema kwa kimombo, 'its a one in a lifetime event'. Baadhi ya 'pacesetters' 42, wanariadha mashuhuri kutoka kote duniani, ambao wakakimbia pamoja na Eliud ili kumsaidia kutimiza malengo yake.
ineos-159-challenge-organisers-pull-out-all-stops-800x600.jpg
 
aiseee dahh ni sheedah mazeee...jamaa anatupiga promo ya hatareeeee, ila dah kwa wenzetu naona safari tv inawaonesha wahdzabe wakikula kobee!!
Huyu kwanini msiseme ni kutoka "East Africa", au East Africans ni Diamond na Alikiba na Harmonize tu lakini ikifika upande wa wakenya kufanya vizuri hakuna EAC?.

Tukikataa EPA, free movement of people and businesses, hapo ndio mnaikumbuka EAC kwasababu inawaumiza. Ubinafsi na kupenda sifa ndio ugonjwa wenu.
 
Shughuli tayari imeanza dakika ya 13:01 live on Kwese Sports, Supersport on Dstv, NTV, Citizen Tv.
 
42 km kwa masaa mawili....

Yaaan atakimbia km 21 kwa lisaa limoja,au 21km kwa dakika 60

Ni sawa na kusema atakimbia km 0.35 kwa dakika moja

Hii pia ni sawa tu nikisema atakimbia mita 350 kwa dakika moja

Pata picha tu...dakika moja huyu jamaa anakuwa kakimbia umbali sawa na viwanja vya mpira vitatu na nusu

Zaidi ni sawa na kusema atakimbia mita 5.8 kwa sekunde moja!!

Hehehehe, mita 5.8 kwa sekunde!! yetu macho,ngoja tusubili tujionee
 
Harmonize ndo nan
Huyu kwanini msiseme ni kutoka "East Africa", au East Africans ni Diamond na Alikiba na Harmonize tu lakini ikifika upande wa wakenya kufanya vizuri hakuna EAC?.

Tukikataa EPA, free movement of people and businesses, hapo ndio mnaikumbuka EAC kwasababu inawaumiza. Ubinafsi na kupenda sifa ndio ugonjwa wenu.
 
42 km kwa masaa mawili....

Yaaan atakimbia km 21 kwa lisaa limoja,au 21km kwa dakika 60

Ni sawa na kusema atakimbia km 0.35 kwa dakika moja

Hii pia ni sawa tu nikisema atakimbia mita 350 kwa dakika moja

Pata picha tu...dakika moja huyu jamaa anakuwa kakimbia umbali sawa na viwanja vya mpira vitatu na nusu

Zaidi ni sawa na kusema atakimbia mita 5.8 kwa sekunde moja!!

Hehehehe, mita 5.8 kwa sekunde!! yetu macho,ngoja tusubili tujionee

Asante, analysis kali sana hii, tayari ameanza, naona wote wako very relaxed, njia yote imefurika watu wanamshabikia balaa, masaa haya mawili dah nahisi kama siku nzima kwa jinsi moyo unanidunda.
 
Huyu kwanini msiseme ni kutoka "East Africa", au East Africans ni Diamond na Alikiba na Harmonize tu lakini ikifika upande wa wakenya kufanya vizuri hakuna EAC?.

Tukikataa EPA, free movement of people and businesses, hapo ndio mnaikumbuka EAC kwasababu inawaumiza. Ubinafsi na kupenda sifa ndio ugonjwa wenu.
Umewabana vibaya mno!
 
42 km kwa masaa mawili....
Yaaan atakimbia km 21 kwa lisaa limoja,au 21km kwa dakika 60
Ni sawa na kusema atakimbia km 0.35 kwa dakika moja
Hii pia ni sawa tu nikisema atakimbia mita 350 kwa dakika moja
Pata picha tu...dakika moja huyu jamaa anakuwa kakimbia umbali sawa na viwanja vya mpira vitatu na nusu
Zaidi ni sawa na kusema atakimbia mita 5.8 kwa sekunde moja!!
Hehehehe, mita 5.8 kwa sekunde!! yetu macho,ngoja tusubili tujionee
Dah, pata picha mita 5 ndani ya sekunde.
 
Back
Top Bottom