Elimu ya usawa wa kijinsia bado inahitajika Afrika

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,268
Gender ni jinsia ya kike na kiume. Afrika mtoto wa kiume anapewa nafasi kubwa katika famila tangu akiwa mdogo. Mfano tu mama kunyanyaswa na mumewe kwakua hana mtoto wa kiume.

Kuna familia unakuta wamezaliwa mabinti na wavulana. Imetokea mabinti ndiyo wenye uwezo wa pesa, watasaidia uchumi wa nyumbani lakini kwenye maamuzi ya kifamilia hawashirikishwi.

Mgawanyo wa ardhi pia humpendelea mtoto wa kiume. Wanaamini mtoto wa kike ataolewa. Sasa ikitokea hukuolewa au umeolewa mume ndoa ya wake wengi na ardhi imekwenda kwa mke mkubwa

Kuna kisa nilikisoma gazetini, mama analalamika wakati wa kulima mume wake anashinda chini ya mfenesi anacheza bao na rafiki zake. Analima mpunga mwenyewe. Wakati wa mavuno mume ndiye anahesabu magunia na kutafuta soko.

Pesa yote anashika yeye. Tena si ajabu pesa ya mauzo ikawa mahari ya kuoa mke mwingine.
 
equality.png
 
Sema haya maisha mnayaona magumu baada ya kuingiza uzungu.

Maisha yetu yalikuwa na mfumo mzuri kabisa.

Hivi katika mmomonyoko wa maadili ufa umepanuka kipindi hiki zaidi au enzi za mababu zetu? Wanawake walipewa heshima yao walipostahili na jinsia zote ziliheshimiana wake kwa waume.

Mwanamke hakupewa urithi kwasababu ilifahamika mwanaume ndiye mlinzi na mhudumu wa familia. Hukusikia kwa kiasi tusikiacho leo wanaume hawahudumii familia au kuyakimbia majukumu.

Leo wanawake mna mali wanaume nao wanamali ila hizo familia hazikaliki kila mmoja anampanda mwenzake kichwani.
 
Daby,
Wengine ni ma miss mpaka 70’s wakati nyumbani hukupewa ardhi wakijua utalima kwa mume wako.
 
Wengine ni ma miss mpaka 70’s wakati nyumbani hukupewa ardhi wakijua utalima kwa mume wako.
Sky hata sio zamani...miaka ya 90 kwenye jamii yangu mwanamke au mwanaume akifikosha umri fulani ambao iliaminika amekuwa mtu mzima ilikuwa aibu kutokuwa kwenye ndoa.


Jamii ya kimagharibi italitafsiri hili kama sio suala baya. Wao wanaamini si kila mmoja ana ndoto ya kuoa au kuolewa.

Lakini itazame ndoa kwa mapana yake. Inapunguza umalaya, inaunganisha jamii pamoja, inasitiri wenza na kujenga jamii vizazi kwa vizazi.
 
Sky hata sio zamani...miaka ya 90 kwenye jamii yangu mwanamke au mwanaume akifikosha umri fulani ambao iliaminika amekuwa mtu mzima ilikuwa aibu kutokuwa kwenye ndoa.


Jamii ya kimagharibi italitafsiri hili kama sio suala baya. Wao wanaamini si kila mmoja ana ndoto ya kuoa au kuolewa.

Lakini itazame ndoa kwa mapana yake. Inapunguza umalaya, inaunganisha jamii pamoja, inasitiri wenza na kujenga jamii vizazi kwa vizazi.
Zamani baba alimuoza mtoto kwa rafiki yake. Mzee alitambua ni mtu wa aina gani anamuoa binti yake. Binti pia anakua na staha kwa mume kwakua pia ni rafiki wa baba.
 
Zamani baba alimuoza mtoto kwa rafiki yake. Mzee alitambua ni mtu wa aina gani anamuoa binti yake. Binti pia anakua na staha kwa mume kwakua pia ni rafiki wa baba.
Sasa hivi mnamaliza chuo mnakutana kazini...

Mmoja anampendea mwenzake chura mwingine uhandsome na uwezo wa kumlipia kodi ya chumba na make ups.

Muda ukisogea unaona mbona chura za kawaida saana...huyu wa kike naye akiizoea kazi anaona ataweza kujilipia kodi mwenyewe na wanaume wanaoweza kumfanyia zaidi wapo.

Tupo katika hatua mbaya ya maisha saana. Namiss kipindi unampendea mwanamke uchakarikaji wake kwenye kukamua n'gombe.
 
Lea watoto wenu wa kike katika malezi ya kujitambua.

Kujithamini

Na kujisimamia na kuwa na misimamo

Kujitafutia

Kujijali


Kujua maisha yake ni ya thamani na ukamilifu wake hautegemei ndoa/ mwanaume


Then mengine yatasimama

Hutosikia malalamiko ya alime yeye auze mwengine. kwanza ataanzia wapi kuuza tu

Hutosikia wameacha kazi au biashara kwa kuwa kuna binadamu wamekutana na meno 32 akamwambia aache kazi/biashara

Hutosikia binti kageuzwa punching bag......

Kesi za kuambiwa "tuzae kwanza" zitapungua kwa asilimia kubwa


Malezi

Malezi

Malezi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye swala la mzazi wakike kupewa lawama baada ya kukosa mtoto wakiume hua Inategemea na akili za huyo mwanaume zilivyo.


Kihalisia mtu mwenye utimamu huwezi kumlaumu mkeo kwa kutopata mtoto wa kike wakati hana tatizo la ugumba

Jamii za wasukuma na wamang'ati mtoto wakike ni dili sana kuliko wakiume, kwasababu mtoto wakike akiolewa familia itanufaika kwa kupokea ng'ombe nyingi.
 
Back
Top Bottom