Elimu ya Tanzania haiishi changamoto, NBAA sasa wameamua kuuza mitihani ya CPA

The Evil Genius

JF-Expert Member
Mar 21, 2014
5,452
17,156
Jana nilikuwa naongea na bwana mdogo anafanya mitihani ya wahasibu ya CPA mbayo inaanza jumanne. Bwana mdogo amefanya hii mitihani muda mrefu sasa jana namuuliza unamaliza lini mbona kila mara unarudia rudia, dogo akajitetea kwamba kutokana na shughuli zake huwa anakosa muda wa maandalizi vizuri ya mitihani lakini akaniambia kitu kilichonishangaza.

Dogo akasema alipofaulu mtihani wa term hii basi mwakani mwezi wa 2 atanunua mitihani. Nikamuuliza kununua kiaje, akasema bodi ya uhasibu, NBAA imeanzisha utaratibu wa mitihani ya katikati ambayo gharama yake ni kubwa ila hakuna kushindwa/fail. Kwamba atajitoa mhanga alipie mitihani 2 milioni 1.1 ili afaulu kwani mitihani hiyo ya Mid sessions ni kama vile NBAA huwa wanawauzia kwa bei kubwa.

Akaniambia kwa sasa ni wewe kuchagua, ufanye mitihani ya kawaida ya ratiba za board kwa mwezi 5 na 11 kwa bei ndogo ya laki moja na nusu kwa mtihani ama ununue mtihani kwa mid sessions kwa mtihani mmoja kwa laki 5 na elfu hamsini ufaulu.

Dogo anasema hii ya katikati hata hihitaji kuwa maandalizi mazuri ili ufaulu, unafaulu tu kwani ni rahisi sana ndio maana wanasema huwa ni kama inauzwa ila hii ya ratiba za kawaida kama huna maandalizi ya kutosha hutoboi, mitihani migumu sana.

Dogo anasema matajiri wengi ana watoto wa matajiri ama mwenye uwezo sasa hawafanyi ya kawaida, wanafanya mid sessions ambako money talks, unalipa hela nyingi unakuwa na uhakika wa kufaulu, hii ya ratiba za kawaida ndio wanafanya choka mbaya wengi kwani bei yake ni rahisi ila inahitaji msuli mkubwa.

Kwamba kaa sasa ni wewe kuchagua utumie Pesa yako uwe na uhakika wa kufaulu ama utumie muda wako kujisomea na kulipa kidogo ila hakuna uhakika wa kufaulu mitihani.

Siku Hizi taaluma Tanzania zimekuwa ni hovyo hovyo tu, juzi mtihani wa madaktari umevuja wazi kabisa wamama walikuwa wanafungia vitumbua kabla hata mtihani haujaanza.

Kwa hiyo leo hii ukisikia mtu ana CPA wala usishtuke, siku hizi zinauzwa na kununuliwa kisheria kabisa.

Elimu ya Tanzania haitaisha vituko.
 
Hahaha..
Kwamba tunapa watu waliobambikiziwa uhasibu feki !!!

Angalau siku hizi unaweza kufanya kazi nyingi za uhasibu kwa software hata Kama we siyo mhasibu
 
Kwa sasa hapa Tz, kama;
Urais unanunua.

Ubunge unanunua.

Udiwani unanunua.

Ujumbe wa serikali za mtaa unanunua.

Usheikh unanunua.

Uchungaji unanunua.

Umufti unanunua.

Uaskofu unanunua.

Kipi kingine kinaweza kisiuzwe au kununuliwa hapa Tz?
 
Sio kweli Mkuu,

Hiyo mitihani ya Mid session sio Kwa masomo yote ya level husika. Ni masomo machache Sana Yaani hayazidi masomo mawili Kwa kila level.

Na ni masomo yale heavy kidogo.

Tupunguze kushadadia vitu vya kusikia pasipo Kuwa na uhakika navyo Mkuu.
 
Kwa sasa hapa Tz, kama;
Urais unanunua...
Ubunge unanunua....
Udiwani unanunua....
Ujumbe wa serikali za mtaa unanunua...
Usheikh unanunua....
Uchungaji unanunua....
Umufti unanunua....
Uaskofu unanunua....

Kipi kingine kinaweza kisiuzwe au kununuliwa hapa Tz?
Mbunye pia
 
Jana nilikua naongea na bwana mdogo anafanya mitihani ya wahasibu ya CPA mbayo inaanza jumanne. Bwana mdogo amefanya hii mitihani muda mrefu sasa jana namuuliza unamaliza lini mbona kila mara unarudia rudia, dogo akajitetea kwamba kutokana na shughuli zake hua anakosa muda wa maandalizi vizuri ya mitihani lakini akaniambia kitu kilichonishangaza.

Dogo akasema alipofaulu mtihani wa term hii basi mwakani mwezi wa 2 atanunua mitihani. Nikamuuliza kununua kiaje, akasema bodi ya uhasibu, NBAA imeanzisha utaratibu wa mitihani ya katikati ambayo gharama yake ni kubwa ila hakuna kushindwa/fail. Kwamba atajitoa mhanga alipie mitihani 2 milioni 1.1 ili afaulu kwani mitihani hiyo ya Mid sessions ni kama vile NBAA hua wanawauzia kwa bei kubwa.

Akaniambia kwa sasa ni wewe kuchagua, ufanye mitihani ya kawaida ya ratiba za board kwa mwezi 5 na 11 kwa bei ndogo ya laki moja na nusu kwa mtihani ama ununue mtihani kwa mid sessions kwa mtihani mmoja kwa laki 5 na elfu hamsini ufaulu.

Dogo anasema hii ya katikati hata hihitaji kua maandalizi mazuri ili ufalu, unafaulu tu kwani ni rahisi sana ndio maana wanasema hua ni kama inauzwa ila hii ya ratiba za kawaida kama huna maandalizi ya kutosha hutoboi, mitihani migumu sana.

Dogo anasema matajiri wengi ana watoto wa matajiri ama mwenye uwezo sasa hawafanyi ya kawaida, wanafanya mid sessions ambako money talks, unalipa hela nyingi unakua na uhakika wa kufaulu, hii ya ratiba za kawaida ndio wanafanya choka mbaya wengi kwani bei yake ni rahisi ila inahitaji msuli mkubwa.

Kwamba kaa sasa ni wewe kuchagua utumie Pesa yako uwe na uhakika wa kufaulu ama utumie muda wako kujisomea na kulipa kidogo ila hakuna uhakika wa kufaulu mitihani.

Siku Hizi taaluma Tanzania zimekua ni hovyo hovyo tu, juzi mtihani wa madaktari umevuja wazi kabisa wamama walikua wanafungia vitumbua kabla hata mtihani haujaanza.

Kwa hiyo leo hii ukisikia mtu ana CPA wala usishtuke, siku hizi zinauzwa na kununuliwa kisheria kabisa.

Elimu ya Tanzania haitaisha vituko.
The underboss! huyo dogo ni vizuri akakueleza vizuri kwa nini anafeli lakini anachokisema siyo sahihi.

Mitihani ya NBAA kwa ajili ya kuwa CPA(T) ni laini sana kwa wale waliopikika au waliojipika vizuri kwenye course husika.Hakuna kitu kinaitwa kuvuja au kuuza mitihani ya NBAA huyo dogo kufeli kwake kusimfanye aanze kutoa mapovu kwa kati ya Bodi na mitihani inayoheshimika katika nchi hii.Mi ni shuhuda nimefanya mitihani husika na I'm certified.

Hiyo mitihani ya Mid-session ya NBAA inawalenga wale waliohitimu ACCA ambao wanataka watambuliwe kama CPA(T) na kumaliza mitihani husika kwa Wakati.Na mitihani wanayofanya ni ile tu ambayo inahusu issues za kiuhasibu kwenye mazingira ya Tanzania pekee to be specific Tanzania Tax Laws and Practice na ndio maana mitihani hii ni ghali kwa kuwa hata mitihani ya ACCA ni ghali ukilinganisha na ya NBAA.

Nashauri huyo dogo atubu.

Article.
 
The underboss! huyo dogo ni vizuri akakueleza vizuri kwa nini anafeli lakini anachokisema siyo sahihi.

Mitihani ya NBAA kwa ajili ya kuwa CPA(T) ni laini sana kwa wale waliopikika au waliojipika vizuri kwenye course husika.Hakuna kitu kinaitwa kuvuja au kuuza mitihani ya NBAA huyo dogo kufeli kwake kusimfanye aanze kutoa mapovu kwa kati ya Bodi na mitihani inayoheshimika katika nchi hii.Mi ni shuhuda nimefanya mitihani husika na I'm certified.

Hiyo mitihani ya Mid-session ya NBAA inawalenga wale waliohitimu ACCA ambao wanataka watambuliwe kama CPA(T) na kumaliza mitihani husika kwa Wakati.Na mitihani wanayofanya ni ile tu ambayo inahusu issues za kiuhasibu kwenye mazingira ya Tanzania pekee to be specific Tanzania Tax Laws and Practice na ndio maana mitihani hii ni ghali kwa kuwa hata mitihani ya ACCA ni ghali ukilinganisha na ya NBAA.

Nashauri huyo dogo atubu.

Article.
Kwa mwaka kuna wahitimu wa ngapi wa ACCA hadi wawekewe sessions yao peke yao? Kwamba mid sessions imewekwa kwa watu wanaomaliza ama wenye ACCA pekee? Kwa hiyo wanaotakiwa kufanya hiyo mitihani ni waliomaliza ACCA tu?

Kwani hao wenye ACCA ambao kama wapo wengi kiasi hicho hadi wawekewe sessions zao hawawezi kufanya mitihani ya kawaida?

Kwa hiyo justification yako ya bei ni kwa sababu ACCA ni gharama kuliko hii ya NBAA, je kipato cha waingereza ama watu wanaofanya hiyo ya ACCA inalingana na kipato cha watanzania?

Wewe hujuoni kama ni mmoja wapo ya wlionunua hiyo mitihani maana una hoja dhaifu halafu unajiita certified.
 
Sio kweli Mkuu,

Hiyo mitihani ya Mid session sio Kwa masomo yote ya level husika. Ni masomo machache Sana Yaani hayazidi masomo mawili Kwa kila level.

Na ni masomo yale heavy kidogo.

Tupunguze kushadadia vitu vya kusikia pasipo Kuwa na uhakika navyo Mkuu.
Yakiwa heavy kidogo ndio inabidi yanunuliwe, sio?
 
Kwa sasa hapa Tz, kama;
Urais unanunua...
Ubunge unanunua....
Udiwani unanunua....
Ujumbe wa serikali za mtaa unanunua...
Usheikh unanunua....
Uchungaji unanunua....
Umufti unanunua....
Uaskofu unanunua....

Kipi kingine kinaweza kisiuzwe au kununuliwa hapa Tz?
mbususu unanunua
 
Kwa mwaka kuna wahitimu wa ngapi wa ACCA hadi wawekewe sessions yao peke yao? Kwamba mid sessions imewekwa kwa watu wanaomaliza ama wenye ACCA pekee? Kwa hiyo wanaotakiwa kufanya hiyo mitihani ni waliomaliza ACCA tu?

Kwani hao wenye ACCA ambao kama wapo wengi kiasi hicho hadi wawekewe sessions zao hawawezi kufanya mitihani ya kawaida?

Kwa hiyo justification yako ya bei ni kwa sababu ACCA ni gharama kuliko hii ya NBAA, je kipato cha waingereza ama watu wanaofanya hiyo ya ACCA inalingana na kipato cha watanzania?

Wewe hujuoni kama ni mmoja wapo ya wlionunua hiyo mitihani maana una hoja dhaifu halafu unajiita certified.
Idadi ya Wanaomaliza mitihani ya ACCA inapatikana kwa Wahusika .Kama unahitaji nakushauri ufanye ufuatiliaji kwa Wahusika.Mitihani ya Mid- examination session ya NBAA inawalenga waliomaliza ACCA ,hata hivyo kutokana na sababu mbalimbali hata wale walio kwenye normal examinations sessions za NBAA hawazuiliwi kufanya mitihani husika ikiwa watameet General NBAA's Examinations By Laws pamoja na Terms and conditions za papers husika.

Nakushauri upokee Ujumbe na umfikishie dogo mbona unataka kuleta ugumu lakini kwa bahati nzuri ikiwa wewe ndio mhusika lakini umejificha kwenye kichaka cha dogo nakushauri komaa acha ujinga na wewe uitwe CPA(T).

ARTICLE.
 
Back
Top Bottom