Elimu ya sanaa na ufundi shuleni irudishwe

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
Sisi tuliosoma enzi za awamu ya kwanza, enzi za Chama kushika hatamu, tunakumbuka elimu ya sanaa na ufundi. Hili lilikua somo kamili, kulikua na walimu waliohitimu mafunzo hayo.

Shule zilikua na karakana, wavulana walifundishwa useremala (labda nimekosea) na uwashi. Hata ujenzi wa madarasa na majengo ya shule baadhi ya kazi zilifanywa na wanafunzi wa kiume kuanzia darasa la tano, sita mpaka la saba.

Wasichana tulifundishwa kushona, mara nyingi mwalimu alikua ni wa kike. Pamoja na kuwa cherehani ilikua moja au mbili lakini kila mtu alipata nafasi ya kujifunza basic knowledge ya kushona.

Nimekutana na raia wengi kutoka nchi zilizokua za Soviet Union. Wanaume wote wa nchi hizi ni wajenzi wazuri. Waliniambia kuwa hii ni sehemu ya elimu nchini kwao. Hata asiyeenda chuoni anakua na ujuzi wa kuanzia maisha.

Hii dhana Mwalimu Nyerere alituanzishia. Ikiwapendeza mnaweza kuirudisha mashuleni.
 
Sky Eclat , Ijumaa ya majuzi Wizara yenye dhamana ya elimu iliandaa mkutano wa wadau wa elimu. Sehemu fulani ya mkutano huo ilirushwa mubashara kwenye redio na runinga. Hoja unayoisema ni miongoni mwa hoja zilizoibuliwa. Jumamosi wiki hii wadau walikaribishwa kwenye mkutano kama huo utakaofanyika Dodoma.

REJEA:
 
Sky Eclat , Ijumaa ya majuzi Wizara yenye dhamana ya elimu iliandaa mkutano wa wadau wa elimu. Sehemu fulani ya mkutano huo ilirushwa mubashara kwenye redio na runinga. Hoja unayoisema ni miongoni mwa hoja zilizoibuliwa. Jumamosi wiki hii wadau walikaribishwa kwenye mkutano kama huo utakaofanyika Dodoma.

REJEA:

Kwa kufanikisha hili, ikiwezekana kuchukua mafundi wenye ujuzi watakaopenda kufundisha wapelekwe chuoni. Wana uhakika wa ajira baada ya mfunzo.
 
Ulaya somo la ufundi uwashi na useremala ilikua ni muhimu kwa kila mtoto wa kiume. Hii dhana walikua nayo tangu katika utawala wa Warumi. Hii imesaidia kuipa Ulaya na Makoloni maendeleo katika majengo.
 
Back
Top Bottom