Elimu ya mgombea urais tz kikatiba ni kiwango gani? Ktk katiba mpya iweje?

Bilionea one

Member
Aug 13, 2012
90
47
Hivi kwa mujibu wa katiba yetu, mtu anayepaswa kuwa mgombea urais wa Tanzania level yake ya Elimu ni kiasi gani cha elimu? Naomba kufahamishwa na si kutukunwa. Aulizaye hujibiwa!

Kwenye uliza uliza yangu mtaani nimeambiwa ni lazima awe na degree. Je, kama ndivyo ni sawa? Je, hatujawaacha wengine nje ya ulingo?

Kama kiwango nilichoambiwa mtaani (shahada 1) ni kweli, je, katika katiba mpya tuiendeleze kiwango hicho cha elimu.

Tume ya katiba mpya inakuja huku kwetu Kasulu,kigoma nami ningependa niseme kwamba kiwango kiwe degree moja, ILA SASA sijui kama hiyo degree ndo iliyopo sasa au la.

Mimi binafsi nadhani mawaziri wasio na elimu ya kutosha ni sehemu ya tatizo.
 
Back
Top Bottom