sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,032
Maisha ni safari, nimetoka mbali, leo nmekumbuka maisha nliyopitia ya kuishi vyumba vya kupanga.
Kiukweli ni ndoto ya kila kijana kuanza kuishi maisha ya getoni iwe single room ama self-contained kabla hajajenga au kununua nyumba yake.
Nikiwa kama mtu nliewahi kupitia maisha hayo, nlikumbana pia na changamoto zake katika ishu za kuwekea kipaumbele kuishi sehemu isiyo na mmiliki
Basi nitatumia teknolojia hii ya intaneti kuwamegea japo ka elimu kidogo kupitia humu JamiiForums.
Kwanza niweke wazi Wapangaji wengine ni wastaarabu ila Kuna wengine ni vichomi ndo wanaopelekea mtu akitaka chumba lazima aulizie kama mwenye nyumba anakaa hapohapo ili hio nyumba aikwepe.
Sababu ni hizi:
Kukosa amani ukichelewesha kodi. Yani mtu anaekudai kodi anakukosesha raha maana mpo nyumba moja, Anaweza kukudai Kodi ukasema hauna , kimbembe kipo ukipika nyama atakuja mlangoni kukukaripia hela ya kumlipa huna ila unakula nyama, sasa anataka ulale njaa? Pia kwa wale wa viti virefu mkikutana huko bar anaweza kukukata hilo jicho ukaishiwa amani acha tu, sasa anatake usistarehe?
Wivu - Wengine watoto wao unakuta wamenaliza vyuo ila hawana kazi na wewe una kazi basi huwa kuna wivu, ukitwanga kitunguu swaum tu ndani anakufuata na maneno hodi hodi kwanini unatoboa ukuta wangu unajua bei ya siment wewe.
Wengi huwa na funguo spea, hali hii huwa inawapa wasiwasi na woga wapangaji huenda mwenye nyumba huwa anapiga chabo wakiwa hawapo.
Usumbufu wa bili za maji na umeme, Michango itayokusanywa kwa wapangaji mara nyingi ni kwa ajili ya matumizi yake, bili zikitoka hawaonyeshi mnaambiwa tu ni kiasi kazaa, ukiuliza utackia kama umechokaa hama.
Kubanwa Uhuru, Vijana wanaondoka nyumbani na kwenda kupanga ili kuwa huru lakini anapoenda kumkuta tena mwenye nyumba inakuwa kama bado anaishi nyumbani, masharti kibao Mara usichelewe kurudi, Usiingize mwanamke, Kupeleleza kila unachoingiza room, n.k. jamani hivi vitu ni serious msidhani ni story.
Kiukweli ni ndoto ya kila kijana kuanza kuishi maisha ya getoni iwe single room ama self-contained kabla hajajenga au kununua nyumba yake.
Nikiwa kama mtu nliewahi kupitia maisha hayo, nlikumbana pia na changamoto zake katika ishu za kuwekea kipaumbele kuishi sehemu isiyo na mmiliki
Basi nitatumia teknolojia hii ya intaneti kuwamegea japo ka elimu kidogo kupitia humu JamiiForums.
Kwanza niweke wazi Wapangaji wengine ni wastaarabu ila Kuna wengine ni vichomi ndo wanaopelekea mtu akitaka chumba lazima aulizie kama mwenye nyumba anakaa hapohapo ili hio nyumba aikwepe.
Sababu ni hizi:
Kukosa amani ukichelewesha kodi. Yani mtu anaekudai kodi anakukosesha raha maana mpo nyumba moja, Anaweza kukudai Kodi ukasema hauna , kimbembe kipo ukipika nyama atakuja mlangoni kukukaripia hela ya kumlipa huna ila unakula nyama, sasa anataka ulale njaa? Pia kwa wale wa viti virefu mkikutana huko bar anaweza kukukata hilo jicho ukaishiwa amani acha tu, sasa anatake usistarehe?
Wivu - Wengine watoto wao unakuta wamenaliza vyuo ila hawana kazi na wewe una kazi basi huwa kuna wivu, ukitwanga kitunguu swaum tu ndani anakufuata na maneno hodi hodi kwanini unatoboa ukuta wangu unajua bei ya siment wewe.
Wengi huwa na funguo spea, hali hii huwa inawapa wasiwasi na woga wapangaji huenda mwenye nyumba huwa anapiga chabo wakiwa hawapo.
Usumbufu wa bili za maji na umeme, Michango itayokusanywa kwa wapangaji mara nyingi ni kwa ajili ya matumizi yake, bili zikitoka hawaonyeshi mnaambiwa tu ni kiasi kazaa, ukiuliza utackia kama umechokaa hama.
Kubanwa Uhuru, Vijana wanaondoka nyumbani na kwenda kupanga ili kuwa huru lakini anapoenda kumkuta tena mwenye nyumba inakuwa kama bado anaishi nyumbani, masharti kibao Mara usichelewe kurudi, Usiingize mwanamke, Kupeleleza kila unachoingiza room, n.k. jamani hivi vitu ni serious msidhani ni story.