Elimu ya juu sio lazima kwa watanzania serikali yathibitisha

Norway, Sweden hizi ni mfano wa nchi ambazo zimendelea, na elimu ya juu ni bure, ni nao ushahidi, kuna marafiki zangu ambao ni watanzania wansoma huko na wanasema elimu huko ni bure

Gosheni,
Hizi habari siku zote huwa mtu unapewa nusunusu au unaelewa na kukumbuka kile unachotaka kukumbuka. Wakati nikisoma , nilifika Sweden na kuelewa system, zao. Kwanza kwa kuanzia ni kuwa wao hawasomi bure ila wanakopeshwa ada na baadaye wanakuja kulipa. Wengi ili kupata shule kwani kwao ni shida na aghali, basi huwa wanakimbilia nchi za Estern Europe hasa masomo ya Uganga na huko wakimaliza, nchi zao zinaitambua hiyo degree kwani imetoka ndani ya European Union. Akianza kazi anaanza kukatwa. Hivyo ndugu yangu hamna cha bure.
Ila kwa Sweden ambako nilifika, jamaa wana system nzuri sana. Kwa mfano masomo ya ufundi (Engineering), haya husoma watu wachache sana na ikibidi hata wakali huletwa kutoka nje. Huko bwana inabidi kweli uwe mkali kwani ukilazimisha YATAKUSHINDA. Sasa hawa Wahandisi tuseme kama 100 wanakwenda kwenye viwanda vya akina Blaupunkt, Volvo, Ericksson, Saab, Scania, nk na hawa kazi yao inakuwa kufanya utafiti na ugunduzi wa vifaa au bidhaa mpya, na wakishafanya hivyo wanaingia kwenye kazi ya kuplan na kutengeneza/kuunda mkanda wa production. Wakishamaliza hapo ndipo wanaita Mafundi mchundo kama mimi na kuanza kuwaonyesha jinsi kila kitu kinavyofanya kazi kwa lugha ya kitaalamu. Wakimaliza hapo sasa wanachukuliwa akina form 4 au darasa la saba, wanafundishwa kazi kila mtu na ki-section chake. Jamaa wanapiga mzigo na anakuwa hajui hata anatengenza nini ila wale technicians na wahandisi. Hivyo ukiangalia ukweli ni kwamba huhitaji kuwa na Wasomi in Quantity ila quality.

Pia wenzetu wana vyuo vingi sana vidogovidogo kwa ajili ya kusomea masomo madogomadogo kama kwenye ukulima, mifugo, nk. Ni kama vyuo vya kilimo Tumbi, Ukiliguru, Ilonga etc. Ila huko wanafanya zaidi practical. Nafikiri kwa Tanzania tunahitaji hii system. Kama zile secondary za Lowassa zingelitakiwa kufanya hii kazi. Kwa mfano huku kwetu Sikonge tungeliletewa vyuo ambavyo vijana wanasomea kilimo cha kisasa, ufugaji wa kisasa na biashara kidogo ili watu wapate mwanga wa hizo shughuli zao na kuweka mahesabu ili kujua anapata hasara au lah.
 
Last edited:
Norway, Sweden hizi ni mfano wa nchi ambazo zimendelea, na elimu ya juu ni bure, ni nao ushahidi, kuna marafiki zangu ambao ni watanzania wansoma huko na wanasema elimu huko ni bure

Gosheni,

Kuna nchi nyingi tu hapa duniani ambako elimu kuanzia chini mpaka juu ni ya bure. Hizo nchi ni pamoja na ulizozitaja na pia German lakini pia sio bure kwa maana unayoisema wewe. Hizo nchi ni kwamba hakuna tuition fee lakini mambo mengine yote yanalipiwa.

Kama ni mgeni basi unatakiwa kuwa na uwezo wa kuishi huko, kitu ambacho bado ni pesa nyingi. Kama ni mwenyeji basi wananchi wengine wamekatwa kodi na ndio maana kodi ya Scandinavia iko juu sana. There is no free lunch mkuu, hizo ni system tofauti tu juu ya namna ya kupata pesa za kusomesha vijana wetu. Hata Tanzania huko nyuma elimu ilikuwa ni bure bora uwe na qualification zinazotakiwa.

Ni rahisi kusema Scandinavia elimu ni bure kwasababu kuna Watanzania wanasoma bure, huwezi kujua wako pale kwa misingi ipi hata kama bado ni Watanzania.

Pamoja na Scandinavia kutokuwa na tuition fee lakini bado watu waliosoma mpaka elimu ya juu hawafikii asilimia kubwa. Wala serikali haifanyi juhudi kutaka hiyo asilimia iongezeke.
 
1. Secondary education should be compulsory and not Univ education, although with the latter we can run a competitive economy.
2. An educated nation itaondokana na kasumba za kuchagua viongozi based on ushabiki and celebrity status.
3. We need university educated personnel in all walks of government ranks, la sivyo our Form 6 personnel in government authorities will always be outpaced in thinking by the educated ones who make shady deals.

"An educational system has to give the people of a given culture the ability to make the world and their own lives intelligible. It is through the creation of intelligibility that meaningful education spurs the outburst of daring, initiative, invention and constructive activity." Justinian F Rweyemamu

Tanzania's stock of knowledge needs to be expanded, and this is by having a considerable % of the population with Univ. or professional education.
 
1. Tena mimi kwa upande wa madaktari..tushomesheni kidogo tu...hata may be 100! kuna haja gani kwa sasa Tz wanamaliza udaktari wanafunzi kama 300 kwa mwaka..halafu baada ya miaka mitatu 70% ya hawa wameshatoroka nchi au wanafanya kazi zingine? Je sii wanasoma kwa mkopo lili kusaidia wananchi wetu? Yet hospitali zetu hazina madktari kabisa haswa wilayani!

2. Bora kuweka pesa nyingi kusomesha watu wa kati kama Assistant Medical Officers (AMO) ambao wao hawatoroki na hospitali nyingi ndio wapo wanachapa kazi kama kawa!

3. As a country elimu ya ufundi kwa watz wengi wanaomaliza sekondari.. ndo muhimu! Sera iwe kila wilaya iwe na vyuo viwili aina ya veta!
 
Last edited:
Gosheni,

Mbona alichosema huyo naibi waziri ni sahihi kabisa? Hakuna nchi hapa duniani ambayo ina uwezo na nia ya kusomesha watu wake wote mpaka elimu ya juu.

Efficiency kwenye society yoyote inategemea diversity ya watu wake. Inatakiwa kuwe na wasomi wa vyuo vikuu kama madaktari, walimu, wanasheria, wachumi nk lakini pia mafundi mchundo, makuli, wabeba box nk. ambao hawahitaji elimu ya juu ili kuweza kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Inatakiwa tutumie pesa nyingi kuongeza uwezo wa VETA, secondary schools ili wananchi wetu wawe na at least basic education inayoweza kuwafanya wafanye kazi zao kwa ufanisi.

Pia elimu nzuri ni ile inayomwandaa mwananchi kuwa tayari kupambana na mazingira yake, kwa mfano mkulima kuwa na uwezo wa kuongeza ufanisi kwenye kilimo nk.

Nchi zilizoendelea wananchi waliosoma mpaka level ya vyuo vikuu hawazidi asilimia 50. Kwa mfano UK, Labaour walitaka at least asilimia 50 ya vijana waende vyuo vikuu, ahadi hiyo imeshindwa vibaya na matokeo yake zimeanzishwa baadhi ya courses ambazo hazina maana kabisa. Baadhi ya Wanafunzi wakimaliza wanakuwa useless na bila kuwa na ujuzi wa kuweza kuwasaidia kupambana na maisha. Je tunataka elimu za namna hiyo?

Kwa Tanzania kama tutafikia 30% ya vijana wetu kufikia level ya university itakuwa hatua kubwa sana. Wanaobaki wanaweza wanaweza kugawanyika katika makundi mbalimbali kuanzia elimu ya kati mpaka wale ambao hawana formal education.

Nadhani mada hii ilifaa ijadiliwe katika management forums. Mkuu unacho kisema ni sahihi kabisa japo ni vigumu sana kuingia katika fikra za mtu wa kawaida. Nadhani linahitaji saikologia fulani kueleza jambo hili maana linachanganya raia hapa.
 
Wanachama:

Kitu cha maana hapa usiwe mjadala wa elimu ya juu. Maana elimu ya juu ni elimu ya chuo kikuu.

Kwa upande wangu ningependelea elimu ambayo itawawezesha watu kutumia vipaji vyao walivyopewa na Mungu wao.

Mpaka sasa elimu ya Tanzania imeundwa kupata university professors. Kwa maana kwamba watu hawasomi kukuza vipaji vyao bali wanashindana kupata matokeo mazuri ya kumwezesha kuendelea na daraja la juu la elimu.

Mwanafunzi wa shule ya msingi anafanya juhudi kubwa afaulu kwenda sekondari. Mwanafunzi wa sekondari anafanya juhudi kubwa hili aende high school. Na wa high school anafanya juhudi hili aende university.

Na matokeo yake tunao wahitimu wengi na wengine wana Phd, lakini hawana PASSION na vile wanavyofanya.

Watanzania tungekuwa tunasoma kwa passion na kuacha kushindana, naamini tungeweza kugundua thamani ya elimu. Kwa mfano elimu ya kidato cha sita, ni elimu ya mwaka wa kwanza wa chuo kikuu. Na kwa nchi nyingine ni elimu ya mwaka wa kwanza na wa pili ya chuo kikuu.

Lakini mpaka sasa wanafunzi wengi wa kidato cha sita, wasipopewa mafunzo fulani, wanakuwa useless kabisa.

Kwa maoni yangu, ni lazima tubadili mwelekeo. Tusiendelee kulalamikia elimu kuwa ndio chanzo cha kuwa na maendeleo finyu. Idadi ya watanzania waliosoma sio kubwa lakini inatosha kuwa chachu ya maendeleo thabiti. Ni ufanisi wa wasomi wetu wachache katika sekta walizokuwepo utakaofanya expansion wa elimu ya juu kwa sehemu kubwa ya wananchi kuwa na maana.

Hata nchi zilizoendelea zilikuwa na wasomi wachache miaka ya nyuma. Lakini ni mfanikio ya wasomi hao wachache yaliofanya nchi hizo kuendeleza elimu ya juu. Kwa mfano 1975 ni 10% ya waingereza walikuwa na elimu ya chuo kikuu. Na sasa hivi imezidi 40%.

Hivyo kuna uwezekano mkubwa kuwa wakati wanakuja kututawala asilimia ya wenye elimu ya chuo kikuu ilikuwa sawa na ya kwetu.
 
Tofautisha bure na lazima, hata huko Norske, Sverige na Deutschland usijidanganye kwamba elimu inatolewa "bure". Inawezekana kukawa hamna "tuition fee" lakini wananchi wao wanalipa kwa namna nyingine, kama vile kwa kukatwa kodi kubwa.

Sisi unemployment / underemployment iko rampant, kwa hiyo hata uzalishaji hatuna, kodi hatulipi, halafu na elimu ya bure tunataka hapo hapo.

Serikali ikituambia ukweli kwamba elimu ya juu si lazima, na serikali haina uwezo wa kutusomesha wote, tunaona kama tumetukanwa.

Mimi kawaida niko mbali kabisa na kuitetea serikali, lakini wananchi tunapobweteka katika fikra za katikati ya karne iliyopita inakera na ni lazima niseme.

Bure kwa maana kuwa hawalipi tuition fees. Hilo la kodi ni usanii. Wangeweza kutoza kodi kubwa na kulipisha elimu. Swali liloulizwa ni nchi gani iliyoendelea ambako wananchi wake wanasoma bure. Jibu umepewa.
 
Hebu acheni mzaha, Phillipenes nchi ndogo kama kisiwa cha pemba inawanafunzi vyuo vikuu millioni mbili, inamaana wao wanahitaji zaidi elimu hii kuliko watz!
 
William Kamkwamba: How I built my family a windmill

William Kamkwamba on building a windmill | Video on TED.com

katoma,

.....mshikaji...yaani nimefurahishwa sana sana na kijana William.....inshort this is what we are talking about....kuna vitu ambavyo basic kabisa tunaweza kufanya.....kama ni support ni ndogo sana.......nina imani ndugu zangu wa maeneo ya Same.....wanaweza kufaidika na elimu hiyo........

Kudos....William......huyu kijana yuko wapi sasa hivi....hawa ndio inabidi kuwapiga tafu kweli kweli...........
 
Last edited:
Bure kwa maana kuwa hawalipi tuition fees. Hilo la kodi ni usanii. Wangeweza kutoza kodi kubwa na kulipisha elimu. Swali liloulizwa ni nchi gani iliyoendelea ambako wananchi wake wanasoma bure. Jibu umepewa.

Fundi Mchundo, heshima zako mkuu, niliuliza hilo swali. Wenzangu, Mtanzania na Sikonge wamejibu, na ningejibu kama walivyojibu wao. Jibu lako halikuwa sahihi kwa sababu hakuna elimu ya juu BURE duniani. You dismissed high taxation as a way of paying for that higher education, but you are wrong. Unafikiri kutozwa kodi ya juu for your entire life ni mchezo? How many percent of Tanzanians pay taxes legally? Ni sisi wajinga wachache ambao ni about 10% of the population if not less. I am tired of the fact that 80% of the population want a free lunch with OUR TAXES!!!! I am sorry, very sorry but we have worked hard and continue to work hard and do not even see profit of our companies! We have families that derive their living from our companies, and we contribute more than we should in taxes. And then we have people lining up saying that higher education is a right! No way! It is a priviledge! We want our taxes reduced so our children can live comfortably.
I am not a socialist and never was! I would reform loan system in banks etc, if you are poor and you want to study in university or college,take a loan and spend your life paying it back. It is time to free up the potential of this country instead of tying us down with taxes and utopian plans of freebies for everyone!
Sorry for the outburst, but I am tired of watanzania kudanganyana eti free higher learning is a right!
FYI Eddy huko Philippines mi napaelewa vizuri nina family connection, and higher learning is not for FREE!! Kuna wanafunzi wengi vyuoni na hii inatokana na wazazi kuwa tayari ku-sacrifice watoto wao wasome! let's get our facts right!
 
Norway, Sweden hizi ni mfano wa nchi ambazo zimendelea, na elimu ya juu ni bure, ni nao ushahidi, kuna marafiki zangu ambao ni watanzania wansoma huko na wanasema elimu huko ni bure


...huko tax ni zaidi ya 50%...mko tayari kuipa serikali zaidi ya nusu ya income zenu?
 
...huko tax ni zaidi ya 50%...mko tayari kuipa serikali zaidi ya nusu ya income zenu?

Count me out, Koba!!! Most people wanaotetea elimu ya juu ya bure na kutumia example ya Sweden, have no idea what it entails, they just want freebies. You have to work hard (everybody!!!) to achieve what Sweden achieved, and make sacrifices. but then kila mtu alipe kodi, si mtu anasema ooo! Mi mwuza mitumba silipi kodi! Everyone!!
 
Hebu acheni mzaha, Phillipenes nchi ndogo kama kisiwa cha pemba inawanafunzi vyuo vikuu millioni mbili, inamaana wao wanahitaji zaidi elimu hii kuliko watz!

Philipines yenye polulation zaidi 90 mil. na GDP zaidi ya $ 320 Billion utailinganishaje na Pemba? (au hata TZ?) Vitu viwili tofauti ..
 
Philipines yenye polulation zaidi 90 mil. na GDP zaidi ya $ 320 Billion utailinganishaje na Pemba? (au hata TZ?) Vitu viwili tofauti ..

Cynic, mkuu mi nakwambia watu wanapenda kurusha tu mifano, bila kuangalia backgruond na mazingira na historia!
 
Hebu acheni mzaha, Phillipenes nchi ndogo kama kisiwa cha pemba inawanafunzi vyuo vikuu millioni mbili, inamaana wao wanahitaji zaidi elimu hii kuliko watz!

Eddy,

Data zako zimekaa ,kiupande upande kweli kweli. Angalia facts kuhusu Philippines hapa chini, wako karibu mara tatu ya Watanzania:

88.57 million Filipinos in 2007

Final results of the latest Census of Population (POPCEN 2007) conducted by the National Statistics Office (NSO) placed the Philippine population at 88,574,614 persons as of August 1, 2007. Said results down to barangay level were made official with the signing by President Gloria Macapagal-Arroyo of Proclamation No. 1489 on April 16, 2008.
 
Tafadhali nipatie chanzo cha hari yiyo ili niweze kuchangia.......

Ninavyofahamu mimi, lengo la kwanza kabisa la vyuo vya elimu ya juu hapa nchini ni kutoa wataalamu mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa taifa kwani si kila mtanzania anaweza kumudu kusoma vyuo vya gharama ya juu nje ya nchi. Suala linalobaki sasa ni jinsi elimu hiyo inavyotolewa na vyuo hivi nchini: Aidha kama ni bure au kwa watanzania kuchangia.

Tafadhali naomba chanzo cha habari hii. Kama NW-Elimu ametoa kauli hiyo, basi inatia shaka kwa uwezo wa baadhi ya viongozi hapa nchini.
 
Back
Top Bottom