Elimu ya Bongo na ya Nje Ipi Bora?

Tebajanga

Member
Sep 14, 2011
68
102
Jamani Hivi Elimu inayotolewa humu nchini kwetu na hiyo ya nje ipi ni bora?
Nchi za nje hasa sa bara la marekani, ulaya na aisia, mbali na africa!
 
nje unamanisha wapi

east africa,south africa,algeria,marekani,ulaya,india,china,malaysia?
 
Inategemea na mahitaji yako. Elimu ni dhana pana sana. Wapo wanaotoka huko nje kuja humu ndani kusoma.
 
Jamani Hivi Elimu inayotolewa humu nchini kwetu na hiyo ya nje ipi ni bora?

Njia rahisi ukitaka kupima kama elimu yetu ni bora angalia vitu vifuatavyo then utoe majibu wewe mwenyewe.
1. Je tuna waalimu wenye ubora unaotakiwa au bora waalimu?
2. Nyenzo na zana kujifunzia, je zina ubora unaotakiwa?
3. Majengo (madarasa, maabara) je yako katika ubora unaokubalika kimataifa
4. Uwiano baina ya waalimu na wanafunzi ni sahihii kulingana na viwango vinavyotakiwa?
5. Vipi uwepo wa vitabu vya rejea na kiada, vipo vya kutosha au longolongo kibao?
6. Hizo shule au vyuo vinawezeshwa kifedha vya kutosha kuweza kuhimili mikiki ya kuendesha shughuli za kujifunza na ufundishaji?
7. Uongozi wa shule au chuo ukoje? Je ni wababaishaji au wanaendesha shule kitaalamu (professionalism)
8. Technolojia inayotumika hapo chuoni, je ni ya mwaka 47 au ile inayoendana na wakati tuliopo?

Nadhani kwa vigezo hivyo ntakuwa nimekusaidia kujua kama kweli elimu ya nchi yetu ni bora au iko chini ukilinganisha na nchi nyingine iwe ndani ya afrika au nje ya bara la Afrika. Japo kwa haraka haraka tu vyuo vya wenzetu na haswa Ulaya na Marekani ya kaskazini wamejitahidi sana kwenye maeneo mengi!

Wengine wanaweza ongezea!
 
Inategemea na nje ni nchi gan..bt me m2 aliyesoma india na malaysia haniwezi kwa lolote na elimu yangu ya kibongo bongo..flag natoa kwa graduates frm USA,UK na canada.
 
Inategemea na nje ni nchi gan..bt me m2 aliyesoma india na malaysia haniwezi kwa lolote na elimu yangu ya kibongo bongo..flag natoa kwa graduates frm USA,UK na canada.

sema kaka nawdeiz india wako vizuri sana esp kwny technology na udaktari in most universities overthere
 
Kubishana elimu dunia ipi ni bora kati ya Tanzania na Ulaya au Australia au Amerika Kaskazini ni kupoteza muda bila faida yoyote.Labda mjilinganishe na vinchi vingine huko kama Somalia,Burundi,Congo,Eritrea etc na hata hao wahindi na Malaysia mnaowabeza wako vizuri sana kuliko nyie mnaotegemea madesa kufaulu mitihani.
 
Inategemea na kitu unachotaka kusomea, lakini kwa current status ya nchi yetu in general ni bora kusoma nje sababu elimu yao inaonekana kuwa bora kuliko elimu ya hapa kwetu ingawa hapa kwetu kuna baadhi ya taasisi zinatoa elimu safi.
 
Labda uniambia nn tofauti ya m2 mwenye cheti cha shahada ya kwanza cha nje ya nchi na cha bongo
 
Bongo porojo nyingi sana .Siasa kwenye elimu ndio inapelekea Elimu kushuka ubora kila kukicha.Hao wanaosema India ,China, Malaysia sijui kama mnatakwimu sahihi.Tanzania chuo kinachoongoza kwa Ubora ni UDSM ambapo Kwa East Africa ni chuo cha 3 kwa ubora baada ya Makerere na University of Nairobi.UDSM kwa africa ni chuo cha 38 ambapo Hakuna chuo kingine cha Tanzania kwenye 100 bora za vyuo vya Africa.Kwa dunia nzima UDSM ni chuo cha 3,438 kwa ubora.
Sasa sizani kama kuna mikakatii madhubuti ya kuboresha Elimu ,Ndio maana wengi wanaosoma vyuo vya nje(Haswa kwa vyuo vya Malaysia,China,Japan,nd Korea , Indonesia,Philipines and Russia ) wakirudi wanakuwa na uwezo (wamepanuka kimawazo/fikra ) hii ni kutokana wengi wanaoenda kusoma vyuo vya katika nchi hizo wanapata Scholarship na wanakwenda kusoma kwenye vyuo vyenye ubora .
Sasa turudi huko UK ,watanzania wengi wanaenda kusoma vyuoka kama Mwana FA alisoma chuo kinaitwa Coventry ambacho ni chuo cha 1,713 kwa ubora duniani ( Kuna vyuo Africa vinakizidi kwa Ubora hata East africa-Makerere ni cha 1,256 duniani ),vyuo vingine ni kama London Business School 1,524 na University of London -1,683.Ukilinganisha ni kwamba Watanzania wanaoenda Asia wanasoma vyuo bora kuliko wanaoenda UK ambako kusoma kwenye vyuo vyenye ubora wa juu zaidi kwa UK ni gharama kubwa hata qualification zinazohitajika ni za juu kwa baadhi.Wengi hawawezi kwa sababu wanakuwa wanajilipia wenyewe ama wazazi wao.
Wapo watanzania wachache sana wanaosoma/waliosoma kwenye vyuo vilivyopo kwenye 100 USA na kwingineko ,ila kwa miaka mingi watanzania wengi wanasoma vyuo vya UK,Russia na Asia kwa wingi ukilinganisha na USA na kwingineko.Bila kusahau Kenya na Uganda wapo wengi pia.

Rank ya vyuo bora kwa Tanzania
Jina nafasi kwa dunia
1.UDSM 3,438
2.SUA 8,427
3.Hubert Kairuki Memorial University 8,819
4.Open University of Tanzania 9,335
5.Mzumbe University 10,107
6.Muhimbili University College of Health Sciences 11,191
source
Ranking Web of World universities: Top Africa
 
bongo tnababaisha tu tatizo vitendea kazi hakuna..................unaingia libraly ya chuo iko empty ka hall tupu
 
Sio kweli kwamba chuo kikuu bora kwa Tanzania ni UDSM, Kwani ubora wa chuo huwa unategemea zao linalotolewa na hiyo RANK uliyoitoa ulifocus kwenye nini? je ubora wa elimu? umri wa chuo? mazingira ya chuo? au umetumia vigezo gani? msipende kusikiliza mawzo ya wanasiasa kwenye swala la elimu hapa kwenye taifa letu.
MBONA MAFISADI WENGI WAMESOMA UDSM??????? SASA JE UBORA WA HICHO CHUO NI NINI????
Kwa upande wangu mimi naona chuo kikuu bora hapa ketu ni SUA, na kwa upande wa elimu ya nje na ya ndani huwa mimi naona elimu ya ndani ya taifa lako huwa ni bora sana kwa kianzio (graduates) kwani wapo watu ambao wamesoma vyuo vya nje ambavyo hata TCU bado haivitambui.
 
Sio kweli kwamba chuo kikuu bora kwa Tanzania ni UDSM, Kwani ubora wa chuo huwa unategemea zao linalotolewa na hiyo RANK uliyoitoa ulifocus kwenye nini? je ubora wa elimu? umri wa chuo? mazingira ya chuo? au umetumia vigezo gani? msipende kusikiliza mawzo ya wanasiasa kwenye swala la elimu hapa kwenye taifa letu.<br />
MBONA MAFISADI WENGI WAMESOMA UDSM??????? SASA JE UBORA WA HICHO CHUO NI NINI???? <br />
Kwa upande wangu mimi naona chuo kikuu bora hapa ketu ni SUA, na kwa upande wa elimu ya nje na ya ndani huwa mimi naona elimu ya ndani ya taifa lako huwa ni bora sana kwa kianzio (graduates) kwani wapo watu ambao wamesoma vyuo vya nje ambavyo hata TCU bado haivitambui.
<br />
<br />
waaaaaaaaat,SUA????
 
Sio kweli kwamba chuo kikuu bora kwa Tanzania ni UDSM, Kwani ubora wa chuo huwa unategemea zao linalotolewa na hiyo RANK uliyoitoa ulifocus kwenye nini? je ubora wa elimu? umri wa chuo? mazingira ya chuo? au umetumia vigezo gani? msipende kusikiliza mawzo ya wanasiasa kwenye swala la elimu hapa kwenye taifa letu.
MBONA MAFISADI WENGI WAMESOMA UDSM??????? SASA JE UBORA WA HICHO CHUO NI NINI????
Kwa upande wangu mimi naona chuo kikuu bora hapa ketu ni SUA, na kwa upande wa elimu ya nje na ya ndani huwa mimi naona elimu ya ndani ya taifa lako huwa ni bora sana kwa kianzio (graduates) kwani wapo watu ambao wamesoma vyuo vya nje ambavyo hata TCU bado haivitambui.

ivi kumbe TCU ina jukumu la kutambua hadi vyuo vya nje?? na hao SUA wamefanya kipi kipya ukizingatia kilimo ndo kinazidi kudorora, hapa bongo serikali kila siku iko kwenye mchakato mara ooh tuko mbioni mara ooh 2meunda kamati lakini ndo ivo nchi iko gizani na kuna waatalam kibao lakini hawapewi nafasi
 
Mkuu kabla sijatoa suggestion zangu kwanza nijue wewe unacompare elimu ya bongo na ya nje katika level ipi? Chekechea, msingi, O level, A Level, Undergraduate, Postgraduate au PHD level? be specific mzee.....
 
Mkuu kabla sijatoa suggestion zangu kwanza nijue wewe unacompare elimu ya bongo na ya nje katika level ipi? Chekechea, msingi, O level, A Level, Undergraduate, Postgraduate au PHD level? be specific mzee.....
<br />
<br />
level zote.
 
Back
Top Bottom