Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,297
- 18,896
Post zangu kwenye thread hii zitakuwa ni ndefu kidogo kwa kina kuliko nilvyozowea kuandika. Mara kwa mara zitakuwa zinaambatana na video za Youtube kusupport maneno yangu. Zisome ukizingatia hali hiyo.
Muziki ni mtiririko wa sauti zilizopangwa kwa urefu wa muda tofauti tofauti ili kutuma ujumbe fulani wa kisaikolojia na kifiziolojia kwenye mwili wa msikilizaji. Inaaminika kuwa mawasiliano ya kwanza ambayo binadamu huzaliwa nayo ni muziki. Watoto wanapozaliwa hujua miziki miwili tu: kulia na kucheka
Ingawa vicheko vya watoto vina ujumbe mmoja tu kuwa nimefurahi, vilio vyao huwa vinatuma jumbe mbalimbali, akina mama wazazi wao huzeielewa jumbe hizo haraka sana. Kuna jumbe za kusema nimechoka, kuna jumbe za kusema sikutaki, na kadhalika, kama inavyoelezwa hapa
Nimeanzisha thread hii ili kujadiliana utaalamu wa muziki kwa kutumia Kiswahili rahisi. Binafsi nitaitumia kwanza kuelezea nadharia ya muziki kadri ninavyoielewa ambayo nina imani kuwa kuna wanaoifahamu vizuri zaidi na wasioifahamu kabisa. Ninataka kulenga wale wasioifahamu, hasa vijana chini ya miaka 30.
Baada ya kupitia nadhania hiyo, nitaiunganisha na tungo mbalimbali zilziowahi kutokea na kuzichambua kelezea kwa nini tungo fulani za muziki hupendwa na wasikilizaji kwa muda mrefu sana na nyingine huingia sokoni na kutoweka kama vile hazikuwahi kuwepo.
Karibuni
Muziki ni mtiririko wa sauti zilizopangwa kwa urefu wa muda tofauti tofauti ili kutuma ujumbe fulani wa kisaikolojia na kifiziolojia kwenye mwili wa msikilizaji. Inaaminika kuwa mawasiliano ya kwanza ambayo binadamu huzaliwa nayo ni muziki. Watoto wanapozaliwa hujua miziki miwili tu: kulia na kucheka
Ingawa vicheko vya watoto vina ujumbe mmoja tu kuwa nimefurahi, vilio vyao huwa vinatuma jumbe mbalimbali, akina mama wazazi wao huzeielewa jumbe hizo haraka sana. Kuna jumbe za kusema nimechoka, kuna jumbe za kusema sikutaki, na kadhalika, kama inavyoelezwa hapa
Nimeanzisha thread hii ili kujadiliana utaalamu wa muziki kwa kutumia Kiswahili rahisi. Binafsi nitaitumia kwanza kuelezea nadharia ya muziki kadri ninavyoielewa ambayo nina imani kuwa kuna wanaoifahamu vizuri zaidi na wasioifahamu kabisa. Ninataka kulenga wale wasioifahamu, hasa vijana chini ya miaka 30.
Baada ya kupitia nadhania hiyo, nitaiunganisha na tungo mbalimbali zilziowahi kutokea na kuzichambua kelezea kwa nini tungo fulani za muziki hupendwa na wasikilizaji kwa muda mrefu sana na nyingine huingia sokoni na kutoweka kama vile hazikuwahi kuwepo.
Karibuni