elimu na bei

mrlonely98

Member
Nov 6, 2009
94
6
Asalaam jamani kuna swali nataka niulize tunasikia kwamba zipo shule nyingi za private ambazo zinapandisha bei ya elimu kila mwaka je nini kinafanyika kuzuiahili itafika wakati hatutaweza kubeleka watoto wetu kupata elimu bora
 
Asalaam jamani kuna swali nataka niulize tunasikia kwamba zipo shule nyingi za private ambazo zinapandisha bei ya elimu kila mwaka je nini kinafanyika kuzuiahili itafika wakati hatutaweza kubeleka watoto wetu kupata elimu bora

Kinachotakiwa kufanyika, Ni Wazazi kuishinikiza Wizara ya Elimu ili kuhakikisha fees katika shule hizo zisiwe zinapanda kiholela na pia kila shule inapotaka kupandisha fee yake itume maombi wizara ya Elimu na kutoa sababu zake zilizoifanya shule hiyo/hizo ziombe kuongeza fees.

Kuwe na kamati pale Wizarani ambayo itayapitia maombi hayo ya kupandisha fees na kama haikuridhika na sababu za kupandisha fees basi shule zisiruhusiwe kupandisha kiholela fees hizo.
 
Kwa ufahamu wangu hizi shule zimekuwa na kamaati inayoitwa kamati ya wazazi, nasema inasemekana kwa kuwa sijui hata zinachaguliwaje. NImekuwa mteja wa hizi shule kwa kitambo sasa, kila siku utasikia kamati ya wazazi imeamua tupandishe kiasi fulani ili kufidia gharama za uendesahaji. Hizo gharama ni kiasi gani utajulishwa, na zimefikaje huko pia hutajulishwa. Kasoro kubwa ni wizara ya elimu, kuna kitengo maalum kinachoshughulika na hizi shule, kanafanya nini hata haijulikani. Maana hizi shule ziko huru sana kufanya zinazotaka, kana wakati moja ya shule hizi ilituahidi kama serikali ikiwapunguzia kodi nao watashusha bei. Cha kushangaza ndio ikapandisha hata baada ya serikali kushusha kodi, na hakuna aliyewauliza kulikoni.
 
Kwa ufahamu wangu hizi shule zimekuwa na kamaati inayoitwa kamati ya wazazi, nasema inasemekana kwa kuwa sijui hata zinachaguliwaje. NImekuwa mteja wa hizi shule kwa kitambo sasa, kila siku utasikia kamati ya wazazi imeamua tupandishe kiasi fulani ili kufidia gharama za uendesahaji. Hizo gharama ni kiasi gani utajulishwa, na zimefikaje huko pia hutajulishwa. Kasoro kubwa ni wizara ya elimu, kuna kitengo maalum kinachoshughulika na hizi shule, kanafanya nini hata haijulikani. Maana hizi shule ziko huru sana kufanya zinazotaka, kana wakati moja ya shule hizi ilituahidi kama serikali ikiwapunguzia kodi nao watashusha bei. Cha kushangaza ndio ikapandisha hata baada ya serikali kushusha kodi, na hakuna aliyewauliza kulikoni.

Tatizo ni kwamba Wizara husika imelala usingizi mzito na kuacha mambo yakiendeshwa kienyeji bila hata kutathmini kwamba upandishaji wa fees unastahili kutokana na sababu zilizotolewa na kamati za wazazi kwa kushirikiana na uongozi wa shule.

Ingeweza kuwekwa hata percentage fulani kwamba fees zisipandishwe zaidi ya asilimia 3 au 5 kwa mwaka na wafanye hivyo baada ya kutoa sababu za kuridhisha zitakazokubalika na Wizara ya Elimu, lakini imekuwa ni bora liende tu kila mwaka mpya ukiingia wanapandisha fees wakati mishahara ya wazazi wengi haikuongezeka. Ndiyo nchi yetu hiyo mambo shakalabaghala!
 
Editvitabu.jpg
 
Kuwepo na sera ya kukagua mahesabu ya shule hizi.
Kwakua anaeanzisha shule analenga kupata faida basi hiyo faida iwe na kikomo kulingana na mtaji aliowekeza,hili litawezekana kama wizara itaamua kufuatilia hatua zote za kuanzisha shule husika.
Hii inaonekana kama ngumu lakini inawezekana.Pia Serikali inaweza kuweka kiwango cha juu cha ada pamoja na gharama zingine kwa shule hizo bila kutegemea vikao vya wazazi ambao mara nyingi ni sehemu ya wamiliki au wanaweza kurubuniwa na wenye shule kwani wahudhuriaji wa vikao hivyo ni wachache.
NB. Kiwango cha juu cha ada kinawekwa kwa kuchukua shule ambayo ina viwango bora kwa kila kitu ikiwepo maabara nzuri,maktaba kubwa pamoja na sifa za juu zitakazo wekwa na wizara ya elimu iliyo makini.
 
Tatizo ni kwamba Wizara husika imelala usingizi mzito na kuacha mambo yakiendeshwa kienyeji bila hata kutathmini kwamba upandishaji wa fees unastahili kutokana na sababu zilizotolewa na kamati za wazazi kwa kushirikiana na uongozi wa shule.

Ingeweza kuwekwa hata percentage fulani kwamba fees zisipandishwe zaidi ya asilimia 3 au 5 kwa mwaka na wafanye hivyo baada ya kutoa sababu za kuridhisha zitakazokubalika na Wizara ya Elimu, lakini imekuwa ni bora liende tu kila mwaka mpya ukiingia wanapandisha fees wakati mishahara ya wazazi wengi haikuongezeka. Ndiyo nchi yetu hiyo mambo shakalabaghala!

Hizo asilimia ziendane na gharama halisi za upandaji wa gharama za maisha/vitu.
 
Unakuta mtu kaanzisha shule kama mradi/kuwekeza lakini anaanza na madarasa mawili na kila mwanafunzi anayejiunga hapo anaambiwa atoe fedha ya tahadhari na ya majengo!?
Hii inakuaje wakati wewe umewekeza na unatakiwa uchukue tahadhari mwenyewe bila kumhusisha mwanafunzi? Pia kama shule itakumbwa na matatizo kama ya kuungua,wanafunzi hukosa masomo ilhali alitoa pesa ya tahadhari? Kama alitoa pesa ya tahadhari'inatakiwa likitokea tatizo kama hilo na wanafunzi kushindwa kusoma hapo kwa muda,mmiliki awatafutie shule kwa muda kwa kutumia pesa hiyo ya tahadhari!!
 
Asalaam jamani kuna swali nataka niulize tunasikia kwamba zipo shule nyingi za private ambazo zinapandisha bei ya elimu kila mwaka je nini kinafanyika kuzuiahili itafika wakati hatutaweza kubeleka watoto wetu kupata elimu bora

Elimu bora na bei poa? Hivi vitu haviendi sambamba. Ili elimu izidi kuwa bora bei inabidi zipande kufidia vifaa, walimu na mazingira bora. Cha muhimu hapa ni kuwa na choice.
 
Inakuwa vigumu kiasi kwa wizara kudhibiti hili kwa sababu kadhaa:
1. Once wizara imeshindwa kuboresha shule ambazo kikweli yenyewe inahusika na kwenda kuanza kushughulika na shule za binafsi itaonekana kwamba is unfair kwa kuwa kwa waliowengi private schools sio the only choice you can opt otherwise.
2. No one cares about education system ya nchi hii kwa sababu mtu akishaukwaa uwaziri anachofanya ni kwenda kumsomesha mtoto wake nje ya nchi, hivyo kuangalia nini kinaendelea ndani ya nchi kuhusu elimu hakuna anayejali.
Hivyo kuhusu suala la elimu tumeachiwa wazazi tuamue au kwa lugha rahisi ni: Kila mtu atauchukua mzigo wake mwenyewe siku hiyo ikifika.
Tanzania yenye elimu bora inawezekana kama wakuu wa nchi nao watoto wao watasoma kwenye shule za kata.
 
Asalaam jamani kuna swali nataka niulize tunasikia kwamba zipo shule nyingi za private ambazo zinapandisha bei ya elimu kila mwaka je nini kinafanyika kuzuiahili itafika wakati hatutaweza kubeleka watoto wetu kupata elimu bora

kwengine hapagusiki. :p

International School of Tanganyika, IST

Fee Schedule 2009/2010

Early education USD 10300
Kindergarten USD 11900
Grade 6-8 USD 14600
Grade 9-10 USD 15700
Grade 11-12 USD 20000

http://www.istafrica.com/downloads/admission09-10/Fees Schedule & guidelines SY 2009-10.pdf
 
Elimu bora na bei poa? Hivi vitu haviendi sambamba. Ili elimu izidi kuwa bora bei inabidi zipande kufidia vifaa, walimu na mazingira bora. Cha muhimu hapa ni kuwa na choice.
sina uhakika kama una mtoto unaemsomesha kwa ada ya uhalali, vinginevyo ya kifisadi, au umetuma post hii ukiwa umechoka kutokana na kazi yako ya ukuli
 
Back
Top Bottom