Bonheur Travels Tanzania
JF-Expert Member
- Dec 29, 2020
- 252
- 499
Ndugu WanaJF,
Tunaendelea na 'misheni' yetu ya kutoa elimu kwa umma hapa JamiiForums kuhusiana na masuala mbalimbali ya safari za ndege, utalii na mambo yanayoshabihiana na hayo.
Kupitia thread hii, utajifunza faida zipatikanazo wakati unasafiri na namna ya kufanya #UtaliiNaKitabu hasa katika kipindi hiki cha sintofahamu ya janga la corona.
Tutakuwa LIVE hapa JF kukuletea updates za uchambuzi wa kitabu cha riwaya ya malezi kiitwacho #LoveBombs kilichotungwa na Mwalimu Richard Mabala (maarufu Mabala The Farmer).
Uchambuzi huu utarushwa MUBASHARA pia kupitia televisheni ya ITV kesho Jumamosi tarehe 20 Februari 2021. Muda ni kuanzia saa 3 asubuhi.
Tunashirikina na Mwalimu Mabala kukuletea uchambuzi huu kupitia kampeni yetu ya #SafiriNaKitabu tutakayoitangaza rasmi hivi karibuni!
Endelea kuwa nasi..
----
UPDATES:
Muda wowote kutoka sasa tutakuletea mahojiano ya moja kwa moja kutoka studio za ITV/Mikocheni, ambapo Mwalimu Richard Mabala kupitia kipindi cha Watoto Wetu, atatoa elimu ya malezi inayopatikana kwenye kitabu chake cha #LoveBombs.
Ikumbukwe kuwa hii ni sehemu ya mfululizo wa dhamira yetu ya kutoa Elimu kwa Umma juu ya Usafiri wa Anga, Utalii, Safari na mengineyo kuelekea katika uzinduzi wa programu ya #SafiriNaKitabu #TaliiNaKitabu #KitabuNiZawadi ambayo tutawashirikisha rasmi hivi karibuni.
Kama upo karibu na TV basi wakati ndio huu, unaweza kuweka ITV kufuatilia moja kwa moja yanayoendelea studio au endelea kuungana nasi kwenye uzi huu tutakuletea moja kwa moja yanayojiri..
Video: Mahojiano ITV na Mwandishi Mabala
-----
UPDATES:
Swali: Karibu sana katika studio za ITV ndugu Richard Mabala. Unaweza kutueleza historia ya hii kazi yako japo kwa ufupi na sasa hivi unafanya nini?
Mabala: Kwa sasa mimi ni mstaafu.. Miaka mingi nilikuwa nimejikita zaidi kwenye kutoa mafunzo kwa vijana hasa kuhusu ujinsia na kujitambua.. Ninachofanya kwa sasa ni kuendelea na kazi ninayoipenda ya kuandika vitabu.
Mabala: Safari yangu ya uandishi wa vitabu ilianzia kwenye utunzi wa mashairi. Namkumbuka mwandishi anaitwa Kajube. Alikuwa mwandishi mzuri sana wa mashairi (siku hizi ameacha). Miongoni mwa vitabu vyangu maarufu ambavyo naye yumo ni "Summons". Watu walikuwa wakinisifia kuandika story nzuri za Afrika.
Baadae nikaja kuingia kwenye riwaya.
Pia niliwahi kupitia kitabu cha Three Suitors One Husband mpaka baadhi ya watu wakadhani mimi ndiye mwandishi.
Mabala: Vitabu vya Hawa the bus driver na Mabala the farmer sikutaka viingie kwenye kufanyiwa mitihani. Nilitaka tu kuandika watu wasome wafurahi na wajifunze.
Mabala: Baada ya vitabu hivyo kufanya vizuri baadae nikaona niingie kwenye uandishi wa vitabu vya watoto, Niliandika vitabu vingi kikiwemo cha kitabu cha Hadithi ya Sara, Kurwa na Doto na vingine.
Mabala: Mwanafunzi wangu mmoja aliwahi kuniambia, mwalimu mimi napenda sana kitabu cha Mabala the farmer, lakini kwanini usituandikie na riwaya badala ya kusoma za waandishi kutoka Nigeria, Ghana na Kenya? Ndipo nikaanza hayo mawazo ya uandishi wa riwaya..
Kitabu cha riwaya ambacho nimekiandika na kukichapisha tayari ni hiki cha Love Bombs.
Mabala: Wazo la Love Bombs nililipata baada ya kuona kuna mtoto kila mara alikuwa na tabia ya kumwambia mama yake; kwanini kila kitu mpaka tugombane? Huyu hakuwa mwanangu lakini nilipata kitu cha kuandika kupitia mgogoro huo.
(Endelea kusoma zaidi kwenye post zinazofuata)..
Tunaendelea na 'misheni' yetu ya kutoa elimu kwa umma hapa JamiiForums kuhusiana na masuala mbalimbali ya safari za ndege, utalii na mambo yanayoshabihiana na hayo.
Kupitia thread hii, utajifunza faida zipatikanazo wakati unasafiri na namna ya kufanya #UtaliiNaKitabu hasa katika kipindi hiki cha sintofahamu ya janga la corona.
Tutakuwa LIVE hapa JF kukuletea updates za uchambuzi wa kitabu cha riwaya ya malezi kiitwacho #LoveBombs kilichotungwa na Mwalimu Richard Mabala (maarufu Mabala The Farmer).
Uchambuzi huu utarushwa MUBASHARA pia kupitia televisheni ya ITV kesho Jumamosi tarehe 20 Februari 2021. Muda ni kuanzia saa 3 asubuhi.
Tunashirikina na Mwalimu Mabala kukuletea uchambuzi huu kupitia kampeni yetu ya #SafiriNaKitabu tutakayoitangaza rasmi hivi karibuni!
Endelea kuwa nasi..
----
UPDATES:
Muda wowote kutoka sasa tutakuletea mahojiano ya moja kwa moja kutoka studio za ITV/Mikocheni, ambapo Mwalimu Richard Mabala kupitia kipindi cha Watoto Wetu, atatoa elimu ya malezi inayopatikana kwenye kitabu chake cha #LoveBombs.
Ikumbukwe kuwa hii ni sehemu ya mfululizo wa dhamira yetu ya kutoa Elimu kwa Umma juu ya Usafiri wa Anga, Utalii, Safari na mengineyo kuelekea katika uzinduzi wa programu ya #SafiriNaKitabu #TaliiNaKitabu #KitabuNiZawadi ambayo tutawashirikisha rasmi hivi karibuni.
Kama upo karibu na TV basi wakati ndio huu, unaweza kuweka ITV kufuatilia moja kwa moja yanayoendelea studio au endelea kuungana nasi kwenye uzi huu tutakuletea moja kwa moja yanayojiri..
Video: Mahojiano ITV na Mwandishi Mabala
-----
UPDATES:
Swali: Karibu sana katika studio za ITV ndugu Richard Mabala. Unaweza kutueleza historia ya hii kazi yako japo kwa ufupi na sasa hivi unafanya nini?
Mabala: Kwa sasa mimi ni mstaafu.. Miaka mingi nilikuwa nimejikita zaidi kwenye kutoa mafunzo kwa vijana hasa kuhusu ujinsia na kujitambua.. Ninachofanya kwa sasa ni kuendelea na kazi ninayoipenda ya kuandika vitabu.
Mabala: Safari yangu ya uandishi wa vitabu ilianzia kwenye utunzi wa mashairi. Namkumbuka mwandishi anaitwa Kajube. Alikuwa mwandishi mzuri sana wa mashairi (siku hizi ameacha). Miongoni mwa vitabu vyangu maarufu ambavyo naye yumo ni "Summons". Watu walikuwa wakinisifia kuandika story nzuri za Afrika.
Baadae nikaja kuingia kwenye riwaya.
Pia niliwahi kupitia kitabu cha Three Suitors One Husband mpaka baadhi ya watu wakadhani mimi ndiye mwandishi.
Mabala: Vitabu vya Hawa the bus driver na Mabala the farmer sikutaka viingie kwenye kufanyiwa mitihani. Nilitaka tu kuandika watu wasome wafurahi na wajifunze.
Mabala: Baada ya vitabu hivyo kufanya vizuri baadae nikaona niingie kwenye uandishi wa vitabu vya watoto, Niliandika vitabu vingi kikiwemo cha kitabu cha Hadithi ya Sara, Kurwa na Doto na vingine.
Mabala: Mwanafunzi wangu mmoja aliwahi kuniambia, mwalimu mimi napenda sana kitabu cha Mabala the farmer, lakini kwanini usituandikie na riwaya badala ya kusoma za waandishi kutoka Nigeria, Ghana na Kenya? Ndipo nikaanza hayo mawazo ya uandishi wa riwaya..
Kitabu cha riwaya ambacho nimekiandika na kukichapisha tayari ni hiki cha Love Bombs.
Mabala: Wazo la Love Bombs nililipata baada ya kuona kuna mtoto kila mara alikuwa na tabia ya kumwambia mama yake; kwanini kila kitu mpaka tugombane? Huyu hakuwa mwanangu lakini nilipata kitu cha kuandika kupitia mgogoro huo.
(Endelea kusoma zaidi kwenye post zinazofuata)..