manigum27
Member
- Mar 24, 2017
- 57
- 53
Habari wana JF. Kwa mara ya kwanza napenda kutoa Elimu juu ya Huduma ya meno Bandia ya Moja kwa moja Yasiyotoka ( Crown na Bridge).
Meno ama Jino ni kiungo Muhimu sana katika mwili wa Binadamu kama Viungo vingine hivyo ni Vyema kuyatunza na kulinda kama viungo vingine.
Faida za meno ni nyingi ingawa sitaongelea zote kwa undani
1. Husaidia Kwenye Muonekano mzuri wa Sura.
2. Husaidia katika Matamshi ya maneno (Kuongea)
3. Husaidia katika kumeng'enya Chakula.
4...........
*Crown ni nini? Crown ni sawa na Kusema Kofia hili ni Jino ambalo linatengenezwa ili kurudishia sehemu ya Jino ambalo limetoboka na hivyo crown hutumika kuvalisha baada ya kufanyia matibabu ya kusafisha na kuziba kwa Dawa Maalumu.
*Bridge ni nini? Bridge ama Daraja kwa lugha ya Wageni ni Meno ambayo hutegemea meno mengine kushika pande zote mbele na nyuma ya Jino ambalo limetoka.
ZIRCONIA (Crown and Bridge)
Ni Meno ambayo hutengenezwa Maabara kama meno Mengine Tofauti na haya ni Kuwa hayana Chuma kwa ndani
Ni Imara, Mazuri na yana Ufanano wa kiasi kikubwa na meno ya Asili.
* Wapi Unaweza Pata huduma hii?
Huduma hii utaipata kwa Daktari yeyote wa Meno ambaye mwenye Ujuzi na Uzoefu katika kazi ya meno Bandia.
Zifuatazo ni Hatua Ambazo Daktari hufuata hadi kufanikisha zoezi zima la Kuweka meno Bandia ya Moja kwa moja.
1. Hatua ya kwanza ni Daktari Atachonga jino ambalo linatakiwa kuvalishwa Crown ama Bridge Picha zinajionesha.
2. Akishamaliza kuchonga Jino husika atachukua vipimo ambapo Mgonjwa hung'ata ama huwekewa kipimo chenye Dawa maalumu ambayo huchukua Picha ya meno baada ya hapo Vipimo vitatumwa Maabara kwa ajili ya hatua za utengenezaji.
3. Maabara wakipokea Vipimo watatengeneza Mould Ya meno kwa Udongo maalumu ili kupata picha ya meno yaliyotoka na yaliyobakia.
3. Mould ya meno ikipatikana Mtengenezaji huchukua hivyo Vipimo na kuanza kuvifanyia kazi kutokana na maelekezo ya Daktari .
4. Kwa Meno ya Ziconia model ama cast huscaniwa na kubadilishwa kutoka kwenye hard copy kwenda soft copy kwa Vifaa maalumu.
5. Baada ya Kuscan model hufanyiwa design na hatua ya mwisho hutumwa kwenye milling machine ambayo itachonga hayo meno na hatua inayofuata baada Kwa meno ya Zirconia huwekwa kwenye machine ya kufanya yawe Magumu na Imara.
Tayari kwa Matumizi .
Mwisho Meno ni Lulu yalinde, Yatunze na kamwe usithubutu kufungua Soda kwa meno ni Hatari.
Sina cha ziada chini ni moja ya kazi ambazo zinafanyika hapa Kwenye Maabara kubwa Hapa Tanzania na Afrika Mashariki ambayo ipo Dar es salaam.
Tunashirikiana na Dental clinic zote za Dar es salaam na Mikoani na Nchi za Jirani.
Meno ama Jino ni kiungo Muhimu sana katika mwili wa Binadamu kama Viungo vingine hivyo ni Vyema kuyatunza na kulinda kama viungo vingine.
Faida za meno ni nyingi ingawa sitaongelea zote kwa undani
1. Husaidia Kwenye Muonekano mzuri wa Sura.
2. Husaidia katika Matamshi ya maneno (Kuongea)
3. Husaidia katika kumeng'enya Chakula.
4...........
*Crown ni nini? Crown ni sawa na Kusema Kofia hili ni Jino ambalo linatengenezwa ili kurudishia sehemu ya Jino ambalo limetoboka na hivyo crown hutumika kuvalisha baada ya kufanyia matibabu ya kusafisha na kuziba kwa Dawa Maalumu.
*Bridge ni nini? Bridge ama Daraja kwa lugha ya Wageni ni Meno ambayo hutegemea meno mengine kushika pande zote mbele na nyuma ya Jino ambalo limetoka.
ZIRCONIA (Crown and Bridge)
Ni Meno ambayo hutengenezwa Maabara kama meno Mengine Tofauti na haya ni Kuwa hayana Chuma kwa ndani
Ni Imara, Mazuri na yana Ufanano wa kiasi kikubwa na meno ya Asili.
* Wapi Unaweza Pata huduma hii?
Huduma hii utaipata kwa Daktari yeyote wa Meno ambaye mwenye Ujuzi na Uzoefu katika kazi ya meno Bandia.
Zifuatazo ni Hatua Ambazo Daktari hufuata hadi kufanikisha zoezi zima la Kuweka meno Bandia ya Moja kwa moja.
1. Hatua ya kwanza ni Daktari Atachonga jino ambalo linatakiwa kuvalishwa Crown ama Bridge Picha zinajionesha.
2. Akishamaliza kuchonga Jino husika atachukua vipimo ambapo Mgonjwa hung'ata ama huwekewa kipimo chenye Dawa maalumu ambayo huchukua Picha ya meno baada ya hapo Vipimo vitatumwa Maabara kwa ajili ya hatua za utengenezaji.
3. Maabara wakipokea Vipimo watatengeneza Mould Ya meno kwa Udongo maalumu ili kupata picha ya meno yaliyotoka na yaliyobakia.
3. Mould ya meno ikipatikana Mtengenezaji huchukua hivyo Vipimo na kuanza kuvifanyia kazi kutokana na maelekezo ya Daktari .
4. Kwa Meno ya Ziconia model ama cast huscaniwa na kubadilishwa kutoka kwenye hard copy kwenda soft copy kwa Vifaa maalumu.
5. Baada ya Kuscan model hufanyiwa design na hatua ya mwisho hutumwa kwenye milling machine ambayo itachonga hayo meno na hatua inayofuata baada Kwa meno ya Zirconia huwekwa kwenye machine ya kufanya yawe Magumu na Imara.
Tayari kwa Matumizi .
Mwisho Meno ni Lulu yalinde, Yatunze na kamwe usithubutu kufungua Soda kwa meno ni Hatari.
Sina cha ziada chini ni moja ya kazi ambazo zinafanyika hapa Kwenye Maabara kubwa Hapa Tanzania na Afrika Mashariki ambayo ipo Dar es salaam.
Tunashirikiana na Dental clinic zote za Dar es salaam na Mikoani na Nchi za Jirani.