Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,087
- 6,568
Tatizo la uhaba wa madarasa limekuwepo kwa muda mrefu na lilianza kushamiri hasa miaka ya tisini.
Ukweli ni kuwa sababu kubwa ni ongezeko la idadi ya watoto wanaotakiwa kujiunga na elimu ya msingi na sekondari kwa ujumla.
Kuleta visingizio kuwa eti awamu ya tano kuanza kutoa elimu bure ndio sababu ya ya idadi ya wanafunzi imeongezeka na hivyo kusababisha ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaotakiwa kujiunga na elimu ya sekondari na msingi ni hoja hafifu na duni kabisa.
Mwaka 2019-2020 serikali ilibainisha wazi kuwa wanafunzi wapatao 58,666 walishindwa kuendelea na masomo baada ya kukosa madarasa. Na kwa aibu kubwa ilitenga bil 29 tu ili kukabili hili tatizo. Lakini hakuna kilichotatuliwa.
Ifahamike tangu miaka ya tisini mpaka leo ni shule chache sana ambazo zina uwezo wa kusomesha wanafuzi 45 ndani ya darasa moja. Na tatizo hili lipo kwa zaidi ya miaka 40 hapa Tanzania.
Kama serikali ina nia thabiti ya kusomesha watoto wetu kwa standard zinazotakiwa kwa nini isitatue hili tatizo wakati inazo pesa?
Kwa nini isiunde kikosi kazi maalumu na kujenga madarasa yanayotosha ndani ya miezi miwili,maana darasa halihitaji gharama kubwa na ufundi mkubwa? Maana tunaambiwa kila siku pesa zipo,sasa kwa nini msitenge pesa za kutosha kumaliza kero ndogo kama hii?
Ukweli ni kuwa sababu kubwa ni ongezeko la idadi ya watoto wanaotakiwa kujiunga na elimu ya msingi na sekondari kwa ujumla.
Kuleta visingizio kuwa eti awamu ya tano kuanza kutoa elimu bure ndio sababu ya ya idadi ya wanafunzi imeongezeka na hivyo kusababisha ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaotakiwa kujiunga na elimu ya sekondari na msingi ni hoja hafifu na duni kabisa.
Mwaka 2019-2020 serikali ilibainisha wazi kuwa wanafunzi wapatao 58,666 walishindwa kuendelea na masomo baada ya kukosa madarasa. Na kwa aibu kubwa ilitenga bil 29 tu ili kukabili hili tatizo. Lakini hakuna kilichotatuliwa.
Ifahamike tangu miaka ya tisini mpaka leo ni shule chache sana ambazo zina uwezo wa kusomesha wanafuzi 45 ndani ya darasa moja. Na tatizo hili lipo kwa zaidi ya miaka 40 hapa Tanzania.
Kama serikali ina nia thabiti ya kusomesha watoto wetu kwa standard zinazotakiwa kwa nini isitatue hili tatizo wakati inazo pesa?
Kwa nini isiunde kikosi kazi maalumu na kujenga madarasa yanayotosha ndani ya miezi miwili,maana darasa halihitaji gharama kubwa na ufundi mkubwa? Maana tunaambiwa kila siku pesa zipo,sasa kwa nini msitenge pesa za kutosha kumaliza kero ndogo kama hii?