Elia F Michael
Member
- Mar 3, 2018
- 75
- 799
Idadi ya wajumbe waliopiga kura;.....140
Kura zilizopigwa...140
Kura zilizoharibika....01
Mchanganuo wa kura walizopata wagombea;
1. Ashura Masoud Mashaka ..............11
2. Elia F Michael.....121
3.Gaston Shundo Garubindi................07
Leo tar 08/07/2018 chama changu kupitia Kikao cha kamati kuu kwa pamoja wamenipitisha kugombea nafasi ya Ubunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia jimbo la Buyungu. Nipende kushukuru kwa heshima hii kubwa ambayo wanachama kupitia viongozi wameona niwakilishe chama.
Lakini pia nitoe shukrani kwa chama cha ACT-WAZALENDO kupitia Kaka yangu Zitto Kabwe ambaye yeye pamoja na chama chake wameamua kuniunga mkono. Naomba niwahakikishie Wana Buyungu na wapenda Demokrasia wote kwamba nia ninayo,uwezo ninao na sababu ninazo za kusimama kwenye nafasi hii muhimu katika uwakilishi wa wananchi.
Aidha naamini wananchi wakijua wajibu wao juu ya kulinda maamuzi yao na serikali ikajua wajibu wake kwa wananchi,Buyungu haiwezi kugeuka uwanja wa damu kama ilivyokuwa Kinondoni kwasababu ya kupinga maamuzi ya wananchi ... Naimani Marehemu Kasuku Bilago anaangalia yanayoendelea Buyungu kupitia Ulimwengu wa Roho. Naendelea kumuombea kwa Mungu aendelee kumpa pumziko jema mahala pema peponi,mbegu ulioipanda Buyungu iliota haikukauka,hauko nasi kimwili ila kiroho upo na sisi.
Elia F Michael
Diwani Gwarama,
Mwenyekiti wa madiwani Kanda ya Magharibi. Mgombea wa Ubunge jimbo la Buyungu kupitia CHADEMA
08/07/2018
Kura zilizopigwa...140
Kura zilizoharibika....01
Mchanganuo wa kura walizopata wagombea;
1. Ashura Masoud Mashaka ..............11
2. Elia F Michael.....121
3.Gaston Shundo Garubindi................07
Leo tar 08/07/2018 chama changu kupitia Kikao cha kamati kuu kwa pamoja wamenipitisha kugombea nafasi ya Ubunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia jimbo la Buyungu. Nipende kushukuru kwa heshima hii kubwa ambayo wanachama kupitia viongozi wameona niwakilishe chama.
Lakini pia nitoe shukrani kwa chama cha ACT-WAZALENDO kupitia Kaka yangu Zitto Kabwe ambaye yeye pamoja na chama chake wameamua kuniunga mkono. Naomba niwahakikishie Wana Buyungu na wapenda Demokrasia wote kwamba nia ninayo,uwezo ninao na sababu ninazo za kusimama kwenye nafasi hii muhimu katika uwakilishi wa wananchi.
Aidha naamini wananchi wakijua wajibu wao juu ya kulinda maamuzi yao na serikali ikajua wajibu wake kwa wananchi,Buyungu haiwezi kugeuka uwanja wa damu kama ilivyokuwa Kinondoni kwasababu ya kupinga maamuzi ya wananchi ... Naimani Marehemu Kasuku Bilago anaangalia yanayoendelea Buyungu kupitia Ulimwengu wa Roho. Naendelea kumuombea kwa Mungu aendelee kumpa pumziko jema mahala pema peponi,mbegu ulioipanda Buyungu iliota haikukauka,hauko nasi kimwili ila kiroho upo na sisi.
Elia F Michael
Diwani Gwarama,
Mwenyekiti wa madiwani Kanda ya Magharibi. Mgombea wa Ubunge jimbo la Buyungu kupitia CHADEMA
08/07/2018