EL, RA & JK wamnunua Mwanakijiji!

Status
Not open for further replies.

Hasara

Senior Member
Dec 29, 2006
138
9
SIKUJUA JAMBO FORUMS NI DEAL........

Lowassa,JK wa mnunua Mwanakijiji Bei Mbaya kuhusu Picha Chafu za kashifa na ushaidi mwingi aliyo nayo MWJ kuhusu viongozi hao na wengine ,kwahiyo wameamua kumrudisha kundini kwa pesa nyingi na kumu offer nafasi ya kazi serikalini na hakuna anaye mjua MWJJ kwahiyo akuna cha ushaidi hapa JF kwa hii ndiyo picha ya MWJJ au jina lake la kweli , picha za Kumdhalilisha Rais na hicho ndicho mwanakijiji alikuwa anakitafuta, haya mahojiano yalifanyika kwa simu MWKJJ alikuwa gumzo ikulu na kwenye maofisi ya serikali na ahadi zikifuatia, sikuamili kama mwanakijiji atakubali offer hiyosasa asema yameisha soma hapa ..

Ninacho weza kusema mwanakijiji atusaliti......
kama uhamini mimi ndiye nilimpa mwana kijiji hizo picha na mimi nimesikiliza maongezi ni nimeyasikia na sasa hivi nikimpigia MWKJJ simu apokei mimi ndiye niliye azisha ile thread sasa jamani mbona hivi tunageukana picha zangu deal achukuwe mtu mwingine .
Kashfa ya ufuska dhidi ya Kikwete ( 1 2 3 4 5 ... Last Page)
hasara--''vibweka vya wakubwa''

Nimeamka leo na mawazo ya ajabu sana! Maajabu kiasi cha kunishangaza mimi mwenyewe, na siyo tu kunishangaza bali kunistaajabisha kwa kunishangaza jinsi ninavyoshangaa! Hata hivyo ni mawazo ambayo kwa hakika ni ya mtu aliyefikia ukingoni... Tumepiga kelele hawakushtuka, tumeimba hawakucheza, na tumewaita hawakuitika! Wameamua kuendelea kufanya wafanyalo, kulinda walindalo, na kuendeleza kile kinachoitwa "libeneke".

Hata kama mtu ni shabiki wa timu ya mpira wa soka, kuna wakati ule ushabiki unakutoka hasa timu yako inapobugizwa magoli utadhani mchezo wa mpira wa kikapu. Ukifungwa goli moja unaweza kusikitika lakini bado ukaendelea kuishangalia timu, lakini goli la tatu, la nne, la tano, hata kama ni shabiki wa kuzaliwa inabidi uvue jezi na kuishangalia timu ya upinzani au kuamua kujing'atua uwanjani pole pole!

Bila ya shaka hadi hivi sasa hakuna shaka ni serikali gani tunayo mkononi, tunafahamu kwa hakika kuwa sera yao ya kulindana bado inaendelea, wako pole pole kushughulikia masuala ya mustakabali wa Taifa, na kwa hakika hadi hivi sasa hawana kipaumbele cha utendaji! Serikali haiwezi kufanya kila kitu kwa kiasi kikubwa ndani ya muda ule ule isipokuwa mpaka ichague kipaumbele na kipi kitangulie. Kama ni miundo mbinu, elimu, afya, madini n.k serikali makini ni lazima ijue inataka kuweka msisitizo wapi. Haiwezekani hata kidogo kumridisha kila mtu kwani matokeo yake hakuna atakayeridhika.

Waswahili walisema "panya wengi hawachimbi shimo refu". Maana ya msemo huo inashabihiana kabisa na ile "law of diminishing returns" ambapo inafika mahali faida inazidi kupungua pale vitu fulani (variables) vinazidi kuongezwa. Kwa kuongeza wakulima zaidi kwenye shamba la ekari moja haina maana mavuno yataleta faida zaidi! Kwa jinsi serikali yetu inavyokwenda nina uhakika tumefikia mahali pa diminishing returns na hatuna budi kupunguza vitu fulani.

Tupunguze vitu vya kufanya ndani ya miaka mitano ya mwanzo (sasa mitatu iliyosalia). Rais Kikwete na timu yake wake chini na kuingalia Ilani ya CCM na waamue kwa dhati ndani ya miaka mitatu iliyobakia ni nini kitatiliwa kipaumbele ili ifikapo 2010 angalau vitu hivyo viwe vimefikiwa angalau asilimia 95 ya malengo yake. Kwa kufanya hivi napendekeza kuwa na vipaumbele vya aina mbili.

a. Vipaumbele vya Msingi. Hivi ni vipaumbele ambavyo ni lazima serikali yoyote ihakikishe vinaendelezwa kila mwaka. Vipaumbele hivi vinahusu huduma za jamii (afya, elimu, na maji); vipaumbele vya Usalama (majeshi, ulinzi n.k) na vipaumbele vya miundo mbinu (barabara, umeme, simu n.k).

b. Vipaumbele vya Kati: Hivi ni vipaumbele ambavyo kila serikali inafanyia kazi kwa kadiri ya inavyochaguliwa. Mara nyingi vipaumbele hivi vinafuata sekta maalumu au eneo maalumu la kiuchumi. Lengo la vipaumbele hivi vya kati ni kufikia vipaumbele vya msingi. Maeneo ambayo serikali inaweza kuyatilia maanani katika sehemu hii ni vitu kama : Ubadilishaji wa sheria, utungaji wa taratibu, usimamizi na uchunguzi wa mambo fulani n.k Hivyo masuala kama ya mikataba n.k yangeweza kutiliwa maanani mara moja kwa kubadilisha taratibu na sheria na kufanya uchunguzi ili vipaumbele vya msingi viweze kufanikiwa pasipo matatizo.

Tatizo tulilonalo sasa ni kuwa watawala wetu wanajaribu kufanya mambo mengi kwa muda mfupi kwa kutumia watu wengi zaidi. Hili kwa hakika itakapofika 2010 tutajikuta hatujafanya mengi. Kwa vile watawala wetu wanajaribu kuridhisha kila mtu na kwa maneno yao mengi wanajaribu kufanya kila wawezalo kuonesha wako ontop of everything, na kwa sababu siamini hata kidogo kuwa wataweza kufanya yote waliyoyasema na kuyaahidi, nimeamua kuweka manyanga chini hasa katika suala la kuikosoa serikali.

Nimeamua na mimi kuungana na wale watafutao yale mazuri ya serikali na kuyapigia mbiu na kuyatangaza! Nimekubali yaishe... Nimekubali kuwa wao ndio watawala na walichaguliwa kwa asilimia 80, wanapendwa na wananchi na wanakubalika kutawala miaka mingine hamsini ijayo... kama walivyosema wengine "kama huwezi kuwashinda, jiunge nao".

CCM here I come, naomba kadi au ukada wa aina fulani....
__________________
Hoja Hujibiwa kwa Hoja!
I'm making my Haters, be my motivators - waliposhindwa hoja, sasa huleta vioja!


Posts: 193
Rep Power: 21

Thanks: 33
Thanked 21 Times in 15 Posts
Credits: 5,467

Re: Lowassa Amnunua Mwanakijiji Bei Mbaya

--------------------------------------------------------------------------------

Quote: Mzee Mwanakijiji
mnakumbuka "God Father"... hata wanaodhani wajanja wanaweza kupwa offer they can not refuse.. ni offer ambayo ukikataa utalipa! So, Bi. Senti over the weekend kanitumia ujumbe kutoka mkubwa fulani na wakasema wanipe ofa ambayo siwezi kuikataa.. now baada ya kuisikiliza ofa yenyewe nimeshindwa kuikataa jambo nimeikubali kwa machozi na kulia chonde chonde..

Ila wheelchair yangu ni ile kama ya Stephen Hawkings.. miye nimeketi tu huku mkono mmoja unafanya kazi zake..

hasara
Mwanakijiji ukimwaga Mboga mimi nitamwaga Ugali
picha bado ninazo nitaziweka hapa -umetusaliti
Kashfa ya ufuska dhidi ya Kikwete ( 1 2 3 4 5 ... Last Page)
hasara--''vibweka vya wakubwa''
 
wewe hasara unajua nimecheka na hiki kichwa cha habari, lakini pia vile vile kwa nini uweke porojo ? unajua watu wengi wanasoma hapa, halafu wewe unakurupuka ohhh lowassa kamnunua, yametoka wapi ? najua JF ipo mbele kwa datas, hivyo nitafurahi kama utatugeia hiyo lisiti inayoonyesha mwanakijiji kanunuliwa !

nota bene : nasubiri hiyo lisiti mkuu !
 
Ameamua kwenda kula kale kasungura nini? katatosha kweli wote ukizingatia kuna watu wenye miili mikubwa kama Komba.........

Usitusahau walau utugawie kidogo hata kama ni kucha tutakula tuu,
 
Ameamua kwenda kula kale kasungura nini? katatosha kweli wote ukizingatia kuna watu wenye miili mikubwa kama Komba.........
Usitusahau walau utugawie kidogo hata kama ni kucha tutakula tuu,

Yaani nimecheka kweli hapa kuhusu miili mikubwa ya Komba...

Mwanakijiji na wheelchair yake by the time afike mezani basi tayari Komba kishakula kilakitu.

Poor Mwanakijiji!
 
Ameamua kwenda kula kale kasungura nini? katatosha kweli wote ukizingatia kuna watu wenye miili mikubwa kama Komba.........

Usitusahau walau utugawie kidogo hata kama ni kucha tutakula tuu,

Kasungura na viazi vya kukaangwa....
Na hilo jicho lake moja, ufupi wake (5'2)...I can't wait to see him in the yellow and green....
 
SAID NGUBA UKO WAPI?
njoo ukanushe udaku huu,Lowasa hana uwezo wa kununu fikra za mwanakijiji yeyote,ana uwezo wa kununua fikra za mafisadi..
udaku per say,message ya Mzee Mwanakijiji imebeba ujumbe mzito na lengo La breakfast ni kuamsha hisia kwa watendaji wa serikali ili wajue vipaumbele vya wana wa watanzania..
hoja ya pili,Kutaka kadi ya sisiemu si kusaliti fikra sahihi alizonazo bali ni kuwaamsha wanachama wa ccm,
nina IMANI NA M.M. MWANAKIJ
 
MKJJ atawachezea akili hapa mpaka mtachanganyikiwa. Huyu hata akitaka kwenda CCM hawatamkubali.
 
Kasungura na viazi vya kukaangwa....
Na hilo jicho lake moja, ufupi wake (5'2)...I can't wait to see him in the yellow and green....

Ngabu umesahau pia kuwa Mkjj anatumia wheel chair. Sasa just imagine hiyo picha yake in yellow and green akila kasungura na viazi vya kukaangwa......
 
Kitila Mkumbo,
kwanini CCM wasimkubali Mwanakijiji? Kwa kosa lipi alilofanya?

Rejea mahusiano ya Wassira na Warioba, lakini leo hii Wassira yupo kwenye kamati kuu ya CCM.

Umesahau Hiza Tambwe alivyodai kwamba kuna mashua imepigwa mabomu na Wapemba zaidi ya 100 wamezama baharini? Mbona Makamba amempokea Tambwe CCM?
 
hakuna lisilowezekana ndani ya ccm hata kama ni kuchota BOT mradi ushindi wa kishindo hata kama mgombea hajui ilani inasema kitu gani.......
 
mnakumbuka "God Father"... hata wanaodhani wajanja wanaweza kupwa offer they can not refuse.. ni offer ambayo ukikataa utalipa! So, Bi. Senti over the weekend kanitumia ujumbe kutoka mkubwa fulani na wakasema wanipe ofa ambayo siwezi kuikataa.. now baada ya kuisikiliza ofa yenyewe nimeshindwa kuikataa jambo nimeikubali kwa machozi na kulia chonde chonde..

Ila wheelchair yangu ni ile kama ya Stephen Hawkings.. miye nimeketi tu huku mkono mmoja unafanya kazi zake..
 
Longo longo lingine la jumatatu? Hasara kama umeingizwa mjini nenda mhakamani Lol!!!
 
mnakumbuka "God Father"... hata wanaodhani wajanja wanaweza kupwa offer they can not refuse.. ni offer ambayo ukikataa utalipa! So, Bi. Senti over the weekend kanitumia ujumbe kutoka mkubwa fulani na wakasema wanipe ofa ambayo siwezi kuikataa.. now baada ya kuisikiliza ofa yenyewe nimeshindwa kuikataa jambo nimeikubali kwa machozi na kulia chonde chonde..

Ila wheelchair yangu ni ile kama ya Stephen Hawkings.. miye nimeketi tu huku mkono mmoja unafanya kazi zake..

Mwanakijiji ukimwaga Mboga mimi nitamwaga Ugali :eek:
picha bado ninazo nitaziweka hapa -umetusaliti

Kashfa ya ufuska dhidi ya Kikwete ( 1 2 3 4 5 ... Last Page)
hasara--''vibweka vya wakubwa''
 
Mwanakijiji hebu tuambie hiyo ofa mzee kama italeata maisha bora kwa kila mtanzania why not.
 
Hii ngonjera nzuri sana.... kaja hapa mtu anaitwa Huruma, akaja na yake sasa mambo mtindo mmoja. Hebu tusubiri tuone. Mkjj soma PM nasubiri majibu,,, vita imeanza na hapa umeme umekatwa sehemu yetu tu
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom