Wana jf wenzangu napata utata mkubwa kuhusu bei iliyo pangwa kwa ununuzi wa hizi ELECTRONIC FISCAL DEVICE ambapo yenye bei nafuu kabisa ni Tzs 1,860,000/- lakini ukiangalia chombo chenyewe hakifanani na thamani hiyo ya pesa maana ni sawa na calculator ya kawaida iliyoongezewa ka printer kadogo na memory card ya GB 2 kingine ni WAP ambayo ni teknolojia ya kawaida ambayo hata simu za Tzs 30,000/- huwa nazo. Utata huwo naupata pale ninapoangalia vyombo vingine kama vile laptop ambapo yenye thamani ya wastani wa Tzs 1,200,000/- inakuwa na vitu vingi sana na vya kuweza kufanya kazi sawa na hiyo EFD au hata zaidi sasa hii kwanini iwe ghali kiasi hicho, naomba maoni yenu.