Pure_sapiens
JF-Expert Member
- Dec 25, 2016
- 2,197
- 2,024
Ninandika huku nina majonzi mazito nyoyoni kutokana na tabia ambayo tunayo sisi wanamume. Mwanaume ni kiongozi katika familia na jamii zetu hakuna mwenye kupinga katika hili. Lakini kwa tabia hizi tunazoziendeleza zinatuweka katika daraja la chini kabisa.
Ijumaa karimu bandugu. Kuna haka katabia ambako kameenea katika maeneo mbalimbali katika mikoa yetu. Najua umewahi kuona vichaa hawa wa jinsia ya kike wakiwa na ujauzito.
Inasikitisha sana kuona mwanamke asiye na utimamu wa akili (kichaa) akiingiliwa kimwili hadi kuwa mjamzito bila ridhaa yake. Tena kuna baadhi yao wamezaa hadi watoto watatu na zaidi wakiwa katika ukichaa huo. Yaani inafika kipindi wengine wanachomwa sindano za kuzuia mimba.
Wanaofanya tabià si wengine ila sisi wanamume, tumekumbwa na nini sisi mbona kuna wanawake wengi tu.
Hii tabia ni ya kukemewa sana.
Ijumaa karimu bandugu. Kuna haka katabia ambako kameenea katika maeneo mbalimbali katika mikoa yetu. Najua umewahi kuona vichaa hawa wa jinsia ya kike wakiwa na ujauzito.
Inasikitisha sana kuona mwanamke asiye na utimamu wa akili (kichaa) akiingiliwa kimwili hadi kuwa mjamzito bila ridhaa yake. Tena kuna baadhi yao wamezaa hadi watoto watatu na zaidi wakiwa katika ukichaa huo. Yaani inafika kipindi wengine wanachomwa sindano za kuzuia mimba.
Wanaofanya tabià si wengine ila sisi wanamume, tumekumbwa na nini sisi mbona kuna wanawake wengi tu.
Hii tabia ni ya kukemewa sana.