Elections 2015 Edward Lowassa sio lazima yeye tu ndiye awe Rais wetu 2015, Rais wetu wa 2015 ni...

Mafisadi wajiandaa kuchafua Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake: Taarifa tulizozipata zisizotiliwa shaka ,Ni kwamba Genge la Mafisadi likiongozwa na baadhi ya wahariri na kijana mmoja Mwenye asili ya Kisomali anayetoka kanda ya Ziwa,limejipanga kwa vita ya kuanza kuwachafua, baadhi ya viongozi wa chama na waasisi wa Taifa hili ikiwemo Familia ya mwalimu Nyerere.

Mkakati huo ni mahususi kwa ajili ya kuhakikisha kila anayejiandaa kuchukua fomu kupambana na mgombea wao anachafuliwa kama alivyochafuka Mzee wao anayetaka Urais kwa udi na uvumba.Baadhi ya vijana hao wamepanga kuendesha mkakati huo kupitia Mitandaoni na baadhi ya Wahariri,akiwemo Mhariri aliyeshambuliwa miaka miwili iliyopita na kwenda kutibiwa Afrika kusini.

Wataanza kuendesha mkakati huo kuanzia Jumatatu hii kwa kutumia vyombo vya habari vinavyomilikiwa na mafisadi hao. Hasira hizo zimekuja baada ya JK kutamka CCM haitompitisha mgombea yeyote mwenye doa,hii ni hatari sana!
Nawasilisha,
UKANA SHILUNGO.

kaazi imeanza. huyo kijana wa kisomali bila shaka ni Hussein Bashe na huyo mhariri ni Absalom Kibanda
 
Hizo zote ni hisia na unadhani Lowassa akitupwa na kwenda upinzani then ameshashinda ila nakukumbusha anaweza kwenda upinzani na CCM ikamsimamisha mtu anayekubalika kama Magufuli ambaye naamini hata team Lowassa wanajua ni kizingiti kwao. Na kosa kwenye kampeni za Lowassa ni kudhani pesa pekee ndio muhimili wa kupata urais na kudhani akishapitishwa na CCM ndio kazi imeisha.
Naomba nikueleze siasa zimeshabadilika CCM lazima wawe na mgombea ambaye atawapa wabunge wa kutosha (anayekubalika kwa wananchi) na ukiangalia Lowassa wapambe wake wengi ni waliochafuka kwenye maeneo wanayotoka kama akina Chenge.
Hii inamaana wasipokuwa makini na kudhani wameshapata urais watajuta na utawala unaweza kumshinda kwani idadi ya wabunge ikiwa chache hataweza kutawala hapo ndio hasa Magufuli amewazidi nguvu wengine kwani ndio mtu pekee CCM anayeweza kunadi wagombea na wakakubalika kwa wananchi.
Kitu kingine ni mfumo wa maisha yetu na fikra za wananchi huwa ni negative kwa matajiri, pale mtu anapojinadi ni tajiri tayari kwenye jamii anaonekana ni adui na mwizi hata kama ni pesa halali. Ukutaka kushinda kwenye siasa zetu kuwa mnyenyekevu kuliko kuonyesha utajiri

Magufuli nae ni mulemule. Watu wana data za madudu aliyoyafanya wizarani.. Hana uwezo wa kuwa final striker. Anajitajidi kidogo ila anatakiwa kuwa nyuma ya mshambuliaji wa mwisho. (samahani kwa kutumia football language)
 
Mkuu Acha Usamba, sasa kiukweli inakubidi uuache huo ushamba wako. Kwanza siko hapa kumconvince yoyote kuhusu jambo lolote, bali niko hapa kuusema ukweli wa mambo, sasa kama utakuwa convinced au la, it's up to you!.

Siasa ni kama vita, inachezwa uwanja wa mapambano. Siri ya mafanikio ya shambulizi lolote ni usiri, ili kufanya shambulizi la kushukiza linaloitwa 'surprise attack' au ambush!.

Vivyo hivyo kambi ya Lowasa inajua inafanya nini, huo ukimya ndio silaha zenyewe za maangamizi na ili ushinde, you have "to save the best for the last", kama zamani sisi tulikuwa tunakula wali kuku siku ya sikukuu tuu, au mpaka akija mgeni muhimu. siku ya wali kuku, ukiisha gaiwa kipapatio chako au kanyagio (paja na kidari anakula baba au mgeni), sasa ukila huli nyama yako hadi umalize chakula, tena unaimega kidogo kidogo ili isiishe na mfupa wote unasagwa na meno mpka unakuwa mweupe kabisa!.

Mfano kisa halisi cha Richmond, ni moja ya karata yake muhimu ya turufu, ambapo silence yake ndio turufu ya kumpitishia!, wasipompitishwa kwa sababu za kimezengwe mizengwe, then turufu hiyo ndipo sasa itatumika kama silaha ya maangamizi, CCM wakimwaga mboga, jamaa anamwaga ugali, wakose wote, Ukawa waingie Ikulu!.

Kama unadhani umati wa watu kujaa kwenye mikutano ya kampeni ndio wing wa kura?!, kumbe mnataka tuu matamshi ya matumaini bila mipango thabiti ya utekelezaji?!. Lowassa sio mtu wa maneno mingi, ni mtu wa vitendo virefu!. Hakuna kutoa ahadi zozote hewa za matumaini, bali ni watu wamenyamaza kimya nyie subirieni tuu kuona vitendo na kumpima kwa matokeo na sio kwa ahadi!.

Wasio elewa Tanzania inahitaji nini na Watanzania wanataka ni nini 2015, ni wewe na huo ushamba wako mkuu Acha ushama, ndio maana nimekushauri sasa na wewe uuache huo ushamba wako!.

Pasco.

Umejibu kwa panic sana!
 
hivi nchi hii ni Lowassa ndiyo kaumbwa rais? je siku akifa hakuna mtu mwingine anayeweza? hebu tuwe na hekima kidogo kiongozi makini uwekwa na watu ajiweki mwenyewee Mungu akipanga hakuna wa kupangua
 
halafu kweli mtanzania mzalendo anaweza kufikiria kuwasapoti akina Andrew Chenge Nazir Karamagi AbdulAziz Bashe Peter Serukamba nk siamini mtu makini mzalendo aliye na uchungu na nchi hii km anaweza kushirikiana na hiyo team watu makini wanaondoka moja baada ya mwingine.
 
Pasco. Heshima mbele ong'wise.

kwanza tuhakikishie pasipo na shaka kuwa kilichomtokea mzee ngoyai si tu 'ajali ya kisiasa' bali ni 'chezo'.
 
Last edited by a moderator:
Pasco. Heshima mbele ong'wise.

kwanza tuhakikishie pasipo na shaka kuwa kilichomtokea mzee ngoyai si tu 'ajali ya kisiasa' bali ni 'chezo'.
Adhabu imemalizika, watu wametoka kifungoni jee chezo linaendelea au watu tujikusanye na kujipanga kuianza safari?!.

Pasco
 
Adhabu imemalizika, watu wametoka kifungoni jee chezo linaendelea au watu tujikusanye na kujipanga kuianza safari?!.

Pasco

tujiandae na safari ya jehanam. safari ya matumaini alikuwa nayo nyerere peke yake waliopita wameangusha gari ya ccm. sasa ni zamu ya ukawa yenye dreva makini wengine tupa kule nyuma wawe utingo.
 
Haya shime wajemeni, nia imetangazwa, safari ya matumaini ndio imeanza!, kwenye safari hoja ya msingi sio kuanza kwa safari bali kufika kwenye destination haswa kwa kuzingatia kutanguli sii kufika!.

Pasco
 
Haya shime wajemeni, nia imetangazwa, safari ya matumaini ndio imeanza!, kwenye safari hoja ya msingi sio kuanza kwa safari bali kufika kwenye destination haswa kwa kuzingatia kutanguli sii kufika!.

Pasco

Hatuhitaji SAFARI YA MATUMAINI TUNAHITAJI SAFARI YA UHAKIKA.
Watanzania tutaishi kwa matumaini hadi lini?
 
Hatuhitaji SAFARI YA MATUMAINI TUNAHITAJI SAFARI YA UHAKIKA.
Watanzania tutaishi kwa matumaini hadi lini?
Safari ni hatua, kabla haujapata uhakika wa safari, unatanguliza nia ya kufanya safari, sababu ya safari hiyo ndio matumaini ya safari yako ndipo kisha sasa unatafuta uhakika!.

Lowassa kaweka nia, ana matumaini ya kuondoa Tanzania hii hapa tulipo na kuipeleka kwenye dimensions nyingine. Safari ndio imeanza kuelekea kwenye uhakika wa safari hiyo ambao utatolewa na vikao vya juu vya Chama!.

Pasco
 
...Yule Aliyepangiwa na Mungu!.

Wanabodi,

2015 ndio hii, mimi ni miongoni mwa tuliojibainisha wazi, kumkubali Edward Lowassa as "The One and Only" Best President this country can ever have apart from Nyerere!. Hii haina manna Lowassa ndio lazima awe rais. Rais wa Tanzania kwa 2015 ni yule tuu, aliyepangiwa na Mungu, sio lazima awe ni Lowassa, ila kwa vile Mungu bado hajatuambia amempangia nani, kama aliepangiwa na Mungu ni Edward Lowassa, basi ni lazima awe yeye!.

Nakiri nimekuwa inspred kuandika mada hii, kufuaria mchango wa mwana jf huyu kwenye uzi fulani!

Mkuu So Notorious, kwanza nakubaliana na wewe, Pasco huyu unayemjua sasa ni mshereheshaji tuu wa maonyesho ya Saba Saba na Nanenane, kwa nyie watu wa kisasa. Pasco aliondoka rasmi newroom mwaka 2002 na tangu hapo hajawahi kuajiriwa tena, sasa amebaki kama Mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea. Sasa ili kumjua Pasco, rudisha mawazo yako mwaka 2002 ulikuwa level gani, na kuanzia hapo ndipo turudi nyuma!.

Pasco hajawahi kuwa spokesperson wa Lowassa, hajawahi kufanya kazi yoyote kwa Lowassa, hajawahi kuhudhuria press conference yoyote ya Lowassa, hajawahi kuandika au kuripoti news yoyote ya Lowassa na wala hajawahi kufika Monduli, au kuhudhuria zile sherehe maarufu za Monduli!.

Kitu pekee alichofanya Pasco humu jf, ni kumkubali Lowassa, katika ukweli dhahiri usio na mawaa yoyote kuwa ndani ya CCM, Edward Ngoyai Lowassa, ndie the one and only best presidential candidate CCM has, na ikitokea asipitishwe, then asipitishwe kwa haki, vinginevyo patachimbika!.

Hata hivyo kumkubali kwangu Lowassa, ni personal tuu, tena kwa kujitolea, siko Team Lowassa!, sijawahi kuwepo!, wala sijawahi kupokea hata senti moja kutoka kwa Lowassa!, hivyo hoja ya kumlamba mtu miguu kwangu haipo!, ningekuwa mlamba miguu, ningemlamba Mkapa ambaye mtoto wake nimesoma naye darasa moja sekondari kwa miaka minne!, wakati kwa wengine wote Mkapa ni rais, mimi nimekwenda kwake kama baba fulani!. Ningekuwa ni mtu wa kujikomba komba na kujipendekeza, ningejikomba kwa Riz 1, nimekutana nae UDSM na tunaiva sana, hivyo angenishika mkono anipeleke kwa mshure wake!, why nilambe miguu ya mtu?!. Mimi niko kwenye lile kundi la "Maskini Jeuri" kama kina "Kozi mwana mandanda, kulala njaa kupenda!".

Ila pia nina mtu wangu wa karibu kwenye Team Lowassa, hii ndio timu yenye mkono mrefu kuliko team nyingine yoyote so far!. Tatizo langu na timu hii ni moja tuu, hali ya Afya ya Mzee wetu!, kwa vile rais wa Tanzania 2015, ameishachaguliwa na Mungu, then, alilolipanga Mungu, binadamu hawezi kulipangua!, ndio maana kule nyuma Mungu aliwahi kufanya muujiza wa "Jiwe walilolikataa waashi likafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni!", na kuna mtu alielezwa kuwa "Wewe ni mwamba, na juu ya mwamba huu, nitalijenga taifa langu!", kwa Tanzania hapa tulipofika, tuna mwamba mmoja tuu, "Mwamba wa Kaskazini!"
Lazima awe!, na asipokuwa basi itakuwa Mungu hakumpangia!, hivyo atakayekuwa rais wetu, 2015, ni yule tuu Mungu aliyempangia!.

Wasalaam!.

Pasco.
Wakati wenyewe wanaanza vikao vyao Dodoma, mimi nafanya merejeo ya hii kitu!.
Pasco
 
Hii inaitwa trends kwenye numerology!.
Ni liandikwalo tuu ndilo liwalo!, kama hlijaandikwa, haliwi!.
Pasco.
Lowasa alishawahi kukusaidia kwenye mishemishe zako kule mamtoni-ITALY?, kwa hiyo si kweli kwamba hamfahamiani kabisa
 
Lowasa alishawahi kukusaidia kwenye mishemishe zako kule mamtoni-ITALY?, kwa hiyo si kweli kwamba hamfahamiani kabisa
nisome tena
...

Pasco hajawahi kuwa spokesperson wa Lowassa, hajawahi kufanya kazi yoyote kwa Lowassa, hajawahi kuhudhuria press conference yoyote ya Lowassa, hajawahi kuandika au kuripoti news yoyote ya Lowassa na wala hajawahi kufika Monduli, au kuhudhuria zile sherehe maarufu za Monduli!.

Kitu pekee alichofanya Pasco humu jf, ni kumkubali Lowassa, katika ukweli dhahiri usio na mawaa yoyote kuwa ndani ya CCM, Edward Ngoyai Lowassa, ndie the one and only best presidential candidate CCM has, na ikitokea asipitishwe, then asipitishwe kwa haki, vinginevyo patachimbika!.

Hata hivyo kumkubali kwangu Lowassa, ni personal tuu, tena kwa kujitolea, siko Team Lowassa!, sijawahi kuwepo!, wala sijawahi kupokea hata senti moja kutoka kwa Lowassa!,

Pasco.

Pasco
 
Mkuu Pasco kuna jambo moja umepungukiwa, nalo ni kumsigizia Mungu kwamba atatupangia raisi watz! Nakiri wazi kwamba hili hulitambui kwamba watz hawatapata raisi aliechaguo la Mungu!

Ni dhahiri shahiri kwamba raisi wetu anapangwa na wenye hela na kupitishwa kwa nguvu na tume ya uchaguzi! Haitokaa itokee kwamba watz wampate raisi wa chaguo la Mungu ikiwa tume ya uchaguzi itabaki ile ile na watu wenye hela kafanya maovu bila kuadhibiwa!

Mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi, kila mtz ameshuhudia mbwembwe za akina Edward na hela wanazomwaga ili waingie ikulu, je kwa strategy hii tuiite ni chaguo la Mungu?

Nitaamini kuwa ni chaguo la Mungu pale watz watakapoacha njaa na kuwaza kwa mapana miaka 30 ijayo! Maana mustakabali wa miaka 30 ijayo unategemea maamuzi yetu leo!

Mzee Pasco nakuheshim sana, ila kubali kataa sio Lowasaa wala CCM watakaoleta changes ndani ya hii nchi! CCM inatakiwa ikae pembeni kidogo, ione mapungufu na udhaifu wa serikali wanayosimamia, maana kuna uwezekano mkubwa kwamba hawaoni tatizo lao na la watanz kwa ujumla.

Haiwezekan nusu karne ya uhuru, bado wanafunz wetu wanakalia mawe, haiwezekani nusu karne ya uhuru, TZ haijaweza kujtegemea kiuchumi! Mbaya zaidi kuna misamaha ya kodi ya thamani ya trillion moja kwa mwaka, na bado watu tunakaa kimya!!

Mkuu Pasco, tambua CCM ni mfumo, and body within the party can change it! Nchi hii inahitaji maamuzi magum kutoka kwa watz na sio kwa wanasiasa kama wanavyojitapa! Hainiingii akilin mtu anatangaza nia anasema eti atapambana na "ufisadi" wakati alikua na uwezo wa kufanya hivyo from the beginning, kwa nini hakufanya asubiri kuwa raisi!? Huu ni unafiki uliopitiliza na dharau kwa watz!

Ninachowasihi watz, wawapime wagombea wote na historia yao itazamwe kwa kina! Kipaombele cha kwanza kiwe uzalendo na huruma kwa watz! Mtu anakwapua billion 10 anajibu kwa kiburi kuwa ni hela ya mboga, and yet anataka kuwa mwakilishi wa wananchi. Nitashangaa na kusikitika sana nitakapomwona bunge lijalo karudi.

Tukiamua tunaweza, la msingi tuache njaa na kuwa watumwa kiakili!!

Regards to Pasco!
 
Kanone una matatizo kweli ndugu na hii sheria iliopendekezwa ya habari mtajaa wengi keko na masegerea bazir mramba kahukumiwa jana tuu je lowasa yeye nani kama aliiba aachwe kwenye serikali hiii tuchunge midomo tusifate ushabiki tufanye tafiti za kuaminika ndipo tuongeee mambo
 
Back
Top Bottom