KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,589
- 4,599
Awali ya yote napenda kukiri kwamba sijatumwa wala kutumika na yeyote kuandika juu ya hii mada, ni maoni na mtazamo wangu binafsi na pengine ni mtazamo wa wengine wengi wanaomtazama Lowassa kama ninavyomtazama mimi.
Katika ulimwengu wa siasa, jambo dogo linaweza kujadiliwa kwa marefu na mapana kufikia hitimisho. Binafsi ninaamini baada ya Rais Magufuli kukubalika, kupendwa na kuheshimika ndani na nje ya CCM kwa sasa, anayefuata ni Mzee Lowassa.
Nini kinachombeba Lowassa?
Kila jambo linalotokea katika ulimwengu huu lina sababu zake lakini naamini za wengi kuendelea kumpenda na kumuheshimu Lowassa ni historia yake.
Lowassa ana historia ya upambanaji mkubwa dhidi ya udhalimu na unyonyaji, historia ambaye ni kumbukumbu iliyoacha alama katika uongozi wake alipokuwa katika nafasi mbalimbali kama waziri na hatimaye waziri mkuu. Mchango wa Lowassa kwa taifa hili si wa kubezwa ni wa kukumbukwa na kuenziwa na hili nafikiri ndio sababu ya watu kumpenda na kumuheshimu sana.
Historia ya uchapakazi, tangu akiwa waziri na hatimaye waziri mkuu Lowassa amekuwa mstari wa mbele kutekeleza majukumu yake kwa kiwango kikubwa. Wawili hawa, Rais Magufuli na Mzee Lowassa wana historia zinazofanana katika uchapakazi na kuchukia uzembe. Sifa hii ya uchapakazi imesaidia taifa hili kufanikisha mambo mengi na machache ya kukumbukwa wakati wa uongozi wa mzee Lowassa kama waziri mkuu ni ujenzi wa shule za kata na chuo kikuu cha Dodoma(UDOM) kwa muda mfupi.
Lowassa ni mtu mwenye maono kama alivyo Rais Magufuli, sera kuu ya Rais Magufuli kwenye kampeni za 2015 ilikuwa ni Tanzania ya viwanda kwa lengo la kuiwezesha nchi kuwa na uhuru wa kiuchumi na kuwa uwezo wa kujitemea na sera kuu ya Lowassa kwa wakati huo ilikuwa ni Elimu kwa lengo wa kuwawezesha watu kuwa na uhuru wa fikra. Wote wana maono makubwa sana na wote wanaamini katika Tanzania huru na uhuru wa kiuchumi na kifikra.
Kwanini Lowassa anafaa?
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema ‘mnapochagua mtu chagueni mtu aliyebeba matarajio ya wananchi hasa matarajio yakow ewe mpigakura’. Ninaamini kwamba kiongozi yeyote mwenye maono, uthubutu na misimamo kabeba matarajio yetu sisi wananchi anafaa baada ya Rais Magufuli.
Lowassa anayaishi maneno ya Mwalimu juu ya kudumisha amani. Katika sherehe za miaka 58 ya Uhuru Lowassa amenukuliwa akimnukuu Mwalimu na alisema “ akitokea mtu jeuri na fedhuli na akawaambia mna nini watanzania? Mjibu hivi’ mwambie tuna amani”. Tumeadhimisha miaka 58 ya uhuru wetu kutokana kwa kuwepo kwa amani, na yeyote anayejali na kuheshimu amani kutoka moyoni anafaa kuwa Rais ajaye
Mwalimu nyerere aliwahi kutaja sifa za mgombea urais kupitia CCM, sifa hizo ni: anatakiwa kuwa mtu anayechukia rushwa ,udini na ukabila kwa dhati ya moyo wake na pia anatakiwa kuwa mtu anayejali maskini na wanyonge kwa kuwa nchi yetu ni ya masikini. Binafsi ninaamini Mzee Lowassa anazo sifa hizo.
Hitimisho
CCM ndipo matarajio, Imani na matumaini ya watanzania ilipo chini ya uongozi thabiti ya mwenyekiti wake Dkt. Magufuli, tunaiombe na kumuombea busara na hekima zaidi ya kuongoza nchi yetu. Pia, mzee Lowassa tunakuombea Mungu akutangulie, akulinde na akusimamie.
Katika ulimwengu wa siasa, jambo dogo linaweza kujadiliwa kwa marefu na mapana kufikia hitimisho. Binafsi ninaamini baada ya Rais Magufuli kukubalika, kupendwa na kuheshimika ndani na nje ya CCM kwa sasa, anayefuata ni Mzee Lowassa.
Nini kinachombeba Lowassa?
Kila jambo linalotokea katika ulimwengu huu lina sababu zake lakini naamini za wengi kuendelea kumpenda na kumuheshimu Lowassa ni historia yake.
Lowassa ana historia ya upambanaji mkubwa dhidi ya udhalimu na unyonyaji, historia ambaye ni kumbukumbu iliyoacha alama katika uongozi wake alipokuwa katika nafasi mbalimbali kama waziri na hatimaye waziri mkuu. Mchango wa Lowassa kwa taifa hili si wa kubezwa ni wa kukumbukwa na kuenziwa na hili nafikiri ndio sababu ya watu kumpenda na kumuheshimu sana.
Historia ya uchapakazi, tangu akiwa waziri na hatimaye waziri mkuu Lowassa amekuwa mstari wa mbele kutekeleza majukumu yake kwa kiwango kikubwa. Wawili hawa, Rais Magufuli na Mzee Lowassa wana historia zinazofanana katika uchapakazi na kuchukia uzembe. Sifa hii ya uchapakazi imesaidia taifa hili kufanikisha mambo mengi na machache ya kukumbukwa wakati wa uongozi wa mzee Lowassa kama waziri mkuu ni ujenzi wa shule za kata na chuo kikuu cha Dodoma(UDOM) kwa muda mfupi.
Lowassa ni mtu mwenye maono kama alivyo Rais Magufuli, sera kuu ya Rais Magufuli kwenye kampeni za 2015 ilikuwa ni Tanzania ya viwanda kwa lengo la kuiwezesha nchi kuwa na uhuru wa kiuchumi na kuwa uwezo wa kujitemea na sera kuu ya Lowassa kwa wakati huo ilikuwa ni Elimu kwa lengo wa kuwawezesha watu kuwa na uhuru wa fikra. Wote wana maono makubwa sana na wote wanaamini katika Tanzania huru na uhuru wa kiuchumi na kifikra.
Kwanini Lowassa anafaa?
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema ‘mnapochagua mtu chagueni mtu aliyebeba matarajio ya wananchi hasa matarajio yakow ewe mpigakura’. Ninaamini kwamba kiongozi yeyote mwenye maono, uthubutu na misimamo kabeba matarajio yetu sisi wananchi anafaa baada ya Rais Magufuli.
Lowassa anayaishi maneno ya Mwalimu juu ya kudumisha amani. Katika sherehe za miaka 58 ya Uhuru Lowassa amenukuliwa akimnukuu Mwalimu na alisema “ akitokea mtu jeuri na fedhuli na akawaambia mna nini watanzania? Mjibu hivi’ mwambie tuna amani”. Tumeadhimisha miaka 58 ya uhuru wetu kutokana kwa kuwepo kwa amani, na yeyote anayejali na kuheshimu amani kutoka moyoni anafaa kuwa Rais ajaye
Mwalimu nyerere aliwahi kutaja sifa za mgombea urais kupitia CCM, sifa hizo ni: anatakiwa kuwa mtu anayechukia rushwa ,udini na ukabila kwa dhati ya moyo wake na pia anatakiwa kuwa mtu anayejali maskini na wanyonge kwa kuwa nchi yetu ni ya masikini. Binafsi ninaamini Mzee Lowassa anazo sifa hizo.
Hitimisho
CCM ndipo matarajio, Imani na matumaini ya watanzania ilipo chini ya uongozi thabiti ya mwenyekiti wake Dkt. Magufuli, tunaiombe na kumuombea busara na hekima zaidi ya kuongoza nchi yetu. Pia, mzee Lowassa tunakuombea Mungu akutangulie, akulinde na akusimamie.