Edward Lowassa afanya Propaganda kwenye media eti kashinda 100%

Haki sawa

JF-Expert Member
Oct 3, 2007
4,780
3,208
Kutoka kwa mwandishi wa Lowassa, Abubakary Liongo ametuma taarifa kwa vyombo vya habari kuwa Monduli CCM imeshinda kwa aslimia 100 na anataka dunia iamini hivyo ,eti Monduli ni kama Kilindi, na hilo ni jambo la uongo wa dhahiri kwani anajua wazi kuwa maeneo yafuatayo CCM imeshindwa ;

1. Kitongoji cha Kambi ya Mkaa CCM 13 na CHADEMA 27

2. Loswira Kitongoji , CCM 34 na CHADEMA 56 tena hapa alishinda mlemAvu .

3. Kijiji cha Mgombani CHADEMA imeshinda Vitongoji vinne

4. Kijiji cha NANJA CCM IMeshindwa


Liongo njoo upinge ukweli huu ndipo wahahriri watumie story yako kesho.
 
Wenye upeo mpana kwasasa hatuzungumzii haya matokeo ya mtaa momoja mmoja yakiwa tayari yote tukutane hapa hapa jf.
 
na iv ndo itakavyo kua kwenye matokeo ya jumla utashanga ccm imeshinda kwa 97% kesha wana wa yesu UKAWA watabak na malalamiko yasio na tija mana sis tumezoea kushinda mtandaoni
 
Kuna wa/mpambe wake hapa jukwaani nimemchana bosi wao wameshia kutukana na wala hakuna aliyejenga hoja. Nimewauliza mbunge sio mfadhili, hebu watuambie inakuwaje huyo Lowassa anaweza kwenda misikitin/ makanisani akaweza kutoa hotuba ambayo haulizwi swali lolote lakini hawezi kuchangia chochote huku bungeni ambako ndio majukumu yake yalipo. Kama anaweza kuhutubia kanisani/msikitini kwanini asiwe sheikh au mchungaji anataka kuwa rais. Ndugu ungesikia majibu ya watu anaowalipa kumtetea hapa jukwaani mbona ungechoka. Wameishia kutukana na kukashifu.

Sikuishia hapo nikawaomba wataje mambo matano ya uhakika kwanini tumpe urais hakuna aliyerudi mpaka sasa!! Toka nimemuona alivyopoteza madaraka kwa sakata la richmond nilimsikia siku moja tu akichangia bungeni eti nchi ichukue maamuzi magumu, eti wakatokea wabunge wasiojitambua wakimshangilia rais rais!! Nikauliza mbona juzi tumeshuhudia sakata la escrow hadharani hatukumuona akichangia lolote tuliishia kuwaona akina Lisu, Zitto, Mnyika, Mdee, Simbachawene na hata huyo Chenge. Yeye msimamo wake ulikuwa upi ni pesa za umma au za IPTL. Sasa najiuliza ubora wake uko kwenye nini. Au yeye ni tajiri hivyo tumpe urais kwakuwa wanamlamba miguu wamesema.

Nasema tusipoangalia tutampa nchi hii mmoja wa viongozi wa mtandao wa kiongozi aliyeko juuambaye kaifikisha nchi kwenye kuweza kuingia mikataba zaidi ya kumi na sita kwa mpigo bila wananchi au bunge basi kujua nini kipo ndani bali genge lake tu. Na kwa bahati mbaya sana tunapewa sifa zilezile za kijinga kwamba ni mchapa kazi lakini uchapa kazi wake haufafanuliwi bali watu wanapewa pesa wanakuja kusema ni mchapa kazi. Sifa hizihizi ndio tuliambiwa tuchague rais kijana ambaye picha yake itapendeza kwenye noti. Kweli watanzania tuko tayari tena kutoa uongozi kwa kiongozi ambaye sifa zake ni za uchochoroni tena kwa nguvu ya pesa?
 
na iv ndo itakavyo kua kwenye matokeo ya jumla utashanga ccm imeshinda kwa 97% kesha wana wa yesu UKAWA watabak na malalamiko yasio na tija mana sis tumezoea kushinda mtandaoni
huu mwaka mgumu sana .......wameanza kufa kwenye vituo ,kesho watakufa wa Jf kwa presha .....
 
Wenye upeo mpana kwasasa hatuzungumzii haya matokeo ya mtaa momoja mmoja yakiwa tayari yote tukutane hapa hapa jf.

Ni kweli kabisa unachosema, lazima ccm itakuwa juu kwa matokeo ya kura zote. Lakini ukweli ambao hata wewe unaukwepa ni kwamba wangalau sasa tunaanza kuona wananchi wakijitambua na hasa vijana na kutekeleza wajibu wao.

Mtaani kwetu ni mara ya kwanza kuongozwa na chama cha upinzani hayo ni mabadiliko makubwa. Tena ukizingatia unashinda na timu ambayo wachezaji wako wote na wa timu pinzani wametolewa kwa hila, huku ccm ikiwa refa, mshika kibendera na kamisaa wa mchezo akiwa jeshi la polisi. Hapo hata msiposhinda si itakuwa vichekesho. Ila sasa ukweli uko peupe kwamba ccm sio mshindani kwani hakubali kushindwa.

Tunachowaomba muandae jeshi la kutosha kuwapa ushindi kwani 2015 viti vya ubunge vingi na udiwani lazima viende upinzani na huko bungeni wale walalaji na vigelegele vya kipuuzi kwenye kupitisha miswaada isiyo na tija ndio utakuwa mwisho. Huo ndio ukweli ambao kila mtu sasa anaanza kuutambua.
 
We chalii, weka na matokeo ya CCM kwa Monduli yote.

Pole kwa kazi za siku nzima za kulijenga taifa kupitia JF.

Kesho naomba uende kwenye kazi halali kwani ni uzalendo ulipe kodi. kumbuka nchi inajengwa kwa kufanya kazi na sio kushinda hapa jukwani ukitetea wizi na wezi wa kodi zetu.

Nyinyi ndio chanzo cha nchi yetu kuwa ombaomba kwa wazungu sijui MCC nk. Ulizoea kuwa kishoka kwenye ofisi za serekali kuwasaidia watu mambo yao yaende kwa haraka eti wanatoka mikoani wasikae sana. Sasa ulipaji kwa njia ya mtandao unaingia nchini kwa umri huo usipojirekebisha utakuwa ombaomba uzeeni na kuishia kuacha laana kwa watoto na wajukuu kumbe ulimalizia nguvu kazi hapa JF.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom