Edo Kumwembe: Kuingia uwanjani saa nne asubuhi wakati mechi inachezwa saa kumi na moja jioni ni mateso

Edo Kumwembe: Kuingia uwanjani saa nne asubuhi wakati mechi inachezwa saa kumi na moja jioni ni mateso

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,145
"Kuingia uwanjani saa nne asubuhi wakati mechi inachezwa saa kumi na moja jioni ni mateso. Sio kwamba mashabiki wanataka, hapana, wanajihami. Wanahepuka kadhia ya baadae. Kule kwa wenzetu kila tiketi ina seat number. Mageti yote pia yanafunguliwa na unaingia katika geti la jukwaa lako. Naona watu wanaiweka hii ya kwenda uwanjani mapema kama sifa. Sio sifa. Wenzetu wanaingia dakika 15 kabla ya mechi kuanza na hakuna shida. Wenye mamlaka wanajua sana kuhusu hili"
1758013883373.png


1758013905315.png
 
Kuingia uwanjani saa nne asubuhi wakati mechi inachezwa saa kumi na moja jioni ni mateso. Sio kwamba mashabiki wanataka, hapana, wanajihami. Wanahepuka kadhia ya baadae. Kule kwa wenzetu kila tiketi ina seat number. Mageti yote pia yanafunguliwa na unaingia katika geti la jukwaa lako. Naona watu wanaiweka hii ya kwenda uwanjani mapema kama sifa. Sio sifa. Wenzetu wanaingia dakika 15 kabla ya mechi kuanza na hakuna shida. Wenye mamlaka wanajua sana kuhusu hili.
Ndo maana siendi
 
Iyo inasababishwa na wahuni kutofuata mpangilio wa ticket na sit.
Kama kila shabiki anakaa kwenye sit iliyo onyeshwa kwenye ticket kusingekua na sababu ya kuingia asubuhi kusubiria mechi ya jioni.

Mambo ya miaka ya 80 tunaendeleanayo Leo miaka ya 2000!!
 
Huyu Edo ni mpuuzi flani anajiona yeye mwerevu Sana, yeye inamuhusu nini, yeye kwani anaingia saa ngapi.
Hoja haipigwi Rungu, Haya mambo yapo nchi zetu ambazo tuna muda mwingi sana wa kuchezea kuliko wa kufanya vitu vya msingi. Yaani mechi inachezwa saa 11 uingie uwanjani saa 4 asubuhi masaa 5 yote umekaa uwanjani bila kufanya chochote, Siajabu hata viwanja vyetu havidumu sababu vinatumiwa kwa muda mrefu kwa matumizi ambayo sio sahihi. Kiti ambacho kilipwaswa kikaliwe kwa masaa 2 au 3, kinakaliwa masaa 8. Huyu jamaa ana Hoja hata kama humpendi
 
Ila hao walioenda mapema sijawasikia wakilalamika..labda huyo Edo nae awe tayari yupo uwanjani...asiwalishe watu maneno.
Mimi kaniwakilisha Mkuu, japo sijaenda uwanjani, ila utaratibu wetu wa kuingia viwanjani kwenye hizi mechi kubwa una usumbufu na bugza nyingi sana
 
Back
Top Bottom