Kizimkazimkuu
JF-Expert Member
- Nov 8, 2007
- 337
- 234
..Kesi ya Mwandishi wa habari Jerry Muro hatimaye imefikia mwisho leo kwa yeye na watuhumiwa wenzake wawili kuachiwa huru. Pamoja naye, washitakiwa wengine walikuwa ni Edmund Kapama na Deogratius Mgasa. Nadhani wengi tungependa kuwafahamu hawa ni akina nani, na kivipi walihusishwa na Jerry. Binafsi nimepata kuwaona hawa jamaa katika baa moja kinondoni na Jamaa yangu akaniekeza kuwa pale ndio kijiwe chao...na wamekuwa wakikutana sana hasa kabla ya siku za kwenda mahakamani. Jamaa yangu alicheka sana statement ya polisi kuwa hawa ni watuhumiwa wanaliokuwa wanatafutwa na polisi kwa makosa ya utapeli kwa muda mrefu, ilhali jamaa wanajulikana (hasa maeneo ya K'ndoni) kuwa ni matapeli na mara nyingi hushinda bar za kinondoni G8, John Fedha nk...Kama kuna wanaowajua vizuri; shughuli zao hapa mjini, kama wamewahi kuhusishwa na matukio mengine nk...