Edibily Jonas Lunyamila, miguu ya Dhahabu, kichwa chenye mamlaka ya kusoma alama zote ndani ya Uwanja

TEAM 666

JF-Expert Member
Dec 7, 2017
4,330
8,421
EDIBILY JONAS LUNYAMILA . Macho yangu yameshuhudia mengi na Moyo wangu umebahatika kujawa na hisia tosha kwa Uzalendo wa Taifa langu la Tanzania.

Miaka mingi tumekua tukiimba nyimbo za kuitukuza Nchi yetu na mashujaa na hata kuwasoma katika historia . " Tazama Ramani utaona Nchi nzuri, yenye mito na mabonde mengi ... " au hata ubeti mwingine maarufu " ... jina lako ni tamu sana, nilalapo nakuota wewe, niamkapo ni Heri Mama weee . "Hii yote ni kuipenda Nchi yetu lakini tuna mengi hatuyaimbi na kuyatukuza.

Edibily Jonas Lunyamila, miguu ya Dhahabu, kichwa chenye mamlaka ya kusoma alama zote ndani ya Uwanja, kipaji maridhawa kabisa katika ukanda huu.

Lunyamila.jpg
Ukienda Uganda hadi leo jina La Lunyamila ni Maarufu kuliko Emanuel Okwi ni kutokana na uwezo wa maajabu wa Winga huyu .

Mwaka 1992 katika mashindano ya UMISETA kule Zanzibar kiliibuka kipaji cha Dhahabu kutoka shule ya Sekondari ya Buhangija huko Shinyanga na mwaka huo akaitwa Timu ya Taifa, bahati iliyoje.

Inasemekana Abbas Gulamali ndiye aliyekwenda kumsubiri Edibily Jonas Lunyamila mlangoni mwa chumba cha mtihani ili ampeleke Mwanza kucheza timu ya Taifa.

Nafikiri hii ndiyo sababu akacheza Yanga na mwaka 1993 akaacha alama ya Maisha yake Kule Kampala Uganda. Kwangu Mimi maisha ya soka ya Lunyamila na kipaji chake kinastahili kuimbwa kama kivutio cha Taifa na ni Hadhi ya Nyota Tano.

Nikiwakumbuka watangazaji wa zamani kina Swedi Mwinyi, Juma Nkamia, Ahmed Jongo au Charles Martin Hillary walivyokua wakitangaza soka basi mie jina linalokuja ni Lunyamila.

Unamkumbuka Edibily Jonas Lunyamila kwa lipi au nyakati gani..?
 

Attachments

  • 426868_gallery.jpg
    426868_gallery.jpg
    87.2 KB · Views: 33
Mie namkumbuka kwa kurubuniwa na Yanga wakati anakamilisha taratibu zake pale Frankfurt (kama sijakosea) kwamba aje Tanzania acheze vs Simba pale CCM Kirumba. Na kweli lengo la Yanga lilifanikiwa kwa kushinda 2-0 dhidi ya Simba lakini Lunyamila bahati yake ya kucheza Ulaya ndio ikawa imeishia hapo. Sasa ni kubaki kukumbuka tu ile bahati. Hapa pia namkumbuka Mrisho Ngassa alivyofichwa pale Holiday Inn wakati ile timu ya Sudani ilijipanga kwenda kutoa $15000 kwa mwezi.
 
Mie namkumbuka kwa kurubuniwa na Yanga wakati anakamilisha taratibu zake pale Frankfurt (kama sijakosea) kwamba aje Tanzania acheze vs Simba pale CCM Kirumba. Na kweli lengo la Yanga lilifanikiwa kwa kushinda 2-0 dhidi ya Simba lakini Lunyamila bahati yake ya kucheza Ulaya ndio ikawa imeishia hapo. Sasa ni kubaki kukumbuka tu ile bahati. Hapa pia namkumbuka Mrisho Ngassa alivyofichwa pale Holiday Inn wakati ile timu ya Sudani ilijipanga kwenda kutoa $15000 kwa mwezi.
Ngasa nakumbuka hadi dili la Lov-ham Denmark jamanii??!!!!
 
Naskia amewahi funga goli 6 pekee yake. Ilikuwa mechi kati ya Kagera na Yanga
Ni baada ya kocha wa timu ya Taifa na Kagera sugar marehemu Zakaria Kinanda kudai haku mwitaLunyamila kwenye Timu ya Taifa kwakua ni mchezaji wa kawaida. Bahati mbaya klabu ya Kagera Sugar ilikua ikifundishwa na Kinanda ikakutana na Yanga Yenye Lunyamila pale shamba la bibi. Lunyamila alifanya balaa kubwa, katika ushindi wa Yanga wa 8-0, Lunya alitupia Sita.
 
Mie namkumbuka kwa kurubuniwa na Yanga wakati anakamilisha taratibu zake pale Frankfurt (kama sijakosea) kwamba aje Tanzania acheze vs Simba pale CCM Kirumba. Na kweli lengo la Yanga lilifanikiwa kwa kushinda 2-0 dhidi ya Simba lakini Lunyamila bahati yake ya kucheza Ulaya ndio ikawa imeishia hapo. Sasa ni kubaki kukumbuka tu ile bahati. Hapa pia namkumbuka Mrisho Ngassa alivyofichwa pale Holiday Inn wakati ile timu ya Sudani ilijipanga kwenda kutoa $15000 kwa mwezi.
yanga wanahiki kitabia chakuwarubuni wachezaji mfn. Tegete alitakiwa na timu nyingi za nnje wakambania hadi carer yake ikaishia Yanga


hata Msuva walitaka kumbania lkn and of the day club iliyumba kifedha na Difaa walitoa Dau kubwa ikabid Msuva aondoke bila hivyo angeondoka kama mchezaj huru na club isingepata kitu

Nakumbuka kipindi kile Manji ndo anakabilia na mashtaka kedekede...pesa za Msuva zulitusaidia sana kipindi kile viongozi wayanga walimpa baraka zote
 
Binafsi, nilifanikiwa kushiriki mashindano ya Umisseta kwa kanda ya Mashariki kwa mwaka 1990 na 1991 (au 1991 na 1992. Kumbukumbu imenitoka kidogo). Mashindano haya yalifanyika Zanzibar na Songea. Nilikuwa nacheza mchezo wa kikapu.
Nilivyomwona Zanzibar wakati anacheza, nilijua atakuwa nyota. Alikuwa mchezaji bora kuliko wote kwa asilimia kubwa. Nilijua ilikuwa ni swala la muda tu kabla hajatua kucheza kati ya Simba au Yanga (ningependa sana kama angesajiliwa Simba kwa sababu ni timu yangu lol).
Kwa kweli michezo ya Umisseta inabidi ifufuliwe mara moja. Kulikuwa na wachezaji wengi sana waliokuja kucheza timu mbalimbali za ligi ya daraja ya kwanza. Kwa kanda yetu ya Mashariki, nawakumbuka akina Peter Nkwera, kocha Banyai, etc. Walikuwepo wengine kwenye kanda zingine kama Edibily Lunyamila wa kanda ya Magharibi/Ziwa.
Kwenye mpira wa kikapu, walikuwepo wachezaji karibu wote wa kanda ya Mashariki tuliokuja kucheza vikosi vya Vijana (timu yangu) na Pazi. Nilikuwepo mimi, Patrick Nyembela, Evarist Mapunda, Peter Bulengelo, Eric Temba, Jenga Mapunda, Evarist Mapunda, Atiki Matata, Gaston na Sindila Assey, Kubwa, nk. Hio ni kanda ya Mashariki tu. Inakuonyesha jinsi vipaji vyingi vilivyopatikana.
Nikitoa mfano. Ninaona mfumo wa Umisetta ukitumiwa hapa Marekani ninapoishi. Kuna mashindano ya timu za shule kutoka msingi mpaka vyuoni (NCAA). Nikizungumzia mpira wa kikapu, ndio karibu wachezaji wote maarufu wa kikapu wanapopatikana kuanzia akina Michael Jordan (the GOAT as far as I 'm concerned), Kobe Bryant, Tim Duncan, Shaquille O'Neal, LeBron James, etc. Ndio maana Marekani anatawala mchezo wa kikapu duniani. Sio bahati. Ni mipango. Huwezi kupata timu nzuri ya taifa kama huna misingi mizuri ya kupata vipaji. Naweza kuelezea kwa undani zaidi lakini ngoja niishie hapa.
My 2 cents.
 
Mie namkumbuka kwa kurubuniwa na Yanga wakati anakamilisha taratibu zake pale Frankfurt (kama sijakosea) kwamba aje Tanzania acheze vs Simba pale CCM Kirumba. Na kweli lengo la Yanga lilifanikiwa kwa kushinda 2-0 dhidi ya Simba lakini Lunyamila bahati yake ya kucheza Ulaya ndio ikawa imeishia hapo. Sasa ni kubaki kukumbuka tu ile bahati. Hapa pia namkumbuka Mrisho Ngassa alivyofichwa pale Holiday Inn wakati ile timu ya Sudani ilijipanga kwenda kutoa $15000 kwa mwezi.
Itoshe kusema yanga ni UTOPOLO toka zamani! Cc Shadeeya
 
Ni baada ya kocha wa timu ya Taifa na Kagera sugar marehemu Zakaria Kinanda kudai haku mwitaLunyamila kwenye Timu ya Taifa kwakua ni mchezaji wa kawaida. Bahati mbaya klabu ya Kagera Sugar ilikua ikifundishwa na Kinanda ikakutana na Yanga Yenye Lunyamila pale shamba la bibi. Lunyamila alifanya balaa kubwa, katika ushindi wa Yanga wa 8-0, Lunya alitupia Sita.
Kagera stars ,haikuwa Kagera sugar
 
Ni baada ya kocha wa timu ya Taifa na Kagera sugar marehemu Zakaria Kinanda kudai haku mwitaLunyamila kwenye Timu ya Taifa kwakua ni mchezaji wa kawaida. Bahati mbaya klabu ya Kagera Sugar ilikua ikifundishwa na Kinanda ikakutana na Yanga Yenye Lunyamila pale shamba la bibi. Lunyamila alifanya balaa kubwa, katika ushindi wa Yanga wa 8-0, Lunya alitupia Sita.
Hiyo ina itwa double hart-trick, hatari sana

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom