Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,428
Mwaka jana, kuna mtafiti mmoja kutoka kitengo cha utafiti wa utekelezaji wa sera za nje za China alituuliza ' hivi Africa inataka nini China?' Akiwa na maana waafrica tungetamani kunufaikaje na diplomasia ya kiuchumi kati ya nchi zetu na China ambayo kwa sasa Inaongoza kwa uchumi,teknolojia na upana wa soko duniani. Ukweli ni kwamba hatukuwa na jibu lililonyooka kwamba ni nini hasa tunataka.
Sasa labda niwaulize wenzangu, hivi ni nini Tanzania tunataka kutoka China?
Ikumbukwe pamoja na mambo mengine, China inatekeleza mpango wake mkubwa wa 'Belt and Road' ambao unahusisha kujenga miundombinu kabambe kupitia baharini na nchi kavu kuiunganisha China na mabara mengine ikiwemo Africa ili kufikisha bidhaa zao sokoni kwa wepesi. Wakati huo huo Africa hakuna cha maana tunachouza China kwenye soko la watu 1.3 b.
Kwa sasa kuna hatua nzuri sana zinachukuliwa kuwashawishi Makampuni ya Kichina yaje kuwekeza hasa kwenye viwanda vizito vya electronics, magari na.k ambapo washakubali kufanya hiyo kupitia kampuni zao zaidi ya 800 ambapo tutapata manufaa mbalimbali makubwa kwa kiasi flani.
Pamoja na hiyo, tunashauri maeneo mengine ya kuimarisha ushirikiano kama ifuatavyo;-
1. Tuone namna ya kuwashawishi waweke mtaji na teknolojia kwenye kilimo, mfano cha soya halafu sisi tunachangia ardhi na nguvu, soko liko China. Kwa hiyo pamoja na watu wetu kupata ajira lakini pia tunakuza uchumi kwa namna hiyo. Kila mtu anatoa kile alichonacho kutengeneza faida.Ikumbukwe kwa sasa USA ndio huuza matani na matani ya Soya China na bado uhitaji ni mkubwa sana.
2. Tuwashawishi wawekeze mtaji kwenye ufugaji nyuki kwa kutoa vifaaa halafu watanzania wanafuga kwenye mapori yetu halafu asali tunauza China. Ikumbukwe tuna mapori ya kutosha na ufugaji nyuki hauharibu mazingira.
3. Tutulie tujiulize hivi tunataka nini kutoka China kwenye soko la watu 1.3 b, Kitovu cha teknolojia na uchumi duniani, kisha tuboreshe sera zetu za nje ipasavyo ili kuweza kunufaika zaidi na uhusiano wetu na hawa rafiki zetu.
Nimalizie kwa kuwauliza tena ndugu zangu, hivi tunataka nini kutoka China?
Sasa labda niwaulize wenzangu, hivi ni nini Tanzania tunataka kutoka China?
Ikumbukwe pamoja na mambo mengine, China inatekeleza mpango wake mkubwa wa 'Belt and Road' ambao unahusisha kujenga miundombinu kabambe kupitia baharini na nchi kavu kuiunganisha China na mabara mengine ikiwemo Africa ili kufikisha bidhaa zao sokoni kwa wepesi. Wakati huo huo Africa hakuna cha maana tunachouza China kwenye soko la watu 1.3 b.
Kwa sasa kuna hatua nzuri sana zinachukuliwa kuwashawishi Makampuni ya Kichina yaje kuwekeza hasa kwenye viwanda vizito vya electronics, magari na.k ambapo washakubali kufanya hiyo kupitia kampuni zao zaidi ya 800 ambapo tutapata manufaa mbalimbali makubwa kwa kiasi flani.
Pamoja na hiyo, tunashauri maeneo mengine ya kuimarisha ushirikiano kama ifuatavyo;-
1. Tuone namna ya kuwashawishi waweke mtaji na teknolojia kwenye kilimo, mfano cha soya halafu sisi tunachangia ardhi na nguvu, soko liko China. Kwa hiyo pamoja na watu wetu kupata ajira lakini pia tunakuza uchumi kwa namna hiyo. Kila mtu anatoa kile alichonacho kutengeneza faida.Ikumbukwe kwa sasa USA ndio huuza matani na matani ya Soya China na bado uhitaji ni mkubwa sana.
2. Tuwashawishi wawekeze mtaji kwenye ufugaji nyuki kwa kutoa vifaaa halafu watanzania wanafuga kwenye mapori yetu halafu asali tunauza China. Ikumbukwe tuna mapori ya kutosha na ufugaji nyuki hauharibu mazingira.
3. Tutulie tujiulize hivi tunataka nini kutoka China kwenye soko la watu 1.3 b, Kitovu cha teknolojia na uchumi duniani, kisha tuboreshe sera zetu za nje ipasavyo ili kuweza kunufaika zaidi na uhusiano wetu na hawa rafiki zetu.
Nimalizie kwa kuwauliza tena ndugu zangu, hivi tunataka nini kutoka China?