Eco Bank ukitaka kupata mkopo inakupasa utoe Rushwa kwa wahusika au kama ni gari wakufanyie Deal pa kununua

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Oct 31, 2014
5,321
11,386
Mwezi wa pili sasa mfanyakazi mwenzangu anahangaika na kupata mkopo wa gari bank ya eco. Hawa jamaa walimwambia mahitaji wanayotaka akatimiza ikiwa ni pamoja na kupitisha mshahara kwao.barua toka kwa mwajiri na mkataba.

Wakamwambia atafute gari ya kuanzia mwaka 2007 kuja juu na pia iwe kuanzia namba C au D. Mfanyakaz mwenzangu akafanikiwa kupata. Jamaa wakaanza kumzungusha.kwanza mhusika akadai anataka kadi original ya hiyo gari akae nayo kwa siku 3. Hapo nami nikashangaa why akae nayo siku tatu? Kwa nini asipewe copy kwanza akathibitishe TRA na Police maybe then siku ya mwisho aletewe kadi Original?

Jamaa walipokuja kuletewa kadi wakaanza tena kumzungusha mkopaji na jamaa mhusika wa kutoa huo mkopo akawa kama hataki mteja achukue gari hii ila ana mtu wake ambaye huwa nadhan wanafanya hiyo biashara naye anapata kamisheni.so akawa anamkwepa mteja.

Week iliyopita ndo ikaja onekana anayehusika na mkopo eti anaumwa so mchakato mzima umesimama mpaka akipona. Hii bank inakuwa na mambo ya kiswahili katika mazingira haya ya biashara ya ushindani mimi kuna bank nmepata mkopo within 3 days kila kitu kikawa tayar.

Jamaa anaonekana anataka either apewe rushwa au mteja akubali kununua gari toka kwa muuzaji anayemtaka yeye mfanyakazi wa bank nadhan mwishowe apate kamisheni yake. Huu si utaratibu mzuri kufanya kazi kihuni.

ECO BANK mtafukuza wateja.inawezekana msione kama hili lina impact kubwa lakini nawaambia habari hzi si nzur kwa wateja wenu na wanaowaza kuja kuwa wateja wenu.
 
TAFUTA KESHI MKUU MIKOPO INA TABU YAKE.LAZIMA UWE MVUMILIVU MNO NA DHARAU NA USUMBUFU WA WATOAJI
 
sijajua utaratibu wa hiyo benki... ila nachojua bank zinakopesha hela ila hazikupangii ukanunue wapi..

swali la kizushi.. gari unalotaka nunua ni la biashara au la kutembelea..

kama la kutembelea... achana nalo maana ualilipia na riba na mateso juu... maana unaonekana chanzo chako cha mapato sio kizuri
 
Thread imeandikwa kwa kiswahili lakini bado inaonekana hujaielewa. Kazi kubwa sana.

sijajua utaratibu wa hiyo benki... ila nachojua bank zinakopesha hela ila hazikupangii ukanunue wapi..

swali la kizushi.. gari unalotaka nunua ni la biashara au la kutembelea..

kama la kutembelea... achana nalo maana ualilipia na riba na mateso juu... maana unaonekana chanzo chako cha mapato sio kizuri
 
Kama mtu kaamua kukopa ameshafanya uamuzi na amejitathmini nadhan ushauri wako hauwez kumbadilisha mhusika. Kila mtu ana maamuzi na mipango yake. Inakopa serikal itakuwa mwananchi

TAFUTA KESHI MKUU MIKOPO INA TABU YAKE.LAZIMA UWE MVUMILIVU MNO NA DHARAU NA USUMBUFU WA WATOAJI
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom