Samuel Nyaki
Member
- Feb 23, 2007
- 9
- 0
haya maoni yanaonwa na viongozi wetu wa nchi hizi tatu? kama wanayaona ni vizuri lakini kama hawayaoni inabidi tutafute mbinu kwa vyovyote wayaone.
Rais Jakaya Kikwete amekiri kuwa matatizo yanayojitokeza katika mikataba mbalimbali ambayo serikali imeingia na wawekezaji, yanasababishwa na uwezo mdogo wa baadhi ya wataalamu wa kitanzania wanaoshiriki katika majadiliano ya mikataba hiyo.
Rais Kikwete aliiomba serikali ya Norway kuwapatia mafunzo na mbinu za kisayansi wataalamu hao zitakazowapa uwezo wa kujadiliana na wawekezaji kwa kuweka mbele maslahi ya taifa.
Alitoa ombi hilo juzi alipofanya mazungumzo na Waziri wa Maendeleo na Ushirikiano wa Norway, Bw. Erick Solhein, katika siku yake ya mwisho ya ziara rasmi ya kiserikali nchini hapa.
Alisema Tanzania inawahitaji wataalamu na wakufunzi kutoka Norway, kwa kuwa huko nyuma waliwahi kutoa msaada mkubwa sana wakati wa majadiliano ya mikataba, kiasi cha kuwafanya wakubwa katika taasisi fulani ya kimataifa ya fedha kutofurahiwa na umakini ulioonyeshwa kwa upande wa Tanzania.
`Nakumbuka tulipata mtaalamu mmoja mzuri sana kutoka kwenu, alitusaidia sana kiasi cha kuwaudhi wakubwa kwa wale waliokuwa upande wa mwekezaji, na walipoona wanazidiwa kete walimfanyia njama na kumwondoa. Tunawahitaji tena wataalamu kama yule waje kuwafundisha watu wetu,` alisisitiza Rais.
Alifafanua kuwa hivi sasa Tanzania inaendelea kufanya ugunduzi wa rasilimali nyingi zikiwamo za gesi asilia na madini, hali aliyosema kuwa umakini na utaalamu wa hali ya juu unahitajika ili hatimaye mikataba itakayohusu uendelezwaji wa rasilimali hizo ifanyike kwa umakini na kwa uangalifu mkubwa.
Norway kupitia waziri wake huyo imekubali kulifanyia kazi ombi hilo pamoja na lile la kuisaidia kiuwezo na vifaa Taasisi ya Kuzuia Rushwa (TAKURU).
Katika mazungumzo yao, Waziri huyo alimweleza Rais kwamba, Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa kupewa umuhimu wa pekee katika masuala ya misaada ya kimaendeleo kuliko nchi yoyote barani Afrika ukiacha Msumbiji.
Alisema Tanzania ni nchi iliyo karibu sana na Norway na kwamba uhusiano kati ya nchi hizo mbili na watu wake haujawahi kutetereka tangu ulipoanza wakati Tanzania ilipopata uhuru wake.
Bw. Erick Solhein alisema Umoja wa Kitaifa, utawala unaozingatia demokrasia na haki za binadamu, utamaduni wa viongozi kuachiana madaraka, maendeleo ya kiuchumi na kijamii, kunaifanya Tanzania kuwa nchi ya kupigiwa mfano Afrika.
Alisema Watanzania wanatakiwa kuuenzi Umoja wa Kitaifa ambao uliasisiwa na Baba wa Taifa, kwa kuwa una umuhimu mkubwa katika maendeleo yao na ya nchi yao.
Katika hatua nyingine akiwa hapa nchini pamoja na kukutana na kufanya mazungumzo na viongozi wakuu wa serikali na utawala wa wafanyabiashara, Rais Jakaya Kikwete pia alikutana na kufanya mazungumzo na Watanzania wanaoishi na kusoma hapa Norway.
Katika salamu zao kwa Rais, wanafunzi wa Kitanzania, walisema kuwa wanaunga mkono, uamuzi wa serikali wa kupitia upya majina ya wanafunzi waliopewa mikopo ili kubainisha wenye uhalali na wasio na uhalali wa kupata mikopo hiyo.
Wanafunzi hao walilalamikia tabia ya baadhi ya waajiri serikalini ya kutowapatia ruhusa wafanyakazi ambao wamepata ufadhili wa kwenda kusoma.
Aidha, walisema kuwa wafanyakazi hao hata pale wanaporejea baada ya kuhitimu mafunzo yao, hawatambuliwi wala kupandishwa vyeo.
Kwa upande wa Watanzania wanaoishi hapa, nao katika salamu zao kwa Rais zilizosomwa na mwakilishi wao Bw. Mafta Himid Yusuf, wao waliiomba serikali kuharakisha utoaji wa vitambulisho vya uraia, kwa kile walichosema kuwa vitambulisho hivyo ni muhimu sana katika ulinzi na usalama wa Watanzania na nchi yao.
Aidha, walipendekeza kuwa serikali itilie mkazo uendelezwaji wa matumizi ya lugha ya Kiswahili kama ambavyo mataifa mengine yanavyotoa kipaumbele kwa lugha zao za kitaifa.
Waliishauri pia serikali iwe makini katika mchakato wa uundwaji wa Shirikisho la Afrika Mashariki huku wakisisitiza wananchi waelimishwe kwa kina kuhusu mchakato huo.
Akijibu hoja hizo na nyingine, Rais alielezea kushangazwa na taarifa za kuwapo kwa watendaji serikalini wanaowazuia watumishi wao kwenda kusoma.
Daily News; Thursday,March 08, 2007 @00:05
RESIDENTS of Ilemela District in Mwanza City have called for close co-operation in trade and education before forming an East African federation, the committee collecting views on the federation has been told. One of residents, Ms Flora Lutasigwa, said that she was pessimistic with the process of fast-tracking the regional integration, arguing that there was still a long way for Tanzania, Kenya and Uganda to go before having such a federation.
"We need to co-operate in trade and education, not in the political arena," she said, explaining that the existing peace and tranquillity in Tanzania would greatly be jeopardised if the country agreed to join the regional federation.
The majority of the residents of the area were against the fast-tracking of and the East African federation altogether in doubt that their country would turn into a battlefield, just as it was the case with neighbouring countries of Rwanda and Burundi, whose applications to join the community was give a green light last year.
Another resident in the district, Bryson Nziga, said the tiny East African countries of Rwanda and Burundi were marred by endless civil wars which could easily spread into Tanzania. Mr Nziga also pointed out that Kenya and Uganda too were strongly marred by tribalism to the extent that people of different ethnic groups could not tolerate each other to the extent of they could hardly share an apartment.
With the exception of Tanzania, all other countries were constrained with arable land, he said, explaining that residents of Kenya and Uganda would flock into Tanzania to grab that expansive land available in the country. Another resident, Josiah Kagati, said Kenya and Uganda were well prepared for the federation as the majority of the people in those countries have good educational background compared to Tanzanians.
He said Kenyans were practising modern agriculture while the agricultural sector in Tanzania still relied on smallholder farmers using hand-hoes. Mr Kagati told the forum that Tanzanians would be the losers in the proposed federation as Kenyans would invest in large-scale farming and employ Tanzanians as casual labourers in their own motherland.
Ilemela residents say time not ripe for EA federation
PATI MAGUBIRA, Mwanza
Federation si nzuri kwa nchi yetu Tanzania.
1. Wakenya na Waganda wana elimu nzuri kushinda sisi.
Serikali yetu itafanya vibaya kama haitasikiliza maoni ya wananchi. Kama serikali pale baada ya Uhuru wetu ilikuwa na lengo la kuunda Federation basi ingewaandaa watanzania.
1.Serikali ingewaandaa watanzania kielimu. Hapa tungefanya Education system moja kwa Kenya, Uganda na Tanzania. Wengine sisi tumesoma Chuo Kikuu Cha Nairobi na tumeona tofauti ya elimu katika nchi zetu hizi mbili.