East African Federation (EAF) public Views

haya maoni yanaonwa na viongozi wetu wa nchi hizi tatu? kama wanayaona ni vizuri lakini kama hawayaoni inabidi tutafute mbinu kwa vyovyote wayaone.
 
Muungano wowote una faida na hasara. sasa kama ni kufikiria kuungana au kutoungana ama kama ni muungano wa aina gani mimi nafikiri sio jambo la kusema tupige kura au viongozi wa siasa waamue, bali jambo la kwanza ni kutafuta wataalamu wa uchumi, wa siasa na wajamii wachambue faida na hasara ili waone kama ni Muungano kuwepo je ni maeneo gani tuungane ili tupate faida. kama hakuna faida sioni haja ya muungano.
Katika Muungano Tunategemea kupata faida Kiuchumi, ama Kisiasa ama kijamii.

sasa nikiangalia Tanzania Kisiasa naona imepiga hatua kuliko hawa washirika anaotaka kuungana nao hivyo tunategemea kuvutwa nyuma kidogo na hawa wenzetu na sisi tutawavuta mbele kidogo

nikiangalia kijamii bado naona watanzania tumestaarika kuliko wenzetu maana ni mara chache kubaguana nikilinganisha na wenzetu.

Hivyo kama ni kufaidika ni katika nyanja ya kiuchumi tu tunaweza kutegemea faida ya huu muungano ila hapa changamoto ni je hivi kweli Tanzania itapiga hatua au itarudi nyuma.

Hapa mimi nikiangalia mazoea ya watanzania na wenzetu, nikiangalia tofauti za kiuchumi na wenzetu, nikiangalia mtizamo wa watanzania na wenzetu sioni mafanikio ya kiuchumi.

kwa tabia yetu ya kudharauriana na kusifu vitu vya nje hata kama havina ubora vya nje mfano leo hii ukitafuta msimamo kwa ubora wa vyuo vikuu duniani University of Dar es salaam inaongoza kwa east afrika ikivizidi mbali university of nairobi na Makerere ikiwa ya tatu, lakini ukimuuliza mtanzania leo hii kwa kujenga dhana tu yeye kichwani mwake atakuambia elimu ya kenya na uganda iko juu kuliko ya tanzania.
Watanzania bado wana dhana ya kuwa elimu ni kiingereza hivyo mtoto akisomea kenya au uganda akirudi anaongea kingereza wanasema elimu hiyo ni bora hata kama mtoto kimmarifa yuko nyuma. hatuwezi kuungana na kupata faida bila kuwakomboa watanzania kifikra kwanza.

leo hii uchumi wa wenzetu uko juu, eti tunaweka miaka mitano kuusawazisha, hivi hii miaka mitano imetolewa na wachumi wataalamu wenye ujuzi au wachumi wa vyeti au wanasiasa? sijaelewa bado. Tanzania tulikuwa tumenza kupiga kasi kiuchumi hivyo hofu yangu ni kasi hii kurudishwa nyuma na haya mambo ya muungano.

Tatizo kubwa kwa watanzania tumekuwa tukidhani mafanikio ni ulipewa cheo gani au ulianzisha nini! utamkuta mtu anajivuna amekuwa meneja wa kampuni fulani miaka kadhaa huku kampuni hiyo ilifirisika enzi zake za uongozi. mtu anajivuna kuanzisha kitu ambacho kuwepo kwake ni mzigo kwa wananchi
mimi nafikiri mafanikio sio cheo ulichopewa bali ni ulifanya nini ulipopewa cheo hicho, mafanikio sio ulianzisha nini bali ulichoanzisha kimesaidiaje kutatua shida za walengwa. Hivyo wanasiasa wanaofikiria kupata mafaniko kwa kuwekwa katika historia kuwa walianzisha umoja wa afrika mashariki wakumbuke iwapo umoja huo utaleta adha kwa watanzania watalaumiwa kwa adha hizo na hivyo wangeonekana mashujaa kwa kuukataa muungano usio na faida kwa watanzania.

Ushauri wangu kwa watanzania ni kwamba kama tunataka kupata maendeleo tuelekee afrika ya kati kwa nchi kama kongo, rwanda na burundi. hizi nchi zimekuwa na vurugu mda mrefu hivyo hawakuweza kuzalisha hivyo viwanda vinavyochipuka hapa nchini vitapata soko huko na hakuna mategemeo ya kupata soko katika afrika mashariki kwa majirani zetu bali wategemee bidhaa za ushindani kutoka huko, afrika ya kati wamevurugana mda mrefu hivyo kitaaluma wako nyuma tunaweza kupata ajira kwa watu wetu huko na hata watu watakaokuwa wakitoka huko kuja huku ni watu wa kuchapa kazi na kuzalisha sio kama nchi hizi tunazotaka kushirikiana nazo ambazo watakuja kuangalia "well paying jobs only"

Na vilevile napenda kuwashauri wanasiasa wajenge mazoea ya kuwatumia wataalamu wao wawe wasemaji kwenye majukwaa ila watumia wataalamu husika kuchambua mambo hayo kabla ya wao kuyavaria njuga kwenye majukwaa kama hawakuwa wakifanya hivyo.

Vile vile tuwaandae watu wetu na changamoto za miungano, tuwajenge kiushindani tuache kupeana au kulindana katika nyadhifa
 
MODERATOR USITOE HII TENA PLS.

Kikwete was quoted in the press in Norway begging them to send experts to train Tzs on how to read and prepare contracts. At this rate Tz tutafika hivi jamaani? And we are busy saying hatutaki EC.

Rais Jakaya Kikwete amekiri kuwa matatizo yanayojitokeza katika mikataba mbalimbali ambayo serikali imeingia na wawekezaji, yanasababishwa na uwezo mdogo wa baadhi ya wataalamu wa kitanzania wanaoshiriki katika majadiliano ya mikataba hiyo.

Rais Kikwete aliiomba serikali ya Norway kuwapatia mafunzo na mbinu za kisayansi wataalamu hao zitakazowapa uwezo wa kujadiliana na wawekezaji kwa kuweka mbele maslahi ya taifa.

Alitoa ombi hilo juzi alipofanya mazungumzo na Waziri wa Maendeleo na Ushirikiano wa Norway, Bw. Erick Solhein, katika siku yake ya mwisho ya ziara rasmi ya kiserikali nchini hapa.

Alisema Tanzania inawahitaji wataalamu na wakufunzi kutoka Norway, kwa kuwa huko nyuma waliwahi kutoa msaada mkubwa sana wakati wa majadiliano ya mikataba, kiasi cha kuwafanya wakubwa katika taasisi fulani ya kimataifa ya fedha kutofurahiwa na umakini ulioonyeshwa kwa upande wa Tanzania.

`Nakumbuka tulipata mtaalamu mmoja mzuri sana kutoka kwenu, alitusaidia sana kiasi cha kuwaudhi wakubwa kwa wale waliokuwa upande wa mwekezaji, na walipoona wanazidiwa kete walimfanyia njama na kumwondoa. Tunawahitaji tena wataalamu kama yule waje kuwafundisha watu wetu,` alisisitiza Rais.

Alifafanua kuwa hivi sasa Tanzania inaendelea kufanya ugunduzi wa rasilimali nyingi zikiwamo za gesi asilia na madini, hali aliyosema kuwa umakini na utaalamu wa hali ya juu unahitajika ili hatimaye mikataba itakayohusu uendelezwaji wa rasilimali hizo ifanyike kwa umakini na kwa uangalifu mkubwa.

Norway kupitia waziri wake huyo imekubali kulifanyia kazi ombi hilo pamoja na lile la kuisaidia kiuwezo na vifaa Taasisi ya Kuzuia Rushwa (TAKURU).

Katika mazungumzo yao, Waziri huyo alimweleza Rais kwamba, Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa kupewa umuhimu wa pekee katika masuala ya misaada ya kimaendeleo kuliko nchi yoyote barani Afrika ukiacha Msumbiji.

Alisema Tanzania ni nchi iliyo karibu sana na Norway na kwamba uhusiano kati ya nchi hizo mbili na watu wake haujawahi kutetereka tangu ulipoanza wakati Tanzania ilipopata uhuru wake.

Bw. Erick Solhein alisema Umoja wa Kitaifa, utawala unaozingatia demokrasia na haki za binadamu, utamaduni wa viongozi kuachiana madaraka, maendeleo ya kiuchumi na kijamii, kunaifanya Tanzania kuwa nchi ya kupigiwa mfano Afrika.

Alisema Watanzania wanatakiwa kuuenzi Umoja wa Kitaifa ambao uliasisiwa na Baba wa Taifa, kwa kuwa una umuhimu mkubwa katika maendeleo yao na ya nchi yao.

Katika hatua nyingine akiwa hapa nchini pamoja na kukutana na kufanya mazungumzo na viongozi wakuu wa serikali na utawala wa wafanyabiashara, Rais Jakaya Kikwete pia alikutana na kufanya mazungumzo na Watanzania wanaoishi na kusoma hapa Norway.

Katika salamu zao kwa Rais, wanafunzi wa Kitanzania, walisema kuwa wanaunga mkono, uamuzi wa serikali wa kupitia upya majina ya wanafunzi waliopewa mikopo ili kubainisha wenye uhalali na wasio na uhalali wa kupata mikopo hiyo.

Wanafunzi hao walilalamikia tabia ya baadhi ya waajiri serikalini ya kutowapatia ruhusa wafanyakazi ambao wamepata ufadhili wa kwenda kusoma.

Aidha, walisema kuwa wafanyakazi hao hata pale wanaporejea baada ya kuhitimu mafunzo yao, hawatambuliwi wala kupandishwa vyeo.

Kwa upande wa Watanzania wanaoishi hapa, nao katika salamu zao kwa Rais zilizosomwa na mwakilishi wao Bw. Mafta Himid Yusuf, wao waliiomba serikali kuharakisha utoaji wa vitambulisho vya uraia, kwa kile walichosema kuwa vitambulisho hivyo ni muhimu sana katika ulinzi na usalama wa Watanzania na nchi yao.

Aidha, walipendekeza kuwa serikali itilie mkazo uendelezwaji wa matumizi ya lugha ya Kiswahili kama ambavyo mataifa mengine yanavyotoa kipaumbele kwa lugha zao za kitaifa.

Waliishauri pia serikali iwe makini katika mchakato wa uundwaji wa Shirikisho la Afrika Mashariki huku wakisisitiza wananchi waelimishwe kwa kina kuhusu mchakato huo.

Akijibu hoja hizo na nyingine, Rais alielezea kushangazwa na taarifa za kuwapo kwa watendaji serikalini wanaowazuia watumishi wao kwenda kusoma.


Isome hapa: http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=2040

Ndio maana Moderator ALIIFUTA HUKU
 
PERSEVERANCE: Retired army sergeant Musa Salum, a World War Two veteran now aged 88, is given a ride by his grandson Hamad Said as he continues to follow up on his East African Community pension claims in downtown Dar es Salaam yesterday.

Source This Day (Tanzania)http://www.thisday.co.tz/
EAC01.jpg
 
Jamani,

Tanzania Kuna Kenya Commercial Bank. Imefunguliwa kabla ya hii jumuia kuundwa. Je Kuina benki gani ya kitanzania nje (kwa mfano), au kuna tawi gani la biashara kubwa ya kitanzania nje ya nchi ya Tanzania ?. Kwani kinachoizuia Tanzania au wafanya biashara wa Ki-tanzania kufanya hivyo ni kutokuwa na jumuia ?. Mbona wenzetu wanaweza hata kabla jumuia haijaundwa?

Lets be careful with our thinking. Jumuia haitaiogezea nchi ya Tanzania uwezo wowote kiuchumi kama fikara za nchi na za watanzania bado ni zile za ujamaa na kujitegemea na kutokuwa na ujasiriamali. Jumuia ya afrika mashariki haito wafundisha watanzani kuwa wajasiriamali. Ila itawawezesha wenzetu Wakenya na waganda ambao ni aggressive by nature and by virtual of their historical reason (Hasa wa Kenya) kutwaa nafasi zote za kiuchumi zilizo tanzania na ambazo watanzania wamezikalia. Jumuia hii itawapa haki hiyo.

Hapa nina maanisha kuwa Watanzania kwa hulka yetu yakitanzania hatupo tayari kwa hili. Tuta buruzwa vibaya vibaya. Inabidi serikali ione hili tatizo mapema ili iweze kulinda maslahi ya watanzania wake. Sio baadaye ije ijilaumu kama anavyosema JK sasa kuwa eti uwezo duni wa wataalamu wetu ndio umesababisha tanzania kuingia mikataba mibovu.

Mkataba ya jumuia ya afrika mashariki utakuwa mbovu sana tu kwa Watanzania. Hasa wakenya wata-kula nyama ya watanzania na wana uchu kweli kweli.

Regards

Venividivici

I came, I saw , I concurred.
 
Veni, vidi vici!!
Perfect latin phrase!
Kama Julius Ceaser alivyotamba mbele ya Roman Senate baada ya vita ya Zela "Battle of Zela"!
Inabidi viongozi wetu wafumbue 'majicho' na masikio yao ili wakenya na waganda wasije kujigamba.. VENI VIDI VICI!!!!!!!!!!!
 
Hatuwezi kuungana na Kenya na Uganda kwani matatizo yao ya ndani bado kitendawili,kasikazini mwa uganda uasi umetawala, Kenya kuna ukabila mwingi na ubaguzi.

mtanzania huwezi kupata kazi kenya na ukipata raia watakuua kama sio mkenya,nimebahatika kuomba kazi kule busia kenya kidongo ningeuawa na raia kwa kupola kazi zao.

Tutapata nini? Eti soko huria kwani sisi tutauza nini Kenya na Uganda au uhuria wa soko ni sisi kununua tu, jumuiya ilikufa wakenya wakapora kila kitu kwanza warudishe mali zetu walizopora ikiwamo viwanda.

wakenya si watu wa kuungana nao bora Msumbiji.
 
Ilemela residents say time not ripe for EA federation
PATI MAGUBIRA, Mwanza
Daily News; Thursday,March 08, 2007 @00:05

RESIDENTS of Ilemela District in Mwanza City have called for close co-operation in trade and education before forming an East African federation, the committee collecting views on the federation has been told. One of residents, Ms Flora Lutasigwa, said that she was pessimistic with the process of fast-tracking the regional integration, arguing that there was still a long way for Tanzania, Kenya and Uganda to go before having such a federation.

"We need to co-operate in trade and education, not in the political arena," she said, explaining that the existing peace and tranquillity in Tanzania would greatly be jeopardised if the country agreed to join the regional federation.

The majority of the residents of the area were against the fast-tracking of and the East African federation altogether in doubt that their country would turn into a battlefield, just as it was the case with neighbouring countries of Rwanda and Burundi, whose applications to join the community was give a green light last year.

Another resident in the district, Bryson Nziga, said the tiny East African countries of Rwanda and Burundi were marred by endless civil wars which could easily spread into Tanzania. Mr Nziga also pointed out that Kenya and Uganda too were strongly marred by tribalism to the extent that people of different ethnic groups could not tolerate each other to the extent of they could hardly share an apartment.

With the exception of Tanzania, all other countries were constrained with arable land, he said, explaining that residents of Kenya and Uganda would flock into Tanzania to grab that expansive land available in the country. Another resident, Josiah Kagati, said Kenya and Uganda were well prepared for the federation as the majority of the people in those countries have good educational background compared to Tanzanians.

He said Kenyans were practising modern agriculture while the agricultural sector in Tanzania still relied on smallholder farmers using hand-hoes. Mr Kagati told the forum that Tanzanians would be the losers in the proposed federation as Kenyans would invest in large-scale farming and employ Tanzanians as casual labourers in their own motherland.
 
Federation si nzuri kwa nchi yetu Tanzania.
1. Wakenya na Waganda wana elimu nzuri kushinda sisi.

2. Wakenya na Waganda wana uchumi mzuri kuliko Tanzania.

3. Fedha ya Tanzania sasa hivi huwezi ukaitumia Kenya wala Uganda na hivi sasa tuna Shirikisho la Afrika ya Mashariki.

4. Tanzania haina barabara madhubuti, haina reli madhubuti wala haina bandari za kisasa. Njia zetu mbovu na madaraja yetu mabovu na mvua ikinjesha kidogo tu basi nchi nzima iko hatiani.

5. Tanzania haina ndege za kujivunia ingawaje ina viwanja vingi vya ndege.

6. Watanzania ni watu wa amani, vita sisi hatuvijui, bali ni vile tu ambavyo tulilazimishwa na Iddi Amini wa Uganda. Waganda wana vita huko kwao kaskazini. Waburundi na Wanyaruwanda vita vyao vya kikatiti tumevisikia na matokeo yake mpaka sasa twayaona.Wakimbizi kutoka Rwanda na Burundi waetapakaa Tanzania.

7. Uhuru wetu, madini yetu,misitu yetu na gesi yetu, mbuga,nahari na maziwa ni mali ya Watanzania na vizazi vijavyo vya Tanzania.

Hatuna haja ya Federation yeyote si sasa hivi wala baada ya miaka 100 ijayo. Afadhali tufe kwa umasikini wetu na kuepuka kuwa watumwa milile sisi na vizazi vyetu kwa ajili ya manufaa ya Wanasiasa wachache.

Kama Tanzania itakuwa na Wanasiasa washupavu na wenye nia ya kuiendelaza nchi tunaweza kufanikiwa bila ya Federation yeyote. Madini yetu ya dhahabu,Nickel,Chuma, Makaa ya mawe pamoja na gesi ni silaha madhubuti katika mapambano ya kuondoa Umasikini Tanzania.

TUSIKUBALI KUFANYWA WATUMWA MILELE. MIKATABA YOYOTE INAWEZA KUFUTWA. MSITAFUTE KISINGIZIO CHA KUWA CHA KUTOKUWA NA WATAALAMU KWANI MLIKUWA NAO.
 
Kikwete we ni msanii
na usanii huu utatufikisha kubaya,lazima utambua amebeba roho za wtz milioni nyingi, ukiendeleza usanii utazidi kuangamiza wtz,
Tumekubali tz hakuna wataalamu wa kuingia mikataba ndio heko nakupa, tano JK sasa swali linakuja,umepata wapi????? hao wataalamu wanaosaiini huo mkataba unaoendelea wa EAF.

Huoni unafanya watu wazima wenye elimu zao watoto???na wasio jua kitu yani majuha? chonde chonde chonde JK acha usanii fanya kazi uliopewa na wanachi wako, tulikuchagua uiongonze Tanzania na ndivyo mkataba wetu ulivyo kati yako na sisi haya ya EAF unayatoa wapi?

Anyway cha muhimu umekiri kua kwa sasa hakuna watanzania wanaoweza kuingia mkataba wowote ukawa na manufaa kwa watanzania,hivyo hilo la EAF achana nalo mpaka pale Tanzania itakapopata wataalamu wanaoweza kuingia mikataba yenye manufaa kwa watanzania

Kama kweli unawapenda wtz achana nalo, kipimo ni kidogo tu angalia serikali mnavyoingia mikataba kienyeji enyeji hata nadhani kuliko yule babu yetu Chief Mangungo wa usovero angalia IPTL,RICHMONDS,hao walio kua TANESCO huko kwenye madini ,kama mikataba midogo na kiduchu mnooooooooo namna hii inawashinda je?mtaweza ya Tanzania mzima na wtz wote kwa pamoja????? hapo hakuna swali hakika hamuwezi .

RICHMOND mtu mmoja wawili wamechukua chao bila kuzalisha chochote na kuiuza kampuni na mmemshindwa je? hayo ma nchi yote mnayotaka kuungana nayo si ndio yataliza hadi paka wetu ndani?
Jamani sometimes mnatia aibu sana viongozi waliosoma na kuelimika mnafanya mambo afadhali ya kiongozi wa jadi akina Mirambo ,Mkwawa na wengine.

Wanaoshabikia EAF narudi kwenu niambieni hata mkataba mmoja ilioingia serikali na ukawa na mafanikio??? ?? niambieni hata kama kuna mkataba serikali imeiingia ikafanikiwa hata kama wa kuuza mbuzi sokoni niambieni tu??uwe wa kuuza maharangwe semeni tu??? mi naona serikali ilichofanikiwa ni kuwafanya wtz makondooo, mabwege na makubwa jinga hapo nitakiri huyo prof mzima anayekusanya mawazo inabidi tuhoji uelewa wake,ni uelewa wa u prof au la!!!!!!!

JK ,asiyejua kufa akachungulie kaburi
kulaleki walai wtz tunalichungulia kaburi
 
Hivi elimu ambayo Kenya na Uganda wanasifiwa ni ipi? Ya kuongea kiingereza?
 
Elimu wanaosifiwa ni kweli wanayo nayo si nyingine bali
yakubeba ajira zenu na mali ghafi zenu ,mmegawia makaburu na wazungu sasa ngoja mwape waganda na wakenya nao wabebe.

Unajua mambo haya ndio hua yanasababisha tafrani(vita)
wananchi wanasema hapana wewe mtu mmoja na ka group kadogo mnawalazimisha kujiunga hapo akitokea muhuni kuchochea vita ni rahisi mno.

Maana anajua wananchi hawataki sasa kwa rais anayetaka amani lazima awe makini sana na haya
 
Serikali yetu itafanya vibaya kama haitasikiliza maoni ya wananchi. Kama serikali pale baada ya Uhuru wetu ilikuwa na lengo la kuunda Federation basi ingewaandaa watanzania.

1.Serikali ingewaandaa watanzania kielimu. Hapa tungefanya Education system moja kwa Kenya, Uganda na Tanzania. Wengine sisi tumesoma Chuo Kikuu Cha Nairobi na tumeona tofauti ya elimu katika nchi zetu hizi mbili.

2.Kitu kinachofanya sasa hivi watanzania wapinge hiyo Federation ni kuona kwamba ile EAST AFRICAN COMMUNITY ilivunjika wakati Mzee J.K.Nyerere alipogombana na Iddi Amini. Wote walikuwa ni marais. Sasa ni kitu gani ambacho leo chasema marais wa nchi hizo amabazo zinataka hiyo Federation hawatakorofishana tena?

3.Tanzania tumelipa na kupata gharama kubwa sana kwa kuvunjika kwa East AFRICAN COMMUNITY.
4. Mikataba yetu ya AIR TANZANIA na South Africa Airways pia ni fundisho kwa serikali. Watu walinungunika lakini hawakusikilizwa mpaka makasa ulipotokea.

5. Kabla ya Uhuru tulikuwa na migodi ya Dhahabu(Sekenke Gold Mine) ni mfano mmoja na Almasi Mwadui. Mbona makaburu waliomiliki migodi hiyo ya dhahabu walitia maji mashimo yote hakafu wakakimbia South Africa?

6. Hivi leo makaburu hao hao wamerudi nchini na tumewapa benki zetu na madini yote ya dhahabu nchini. Lakini ule mgodi wa dhahabu wa Sekenke ambao mpaka sasa hauwezi kuchimbwa kwa sababu ya maji uko chini ya serikali(STAMICO).

NCHI YETU TUNAWEZA KUIJENGA WENYEWE KWA NGUVU ZETU NA BUSARA ZETU NA USHIRIKIANO WETU.

KAMA CHINA IMEWEZA KUFANYA HIVYO BILA YA SHIRIKISHO LOLOTE SEMBUSE TANZANIA NA MALI YOTE TULIYOKUWA NAYO SASA HIVI?
 
Serikali yetu itafanya vibaya kama haitasikiliza maoni ya wananchi. Kama serikali pale baada ya Uhuru wetu ilikuwa na lengo la kuunda Federation basi ingewaandaa watanzania.
1.Serikali ingewaandaa watanzania kielimu. Hapa tungefanya Education system moja kwa Kenya, Uganda na Tanzania. Wengine sisi tumesoma Chuo Kikuu Cha Nairobi na tumeona tofauti ya elimu katika nchi zetu hizi mbili.

Dr Khamisi umekezania sana kutueleza kuwa kuna tofauti kubwa ya kielimu, mbona hutuelezi hizo tofauti za elimu kati ya Kenya na Tanzania?

Pili, kama wewe umejua ubora wa elimu wa chuo kikuu cha Nairobi kwa kuwa umesoma huku, haya ya chuo kikuu cha Dar umeyajulia wapi na kwa vipi?

Pili, kwa mujibu wa vigezo vya kimataifa vya kupima ubora wa elimu ya juu, chuo kikuu cha dar es salaam kinaongoza katika afrika mashariki na hata kusini mwa ukanda wa Limpompo, sasa hiyo ya kuwa elimu ya Nairobi ni bora kuliko ya dar umeyatoa wapi?

Hebu tumia udaktari wako kutuweka sawa hapa kwa kutumia vigezo vya kisayansi zaidi kuliko hisia!
 
Ndugu sio kwamba tu nimesoma chuo kikuu cha Nairobi bali vyuo kadhaa ya Ulaya pia. Mimi mwenyewe nimewafundisha wanafunzi wa Tanzania ambao walisoma Makerere University na wengine ambao walitoka Chuo Kikuu Dar es Salaam na pia Nairobi.

Niliwafundisha kazi nilipokuwa Tanzania. Tafauti katika masomo kwenye vyuo vyetu vya Afrika Mashariki ipo, tena kubwa. Baada ya kuwafundisha wanafunzi hawa nilitowa mapendekezo yangu kwamba waende ngambo kwa masomo zaidi ya M.Sc.Baadhi yao walipelekwa na sasa weing wao ni Directors.
 
Ninavyoona ni kwamba tunajitahidi kukurupuka katika maamuzi yetu. Sidhani kwamba kweli kuna tafiti muhimu zote zinazotakiwa kufanyiwa kazi kama zimetekelezwa. Ninachoweza kuona sasa hivi ni kwamba viongozi wa ngazi za juu wameng'ang'ania kukubaliana kitu kisichoeleweka na kukaidi maoni yanayotolewa na wananchi.

Viongozi wa nchi nadhani wanachokiangalia sasa ni ile kuweka historia tu kwamba katika kipindi chake kuna suala alilifanya. Ninaomba tuache kutafuta historia, tuangalie ni nini tutafaidi na nini tutapoteza na tena tusizingatie kizazi hiki cha sasa tu, hebu tuangalie kizazi kijacho kinanufaika vipi na maamuzi yetu ya sasa.

Tunalingana vipi na Wakenya katika upande wa elimu, tunalingana vipi na Wakenya katika upande wa kiuchumi,Tunalingana vipi na Wakenya katika upande wa siasa, tunakubaliana vipi kuhusu utumiaji wa rasilimali tulizonazo, tumeweza kutatua migogoro ya majirani zetu kabla hatujawaalika au ndio tunaikaribisha katika sebule zetu(itikadi inatofautiana).

Naomba nieleweke, suala sio kulingana kiuchumi,siasa,elimu n.k. tumeshaona kuna tofauti katika pande hizo, tumeshafanya uchunguzi yakinifu tukajua tutawezaje kuhakikisha hatuendelei kupoteza na kunufaisha majirani zetu?

Naomba kutoa wito kwa wahusika, mimi kama Mtanzania hili suala naona tuna kurupuka, tunahitaji muda kuangalia. Nawaomba pia wahusika tukae macho kusikiliza ni nini wananchi wanakisema badala ya kuacha maoni yao yakielea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom