EA Radio: Maxence Melo (Mwanzilishi wa JamiiForums) anaongelea kuhusu watu kudhalilishwa mitandaoni

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,444
7,801
Namsikia mwanajamvi mwenzetu EA Radio akiwa na Zembwela, mtangazaji anaibua hoja ya mitandao kutumika kudhalilisha watu na kadhalika, seduce me inasindikiza kusubiri mjadala. Nitawajuza majadiliano..
======



Zembwela anaanza kwa kusema yeye ni mmoja wa mashabiki wa wake kwa maana ni mmoja wa vijana ambao wanathubutu, wanapenda na wanafanya. Zembela anauliza, nini kinasukuma watu kutumia mitandao tofauti na madhumuni hasa ya kupashana habari, kuelimishana!

Maxence: Nakushukuru hasa kwa kuonyesha hasira zako kwa yanayotokea, hata siku za nyuma nilisema, mimi sidhani kama kutengeneza sheria, kukimbilia kuzileta na kuanza kuzitekeleza haraka itaokoa kile tunachokiona.

Tunachokiona mitandaoni ndio jamii ya watanzania, mtu anapokuwa nyuma ya keyboard anapata uhuru wa kujipambanua, yeye ni nani haswa. Kama JamiiForums, malengo yetu makuu ni matatu ambayo ni kukujuza kinachojiri kwa namna yoyote, kukuunganisha na watu na kukuburudisha.

Wanaouza visu nadhani wanauza kwa ajili ya kukatia nyama lakini wapo wanaotumia kukatia shingo za watu, unaweza kuiona fimbo ukadhani kwa ajili ya kuulia nyoka lakini mtu akatumia kumpiga binadamu na kumuua.

Pia hii inatumika kwenye mitandao, imetengenezwa kwa nia njema ila watumiaji wanaweza wakatumia tofauti na tunavyotarajia, nilienda mikoani nikakutana na mteja wetu ambae anaitumia JamiiForums tofauti hata na sisi tulivyotarajia, hatukuwahi kufikiria watu wanatumia JamiiForums kwa mtindo huo.

Kwa hio najua hata wengine wanapoingia Facebook, kuna watu wanaingia kupunguzia stress zao, kuna wengine wanaingia kuwasiliana na rafiki zao, wengine wanaingia kwa ajili ya kuibia watu, wengine kwa ajili ya kuarifu watu na wengine hawajui nini kimewapeleka wakajikuta wamedumbukia mle.

Dhamira ya mtu ndio inayopelekea yanayotokea yatokee.

Hata ukitengeneza sheria nzuri kiasi gani lakini tuelewe lazima tuanzie kwenye misingi, tunakuja na vitu vinatokea vinaisha. Bahati mbaya tangu tumeingia kwenye utandawazi, hatuwezi kukwepa kinachotokea.

Tuna kizazi ambacho mtoto anamaliza darasa la saba, mtoto anapewa simu ina kila kitu, haina restriction ya aina yoyote. Mwaka 2009 mapinduzi yaliingia Tanzania, tulipata mkongo wa Taifa na mtandao ukawa available kwa watu wengi.

Nchi yetu ilifanya vyema kukubali utandawazi, wengi wanafanya vyema sema kuna watu wachache lakini wanaweza kupaza sauti.

Zaidi soma=Maxence Melo: Watanzania wengi waoga pia kuna taasisi zinaogopwa hazipewi changamoto mtandaoni
 
Sidhani kama tunaweza kulazimishana kutengeneza sheria za kijinga zaidi ili kufit ujinga wetu bali tutengeneze sheria za 'kielevu' ili nasi zituinue tuwe waelewa.
Mfano mdada anapost picha amelala na mwanamume (almost porn) na kesho yake anakuja mwanamume anakiri eti ni kweli na wamezaa pamoja. Hakuna hatua inayochukuliwa kwa sababu wanasema eti ni celebrity na ndio maisha yao lakini picha hiyo hiyo akiipost mwingine unasikia anafutwa na polisi au TCRA!
 
Ni bora atoe somo kwa serikali ya kidikteta inayojaribu kutunga sheria kandamizi ili kudhibiti uhuru wa kutoa maoni. Kila la kheri Mr. Maxence Melo.
 
Kama anayosema maxence kuhusu TCRA ni yakweli...bas Hiii sirikali uchwara ni ya kipuuzi kabisa... iko bize kila siku kutunga masheria ya kipuu.uuziiii ili kutubana raia...huu ni ujinga wa sirikali wa kiwango cha juu kabisa.....
Sirikali haina mikakati kabisa yaniii..shame
 
Maxence anaulizwa

Swali by zembwela-"Unaweza kuwasaidia polisi kuwakamata wenye makosa ya mitandaoNi"

Anajibu yeye hawezi kuwasaidia polisi kwasababu sio kazi yake,taratibu zinajulikana za kuwakamata wahalifu..

Jamaa yuko makini sana Maxence...aendelee hivyo Max maana humu tunawindwa sanaaa.

Malaika alishaesema anatamani mitandao ifutwe yooote..wafute Ile mingine huu watuachie
 
Max ashamaliza mahojiano, kesho tar 20/9/2017 kutakuwa na Dkt.Mitimingi ataelezea kuhusu kukamatwa wanamitandao kwa uonevu....
Viva max
 
Watu kama hawa wakina Maxence Melo Mubyazi nchi nyingine kama USA wanakuwa hazina ya nchi.

Lakini apa Africa hatutambui mchango wake katika Jamii
Mtu kama Bill Gates au JacMa wanaeshimika na serikali zao.

Na hapa Tanzania, mchango wa Maxence Melo Mubyazi ulitakiwa uheshimike kwa serikali. Kuweza kuwa na FORUM ya kuwaunganisha nchi tena kwa hapa Tanzania, sio swala la mchezo mchezo
 
atu kama hawa wakina Maxence Melo Mubyazi nchi nyingine kama USA wanakuwa hazina ya nchi. Lakini apa Africa atutambui mchango wake katika Jamii
Mtu kama Bill Gates au JacMa wanaeshimika na serikali zao. Na apa Tanzania, mchango wa Maxence Melo Mubyazi ulitakiwa ueshimike kwa serikali. Kuweza kuwa na FORUM ya kuwaunganisha nchi tena kwa apa Tanzania, sio swala la mchezo mchezo
Nchi haina Viongozi wenye maono, nimemsikiliza Max anasema nabii hakubaliki kwao ila kuna nchi nyingi tu amekuwa msaada
 
Maxence ni mtu makini...
Huyu mkuu Melo amifanya nifikirie kupendekeza uwepo wa mbunge wa jimbo la mitandaoni. Vyama vyetu ni vema wakalifikirua hilo. Kama kuna mbunge toka elimu ya juu,vyama vya wafanyakazi,vyuo vikuu,kwa nini asiwepo mwakilishi wa kundi hili kubwa sana la jamii,wanamtandao!?
Melo for Mtandaoni 2020..
 
Maxence Melo angekuwa USA au Europe angekuwa mtu mkubwa sana. Angefanya biashara kubwa sana. Lakini kwa apa Tanzania, hata makampuni kuingia biashara wanasua sua, Sema vijana tunatakiwa tuibebe na tuipiganie sana Jamii Forum iendelee kudumu, maana wengi umu wamepata fursa za ujasiliamali na michongo kibao
 
Huyu mkuu Melo amifanya nifikirie kupendekeza uwepo wa mbunge wa jimbo la mitandaoni. Vyama vyetu ni vema wakalifikirua hilo. Kama kuna mbunge toka elimu ya juu,vyama vya wafanyakazi,vyuo vikuu,kwa nini asiwepo mwakilishi wa kundi hili kubwa sana la jamii,wanamtandao!?
Melo for Mtandaoni 2020..
Nadhani Melo ni zaidi ya Mbunge mkuu!! I stand to be corrected
 
Back
Top Bottom