Dynamic Productivity; Tija na Maarifa

Kuna mjumbe mmoja kule nyuma amesema kuwa Mtanzania wa kima cha chini hawezi kumudu maisha.Ni kweli.Ila nabishana nae anaposema kuwa Marekani mtu wa kima cha chini anaefanya kazi kwa masaa 40 kwa wiki anayaweza maisha.Hapa nasema NO.
Ukiwa na masaa 40 kwa marekani huku ukilipwa dola 10 kwa saa,ina maana kwa wiki una $400 na kwa wiki una $1600 hapo ni bado hujatoa tax ambayo kwa namna yeyote ile huwezi kuikwepa.Baada ya hapo toa bili ya appartment say $700,gas say $100,Umeme na maji,simu,Chakula,bado Insurances kama za Afya,gari nk bado mkopo wa gari hujamaliza $800.HAKIKA HUTABAKI NA KITU CHOCHOTE MWEZI unaofuata

Majita:
Ni kweli kima cha chini sikuzote hakiwezi kutosheleza mahitaji. Lakini mimi nafikiri system ya utoaji mishahara pia inachangia. Tukitumia mfano wako, tutaona kwamba sio tu hiyo $400 inakuwa earned kila week, bali pia inalipwa kila week. Sasa basi, pamoja ya kwamba gross salary ya $1600 ni ndogo sana, lakini bado inakidhi mahitaji mengi kutokana na kukatwa vipande vipande kila week. Labda nijaribu njia nyingine, ukichukuwa watu wawili ambao wanatengeneza $1600 kila mmoja - mmoja analipwa $400 kila wiki na mwignine analipwa $1600 kila mwishoni mwa mwezi, ni yupi atakuwa na nafasi mzuri ya ku-take care bills zake on time? Ni rahisi kuigawanya $400 kwa 7, lakini ni kazi ngumu mno kuigawanya $1600 kwa 30... Afterall, money is such a brain damager...

Kuugawanya mshahara into multiple payments ni aina ya motivation. Wafanyakazi wanakuwa motivated zaidi wakati wa tarehe za paycheck just before and after, na kufa moyo pale wanapoona tarehe ya mshahara hashikiki kwa umbali.
 
Wakati tunaongelea kuporomoka kwa uchumi wa Dunia na kushuka kwa thamani ya shilingi, kuna hili nimeliona tena kutoka kwa Kikwete ambalo amelifanya kuwa ni shina la maendeleo la Taifa la Tanzania na hata jumuiya za kiuchumi.

Akihutubia mkutano mjini Kampala majuzi, Kikwete katoa kauli kuwa COMESA, SADC na EAC zijiunge na kuwa na mshikamano wa kiuchumi hata kisiasa.

Hilo ni sawa kabisa, linalonitatiza mimi ni kung'ang'ania kwa Kikwete kusema kuwa tuwe na soko huria (free market and free trade) na kuongeza kutegemea sekta binafsi.

Kikwete na hata Mkapa walijijenga kwa kudai kuwa maendeleo ya Tanzania yatatokana na Uwekezaji, Sekta Binafsi na Soko Huria. Hilo si dhambi, lakini ubaya wa Sera zao (Mkapa na Kikwete) ni kukosekana kwa msukumo kutoka Serikali yetu kuhakikisha kuwa Wananchi wa Tanzania wanakuwa washiriki wakubwa na wamiliki wa uchumi na si kukimbilia wageni au bidhaa za kuagiza.


Sasa hapa ndipo kilio changu cha kusema CCM adui wa maendeleo kinapokuja. Badala ya CCM kuhamasisha tija, juhudi na maarifa ili kuboresha uzalishaji mali ndani ya nchi na kupitia Wananchi wake, CCM imeonelea kuwa njia pekee ya Tanzania kufanikiwa ni kuingia katika soko huru na uwekezaji wa kutoka nje.

Namnukuu Kikwete kwenye hotuba yake ya Kampala
``A free trade area performs better with a customs union. I appeal to you to reflect the importance of coming together as one after this summit,`` he said.

He explained that good infrastructure served as a bridge to African countries’ development, adding that it was crucial for the regional blocs to decide on ways to make that possible through a fast implementation plan as agreed.

The president also commented on the raging international financial crisis, saying it was now especially difficult for African countries to get outside funding and therefore time for them to devise ways to remain steady and stable without depending too heavily on such assistance.

``We should encourage private sectors, foreign and local, to contribute to the efforts of improving the infrastructure,`` he said.

Anachosahau Kikwete pamoja na nia yake nzuri ni kuwa Tanzania bado haina uwezo wa ndani wa kuzalisha na kujitosheleza, hata zile bidhaa ambazo malighafi zake zinapatikana ndani ya nchi.

Tanzania ya leo ni mnunuzi mkubwa (consumer) na si mzalishaji (producer and supplier) na ndio maana tuna madeni makubwa na kukosekana kwa uwiano wa uuzaji na uagizaji wa bidhaa ambao umekimbilia kuifanya Tanzania ipoteze nguvu ya sarafu yake na hali ya maisha ya Watanzania kuendelea kuwa duni.

Tanzania ya leo haina mpango kabambe wa kuboresha Kilimo, Ufugaji au Uvuvi bila kutegemea Wageni wawekezaji waje kutuokoa. Sasa tutakuwaje na uwezo mzuri kiuchumi ikiwa Kenya, Uganda na Congo bila kusahau Malaysia, Thailand na India ndio watakuwa wakituuzia chakula huku wakulima wetu wakiwa hawana uwezo wa kulima na kujitosheleza au kulisha familia zao?

Ni mfumo gani huu wa Uchumi na kwa utajiri gani Tanzania inakimbilia kuimba kwa sauti kuu kuwa tuwe na Soko huru, huku haina uwezo wa kujitosheleza na inategemea misaada na kuaiza bidhaa?

Watanzania watafaidika nini ikiwa hakuna msukumo wowote wa kubadilisha mfumo wetu wa Uchumi na Uzalishaji kwa kuchochea Tija, Juhudi, Maarifa ili kuunda Taifa linalojitegemea na linalopambana na Umasikini?
 
Mchungaji kesho/leo ni jumapili;

Nayafuatilia mabandiko yako but i feel sorry for you. Sisi tunasoma but unapoteza muda kuandaa then unabandika pasipo kuleta any impact kwenye society yetu.

My suggestion ni kupigana juu kwa juu halafu 2010 tupime mafanikio. Kwa sababu nia ya akina EL, RA NK na kadhalika ya kuwepo kule juu ni kuangalia mfumo sasa wakiona unatoa fair play kwa kila mtu hilo hawaliangalii na wanalipiga vita kuanzia anayechapa mpaka anaesoma.

Kaka do not waste your good time, tupigane haya majangili yaondoke, then tujenge mfumo ulio na tija na fanaka. I will count myself on 2010. We should be SMART

Thanks
 
Mchungaji kesho/leo ni jumapili;

Nayafuatilia mabandiko yako but i feel sorry for you. Sisi tunasoma but unapoteza muda kuandaa then unabandika pasipo kuleta any impact kwenye society yetu.

My suggestion ni kupigana juu kwa juu halafu 2010 tupime mafanikio. Kwa sababu nia ya akina EL, RA NK na kadhalika ya kuwepo kule juu ni kuangalia mfumo sasa wakiona unatoa fair play kwa kila mtu hilo hawaliangalii na wanalipiga vita kuanzia anayechapa mpaka anaesoma.

Kaka do not waste your good time, tupigane haya majangili yaondoke, then tujenge mfumo ulio na tija na fanaka. I will count myself on 2010. We should be SMART

Thanks

Kichwangumu,

TUnaweza kuyafanya yote mawili, kupiga vita ufisadi na kujijenga upya kiuchumi bila kusubiri. Waswahili walisema "chelea chelea utakuta mwana si wako".

Ni lazima tuzungumzie yote na kuelimishana kuhusu yote.

Tukikazania kuongelea ufisadi na kuung'oa ufisadi huku tukisema tusubiri Ufisadi uonoke kwanza ndipo tuanze kuongeza tija, maarifa na juhudi na kujijenga uchumi, tutakuwa tunajidanganya na kujiumiza.

CCM hawataki Mtanzania awe na uwezo wa kujitegemea. Siku Mtanzania akiweza kujitegemea kwa kuwa na maarifa, juhudi, tija na uwezo wa kutosha kuzalisha kujitosheleza, siku hiyo CCM na Ufisadi vitaanguka, maana hapatakuwa na haja ya kudanganya watu wapokee khanga au fulana ili wapigie mtu kura.

Angalia kilio leo kuwa hali ya uchumi ni mbaya na bei za mazao na bidhaa zinaongezeka huku bei ya mafuta katika soko la duni imeshuka kwa karibu 35%!

Najiuliza kama mgeuko wa bei ya mafuta unatupa kaahueni sisi tulioko Marekani ambako uchumi ndio umeangamia vibaya, iweje Tanzania ambayo mambo hayajabadilika sana au kuathirika ishindwe kupata ahueni kwa kushuka kwa bei za mafuta?

Jee tulinunua mafuta kwa bei ya kudumu kwa miaka miwili ijayo (hedging) ndio maana mambo bado machungu? au ni janja ya CCM kuhakikisha kuwa Watanzania wanaumia kiuchumi ili waanze kulainika na kukubali TGakrima ikifika 2010?
 
Hili swala tunalichukulia dogo lakini ni kubwa sana, mkuu nashukuru kwa kuwakumbusha watanzania wajibu wao.

Nchi ni sawa na organisation nyingine yeyote hile, ni sawa na IPP ya mengi ni sawa na Quality group ya Manji. katika organisation kuna tatizo la organisation culture, hii ni muhimu kwa kushape organisation yeyote hile katika kutimiza malengo yake ambayo ni uzalishaji ambao una manufaa kwa wananchi wake.

Je Tanzania tuna culture gani ya uzalishaji?
Sio kwamba nina utani na watu pwani, ila nitawatumia kama mfano kila mtu alinganishe na kabila lake na kuona jinsi gani culture ya uzalishaji inavyohathiri maendeleo ya nchi.

Mzaramo akimka asubuhi anaingia shambani na kuchimba miogo yake miwili kutoka kwenye shina na anakata kipande cha shina na kukichimbia ardhini anarudi nyumbani kwake anapika mihogo yake na kunywa chai, akishiba anaingia kondeni na kupanda miguu mitano ya mpunga kama ni kipindi chake, kama sio kipindi chake haendi shambani kabiasa.

Je mtoto aliyezaliwa na mzaramo huyu atakua anajua kazi ni nini? hili lipo katika makabila yetu yote, machache waliojua umuhimu wa kazi ndio wana maendeleo kidogo, kwahiyo tumekuzwa bila kufundishwa kuwa kazi ni muhimu ndio maana baada ya uhuru nyerere aliwambia watanzania kuwa kazi ndio kipimo cha utu kwani watu waliacha kufanya kazi kabisa.

Ili watu wafanye kazi alikuja na philosophies za Azimio la iringa, siasa ni kilimo na kilimo cha kufa na kupona, hivi vilisaidia kuwasukuma watanzania kuwa na mwelekeo wa kufanya kazi.

Pamoja na kuwa malipo ya kazi za tanzania ni madogo lakini vilevile watu hawafanyi kazi kwa moyo wao wote, watu wanaofanya kazi zinazolipa kidogo utawakuta kwenye baa muda mrefu anaotakiwa kuwa kazini, tunachukulia kuwa maendeleo ni kuonekana huko baa na una pesa bila kujituma kutafuta pesa zaidi.

recently wafanyakazi wanakata tamaa zaidi na matukio yanayoendelea kujitokeza nchini, walimu wameamua kuendesha tuision zao baada ya kuona serikali haijali masirahi yao wakati huo huo mapesa ya serikali yanaishia mifukoni mwa wajanja wachache na hawachukuliwi hatua.

Hii inajenga nchi ya watu wanaoamini kuwa unaweza kuajiriwa na ukafanya kazi zako nyingine wakati wa muda wako wa kazi.

Juhudi zilizochukuliwa na mwalimu hazikuleta mabadiliko kwa kuwa kubadilisha culture ni kitu kinachoitaji uamzi wa watu wote walioko madarakani, kila mtu atimize wajibu wake, hata kwenye kazi za watu binafsi, kama hukuwa makini ukataka kuleta mabadiliko unaweza kujikuta unapata tabu sana.

katika mojawapo ya hotel zetu za kitalii aliletwa meneja Mhindi, akaamua kubadilisha culture ya watanzania kwa kuakikisha wanafanya kazi, what happened ni kuwa jamaa alitegeshewa madawa ya kulevya na kuitiwa polisi, baada ya uchunguzi wakagundua kuwa alikuwa innocent.

Always binadamu anataka kubakia kama alivyo siku zote.

Kwanini wenzetu wanaweza kufanya kazi kwa kujituma bila kusimamiwa?

Hili haliji kama swala la historia kama wazungunzaji wengine walivyosema, wala sio swala la siasa ili linatokana na watanzania wengi kutopenda mabadiliko katika kila kitu wanachokifanya.

Kwenye siasa wanasema bora zimwi likujualo, kazini tunatafuta visingizio wakati ukweli ni kuwa tunaofia mabadiliko yatakuja na nini, wenzetu hawaogopi mabadiliko, wanaona mabadiliko kama challange ambayo wanaikumbatia.

Leo hii ukimwambia mtanzania anayenyayaswa na mwajiri ahache kazi atafute kwingine hawezi kukuibali, tunahitaji kufanya mabadiliko kila wakati tusijione kuwa tulichonacho kinatutosha, hii ndio chachu pekee ya kumtuma mtu yeyote kufanya kazi.

Na sababu nyingine ni kutokuwa na malengo, mtu anafanya kazi hajua anatakiwa kutimiza nini kwenye sehemu yake ya kazi, viongozi wa makampuni wanahitaji kuakikisha kila mfanyakazi anapandaa malengo yake mwenyewe na anyatimiza.

Reward system yetu perhaps nayo inahitaji kuangaliwa, haingii akilini kwa mwezi mtu anakuwa na siku mpaka 10 ambazo hajafika kazini na hakuna wa kumuhuliza, kila siku anaumwa kwanini wasimwachishe kazi kwa kigezo cha afya.
 
Kichwangumu,

TUnaweza kuyafanya yote mawili, kupiga vita ufisadi na kujijenga upya kiuchumi bila kusubiri. Waswahili walisema "chelea chelea utakuta mwana si wako".

Ni lazima tuzungumzie yote na kuelimishana kuhusu yote.

Tukikazania kuongelea ufisadi na kuung'oa ufisadi huku tukisema tusubiri Ufisadi uonoke kwanza ndipo tuanze kuongeza tija, maarifa na juhudi na kujijenga uchumi, tutakuwa tunajidanganya na kujiumiza.

CCM hawataki Mtanzania awe na uwezo wa kujitegemea. Siku Mtanzania akiweza kujitegemea kwa kuwa na maarifa, juhudi, tija na uwezo wa kutosha kuzalisha kujitosheleza, siku hiyo CCM na Ufisadi vitaanguka, maana hapatakuwa na haja ya kudanganya watu wapokee khanga au fulana ili wapigie mtu kura.

Angalia kilio leo kuwa hali ya uchumi ni mbaya na bei za mazao na bidhaa zinaongezeka huku bei ya mafuta katika soko la duni imeshuka kwa karibu 35%!

Najiuliza kama mgeuko wa bei ya mafuta unatupa kaahueni sisi tulioko Marekani ambako uchumi ndio umeangamia vibaya, iweje Tanzania ambayo mambo hayajabadilika sana au kuathirika ishindwe kupata ahueni kwa kushuka kwa bei za mafuta?

Jee tulinunua mafuta kwa bei ya kudumu kwa miaka miwili ijayo (hedging) ndio maana mambo bado machungu? au ni janja ya CCM kuhakikisha kuwa Watanzania wanaumia kiuchumi ili waanze kulainika na kukubali TGakrima ikifika 2010?

Rev Kishoka;

CCM is well established kimaovu hili nahisi unakubaliana na mimi that why uhuni wote huu upo. Hakuna mwenye upendo hata mmoja mana nafasi kwao ni kwa kupeana as if nchi hii ni mali yao.

Hakuna mfanyabiashara hata wa mchele ambaye hana mahusiano na CCM. CCM ni chama cha majambazi. Kuna bar moja pale Mbezi beach ni maarufu kwa kuchoma nyama. najua jina ila sitaji. Kuna mama alikuwa anasikitika sana wakati uchaguzi unakaribia anasema yani kila uchaguzi lazima watoe pesa. Nikamuuliza mama unalipa kodi akasema acha tu.......Hata hawa wafanyabisahara wa mafuta na kila kitu wanaconnection na CCM. CCM ndo wanawafundisha kutolipa kodi ila hio ten% waje wachukue wakati wa chaguzi. Hata huu wa tarime nahisi kuwa wafanyabiashara wamechangishwa baba kama hutaki wanakuuitia TRA na ukiangalia kuna kosa kubwa kwa mfano mimi mara chache sana nikirefuel gari naomba receipt sasa TRA unapeleka kodi gani hapa? Je, kwa nini CCM wasitumie kama fimbo???

My suggestion: Afadhali kuwapa elimu kwanza watu wajue kuwa politics ni sehemu yao na ndio ina determine future plan zao. But watanzania wangapi wanasoma MAKALA za akina Mwanakijiji, Ngurumo, Bagenda na kadhalika? HAKUNA. Nilipo mimi i used to buy This Day, Kulikoni, T/Daima, Mwananchi na Mwanahalisi. Mtu akiona anakuomba asome, habari ya siasa anakwambia mimi sio mwanasiasa geuza nisome michezo.

Mkapa kwenye ile term ya kwanza nilikwa namwelewa ila alizidiwa kete nahisi na mkewe mana siamini kama madudu ya leo yana baraka za benjamin. nasubiri kesi hata moja iitishwe huyu Ana ataumbuka. This is my feelings but hii nchi inatakiwa mtu mwingine tofauti kabisa na CCM ( I would recommend you, though sikujui sana but when i went through your bandikos... mh) apewe ili miaka 3 ya kwana ni mchaka mchaka ambapo wengi watakusifu na baada ya muda nchi yenye neema itakuwa inanukia. Najua second term utashinda kwa simple majority but not kimbunga lakini then after nchi itanyoooka.

Asante
 
Leo jioni nilikuwa nakiangalia kipindi cha 60 minutes katika moja ya studio kubwa za Televisheni hapa Marekani. Kulikuwa na habari mbili zilizonigusa na kunikumbusha JF na majadiliano tunayokuwa nayo.

Hadithi ya kwanza ilikuwa ni kuhusu Bilionea T.Boone Pickens ambaye ana mradi mkubwa ambao ameuanzisha na anataka Serikali ya Marekani iingie kwa nguvu zote. Yeye Pickens ana hekari karibu elfu 70 na anajenga mapangaboi ya umeme wa upepo. Hadi sasa kajenga mapangaboi 2500 na yana uwezo mkubwa sana wa kutoa umeme kwa nyumba zidi ya milioni mbili.

Kilichonigusa kuhusu Pickens si hili la umeme wa nguvu za upepo tuu ambao utaondoa utegemezi wa mafuta na kulinda mazingira, bali ni maisha yake ya utotoni.

Pickens alianza kujifunza kazi na misingi ya kufanya biashara na kujipatia pesa akiwa mtoto mdogo. Kazi yake ya kwanza kama walivyo watoto wengi Marekani ambao ni chini ya miaka 16, ilikuwa ni kusambaza magazeti mtaani asubuhi na mapema. Alianza kwa kuwa na nyumba takribani 28, lakini kwa kuwa alikuwa anahitaji pesa zaidi kwa matumizi aliyokuwa akiyajua yeye pamoja na kuwa Wazazi wake walikuwa na uwezo, alimwendea meneja anayewasimamia na kuomba aongezewe nyumba na kuchukua ruti za wenzake. Nyumba alizokuwa akisambaza magazeti zikaongezeka kutoka 28 mpaka 156 kwa kutaka ushindani zaidi, na hili alilifanya akiwa na miaka 12!

Sasa kawaida ya hapa Marekani baada ya kuuza magazeti na kusaidia wazazi au jirani iwe ni kukata majani au kuosha magari, watoto wakifikisha umri wa miaka 16, huweza kuajiriwa kwenye migahawa na huanza kulipwa ujira karibu kima cha chini na hufanya hivi wakiwa mwaka wa pili au wa tatu sekondari.

Wakienda vyuoni, huendelea na kazi zao za McDonald, Kantini za shule, usafishaji wa majengo ya shule, maktaba na wengine huajiriwa katika maofisi ya waalimu, viwandani, maofisini, na nyumba za kulea wagonjwa.

Pesa wanazozipata ni kwa matumizi yao binafsi na kwa wale walio na nidhamu, huanza kuweka akiba iwe ni savings au hisa!

Wakimaliza masomo, badala ya kukimbilia kutaka kazi za mishahara mikubwa, huanza kazi za kawaida, iwe ni ukarani, ufundi au nyinginezo na huko matunda ya kazi zao hujionyesha na hivyo kupandishwa vyeo na kuongezewa mishahara.

Sasa kumsikia Pickens akielezea alipoanzia kujifunza kazi na ushindani wa kibiashara, nikaona ni jinsi gani sisi tulivyokusa bahati ya kuwa na elimu ya kujipatia pesa kwa kufanya kazi zaidi ya kuwasaidia wazazi iwe ni ng'ombe wa maziwa, mchicha au vijijini ambapo pato la mauzo lilikuwa ni kuongezea kipato cha familia kujikimu.

Pickens: My Energy Plan Is The "Only Plan", Tells 60 Minutes Wind Power, Solar Energy And Domestic Natural Gas Are The Only Choices To End Country's Oil Addiction - CBS News

Lakini cha msingi si suala la kulipwa pesa, bali ni kujifunza kufanya kazi kwa kujituma na si kusukumwa.

Hadithi ya pili ilikuwa ni kuhusu jamaa anaitwa Carr, ambaye alivumbua voice mail na anatumia utajiri wake kusaidia sehemu ya Gorongosa katika jimbo la Sofala nchini Msumbiji.

Kilichoniamsha si utu wa huyu Mzungu pekee kusaidia kurudisha utalii na kuboresha maisha ya hawa ndugu bali ni baadhi ya takwimu zilizotajwa kwenye hichi kipindi.

Mwaka 1992, Msumbiji ilikuwa ndiyo nchi masikini duniani kuliko nyingine zozote. Hii ilitokana si kuwa koloni la Ureno tuu, bali ni ile vita kati ya Serikali ya FRELIMO na waliokuwa "magaidi" wa RENAMO. Zaidi ongezea Malaria na Ukimwi!

Sasa nikajiuliza, iweje Msumbiji, kama Rwanda, Burundi na Congo ambazo wamesota kwa vita na mauaji, leo wameanza kuwasha indiketa kuiacha Tanzania kwenye vumbi?

Kwa mujibu wa Carr, sehemu za vijiji vya Msumbiji vinahitaji zaidi ya zahanati 750. Yeye ameshajenga moja kwa kutumia dola za Marekani laki mbili.

Anachokifanya kikubwa ni kufufua ile mbuga ya wanyama ya Gorongosa.

One Man's Plan To Save A Natural Treasure, U.S. Entrepreneur Is Trying To Help Mozambicans By Reviving Gorongosa National Park - CBS News

Nikajiuza, hivyo basi kama Msumbiji inahitaji zahanati 750 za vijijini ili watu wapate huduma za afya, Tanzania tutahitaji zahanati 1500!

Mahesabu ya haraka yakaniambia kuwa 1500 x 200000 = 300, 000, 000. Hivyo kwa kujenga zahanati nzuri za vijijini 1500 na vifaa vya msingi ikiwa ni pamoja na kuwekea umeme wa jua na visima vya maji tunahitaji takribani kiasi cha dola za Marekani US $400,000,000.00

Sasa ukichukua pesa za misafara ya Kikwete, EPA, Richmond, Ndege, Radar na ufisadi mwingine, si tungeweza kusambaza huduma za afya vijijini hivyo kuanza kupiga vita maradhi ili tuwe na watu walio na afya wenye uwezo wa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa?

Huyu huyu Carr kajenga shule moja kwa US $ 100,000.00 ambayo sina uhakika kuwa ni ya msingi au sekondari, lakini inatumia madarasa kutoa elimu ya watu wazima!

Pamoja na kuwa hoja hii ni kuhusu kufanya kazi, pia mipango ya maendeleo na matumizi ya pesa kwa manufaa yanaingiliana, na ndio maana hizo hadithi mbili zikanikuna na kuonelea nizisimulie hapa jamvini!
 
Rev Kishoka;

CCM is well established kimaovu hili nahisi unakubaliana na mimi that why uhuni wote huu upo. Hakuna mwenye upendo hata mmoja mana nafasi kwao ni kwa kupeana as if nchi hii ni mali yao.

Hakuna mfanyabiashara hata wa mchele ambaye hana mahusiano na CCM. CCM ni chama cha majambazi. Kuna bar moja pale Mbezi beach ni maarufu kwa kuchoma nyama. najua jina ila sitaji. Kuna mama alikuwa anasikitika sana wakati uchaguzi unakaribia anasema yani kila uchaguzi lazima watoe pesa. Nikamuuliza mama unalipa kodi akasema acha tu.......Hata hawa wafanyabisahara wa mafuta na kila kitu wanaconnection na CCM. CCM ndo wanawafundisha kutolipa kodi ila hio ten% waje wachukue wakati wa chaguzi. Hata huu wa tarime nahisi kuwa wafanyabiashara wamechangishwa baba kama hutaki wanakuuitia TRA na ukiangalia kuna kosa kubwa kwa mfano mimi mara chache sana nikirefuel gari naomba receipt sasa TRA unapeleka kodi gani hapa? Je, kwa nini CCM wasitumie kama fimbo???

My suggestion: Afadhali kuwapa elimu kwanza watu wajue kuwa politics ni sehemu yao na ndio ina determine future plan zao. But watanzania wangapi wanasoma MAKALA za akina Mwanakijiji, Ngurumo, Bagenda na kadhalika? HAKUNA. Nilipo mimi i used to buy This Day, Kulikoni, T/Daima, Mwananchi na Mwanahalisi. Mtu akiona anakuomba asome, habari ya siasa anakwambia mimi sio mwanasiasa geuza nisome michezo.

Mkapa kwenye ile term ya kwanza nilikwa namwelewa ila alizidiwa kete nahisi na mkewe mana siamini kama madudu ya leo yana baraka za benjamin. nasubiri kesi hata moja iitishwe huyu Ana ataumbuka. This is my feelings but hii nchi inatakiwa mtu mwingine tofauti kabisa na CCM ( I would recommend you, though sikujui sana but when i went through your bandikos... mh) apewe ili miaka 3 ya kwana ni mchaka mchaka ambapo wengi watakusifu na baada ya muda nchi yenye neema itakuwa inanukia. Najua second term utashinda kwa simple majority but not kimbunga lakini then after nchi itanyoooka.

Asante

Kichwangumu,

Tulishafundishwa siasa, tukakomaa, lakini ni masikini, iweje turudie tena somo la siasa ili tuanze kuwa mahiri na wazalishaji bora?

What has Siasa have to do with Productivity?
 
Could Tanzania be creative and create its own driven economic structure in addition to a culture of productivity?
 
Tumejifunza nini sasa tukizingatia msongamano wa magari Dar umeongezeka na umeme bado si wa uhakika Tanzania?
 
Back
Top Bottom