Dvc (af) sua: Hili la geti linatuumiza.

Tonge

JF-Expert Member
May 7, 2010
695
12
Kwa watanzania wengi madaraka yamekuwa ulevi, mtu akipata madaraka basi kazi yake ni kujiona yuko juuuuuuuu juuuuuuuuu kabisaaa kuliko wengine matokeo yake ni kuwanyanyasa wengine, mfano ni pale mkuu (ADMIN and FINANCE) kuamua kufunga geti la kuingia main campus kwa muda mrefu kisha kuwalazimisha watu wenye magari kupita njia mbaya ambazo kutwa magari hasa madogo huumia au kuharibika na wengine wamepata ajali, ni miezi kadhaa sasa (3) geti kuu linafanyiwa matengenezo je ni la IKULU au Versity? na watu huteseka, hivi kutengeneza deviasion karibu na hilO geti ambayo ni rahisi na salama ingekuaje au kwa kuwa anatumia VX V8? hapati hii adha?. Hayo madaraka yana mwisho ndugu yangu. Mjirekebishe na ulevi huu wa madaraka viongozi manaopewa dhamana ya kuongoza wenzenu.

Wana JF nimelisema hili kama mpita njia kwenye hiki chuo, kwani limenikera sana na limewakera wengi kama mtu ataona si jema basi anisamehe ila hapa JF ndio mahala pangu pa kutoa madukuduku yangu sina pengine kwani nafasi hio sijapewa.Natumaini meseji sent.
 
Huyu Prof.Peleka ni mjeuri sana ndo maana mpaka uzeeni hajaolewa kwa ajili ya upunguwani wake..ananitia kichefuchefu mpaka basi nikikumbuka alivokuwa nanipa below pale VET.
 
Huyu Prof.Peleka ni mjeuri sana ndo maana mpaka uzeeni hajaolewa kwa ajili ya upunguwani wake..ananitia kichefuchefu mpaka basi nikikumbuka alivokuwa nanipa below pale VET.

Ishu ni geti, hizo below ni uzembe wako wa kusoma au brain yako iko slow, ila kuhusu geti naifahamu hiyo adha kama mkaazi wa Morogoro, tayari imekuwa kero kwa wengi.
 
Ninamengi ya kuchangia juu ya adha hii na nyingine nyingi. Sitoi mchango wangu bcos ujumbe wangu hauwezi kuwafikia kwa kuwa ni mambumbumbu wa IT: viongozi wa SUA hawawezi ku-acess electronic based info: wasaidizi wao hawawezi kuwaambia bcos wanaogopwa kama miunguwatu. Ndo maana SUA kilakitu na ovyo na duni.
 
Eeeeh jamani hebu wacheni kuwasema hao Maprofesa wenu. Kama mumeshindwa kupata grade nzuri kutokana na kuchakachua vyeti vyenu vya A level basi mulidhani hapo chuoni mutapita kirahisi? Pale ni kitabu cha sayansi na siyo ngwini.

Eti sasa maprofesa hawawezi kuaccess electronic data wao ni mambumbumbu, jamani wanacommunicate vipi na maprofesa wenzao huko nje na kimataifa? Musijione nyinyi ndiyo munajua sana kwa kuwa tu munaweza kuandika ujumbe kwenye jamii forum. Someni na nyinyi mufikie huo uprofesa kama ni rahisi.

Ama hilo la gate labda fedha hazijapatikana kumalizia hiyo kazi. Fedha zote mwaka huu zimekwenda kwenye uchaguzi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom