...wewe acha acha uongo KOKU ni kifupi cha jina KOKULEBA AU KOKUBANZA AU KOKUGONZA Hakuna birth certificate iliyoandika KOKU kama ulivyosema,inakuaje jina hakulitumia liandikwe kwenye birth cert. na litofautiane na majina ya vyeti vyake vya shule? huyu mwanasheria arudi darasani hajui kitu atamsababishia kifungo huyo mtoto
nahisi unahasira fulani sasa uwongo hapo ukowapi? nikatika kufupisha tu jina, always majina ya Koku yanaendelea lakini nilikuwa namaanisha Padri/Mchungaji hawezi kubatiza mtoto jina la kokutona au Kokubelwa au Kokusima pasipo jina lingine la Kikristo au ulitaka nitaje kwa urefu? hope ulinielewa. Mbona anaitwa Lulu ndio limezoeleka wakati kwenye Birth cert hana? Sio wote wanapenda kutumia majina yao yote cheti kinaonyesha majina mawili lakini unajikuta unatumia jina moja ila baadhi ya ndugu zako wakaribu au katika ukuaji wako wanalifahamu jina hilo. Kama anamakosa atafungwa, acha sheria ifuate mkondo wake. Sio mwanasheria ndio atamsababishia kifungo kwa ajili ya jina?