Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,390
- 31,338
MIJADALA MINGINE
SAKATA LA MAWAZIRI
Sehemu ya I
Waziri wa mali asili na utalii mh Kagesheki amejiuzulu kufuatia tuhuma za Operesheni ya Tokomeza.
Operseheni ililenga kukomesha vitendo vya ujangili vya kuua wanyama kwa njia haramu
Waziri amejiuzulu kwa kuwajibikaji kutokana na matatizo yaliyotokea wizara anayoongoza.
Mh Kagasheki amekuwa mstari wa mbele kupambana na mjangili na kumuomba Rais msaada ili kulinda rasilimali ya taifa ambayo imepungua kwa kiasi cha kutisha.
Mh Kagasheki amekumbuna na kesi zinazohusu meno ya tembo mara nyingi.
Hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kufuatilia kubainika kwa ujangili huo.
Meli zimekamatwa Hong Kong na Zanzibar,wamiliki ni Watanzania wengine wakiwa na nyadhifa za juu.
Tatizo la hujuma za rasilimali za taifa halikuanza leo.
Tunakumbuka kukamatwa wanyama wakisafirishwa hai katika uwanja wa ndege wa KIA.
Ndege ya kuwachukua ilikuwa ya kijeshi na kwa tartibu za kimataifa na hata za kitaifa ni lazima kungekuwepo na taarifa ya ndege kutua na hasa ya kijeshi.
Licha ya kelele nyingi kuhusu hujuma zinazoendelea hakuna kiongozi aliyesimama kuliongelea achilia mbali kuchukua dhama kama aliyochukua Kagasheki.
Tunakumbuka kuhusu uvunaji na usafirishaji wa magogo kutoka katika misitu.
Hakuna aliyewahi kuwajibika kutokana na hilo. Na pia tunakumbuka faru chini ya ulinzi mkali kuuawa.
Faru waliosimamiwa na mh rais kurudishwa nchini
Hiyo ni mifano michache sana kuonyesha chanzo na upana wa tatizo.
Yote hayo yakitokea serikali imekuwa ikipanga bajeti kwa vikosi vifuatavyo(Rejea ripoti ya bunge 2.2.1)
Askari wa kuzuia ujangili (KDU)
Askari wa Wanyapori (TANAPA)
Askari wa Misitu (TSF)
Wakati huo huo kukiwa na idara ya usalama wa taifa (TISS) na jeshi la Polisi
Mawazri, ,manaibu mawaziri, makatibu wakuu na wakurugenzi wa taasisi hizo pamoja na zile zinazoingiliana huteuliwa na mh rais kwa kusaidiana na wasaidizi wake na vyombo alivyopewa kikazi.
Mheshimiwa rais alitangaza kupeleka jeshi kupambana na majangili yaliyoonekana kuzidi nguvu vikosi katika taasisi na wizara hizo. Mhe rais akarudia kauli yake bungeni akisema yapo matatizo yaliyojitokeza yanayohitaji marekebisho wakati wa operessheni hata hivyo ilifanikiwa.
Ni wazi serikali ikiongozwa na Rais na Waziri mkuu walipanga na kusimamia opersheni hiyo.
Ni dhahiri kuwa mtandao wa ujangili ni mpana ambao serikali iliufahamu na haikuweza kuushughulikia[Rejea taarifa ya bunge {6.2: XIV, XVII, XVIII,} {7.0: III,VIII,]
Taarifa inaonyesha waziri Kagasheki hakuhusishwa kama kiongozi wa wizara [7.0: II]
Ni wazi kuwa mtandao wa ujangili uliingia katika serikali (infiltrate) kiasia cha kuweza kupata hata siri za opereshini na hivyo waziri aliwekwa pembeni. [7:IX)
Hivyo kufeli kwa Opereshini chanzo chake ni kutokana na kuingiliwa na viongozi wa serikali na siasa ambao kamati haikuwataja waliotoa maagizo ya operesheni isiguse viongozi wa kisiasa wa ngazi yoyote.(Taarifa ya bunge [7.0: IX]
Na pia kuwatenga viongozi wa Mikoa na Wilaya ulikuwa ni mpango maalumu wa kuhakikisha kuwa mtandao unalindwa kutoka ngazi za juu na kuzuia kelele kutoka eneo lingine.
Duru za siasa tunampongeza waziri Kagasheki kwa uamuzi wake wa kuwajibika na kujiondoa katika kazi ambayo ugumu wake si kupambana na majangili tu bali wanasiasa na viongozi wa serikali ambao ni sehemu ya mtandao au ni wanufaika wa mafao yatokanyo na ujangili kisiasa au kimasilahi.
Mawaziri watatu waenguliwa
Tunaendelea sehemu ya II
https://www.jamiiforums.com/great-t...iasa-hotuba-ya-jk-mwisho-wa-mwaka-2013-a.html
KIFO CHA MANDELA NA YALIYOTOKEA
https://www.jamiiforums.com/newthread.php?do=newthread&f=11
SAKATA LA MAWAZIRI KUFUKUZWA NA KUJIUZLU
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/572764-duru-za-siasa-sakata-la-mwaziri.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...pecial-mgogoro-kambi-ya-upinzani-chadema.html
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/308989-duru-za-siasa-matukio.html
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/167157-duru-za-siasa-mgongano-wa-mawazo.html
SAKATA LA MAWAZIRI
Sehemu ya I
Waziri wa mali asili na utalii mh Kagesheki amejiuzulu kufuatia tuhuma za Operesheni ya Tokomeza.
Operseheni ililenga kukomesha vitendo vya ujangili vya kuua wanyama kwa njia haramu
Waziri amejiuzulu kwa kuwajibikaji kutokana na matatizo yaliyotokea wizara anayoongoza.
Mh Kagasheki amekuwa mstari wa mbele kupambana na mjangili na kumuomba Rais msaada ili kulinda rasilimali ya taifa ambayo imepungua kwa kiasi cha kutisha.
Mh Kagasheki amekumbuna na kesi zinazohusu meno ya tembo mara nyingi.
Hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kufuatilia kubainika kwa ujangili huo.
Meli zimekamatwa Hong Kong na Zanzibar,wamiliki ni Watanzania wengine wakiwa na nyadhifa za juu.
Tatizo la hujuma za rasilimali za taifa halikuanza leo.
Tunakumbuka kukamatwa wanyama wakisafirishwa hai katika uwanja wa ndege wa KIA.
Ndege ya kuwachukua ilikuwa ya kijeshi na kwa tartibu za kimataifa na hata za kitaifa ni lazima kungekuwepo na taarifa ya ndege kutua na hasa ya kijeshi.
Licha ya kelele nyingi kuhusu hujuma zinazoendelea hakuna kiongozi aliyesimama kuliongelea achilia mbali kuchukua dhama kama aliyochukua Kagasheki.
Tunakumbuka kuhusu uvunaji na usafirishaji wa magogo kutoka katika misitu.
Hakuna aliyewahi kuwajibika kutokana na hilo. Na pia tunakumbuka faru chini ya ulinzi mkali kuuawa.
Faru waliosimamiwa na mh rais kurudishwa nchini
Hiyo ni mifano michache sana kuonyesha chanzo na upana wa tatizo.
Yote hayo yakitokea serikali imekuwa ikipanga bajeti kwa vikosi vifuatavyo(Rejea ripoti ya bunge 2.2.1)
Askari wa kuzuia ujangili (KDU)
Askari wa Wanyapori (TANAPA)
Askari wa Misitu (TSF)
Wakati huo huo kukiwa na idara ya usalama wa taifa (TISS) na jeshi la Polisi
Mawazri, ,manaibu mawaziri, makatibu wakuu na wakurugenzi wa taasisi hizo pamoja na zile zinazoingiliana huteuliwa na mh rais kwa kusaidiana na wasaidizi wake na vyombo alivyopewa kikazi.
Mheshimiwa rais alitangaza kupeleka jeshi kupambana na majangili yaliyoonekana kuzidi nguvu vikosi katika taasisi na wizara hizo. Mhe rais akarudia kauli yake bungeni akisema yapo matatizo yaliyojitokeza yanayohitaji marekebisho wakati wa operessheni hata hivyo ilifanikiwa.
Ni wazi serikali ikiongozwa na Rais na Waziri mkuu walipanga na kusimamia opersheni hiyo.
Ni dhahiri kuwa mtandao wa ujangili ni mpana ambao serikali iliufahamu na haikuweza kuushughulikia[Rejea taarifa ya bunge {6.2: XIV, XVII, XVIII,} {7.0: III,VIII,]
Taarifa inaonyesha waziri Kagasheki hakuhusishwa kama kiongozi wa wizara [7.0: II]
Ni wazi kuwa mtandao wa ujangili uliingia katika serikali (infiltrate) kiasia cha kuweza kupata hata siri za opereshini na hivyo waziri aliwekwa pembeni. [7:IX)
Hivyo kufeli kwa Opereshini chanzo chake ni kutokana na kuingiliwa na viongozi wa serikali na siasa ambao kamati haikuwataja waliotoa maagizo ya operesheni isiguse viongozi wa kisiasa wa ngazi yoyote.(Taarifa ya bunge [7.0: IX]
Na pia kuwatenga viongozi wa Mikoa na Wilaya ulikuwa ni mpango maalumu wa kuhakikisha kuwa mtandao unalindwa kutoka ngazi za juu na kuzuia kelele kutoka eneo lingine.
Duru za siasa tunampongeza waziri Kagasheki kwa uamuzi wake wa kuwajibika na kujiondoa katika kazi ambayo ugumu wake si kupambana na majangili tu bali wanasiasa na viongozi wa serikali ambao ni sehemu ya mtandao au ni wanufaika wa mafao yatokanyo na ujangili kisiasa au kimasilahi.
Mawaziri watatu waenguliwa
Tunaendelea sehemu ya II