Duru za Siasa: Marekani (U.S) Chini ya Donald J. Trump

Katika mazingira haya ya covid19 kampeni za uchaguzi zitafanyika vipi? Kutakuwa na mikutano ya hadhara? Kutakuwa na midahalo baina yao?
Mwalimu hili limekuwa suala lenye utata kidogo.
Kwa wagombea , Trump anaonekana kutojali sana suala la Corona kwasababu angependa kwenye base yake awajaze upepo wa habari za kutunga.

Anajua wazi kabisa na alishawahi kusema ''base'' yake inamsikiliza
Huko vijijini ndiko kabisa huwaambii kitu chochote hasa ukizingatia ndiko 'ubaguzi' ulipobobea

Pamoja na hayo , Joe Biden anamtishia sana hasa kumega sehemu ya wapiga kura wa vijijini.
Kuna independents ambao wengi wameondoka kwa Trump kutokana na chaos ya utawala wake

Juzi kulikuwa na ruling kuhusu Obama care na suala la birth control. Washauri wa Trump hawataki kurudisha Obamacare katika mjadala, ni kitu kinachoonekana kuwa maarufu kwasasa kuliko miaka 4 iliyopita.
Kitendo cha Trump kutumia DOJ kumega Obamacare nacho kinamweka mahali pagumu, hana mbadala wake

Kuhusu uchumi nako hali si nzuri. Unemployment ipo 14% kiwango kikubwa tangu depression post WWII
Kwa hili kauli za Trump zitamgharimu kwasababu zinaeleza kutokuwa makinini na Corona na kufika ilipo ambapo Wamarekani 30 milioni wamepoteza ajira zao.

Kampeni zitafanyika kwa mikutano?
Ni suala la muda na ikifika July tutaweza kupata uelekeo.

Kuhusu kura, state zimeanza kufuata mfumo wa kupiga kura kwa njia ya Posta
Trump hataki kabisa upiga huo wa kura

Kukataa kwake ni kwasababu Republicans kwa kutumia ''Gerrymandering na vote suppression'' walifanikiwa

Mfano, waliweka vituo vya kura mbali hasa kwenye maeneo ya Democrats.
Walichelesha kufungua vituo vya kura na wengi kutoweza kupiga kwa wakati
Kubwa zaidi walilazimisha kuwa na ID wakijua hata Raia hasa weusi wengine hawana

Trump hataki kusikia hilo na sasa anatumia DOJ kutaka kuzuia upigaji kura wa namna hiyo.
 
Mwalimu hili limekuwa suala lenye utata kidogo.
Kwa wagombea , Trump anaonekana kutojali sana suala la Corona kwasababu angependa kwenye base yake awajaze upepo wa habari za kutunga.

Anajua wazi kabisa na alishawahi kusema ''base'' yake inamsikiliza
Huko vijijini ndiko kabisa huwaambii kitu chochote hasa ukizingatia ndiko 'ubaguzi' ulipobobea

Pamoja na hayo , Joe Biden anamtishia sana hasa kumega sehemu ya wapiga kura wa vijijini.
Kuna independents ambao wengi wameondoka kwa Trump kutokana na chaos ya utawala wake

Juzi kulikuwa na ruling kuhusu Obama care na suala la birth control. Washauri wa Trump hawataki kurudisha Obamacare katika mjadala, ni kitu kinachoonekana kuwa maarufu kwasasa kuliko miaka 4 iliyopita.
Kitendo cha Trump kutumia DOJ kumega Obamacare nacho kinamweka mahali pagumu, hana mbadala wake

Kuhusu uchumi nako hali si nzuri. Unemployment ipo 14% kiwango kikubwa tangu depression post WWII
Kwa hili kauli za Trump zitamgharimu kwasababu zinaeleza kutokuwa makinini na Corona na kufika ilipo ambapo Wamarekani 30 milioni wamepoteza ajira zao.

Kampeni zitafanyika kwa mikutano?
Ni suala la muda na ikifika July tutaweza kupata uelekeo.

Kuhusu kura, state zimeanza kufuata mfumo wa kupiga kura kwa njia ya Posta
Trump hataki kabisa upiga huo wa kura

Kukataa kwake ni kwasababu Republicans kwa kutumia ''Gerrymandering na vote suppression'' walifanikiwa

Mfano, waliweka vituo vya kura mbali hasa kwenye maeneo ya Democrats.
Walichelesha kufungua vituo vya kura na wengi kutoweza kupiga kwa wakati
Kubwa zaidi walilazimisha kuwa na ID wakijua hata Raia hasa weusi wengine hawana

Trump hataki kusikia hilo na sasa anatumia DOJ kutaka kuzuia upigaji kura wa namna hiyo.
Trump ni janga kwa demokrasi na maendeleo ya Marekani. Kweli aliyezowea vya kunyonga, vya kuchinja haviwezi kabisa. Jamaa alizowea mambo ya mkatomkato, sasa amejikuta katika mazingira yanayohitaji afanye kazi kweli na ameshindwa, amekua ni mtu wa blah-blah na kulaumu watu wengine tu. Alipokuta uchumi wa Obama unaendelea akajichukulia sifa zote kama kweli ndiye aliyeukuza wakati uchumi ulikuwa unaendelea na ile kasi ya Obama. Sasa Uchumi umeporomoka sijui kama ataujenga tena; wao wanadhani mwarobaini wa uchumi ni tax-cut tu; kumbe sivyo. Wakati janga linaanza China, alitakiwa aanze mikakati ya kujikinga nchini kama ambavyo Obama alivyoanza kujenga mikakati ya Ebola wakati bado iko Afrika na ile Avian Flu ilipokuwa bado ingali iko China. Jamaa kwa vile hakutaka mambo ya Obama, alipofika madarakani akavuruga programs zote zilizoachwa na Obama ndiyo maana janga hili limemkuta hana maandaliizi yoyote kwani ile ofisi ya maandalizi ya magonjwa ya milipuko aliyoacha Obama ilikuwa imefungwa, na hivyo serikali yake ikawa haijui la kufanya. Nikijaribu kuangalia, ameilaumu sana China, amemlaumu sana Obama, amewalaumu sana Democrats, amelaumu sana madaktari na manesi wasiokubaliana na approach zake, amewalaumu sana magavana wasiokubaliana na approach zake, amewalaumu waandishi wa habari wanaposema ukweli ambao haumfurahishi, amewalaumu sana wataalamu wanaosema wazi kuwa approach yake ni mbovu. Amebakiza kulaumu wanyama wa porini na miti tu.
 
Marekani siyo Sanctuary Nation, tulidanganywa. US ni suffocating/chocking Nation..... Kumuua Mwafrika kwa goti huku amefungwa mikono nyuma Huko Marekani imetondelea uongo sasa tuna jua kuwa Marekani haina cha kufundisha juu ya haki za binadamu na demokrasia!!!
 
Marekani siyo Sanctuary Nation, tulidanganywa. US ni suffocating/chocking Nation..... Kumuua Mwafrika kwa goti huku amefungwa mikono nyuma Huko Marekani imetondelea uongo sasa tuna jua kuwa Marekani haina cha kufundisha juu ya haki za binadamu na demokrasia!!!
TUJITEGEMEE, kweli uko vizuri kichwani...yaani huoni kabisa matokeo ya kitendo cha kinyama kama hicho nchini Marekani! Je hapa kwetu polisi kuua raia ni hukhsa. Nani alimfahamu huyo George Floyd kabla ya unyama huu uliofanywa na polisi? Lakini leo jina lake linafahamika karibu kila pembe ya dunia kwa sababu Marekani watu huwajibishwa kwa matendo yao bila kujali wana wadhifa gani katika jamii.

Hebu fikiria kama polisi wangefanya unyama huo kwa mwandishi mashuhuri kama marehemu Mwangosi, huo moto nakuhakikishia usingezimika. Maanddamano yanayoendelea sasa hivi yanahusu pia kutokamatwa kwa polisi wengine watatu walioshuhudia kitendo hicho cha kinyama bila kuchukua hatua yoyote kukizuia. Hiyo ndio hali halisi huko Sanctuary Nation, The United States of America!

Na kwa ufahamisho tu, ikitokea polisi wakamuua mtu mwingine katika hayo maandamano, hicho kitendo kitakuwa sawa na kumwaga petroli kwenye moto. Jamani sisi tuendelee kuchezea tu maisha ya Watanzania hapa nyumbani kwetu, huko Marekani ni habari nyingine. Wako baadhi ya Watanzania eti wanashangaa kuwaona waandamanaji kutinga Ikulu na Rais kufichwa, ingekuwa hapa Bongo sijui...!
 
Ha ha haaaa!!!

Mag3, Sanctuary Country gani hii Rais wa US atoa hukumu yeye badala ya mahakama!? Ni article gani hii kwenye katiba ya US inayompa nguvu zote hizo?
,.,.,.,.,.

“You’ve got to arrest people, you have to track people, you have to put them in jail for 10 years and you’ll never see this stuff again,” he added. “We have all the resources – it’s not like we don’t have the resources. So, I don’t know what you’re doing.”

Trump tells governors to ‘DOMINATE’ rioters in scathing phone call
.,.,, ,.,.,
Hata hivyo niliwahi kusema Trump ataiangusha US pole pole kuliko ambavyo Clinton, H. angeiangush kama angekuwa Urais.
 
“You’ve got to arrest people, you have to track people, you have to put them in jail for 10 years and you’ll never see this stuff again,” he added. “We have all the resources – it’s not like we don’t have the resources. So, I don’t know what you’re doing.”

Je umesikia Majibu aliyopewa na hao Magavana? Baada ya wenzake kuhangaika juani, yeye anataka kula kivulini. Kumbuka kwamba katika ukoo wake wote tangu baba yake, ukoo wake pamoja na watoto wake hakuna hata moja aliwahi kuingia jeshini kuitetea Marekani. Yeye si tu ni opportunist, ni tapeli. Acha tu aendelee kulikoroga, iko siku inakuja atalazimika kulinywa na hiyo siku haiko mbali.

Wamarekani si makondoo kama Wabongo na kwa ufahamisho tu Wamarekani wamepitia nyakati ngumu kuzidi hata hii lakini walishinda. Uhuru walio nao waliumwagia damu na kamwe huwezi kuwalinganisha na vitu hivi vya kijinga. Naomba nikuulize TUJITEGEMEE, hivi kwa uelewa wako Wamarekani hasa ni watu gani?

Mkuu wa Polisi kamwambia hivi, "If you can't be constructive, keep your mouth shut!"
 
Mag3 ahsante , japo unajua pa kuanzia, cant make head or tail.

Jana kuna Police 2 wametimuliwa kwa ku 'taser' mtu na kutumia excessive force
Familia iliweka 'private coroner'' majibu yametoka na yatakuwa 'admissible'
Rais Trump anawaomba magavana 'wa activate' national guard katika state zao.Nguvu zake zina mipaka
Rais Trump ana haki ya kutumia first ammendment kutoa maoni, lakini, hayawe zi kuathiri Polisi au Mahakama
Juzi Trump , Melania na Baron walikuwa 'bunker'' wenye nchi walikuwa nje ya kasri jeupe (WH)
Media zinaleta habari za matukio 'live''

Sasa geuza shilingi upande wa pili!
 
Nyerere alituachia masomo mengi sana; lakini leo ninataka niongelee moja ambalo ni relevant kwenye utawala wa Trump. Nyerere alisema "Ukweli una tabia ya kulipiza kisasisi usipoheshimiwa" Mwalimu alisema Ukiona jiwe halafu wewe ukapinga kuwa hilo siyo jiwe na ukaamua kuonyesha hivyo kwa kulipiga teke, utaumia!" Hayo yalikuwa ni maneno ya Nyerere, kwa wale ambao hawajui Nyerere ni nani wanaweza kuyasoma kwenye kijitabu kifupi alichoandika mwanazni mwa mwaka sabini au sabini na moja kikiwa kinaiwa "Tujisahihishe"

Trump huwa hajui kuheshimu ukweli, na sasa utamlipizia kisasi.
 
Walio nje ya Marekani hushabikia siasa za huko kama vile Simba vs Yanga!
Ni watanzania tu, tena eti wanashabikia Trump. Nchi nyingi sasa hivi zinaidharau Marekani kwa sababu ya Trump, heshima yote iliyojengwa na Obama kwa miaka minane ilifutika ndani ya wiki moja tu ya utawala wa Trump, lakini watanzania wengi huwa nawasoma hapa wanavomshabikia. Sijui ni kwa sababu ya kutokumjua au kwa vile wanasikia eti ni tajiri sana.
 
Ni watanzania tu, tena eti wanashabikia Trump. Nchi nyingi sasa hivi zinaidharau Marekani kwa sababu ya Trump, heshima yote iliyojengwa na Obama kwa miaka minane ilifutika ndani ya wiki moja tu ya utawala wa Trump, lakini watanzania wengi huwa nawasoma hapa wanavomshabikia. Sijui ni kwa sababu ya kutokumjua au kwa vile wanasikia eti ni tajiri sana.

Mamilioni ya Wamarekani walimpigia kura Trump. Ndiye Mheshimiwa Rais wa nchi ya Marekani. Kama ambavyo Simba na Yanga zina 50%-50% washabiki, ndivyo na vyama vikuu vya Marekani. Ushabiki hauhitaji kuwa na tafakuri. Ni mapendeleo tu. Kwa hiyo wengine watampenda Trump. Wengine watamnanga Trump. Tafuta bisi hapo ulipo ufurahie senema ya mtifuano wa vyama na wagombea wao huko Marekani. Usichukulie siriaz sana. Kwa watazamaji haiwezekani kubadili matokeo ya uwanjani.
 
Mamilioni ya Wamarekani walimpigia kura Trump. Ndiye Mheshimiwa Rais wa nchi ya Marekani. Kama ambavyo Simba na Yanga zina 50%-50% washabiki, ndivyo na vyama vikuu vya Marekani. Ushabiki hauhitaji kuwa na tafakuri. Ni mapendeleo tu. Kwa hiyo wengine watampenda Trump. Wengine watamnanga Trump. Tafuta bisi hapo ulipo ufurahie senema ya mtifuano wa vyama na wagombea wao huko Marekani. Usichukulie siriaz sana. Kwa watazamaji haiwezekani kubadili matokeo ya uwanjani.
Usikwepe post yako niliyojibu; ulizungumzia walioko nje ya marekani, siyo wamarekani wenyewe au wapiga kura wa marekani. Ninajua kuwa Marekani imegawanyika kiitikadi 47%:47%:6% kwa hiyo hata kwa wamamerakani wenyewe huwezi kusema wengi wanamshabikia hata kama haibadilishi matokeo lakini siyo warrant ya kujenerealize kuwa wengi wanamshabikia. Honestly!
 
Walio nje ya Marekani hushabikia siasa za huko kama vile Simba vs Yanga!
Kwa ufahamisho tu...siasa ya Marekani inashabikiwa duniani kote kwa sababu taifa la Marekani ni taifa la dunia. Hakuna sehemu yoyote duniani utampata mtu ambaye hana uhusiano wowote ule na Mmarekani. Marekani utawakuta Wasukuma, Waarabu, Wachina, Wareno, Wamasai, Warusi, Wahindi, Wazungu, na kila aina ya homo sapiens ulimwenguni.

Rangi zote, makabila yote, dini zote, jinsia zote, tamaduni zote, jamii zote, asili zote, itikadi zote...zinawakilishwa Marekani. Taifa la Marekani linaitwa experiment (bahati mbaya hakuna neno mbadala la Kiswahili zaidi ya majaribio linalotoa tafsiri sahihi ya hilo neno) na lilipitia, limepitia, linapitia na litazidi kupitia mitihani mikubwa ambayo itaendelea kutoa funzo kwa dunia na kuonesha njia.

Safari hii Marekani inapitia tena mtihani mkubwa na matokeo yake yatakuwa funzo kwa dunia nzima. Watu kama Trump ni lazima watokee kama alivyotokea Hitler na watajaribu kutingisha misingi ya experiment na kama misingi hiyo si imara kama inavyoaminika, itayumba. Tumaini ni kwamba kwa miaka zaidi ya 400, misingi hiyo imesimama imara licha ya dhoruba kali kutoka kwa wachafuzi kama Trump.

Je Mmarekani ni nani hasa? Mlenge, inawezekana mnakasha huu unakuzidi kimo lakini lazima ama una ndugu (baba, mama, kaka, dada, mjomba, shangazi, mjukuu, mpwa, shemeji, mjukuu nk. ambaye ni Mmarekani na kama huna huishi katika ulimwengu huu. Marekani ni experiment na ukikua kuna siku utajua kwa nni iliitwa hivyo.
 
Back
Top Bottom