Duru za Siasa: Marekani (U.S) Chini ya Donald J. Trump

Ha ha ha El Jefe, are you for real? You appear to be so out of date buddy. Are you aware for instance that Rudolph W. Giuliani, whose actions as President Trump’s personal lawyer have helped set in motion an impeachment inquiry, abruptly canceled his scheduled paid appearance at a Kremlin-backed conference in Armenia next week? Yes, Rudy Giuliani aka special State Agent aka Trump's Lawyer and of course Putin would be there...

Giuliani’s decision to take part in the conference astounded national security experts. His appearance would have come days after the release of a whistleblower complaint accusing Trump and Giuliani of pressuring Ukrainian officials for damaging information about Democrats. Yeah, chew that! The unfolding scenario has made Washington pasikalike wala kulalika, to borrow a Kiswahili saying!

The shadow knows best...make sure you have your pop-corn ready buddy! It is full steam ahead!

Updates: House subpoenas Pompeo and schedules depositions of five State Department officials...

The chairmen of three powerful House committees subpoenaed Secretary of State Mike Pompeo for documents related to their investigation into President Trump’s controversial call with the leader of Ukraine.

The House panels have also scheduled five depositions beginning next week with State Department officials who would have knowledge of Trump’s engagements with Ukraine (including Rudolph Giuliani?) Who is Giuliani in the State Department anyway?

These are the first concrete steps taken as Democrats seek to build a case for impeachment.

More update:
Kurt D. Volker, the State Department’s special envoy for Ukraine, who got caught in the middle of the pressure campaign by President Trump and his lawyer, Rudolph W. Giuliani, to find damaging information about Democrats, resigned his post on Friday.
"Impeachment" discourse haven't been initiated now by the Dems! You shouldn't disremember that, they have been enmeshed in this delusion for three years. These latest moves are not "the first concrete steps to build a case for impeachment", rather the new steps after numerous failed attempts.

It all started with a Russian collusion story, followed by the House, Senate, FBI and Special Counsel's probes. These were "concrete steps towards impeachment". You even wrote about them right here in your previous posts. Except they led us into the desert.

Every time these hearing against Trump starts, it all seem "new and concrete". But the extent to which you guys disregard them when they lead us nowhere, and shift to probably new ones is flabbergasting!

But I will say this, Trump's actions are not impeachable acts! The desperate Dems used that normal phone call to orchestrate a politically biased "whistle-blower complaint" in order to give "life" to their incorrigible witch hunt activities.

Nevertheless, the important question is, if there was any wrongdoings on the part of Joe Biden's Ukraine involvement, is it worth examining? If the answer is yes, then Congress should at least look into it, if the answer is no, then an explanation should be provided. No double standards!

Its understandable, Giuliani is on the Dems' spotlight, but he is smart, he can handle this.

With regards to the resignations, didn't we witness a similar pattern of people resigning during the Russian collusion probes? That helped inflame the case, right?, but was there any collusion?

Ultimately, I'll not be embroiled into discussing the updates of this TV show because I know exactly how this sequel is gonna play out and how it's gonna end, it is humdrum just like the prequels, but I'm just gonna eat that popcorn anyway.
 
Rais Trump yupo kwenye kitimoto sasa kuliko nyakati zilizopita. Nimefuatilia hii huu mtanange, naona kabisa kuna sababu nyingi za impeachment ila watakwama kwa Seneti.
Kwetu sisi wengine ambao tulishuhudia live yaliyotokea mwaka 1974 yakimhusisha Rais wa wakati huo Richard Nixon, naomba nikumbushe kidogo tu ilivyokuwa kwa kuweka hiki kipande kifupi...(samahani wenzangu kwa lugha)

The 1972 United States Senate elections coincided with the landslide re-election of Republican President Richard Nixon. Despite Nixon's victory, Democrats increased their majority by two seats. After the elections, Democrats held 56 seats and Republicans held 42 seats, with 1 Conservative and 1 independent Senator.

The 1972 United States House of Representatives elections which also coincided with the landslide reelection victory of President Richard M. Nixon. Nixon's Republican Party managed to gain a net of twelve House of Representatives seats from the Democratic Party, although the Democrats retained a majority (255 - 180)

The Watergate scandal began with the June 17, 1972, break-in at the Democratic National Committee headquarters at the Watergate office complex in Washington, D.C., and the Nixon administration's attempted cover-up of its involvement.

When the conspiracy was discovered and investigated by the House of Representatives, the Nixon administration's resistance to its probes led to a constitutional crisis.

The House Judiciary Committee opened its formal impeachment hearings against President Richard Nixon on May 9, 1974. The first twenty minutes were televised on the major U.S. networks, after which the committee switched to closed sessions for the next two months.

In those two intervening years, a Senate investigative committee—along with the criminal trials of the apprehended burglars, and reporting by dogged journalists—pried loose an avalanche of evidence about abuses of power and obstruction of justice in the White House that slowly but steadily shifted public opinion.

During the hearings, President Nixon attempted to preserve his support in the House by wooing senior figures there, including some conservative Democrats, by inviting them to White House functions or evening cruises on the presidential yacht.

Those counts, as well as one for Nixon’s defiance of congressional subpoenas, were powerful enough to convince several Republicans to join the Democrats in supporting Nixon’s ouster.

The House Judicial Committee didn’t pass its articles of impeachment against Nixon until July 1974, a full two years (and one reelection campaign) after the failed burglary and bugging operation that began the unraveling of Nixon’s vast dirty tricks machine.

Shortly before the committee undertook its impeachment votes, poll showed that 53 percent of Americans supported an impeachment of Nixon by the House. The same poll showed that 47 percent thought he should be convicted in a Senate trial, 34 percent thought he should be acquitted, and the rest were unsure.

The televised coverage of committee hearings resumed on July 24. The commercial broadcast networks televised the evening sessions while PBS broadcast the morning and afternoon sessions as well; this was after considerable debate about whether such broadcasts were a good idea.

The first broadcast was an evening session of the committee on the evening of the 24th and started two days of televised opening-statements by committee members. In total there were six days of 13 hours-per-day of televised coverage, watched by millions of Americans.

On the afternoon of Friday, July 26, television viewers watched live as the first Article of Impeachment was read into the record against the President.

With impeachment by the House and removal by the Senate all but certain, on the night of August 8, 1974, Nixon took to the airwaves and delivered an address in which he announced his decision to resign the following morning.

At 11:35 am EST on August 9, 1974, Nixon officially became the first, and so far only, president to resign.
 
Kwa sababu labda hujui umuhimu wa kinachoendelea nchini Marekani, nakupa ushauri tu mdogo; nunua pop-corn, since now it is all system go, just sit down and watch...the genie is outside the bottle! Tick...tack...tick...tac
Mwaka wa tatu huu nashauriwa " kununua pop-corn"...ili niangalie sinema ya kumdondosha Trump, ujue!!!!
 
SIASA ZA DC ZINA NAMNA ZAKE
''MATANGO PORI YAPO PIA, NI RAHISI KUMEZA''

Rais Trump aliingia madarakani kwa siasa za kubabaisha kama alivyofanya katika real estate
Hoja alizojenga zilizama katika kuzua habari na kuifanya iwe kweli hata kama si kweli.

Mifano : Kuwaaminisha baadhi ya Wamerekani kuhusu Uraia wa Rais Obama na kujenga mfarakano wengi wakiamini Taifa lao linatawaliwa na raia wa kigeni.

Kuwaaminisha kuwa upigaji wa kura ulizingirwa na rushwa kiasi cha kuunda tume yake mwenyewe iliyohitimisha kazi hiyo bila hata ukurusa mmoja wa ushahidi au andiko

Kuwaaminisha kuwa atajenga ukuta na watakaolipa gharama ni Mexico.
Hajajenga ukuta bali anakarabati kwa gharama za Wamarekani.

Kawaaminisha Obama aliacha kujaza nafasi za Majaji kwa uzembe tu! wapo walioamini!

Ndivyo ilivyo katika siasa za nje kama Iran na Korea, vituo vya majeshi na vita sehemu kadhaa duniani ikishirikisha Marekani.

Hakuna kipya hata kimoja alichokifanya tofauti.

Ushahidi wa hilo ni suala la Ukraine ambako kwa siri anapita katika nyayo za Obama akitumia madaraka yake vibaya.

Suala la Ukraine amelifanya jipya kwa makusudi ili kupotosha sehemu ya jamii na wale wanaosoma tweet au kumfuata tu bila kuzijua siasa za viunga vya DC na michezo yake.

Kumwingiza Joe Biden kuna sehemu mbili.
Kwanza, hofu ya kwamba atakuwa mpinzani wake mkuu na anafahamu anavyoweza kumvuruga kwani Joe si mgeni DC

Pili,ni mkakati mahususi ili mada isiwe kwanini anamwandama Joe kwa suala lenye majibu.

Ndiyo maana kila mara anasisitiza '' ni muhimu kuchunguza suala la Joe''

Anachokitaka si ushahidi, anajua uchunguzi ulishafanyika, anajua Joe Biden alifanya kila kitu hadharani. Hoja yake ni zile siasa za ulaghai ili watu wahoji jambo lililo wazi kabisa.

Kwanini hakufanya uchunguzi wakati akiwa na House na Senate?
Kwanini hakutumia vyombo vya dola kupata majibu haraka?
Kwanini hakutoka hadharani kama alivyofanya Joe Biden kuhusu suala la kuzuia misaada?
Kwanini GOP hawaungi mkono hoja yake ya uchunguzi?
Kwanini aliachia misaada iende Ukraine baada ya timbwili kubumburuka?

Suala la Biden lilifanyika hadharani si kwa siri na mbinu za kujificha.

Biden alikwenda Ukraine kama VP na alisimama hadharani na kutaka prosecutor aliyekuwa anachunguza rushwa aondolewe.

Hilo alilifanya kwa baraka za US, nchi za Ulaya na mashirika ya kimataifa ambayo hakuna hata moja limejitokeza na kukana!

Yalipotokea maneno kuhusu mwanae ambaye alijiunga na Bodi baada ya uchunguzi, ulifanyika uchunguzi ulioeleza Biden na Mwanae Hunter kutohusika na kashfa yoyote ile.

Wajanja wa Washington wakiwemo Republicans wanaujua ukweli ndiyo maana hakuna anayejitokeza kupiga debe kwani kufanya hivyo ni kuimba nyimbo za Trump na kujianika.

Kwa upande wa Trump, alichokifanya ni kushinikiza kwa siri si kutumia vyombo husika.
Kushinikiza Hunter Biden abambikiwe kesi ili kumuunganisha na Biden.

Kumbuka Trump alikuwa na House na Senate pamoja na WH nini kilimshinda siku zote?

Ujanja wake unagonga mwamba, kwamba, siasa za DC zinakwenda tofauti.
Kumshambulia mpinzani wake kwa kutumia rasilimali za nchi si sahihi.

Kutokana na fyongo ya transcript wigo wa uchunguzi unapanuka na hilo linamtia hofu.

Tofauti na uchunguzi wa Russia hili la Ukraine linahusisha congress iliyoidhinisha pesa.

Nguvu ya Trump ipo ndani ya umaarufu katika Republicans anakoungwa mkono kwa 90%.

Hata hivyo,kwasasa kuna 'fatique' miongoni mwa Republicans.

Trump ni mzuri sana katika kusimamia uongo.

Anaweza kuzusha jambo likateka habari za siku si kwa bahati mbaya bali kuvuruga watu wasiongelea asichotaka kusikia au kinachomwandama.

Trump anaelewa wazi kila akitupa ''tango pori'' hatakosa wa kufakamia bila kutafakari.

Trump anaposema suala la Ukraine lichunguzwe ni kutafuta kuungwa mkono na wafuasi wake wasiojua siasa za DC na wengine wanaomeza tu kila anachosema.

Hivi kwanini asiagize vyombo vyake vya dola vishirikiane na Ukraine kufanya uchunguzi?

Hivi alishindwaje uchunguzi akiwa na House na Seneti eti leo anataka Dem House ifanye uchunguzi?

Katika hili la Ukraine kuna mahangaiko,dhahri shahri ipo taharuki ndani ya kasri jeupe, mpangaji mkazi anaiangalia historia isijidhihiri tena! akiomba mizimu ya miongo kadhaa iliyopita ipungwe na kutulia. Nguvu ya ulaghai inapelea , hamkani si shwari.

Tusemezane
 
....zito kwa kuangalia Republicans walivyopigwa butwaa. Katika hali ya kawaida wengi wangejitokeza kufanya ''spinning''
I guess 'their spinning' is paying off, hasa kwa kuweza kuendelea kumuweka Madarakani Trump kwa 'good three years', toka 'Russiagate drama'. Najua Demo wanauchungu lakini wa reserve energy for betterment of their useful US. Hata hivyo, timbwili zao (DEMO), zimesaidia, maana kama Wamarekani wangekuwa wamoja....vita nyingine Mashariki ya Kati kati yake na Iran ingekuwa imeishaanza.
 
But I will say this, Trump's actions are not impeachable acts! The desperate Dems used that normal phone call to orchestrate a politically biased "whistle-blower complaint" in order to give "life" to their incorrigible witch hunt activities.
Are you sure? Keep on living in your world of alternative facts!
Its understandable, Giuliani is on the Dems' spotlight, but he is smart, he can handle this.
Rudolph Giuliani smart? That country lawyer from a small town? Wow!
Ultimately, I'll not be embroiled into discussing the updates of this TV show because I know exactly how this sequel is gonna play out and how it's gonna end, it is humdrum just like the prequels, but I'm just gonna eat that popcorn anyway.
Good for you, just sit back and enjoy your popcorn, you sure need them!
 
Ultimately, I'll not be embroiled into discussing the updates of this TV show because I know exactly how this sequel is gonna play out and how it's gonna end, it is humdrum just like the prequels, but I'm just gonna eat that popcorn anyway.
@El Jefe, whether you are embroiled or not into discussing the updates of what you call TV show, support for impeachment inquiry has reached 55% and growing...!

One thing is for sure, you do not know exactly how this sequel is gonna play out or how it's gonna end and so keep on enjoying your popcorn.

Moreover the degree of your obsession with authoritarians/leaders with no regard to the rule of Law doesn't really matter at all! This is the USA not some backward country in Africa.



Impeachment support for President Nixon in 1974 was only 53%. For Trump it is 55% and growing. Even one GOP Governor has already joined the call for impeachment




Over 300 ex-US security officials support impeachment probe of President Trump!

Over 300 former officials from U.S. security and foreign policy agencies, including a former director of the National Counterterrorism Center and a one-time deputy secretary of state, on Friday, September 27th endorsed the congressional impeachment inquiry of President Donald Trump.

Their statement said the signatories had served in the administrations of both parties. It also said the signatories did not want to prejudge the conclusions Congress may reach in the inquiry.
“President Trump appears to have leveraged the authority and resources of the highest office in the land to invite additional foreign interference into our democratic processes. That would constitute an unconscionable abuse of power.
It also would represent an effort to subordinate America’s national interests and those of our closest allies and partners to the President’s personal political interest” they wrote in the statement sent to news organizations.

 
NDANI YA VIUNGA VIKUU VYA DC
RAIS TRUMP AWEWESEKA, UKRAINE INABANA

Rais Trump amekuwa mtandaoni akitoa tuhuma ambazo kisheria zinamweka matatani zaidi.

Mathalan, kasema zama zao '' wasaliti'' kwa maana ya whistle blower walishughulikiwa kwa namna yake akimaanisha waliuawa

Kaenda mbali na kutaka kukutana na whistle blower ambaye kisheria analindwa na kwamba alichokifanya kipo ndani ya sheria

Kamtuhumu mwenyekiti wa kamati ya intelejensia akidai akamatwe kwa uhaini(Treason).

Kwa Marekani adhabu ya mhaini ni kuuwawa. Lakini kweli House Rep anaweza kuwa mwenyekiti wa kamati ya intelejensia akawa msaliti na Wamarekani wakamuangalia tu!!

Hayo yote yanajiri kufuatilia hali inayoashiria kulegea kwa ngome ya Republicans wengine wakijitokeza na kueleza masikitiko yao dhidi ya alichokifanya kwa ''Ukraine Transcript''

Senate majority McConnel katika nyakati chache kabisa amejitokeza na kusema ikiwa house itapitisha impeachment na kukawa na 2/3 katika senate hana namna ya kuzuia hilo.

Msimamo wake unaonekana kushinikizwa na Republicans wanaoanza kuchoka kumtetea Rais

Rudy Giullian naye kaitwa na kamati ya Bunge apeleke nyaraka.

Haieleweki kama atakwenda au atatumia ''attorney privilege'' akiwa mwanasheria wa Trump kumkingia kifua na kukingiwa pia

Inspector general(IG) naye katika hali isiyo ya kawaida akiwa ni mteuliwa wa Trump amejitokeza kueleza uhakika wa whistle blower na kufunga kabisa hoja za baadhi ya wafuasi wa Trump ya kuwa whistle blower ana second hand information.

IG anafahamu uongo huo ukirudiwa sana wapo wanaoubeba tu bila chembe ya tafakari na hasa wageni wa siasa za DC wanaojitutumua bila kujua viunga vya DC vinahitaji ufahamu si tweet.

Washington post inaripoti kuwa AG Barr alizungumza na Rais ili aishawishi Australia kutoka ushirikiano kwa ''kamati aliyounda Trump ya kutafuta chanzo cha Dossier na Russia''

Lengo la kamati ni kutaka kumsafisha Trump ili Mueller aonekane muongo, na kwamba, uchunguzi wa Russia ulikuwa bogus na witch Hunt

Hilo linamweka AG Barr katika wakati mgumu ikiwa ni mara ya pili anatuhumiwa kushirikiana na Trump katika ''cover up'' au kutafuta mchawi kupitia tume bogus

Kumbuka suala la Russia lilianza na intelejensia ya Australia..

AG Barr ameiondoa DOJ katika msimamo wa kutofungamana na siasa, huku akiunda tume na Trump wanayofanya kazi kutafuta majibu na si kusbiri taarifa ya uchunguzi wa ''Jaji rafiki'' aliyeteuliwa. Hivi unaundaje tume halafu ukasaidia kupata taarifa?

Uwezekano wa utakiwa kujitoa ''recuse'' katika sakata la Ukraine unaongezeka.
Ikitokea hivyo, tui litakuwa limetiwa maji kwani Barr ni ngome ya Rais Trump

Yote yakitokea inaonekana suala la Ukraine linamchukua Rais Trump zaidi na kila mbinu ya ''kutupa'' uchafu ujadiliwe inashindikana. Hoja iliyoko mbele ni Ukraine na inamtisha sana

Hakuna uhakika kama seneti inaweza kupata 2/3 kwa kuzingatia Republicans walivyogeuka mbwiga "coward'' mbele ya Trump. Kinachomtia hofu ni jinsi suala hili linavyozidi kupanuka

Imefahamika wakati wa simu za Ukraine , SoS Pompeo alikuwepo.

Trump anapofikiria John Bolton aliondoka akiwa mshauri wa usalama katika mtifuano na Pompeo haoni mbele iliyo njema.

Trump hajui nani whistle blower na alipataje habari na ikiwa '' watu wake wanamwendea kinyume''. Hilo linamwacha akiweweseka kila uchao kwa hofu ya ninikitatokea machweo

Kikubwa zaidi ni kwamba baadhi ya watu wake wameanza kutosa jahazi kama Bw Volker ambaye sasa yu huru kusema lolote mbele ya kamati.

Rais Trump anafahamu ni ngumu sana kwa Democrats kupata 67 ya maseneta ambao Republicans ni wengi na wengi wao ni mbwiga.

Kinachomtatiza na kuwatatiza wasaidizi wake ni kuhusu wigo wa watu.

Kwamba, ikiwa atatokea mmoja katika kundi akaenda kombo na kusema jingine zito, kwa ufa unaoanza kujitokeza ndani ya GOP hilo litachochea mparaganyiko na kumwacha pweke.

Kwa maneno mengine, Rais Trump hasumbuliwi na idadi ya mayai ndani ya kikapu

Kinachomsumbua ni wababeji wa kikapu.
Katika hili la Ukraine wabeba kikapu ni hatari kuliko ''mayai ndani ya seneti''

Tusemezane
 
VIUNGANI DC
NI SONGOMBINGO TU

Sakata la Ukraine limeendelea kutikisa viunga vikuu vya DC kwa kishindo.
SoS Pompeo anaonekana kukaidi wito wa kamati za Bunge kuhusu kuhojiwa.

Rudy Giulian bado anacheza mchezo wa kisheria, mara akisema kuna ''attorney privilege'' mara nyingine akisema hakuwa anamwakilisha Rais Trump.

Bw Volker yeye amekubali kuhojiwa na kuangiwa tarehe, na Balozi wa Marekani Ukraine aliyeondolewa 'kinamna' naye pia kakubali kuhojiwa.

Hawa wote walikuwa chini ya Pompeo anayesema '' kamati za Bunge zinawaburuza '' watumishi wa SoS na kuwatia hofu.

Kuna hofu ndani ya Kasri jeupe kwamba wanahojiwa haieleweki kwanini wamekubali na watasema nini.

Katika hatua nyingine isiyotarajiwa, Inspector general anakwenda katika viunga vya Bunge kuongea na kamati za Bunge kuhusu sakata hilo.

Hakuna anayeelewa IG ataongelea nini, lakini inatosha kutia shaka kila upande.

Huenda anakwenda kuzipiga pini kamati za Bunge kuendelea na uchunguzi!
Huenda anakwenda kutoa ushahidi zaidi wa sakata hilo la Ukraine!
Huenda anakwenda kutoa ufafanunuzi kuhusu whistle blower au masuala ya ''kisheria''

Kwa ufupi hakuna anayejua nini kitaongelewa, inatosha kusema tu kuwa kutakuwa na habari kesho. IG ni mtu aliye katikati ya sakata la Ukraine na ana mengi ya kuongea.

Viungani DC macho na masikio yametegwa leo kujua IG analipi geni !

Tusemezane
 
DC NA SAKATA LA UKRAINE
RAIS TRUMP ALIPUKA, NI KUWEWESEKA BILA KITUO

Rais Trump aliamka na Tweet akimalizia siku na mkutano kati yake na Rais wa Finland

Maswali mengi yalimwandama na kubwa linalozungumzwa ni lile aliloulizwa na mwandishi wa Reuter kwamba ''Trump alitaka Rais wa Ukraine afanye nini kwa Joe Biden na Mwanae Hunter''

Swali hilo lilimkwaza Rais na kuishia kumkashfu mwandishi huyo bila kutoa majibu

Hili linaonyesha simu yake ilikuwa na jambo juma yake, kumwandama Joe Biden na Mwanae

Kwa sehemu kubwa Rais Trump alikuwa amepagawa na kiwewe cha impeachment kikimtesa

Katika mwendelezo wa sakata la Impeachment, Inspector general (IG) amefikisha nyaraka mbele ya kamati za bunge. Nyaraka hizo amepewa kutoka ofisi ya SoS, Pompeo.

Nyaraka zinaonyesha ''conspiracy theory'' kuhusu Biden ambayo Rudy amekiri kuwa mwandishi.

Haieleweki undani wa nyaraka lakini zipo taarifa zinazomhusu aliyekuwa balozi wa Marekani nchini Ukraine Bi Masha Yovanovitch aliyetimuliwa na Trump kwa kutokubali ''mpango wa WH''

Kwa mantiki hiyo,nyaraka imemuonyesha Masha Yovanovitch jinsi alivyohujumiwa na mhusika akiwa Rudy Giulian,mwanasheria binafsi wa Trump asiye mwajiwiriwa wa WH au State dep

Hapa pana mtego, Yovanovitch atafika mbele ya kamati za Bunge bila kizuizi na huenda atasema kila anachojua kuhusu mpango huo. Hili linapelekea kimuhe muhe ndani ya kasri jeupe

Mwingine anayefuata ni Kurt Kolver aliyejiuzulu na ambaye state department imesema haiwezi kumzuia kutoa ushahidi kwa privilege yoyote na leo atakuwa mbele ya kamati

Wawili hao, Yonavovitch na Kolver wanaweza kuleta ushahidi wenye mtikiso katika sakata zima.

Habari ilianza kwa whistele blower, ikafuata transcript, wakaja wahusika kama Kurt Kolver na Masha Yonavovitch. Pembeni kuna akina Pompeo ambaye leo amekiri alikuwepo simu ikipigwa.
Yupo mtu anayetajwa sana Rudy Guilian. Bado wanatafutwa watu wa WH na State depart.

Kinachomtisha Trump si idadi ya maseneta wanaomuunga mkono, kwa uhakika 2/3 ya kumuondoa ndani ya seneti ni ngumu.

Hata hivyo, ushahidi na hizi chururu zitaleta ukakasi na 2/3 ikapatikana.
Ndivyo historia inavyotuonyesha tukimwangalia Nixon

Suala hili linaonekana kumchukua Rais Trump kwa uzani mkubwa, awali alidhani ni masihara ukizingatia suala la Russia lilivyokuwa.

Taraatibu anaanza kuelewa 'the gravity' ya suala zima.

Trump ana kila sababu ya kuweweseka mawio au machweo, tui limetiwa maji, kamba inabana

Tusemezane
 
Kinachomtisha Trump si idadi ya maseneta wanaomuunga mkono, kwa uhakika 2/3 ya kumuondoa ndani ya seneti ni ngumu.
Hicho ndicho kitu nimekuwa nikiwashauri wapenzi wa Trump humu JF wakitilie maanani lakini naona wanaamini bunge za Marekani ni kama hili la kwetu Tanzania. Lengo la impeachment inquiry ni kukusanya ushahidi kabla ya kuanza impeachment proceedings. Ushahidi utajadiliwa kwa mapana na marefu ndani ya House kabla ya kuandika articles of impeachment ambazo pia zitajadiliwa na mwishowe kupigiwa kura ndani ya hiyo hiyo House na zikipita zitawasilishwa kwenye Senate.
Hata hivyo, ushahidi na hizi chururu zitaleta ukakasi na 2/3 ikapatikana. Ndivyo historia inavyotuonyesha tukimwangalia Nixon
Uzito wa ushahidi ndio unaweza kumuondoa Trump madarakani na si wingi wa Senators wa GOP ndani ya mahakama hiyo. Tusishangae kuwaona wengi wao wakikimbia kambi na kuunga mkono impeachment kama ushahidi unaridhisha.
Suala hili linaonekana kumchukua Rais Trump kwa uzani mkubwa, awali alidhani ni masihara ukizingatia suala la Russia lilivyokuwa. Taraatibu anaanza kuelewa 'the gravity' ya suala zima.
Kwa bahati mbaya Trump hadi dakika hii bado anaamini kwamba mambo hayawezi yakamgeuka, anaamini kwamba wafuasi wake hawatasalimu amri hata kama ushahidi utakuwa mzito namna gani. Anadhani ukiwa Rais basi hakuna kiumbe duniani anaweza kukuwajibisha na anaamini kwamba anayo nguvu kubwa hata kwa vyombo vya dola. Anachosahau ni kwamba kiongozi aliyechaguliwa kihalali anatakiwa awe mnyenyekevu kwa wananchi kwani Yeye ni mtumishi tu wa Wamarekani na si mtawala kama Putin wa Urusi, Kim il Jung wa Korea Kaskazini wala XI Jinping wa China.
Trump ana kila sababu ya kuweweseka mawio au machweo, tui limetiwa maji, kamba inabana.
Taratibu ukweli mchungu utamwingia na ataanza kutambua kwamba hayuko juu ya Katiba ya Nchi na kwamba kwa Marekani. tofauti na nchi zingine, hakuna dhambi kubwa kama kujaribu kuchezea Katiba ya nchi hiyo. Amelikoroga na sasa awe tayari kulinywa pamoja na uchungu wake...This is the way the cookie crumbles!
 
VIUNGANI DC WIKI HII
TRUMP AONDOA MAJESHI SYRIA
WAPILI YU TAYARI KUTOA USHAHIDI WA UKRAINE

Habari ya leo ni kuhusu Rais Trump kuondoa majeshi Syria na kuwatosa washirika wa Kurd.

Waka Kurd walipigana bega kwa bega na Wamarekani kule Iraq na kule Syria dhidi ya ISIS

Lakini pia Wakurd wana mzozo na Turkey wakionekana kama waasi na wachochezi
Hivyo kwa upande wa Syria, suala la Turkey kuwabonda ni muhimu nafasi ikipatikana

Kuondoa majeshi ya Marekani ni kuwaacha Wakurd ''vulnerable'' kwa kichapo cha Turkey.
Wakati huo huo ni ushindi kwa Russia wanaomasaidi Rais Asaad

Suala la kuondoa majeshi limepokelewa na Wamarekani kwa hisia tofauti.

Republicans wameonekana kuchukizwa na hatua za Trump kwa kuwatosa Wa Kurd.
Hoja ya Republicans ni kwamba, kutabaki Ombwe na hivyo ISIS wanaweza kurejea

Hoja hiyo ni ya ''aibu'' kwani ni Republicans hao hao walimshambulia Obama alipoondoa majeshi Iraq. Kwao, kitendo hicho ni kumeza matapishi na wanaona wataweka wapi nyuso zao.

Miongoni mwa waliomshambulia Obama ni Lindsey Graham mpambe na Rais Trump

Rais Trump hakufanya hivyo kwa bahati mbaya au kwa nia njema.
Hizo ni harakati za kubadili mazungumzo ya Impeachment ili kufifisha hoja iliyopo.

Impeachment inaingia katika wakati mwingine, whistleblower wa pili anajianda kutoa ushuhuda.
Huyu kama wa kwanza anatoka katika intelligence community.

Maana yake ni nini? Ni kwamba, kuna wimbi wa whistle blower linalozidi kujitokeza na haieleweki wangapi waliobaki na wamebeba kitu gani. Hili ndilo linalomtisha sana Rais Trump

Kutishika kwake ni pale anaposema ''mazungumzo kati yake na Rais wa Ukraine yalikuwa ya kawaida na mazuri'' Hiyo ndiyo imekuwa kauli ya Republicans kwa maana hakuna quid pro quo.

Wakati huo huo Rais Trump na SoS wamezuia nyaraka za ''maongezi hayo mazuri'' na kuwapiga pini wafanyakazi kutoka ushuhuda. Je, mazungumzo mazuri yanatishwa na nini?

Rais Trump amemnyooshea kidole secretary Rick Perry kwamba ndiye alimwingiza chaka la kuongea na Rais wa Ukraine kuhusunishati ya gesi.

Perry anakataa akisema hakushinikiza lolote kuhusu Joe Biden.
Hoja nyingine, ikiwa mazungumzo yalikuwa mazuri, Perry anaingiaje ?

Kwa hali yoyote kuondoa majeshi Syria ni mbinu ya kubadilisha mazungumzo ya impeachment.

Kama mtakumbuka huko nyuma tulisema'' tishio si idadi ya mayai ndani ya seneti'' bali wale waliobeba mayai hayo ambao mmoja baada ya mwingine wanatua vikapu kwa kishindo!

Tusemezane
 
Kama mtakumbuka huko nyuma tulisema'' tishio si idadi ya mayai ndani ya seneti'' bali wale waliobeba mayai hayo ambao mmoja baada ya mwingine wanatua vikapu kwa kishindo!
Breaking News: For the first time today's polls show majority of Americans want Trump impeached and removed from office.

Ni ngumu kuamini lakini hii poll imetolewa na watetezi nambari one wa Trump, FOX NEWS! Tusubiri tuone GOP Senators watafanya nini siku Senate watakapotupiwa mpira...je watasuka au watanyoa?
 
Ni ngumu kuamini lakini hii poll imetolewa na watetezi nambari one wa Trump, FOX NEWS! Tusubiri tuone GOP Senators watafanya nini siku Senate watakapotupiwa mpira...je watasuka au watanyoa?
Mkuu umesahau polls za namna hii zilivyotudanganya kuwa H.R.Clinton ndiye angeshinda urais wa US huku zikimponda Trump? Siamini kama umesahau haraka namna hiyo.
 
Kwa ukumbusho tu, polls za mwaka 2016 hazikukosea...H.R. Clinton alimshinda Trump kwa kura zaidi ya milioni tatu!
Aisee...! Kwa hiyo US kuna wizi wa kura, hapa patamu sana. Nadhani hii mada ya kura tuiache kwanza tutairejea baada ya sakata hili la 'kum-impeach Trump' kutokana na Ukrainegate baada ya sakata lile la Russiagate.
Mchana mwema kama Upo Tanzania, asubuhi njema kama upo Bara Amerika na usiku mwema kama Asia ya mbali.
====

Ukraine’s president has insisted that there was nothing improper about a phone conversation he had with Donald Trump, dismissing allegations that the US leader had tried to extort political favors from him.
Volodymyr Zelensky said on Thursday that there was “no blackmail” involved in the call he had with Trump. Democratic lawmakers have accused the US president of withholding military aid to Ukraine as part of a plot to coerce Kiev into launching a probe into the business dealings of the son a top political rival, Democratic presidential candidate Joe Biden.
Zelensky contradicted this narrative, telling reporters that he only learned after their July 25 phone call that the US had frozen hundreds of millions of dollars in military aid to his country. He said that the two leaders didn’t speak about military aid and that it wasn’t a “theme” of their conversation.

A transcript of the phone call was released to the public after an anonymous whistleblower alleged that Trump had sought Ukraine’s help in settling political scores back home.

The incident has “slightly” damaged US-Ukraine bilateral relations, Zelensky conceded. He told reporters that he wasn’t comfortable with releasing full transcripts of his conversations with world leaders, including President Trump. Kiev desires good relations with Washington but does not take orders from abroad, Zelensky added.

The US president said that the military aid was withheld because Kiev has not done enough to fight corruption, but the move has prompted Democrats to launch an impeachment inquiry.
 
Aisee...! Kwa hiyo US kuna wizi wa kura, hapa patamu sana.
Naam, kuna mtu moja tu amewahi kudai kulikuwa na wizi wa kura naye ni Rais Donald Trump wakati akilalamikia idadi ya kura alizopata H.R. Clinton kuzidi alizopata. Alidai kuna kura zilipigwa na watu wasio na sifa hadi akaunda tume kufuatilia lakini hakuna ushahidi wowote uliopatikana.

Aliwahi pia kudai watu waliohudhuria kuapishwa kwake walikuwa wengi kuliko waliohudhuria kuapishwa kwa mtangulizi wake Rais Obama. Marekani haijawahi kumpata Rais muongo, mhuni, zumbukuku na limbukeni kama huyu wa sasa...

Lakini katika yote safari hii kuna hatari ya mbio zake za sakafuni kuishia ukingoni. Kama ni kupatikana, kanasa na hachomoki. Kakutana na mwanamke wa shoka Pelosi! Tuvute tu subira...
 
VIUNGANI WIKII HII
RUDY GIULIANI '' UNDER THE BUS'' KAMA MICHAEL COHEN
MKAKATI WA SYRIA UNA ''BACK FIRE''

Tuanze na marejeo ya bandiko # 992 na 994. Katika sakata la 'Ukraine'' tulisema tatizo siyo whistleblower ni wigo wa washiriki na hao ndio watamweka Rais Trump majaribuni.

Tuliwataja kwa kuanzia, AG Barr, SoS Pompeo, Ambassador Yonavovitch na mshiriki mkubwa Rdolph Giulian, Mayor maarufu wa Marekani aliyegeuka kikaragosi.

Wigo umeendelea na kuwagusa matajiri, mawaziri na mabalozi , achilia mbali washiriki kutoka WH na State depart. Katika hali kama hiyo kuficha 'madhambi' ni ngumu.

Jana, washirika wawili kutoka Ukraine walikamatwa wakitoroka. Washirika hao wamechangia fuko la kampeni la Rais Trump zaidi ya dola 300,000 kiungo chao kikiwa ni Rudy Giuliani

Kukamatwa kwa washirika hao ini tatizo kwani kunatengeneza ''utatu'' wa Washirika(Ukraine), Rudy na Rais Trump. Hilo si geni, linashadidia ushahidi wa whistleblower kuhusu sakata zima

Katika hali ya kujinasua, Rais Trump anamkana Rudy na kwamba hao ni watu wake licha ya ukweli kuwa Trump, Giuliani na washirika hao walikuwa Trump Hotel wakila bata juzi tu.

Trump anajinasua kutoka utatu huo kwani kesi mbele ya mahakama haina kizuizi na hawezi kumtumia Pompeo au Barr. Washirika hao watalazimika kunena mbele ya Hakimu

Kwa unyonge Rudy anasema hatashiriki shughuli za kisheria zinazomhusu Rais naUkraine

Kisa cha Michael Cohen kilianza hivi hivi, mwishowe wakawa mahasimu wakubwa.

Rick Perry, waziri wa nishati naye yupo ukingoni kutoswa chini ya Bus kama Giuliani.

Yule mshauri wake John Bolton tuliyesema aliondoka kwa duku duku, naye anatajwa kama shahidi muhimu na huenda akaitwa mbele ya kamati.
Ikitokea hivyo, SoS Pompeo ana wakati mgumu sana huku WH ikitweta kwa kishindo

Kimbembe hicho kikiendelea kumwandama mkazi wa WH Bw Trump , ile mbinu ya Trump kuondoa majeshi ili kubadili mwelekeo imegonga mwamba.

Republicans wanaonekana kukasirishwa na uamuzi huo na hilo linachagiza wengi sasa kuona ''wakati wa ndama kumuacha mama umetimia''

Kama tulivyosema mabandiko ya nyuma , Wakurd wanachukua kichapo kutoka Turkey

Trump anasemekana kumpigia senate majority Mitchel, ''hala hala mti na macho'' zuia Republicans kwani kamba inavyobana Trump atahitaji ngome ya Republicans.

Kwa uzito wa sakata hata watetezi wanasema alifanya bad judgement lakini hilo haliwezi kuwa sababu ya impeachment.

Hata hivyo Trump ameshikilia msimamo wake kwamba Rais wa Ukraine amekana kushinikizwa.
Trump anaju, wasiojua siasa za viungani na wale wanaounga unga habari wataamini kweli!!

Hivi kweli Ukraine wanaweza kumkana Trump aliyeshikilia mamilioni ya dola zao, wanaomtegemea kiulinzi!

Haiwezekani hata kidogo! inawezekana kwa wageni wa siasa za viungani DC

Huku akiweweseka na kutoa maneno machafu dhidi ya Obama! secretary wake wa Homeland ameachia ngazi jioni hii kwa hiari yake

Taratiibu manahodha wanajitosa majini kwa kuchelea jahazi kuingia maji.

Tusemezane
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom