Duru za Siasa: Marekani (U.S) Chini ya Donald J. Trump

VIUNGANI DC WIKI HII
RAIS Trump aselelea (Hit rock bottom)
Nyuma ya Pazia anataka mazungumzo na Iran, ngoma nzito

Kama kuna anayemfanya Rais mstaafu Obama aonekane kiongozi bora ni Rais Trump.

Rais Trump aliwahi kumwita Rais Obama ''stupid leader'' na kwamba dunia iliwacheka Wamarekani kwa uongozi wake.

Kama hilo lilikuwa kweli, kwasasa dunia haicheki tena bali imepigwa ganzi, butwaa na kutundawaa

Wiki hii baada ya kuahirisha safari ya Poland kuhudhuria maadhimisho ya vita ya dunia, Rais Trump alionekana akicheza golf huku tishio la dhoruba Dorian likizidi kurindima.
Ni Trump aliyemshambulia sana Obama kwamba anacheza golf kuliko Tiger Woods
Katika miaka 3 ya utawala Trump amecheza golf kumzidi Obama ndani ya miaka 8.

Habari kubwa ni ya kiongozi huyo kutofahamu habari zinazotolewa na serikali yake kuhusu hali ya hewa akiwa pia hajui ramani ya nchi yake na kuwa gumzo la kitaifa na kimataifa.

Trump alidai Dhoruba ya Dorian itaikumba Alabama huku akibadilisha ramani ya mamlaka za hali ya hewa ili kukidhi haja yake na si uhalisia wa kitaaluma.

Tatizo si kufanya makosa bali kuyatetea kwa njia za kitoto chini ya hadhi ya ofisi hiyo kubwa.

Rais ametumia kila aina ya ushawishi kuthibitisha madai yake ya uongo bila mafanikio.
Dhalili anayoipata mbele ya jamii yake ni kubwa na ya kusikitisha kwa namna yoyote ile.

Ukuta
Rais Trump anatumia pesa zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za jeshi na miradi mingine ili kujenga ukuta. Ikumbukwa Rais aliahidi ukuta utalipiwa na Mexico, kwasasa unalipiwa na Wamarekani. Haya tuliwahikuyaeleza na kwamba Trump alikuwa akilaghai wafuasi wake.

Hali ya uchumi
Takwimu zinaonyesha kudorora kwa ajira, mwezi wa 8 ukiwa umetengeneza ajira 130, 000 kati ya hizo 25,000 si za kudumu. Vigezo vingine havina mabadiliko makubwa lakini kwa kulinganisha na muda na hali ya uchumi aliyopokea, namba hiyo ni ndogo sana ukilinganisha na mtangulizi wake Obama. Vita yake ya uchumi haionekani kumsaidia

Trump amemshambulia mkuu wa Bank kuu (Reserve Bank) aliyemtea mwenyewe kwa madai kuwa anaongeza riba na hivyo kuathiri uchumi.

Trump anasema wakati wa Obama viwango havikuongezwa bila kufikiri wakati huo uchumi ulikuwa katika recession na kwamba alikabidhiwa uchumi ulioimarika tofauti na mtangulizi wake.

Meli ya Iran
Zipo taarifa za Afisa wa WH kumshawishi Nahodha wa meli iliyokuwa imeshikiliwa na UK aipeleke Marekani. Kama tulivyowahi kusema, UK ilitumika tu na US kuishikilia meli hiyo.

Nahodha aliahidiwa Pesa na kutukumbusha Trump alivyomsema Obama kupeleka pesa Tehran zilizokuwa mali ya Iran kama sehemu ya deal ya Nyuklia, Trump anafanya kile alichokilaani.

Iran Deal
Nyuma ya pazi taarifa zinaeleza maafisa wa Marekani wana haha kuishawishi Iran irudi katika meza ya majadiliano kuhusu silaha za nyuklia.

Trump alikumbana na wakati mgumu wakati wa G7 alipojaribu kuwashawishi wanachama waungane naye kuhusu Iran huku wakimueleza alijitoa katika deal bila kuwaeleza.
Sasa Trump anarudi kule kule kwa Obama kuhusu Deal

Iran yaahidi kurutubisha Nyuklia
Iran nayo imesema sasa haitatekeleza sehemu kubwa ya Deal na nchi za Ulaya na kuanza kurutubisha mitambo yake ya Nyuklia.

Uamuzi wa Iran ni baada ya kuona udhaifu wa Marekani na kwamba Iran inataka nchi za Ulaya zifanye jambo kurahisha maisha magumu yanayotokana na vikwazo.
Hoja yao ni kuwa ndani ya deal hawaoni matokeo yoyote.

Mpango wa US kuishambulia Iran kwa kushirikiana na Israel unaonekana kukwama.
Tatizo linalojitokeza si nguvu za kijeshi za Iran, bali ushawishi wa Iran katika eneo la mashariki ya kati na kwamba kinachotokea kinaweza kuwa kikubwa zaidi ya kinachoendelea Afghanistan

Deal na Talibani
Serikali ya Trump imekuwa katika mazungumzo na Talibani na imekubaliana nao kuondoa askari wake kwa kiwango kutoka nchi hiyo. Mazungumzo na Talibani hayakuanza leo, Republican na Trump walimkashifu sana Obama alipojaribu kukaa mezani na Telebani.
Leo Republicans na Trump wamerejea kule kule kwa Rais Obama

Kwa hadhi ya jengo jeupe la viungani DC Rais Trump kaselelea chini ya Mwamba(hit rock bottom). Kwa siasa za kimataifa sasa anafuata nyayo za Obama. Kwa hali ya uchumi hofu kubwa ni mdororo mikononi mwake.

Hayo yote yanachigiza sehemu ya jamii kuhoji utayari wake kuongoza Taifa hilo wakitilia mashaka uwezo wake kiakili, lakini pia kumfanya Obama ang'are

Tusemezane
 
VIUNGANI DC WIKI HII

Habari ya Taliban kuzungumza na utawala wa Trump imethibitika na hilo lilikuwa litokee katika nyumba ya Rais ya mapumziko ya kikazi 'Camp David''

Kwa kumbukumbu, Camp David ni eneo muhimu la majadiliano kuhusu hali ya usalama wa nchi ya Marekani iwe kisiasa au kiuchumi.

Ni eneo ambalo Waziri mkuu wa Israel Menachem Begin na Rais Anwar Sadat wa Misri walifikia makubaliano ya amani chini ya usimamizi wa Rais Jimmy Carter kwa kile kinachojulikana kama Camp David accords.
Misri ilitambua Israel na Israel ikarudisha Sinai Peninsula lililotokana na vita iliyoanza mwaka 1948

Ni makubaliano hayo ndiyo yaliyoplekea kifo cha Anwar Sadat kwa baadhi ya Waarabu kusema Sadat amewasaliti.

Kwa upande wa Israel huo ulikuwa ushindi mkubwa kwasababu Misri ni Taifa lilikokaribu sana na lenye nguvu za kijeshi.

Tangu wakati huo Misri imekuwa msuluhishi wa mgogoro kati ya Wapalestina na Israel.

Katika hali isiyo ya kawaida, Rais Trump aliwaalika Taliban kwa mazungumzo ya amani Camp David, siku 4 kabla ya maadhimisho ya 9/11 ambako Talibani wakiwa washirika wa Alqaeda walifanya yao dhidi ya Taifa kubwa.

Kuwaalika Taliban ilikuwa kofi la uso dhidi ya Republicans ambao siku zote hawakuta kusikia Rais Obama anaingia majadiliano nao.

Mbaya Taliban walialikwa Camp David kama wageni mashuhuri siku chache kabla ya 9/11

Kufuatia mashambulizi Afghanistan, Rais Trump alikatisha mazungumzo hayo.

Hata hivyo habari za ndani ni kuwa VP Pence na Mshauri wa Usalama John Bolton hawakukubaliana na hatua ya Rais Trump hasa kuelekea 9/11

Nyuma ya pazia kulikuwa na mtifuano kati ya Secretary of state( huku kwetu waziri wa mambo ya nje) na John Bolton mshauri wa Usalama.

Bolton inaelezwa kuwa na misimamo mikali hasa siasa za Korea Kaskazini na Iran na kwamba Pompeo ni mnyenyekevu kwa Trump aliyemtimua John Bolton leo hii.

Bolton kabla ya hapo alikuwa balozi wa Marekani UN na baadaye kuwa mwanasiasa nguli katika Televisheni akimnanga Obama kuhusu siasa za nje.

Leo akitazama nyuma, Bolton atajisikia mnyonge kwani kutimuliwa kwake hakukuwa na stara.

John Bolton ni mshauri wa 3 wa Rais Trump kutimuliwa na katika muda wa miaka 3 .
Rais Trump anaelekea kuwa na mshauri wa 4.

Hili linaeleza siasa za nje za Marekani zilivyo shaghabala chini ya Make America great again.

Ni haki kusema hakuna anayejua Rais Trump anasimamia nini na ana mkakati gani kuhusu siasa za nje. Korea kaskazini hali ni ile ile, Iran hali inazidi kuwa mbaya, huku kukiwa na fukunyuku Japan na Korea kusini.

Vita ya uchumi na China haionekani kusaidia hali wakati nchi washirika wa Ulaya zikionekana kujitenga na Mtawala Trump. Mashariki ya kati hakuna kinachoendelea !

Hayo yote yakiendelea hakuna ushahidi wowote kwamba siasa za Trump zimeweza kufanya mabadiliko aliyoahidi zaidi ya kuvuruga hali ya mambo.

Wakati huo huo Rais wa Taifa hilo lenye nguvu za kiuchumi na ulinzi ameendelea kuwa na malumbano ya hovyo kabisa na kudhalilisha na Raia wa kawaida.

Kwa sehemu kubwa Rais Trump amekuwa kichekesho cha dunia na kama alivyowahi kusema ikiwa dunia iliicheka Marekani kwa siasa za Obama, kwasasa haicheki tena, dunia imepigwa ganzi na kutunduwaa ikijuiliza hii ni Marekani wanayoijua ?

Tusemezane
 
Kila siku huwa najiuliza ile kauli ya "we do not talk to terrorists" au "we do not negotiate with terrorists" sijui imeishia wapi. The Donald ni kituko sana, ashukuru Mungu yeye ni mzungu,. Kila siku huwa najiuliza ingekuwaje kama Obama angefanya robo ya aliyofanya Trump.

Issue ya Bolton ni wazi kabisa, unajua ukiangalia kwenye maswala ya sera ya mambo ya nje Trump na Obama kimisngi hawana tofauti, japokuwa Obama kama rais kwa kiasi fulani alikuwa kulia sana.Naamini Bolton angeweza kudumu kwenye serikali ya Obama kama angekuwepo, kuliko ya The Donald.
 
YALIYOJIRI VIUNGA VIKUU VYA DC
LINGINE LINFUKUTA CHINI CHINI WH

Wiki hii yametokea mengi ndani ya viunga vya DC yakihusisha mambo kadha wa kadha na hasa yanayomgusa Rais Trump kwa namna mbali mbali.

Amshambulia Obama
Rais Trump katika hali isiyo ya kawaida aliamua kumwendea kombo Rais mstaafu Obama.

Kwanza, Rais Trump alimtuhumu Obama kama kiongozi dhaifu aliyeacha kujaza nafasi takribani 150 za majaji wa mahakama kuu ikiwemo supreme court.

Hapa alichotaka kuonyesha ni kuwa nafasi hizo hazikujazwa na Obama kwa uzembe tu.

Ukweli: Kipindi cha pili cha utawala wa Obama, Seneti chini ya McConnel imekataa kuidhinisha mahakimu ikiwemo nafasi ya supreme court ambayo McConnel alikataa kuijadili kwa kisingizio cha uchaguzi upo karibu. Hivyo, habari hiyo haikuwa na ukweli na ilishangaza Rais wa Marekani ima hakujua utaratibu wa kupata majaji au kama kawaida hakuwa na chembe ya aibu

Pili, Rais Trump alimshutumu Rais Obama kwa kuandika vitabu na deal yake katika Netflix na kwamba yeye anatuhumiwa kutumia Hotel na biashara zake peke yake.

Bila aibu wala haya Rais huyo ameshindwa kuelewa kazi za Obama ni za Kiraia na kwamba hayo yametokea akiwa nje ya ofisi na hakuna sheria inayomzuia.

Kuhangaika kwa Trump kulionyesha jambo moja, kwamba, kuna linalomsumbua na anatafuta kuwaondoa watu katika mjadala uliokuwa unaelekea WH.

Whistle blower
Wiki hii House committee ilieleza uwepo wa habari zlizofukiwa zinazohusu WH.

Utaratibu wa Marekani ni kamati husika kujulishwa kuhusu hali mbali mbali za nchi.

Magazeti yakaandika habari za ''mpiga zumari'' kutoka idara ya Usalama wa Taifa.

Mtumishi huyo alifikisha malalamiko yake kwa mkaguzi mkuu wa serikali, IG (Inspector general) kuhusu kusikia maongezi kati ya Rais Trump na kiongozi mmoja yaliyokuwa na matatizo.

IG alifanya uchunguzi na kupeleka taarifa katika idara ya usalama ''DNI'' kuhusu madai hayo yaliyothibitika. DNI iliyapeleka katika idara ya sheria (DOJ) chini ya Bill Barr. aliyeyafukia.

Sheria inasema kamati za Bunge zipewe taarifa za usalama ndani ya siku 7 na kwamba, IG aisema suala hilo ni nyeti na hivyo lifikishwe mbele ya kamati.

Utawala wa Trump umekataa kamati za Bunge zisipewe taarifa ya mpiga zumari iliyohakikiwa na IG na idara ya usalama (DNI) kabla ya kufunikwa na DOJ

Leo magazeti yanataarifu kuwa maongezi yalikuwa baina ya Trump na kiongozi wa Ukraine.
Mazungumzo hayajawekwa hadharani lakini inaonyesha kuna jambo linalofichwa.

'' Habari zinazozagaa ni kuwa Trump aliruhusu pesa ziende Ukraine kwa ujira wa kumchunguza mgombea Urais wa Democrats na VP Bidden kuhusu madai ya rushwa''

Kwamba alimtaka Rais wa Ukraine amfanyie uchunguzi Biden ili iwe kashfa kwa mgombea huyo. Imeripotiwa mara nyingi kwamba, Joe Biden anamnyima Trump usingizi kuelekea 2020

Kama habari hizo ni za kweli, na tutajua muda si mrefu, kuna uwezekano Rais Trump alitumia ofisi ya umma kwa masilahi yake binafsi na kwamba alitumia ofisi dhidi ya Wapinzani wake.

Tunasisitiza, ukweli kuhusu maongezi haujajulikana lakini inatosha kusema kuwa IG amekwenda mbele ya kamati za Bunge na kuthibitisha kuwa madai ni ya dharura na kwa masilahi ya Taifa.

Ieleweke kwamba Rais wa Marekani hajafanya kosa kuongea na viongozi wa dunia hata kama ni mahasimu wa Marekani. Tatizo ni asili ya maongezi na kwamba yalizingatia masilahi ya nchi?

Endapo mazungumzo yatakuwa kinyume na utaratibu na kwamba yanakiuka miiko ya WH na sheria za nchi, kuna tatizo.

Habari hizi ni za awali zinazovuma katika anga za habari za DC na kwamba, tutaendelea kuwajuza nini hasa kinatokea. Inatosha sana kusema '' kuificha habari hii kunazua maswali kuliko majibu'' ni kwanini na maongezil yalilenga nini!

Tusemezane
 
VIUNGANI DC
SAKATA LA ''WHISTLE-BLOWER'' LACHUKUA SURA MPYA

Lile sakata tulilosema hapo juu kuwa linafukuta sasa limechukua sura mpya.
Kikao cha wabunge wa Democrats kimeamua mchato wa kumshtaki Rais ''impeachment'' uendelee katika kamati zake zote.

Seneti nayo imetaka kupata nyaraka za maongezi kati ya Rais Trump na Rais wa Ukraine
WH nayo inasema itatoa ''transcript'' za maongezi leo Jumatano.

Wengi watajiuliza nini hasa kimetokea hadi kufikia hapo?

Ni kwamba wakati wa utawala wa Obama, Urusi ilichukua eneo la Cremia kule Ukraine
Obama na nchi za Ulaya zikakaubaliana kuiunga mkono Ukraine kwa misaada

Makamu wa Rais wakati huo Joe Biden ambaye sasa ni mgombea aikwenda Ukraine kushinikiza prosecutor wa kesi xa corruption aondolewe.
Hilo lilifanyika kwa ushirikiano na nchi za Ulaya.

Wakati huo huo Mtoto wa Biden( Hunter Biden) alikuwa anafanya kazi na kampuni ya Ukraine.

Tuhuma zikatokea kwamba prosecutor aliondolewa kwasababu ya kuchunguza kampuni ambayo Hunter alikuwa mwajiriwa na Board Member.

Iliundwa tume na kuchunguza ikabainika hakuna mahusiano kati ya kampuni iliyochunguzwa na tuhuma za rushwa wala Hunter Biden hahusiki na lolote lile katika aliyochunguzwa.

Biden alipotangaza kuwania Urais, ilionekana dhahiri alikuwa ni tishio kwa Trump.
Kura zote za maoni zikiwemo zilizoendeshwa na TV Fox zilitoa matokea sawa sawa.

Trump akamtuma mwanasheria wake binafsi Rudy Giulian kwenda Ukraine kukutana na Rais Zelewensky ambaye amaechaguliwa muda si mrefu.

Hiyo ilikuwa ziara ambayo Rudy alisema anakwenda kama mwanasheria binafsi kutafuta ukweli kuhusu kesi ya Biden na Hunter Biden. Kwamba, kuna uhusiano kati ya kesi na Biden Family.

Wiki moja iliyopita mwenyekiti wa kamati ya House ya intelejensi Bw. Adam Schiff alitaka maelezo kutoka kwa Director of national intelligence (DNI)kwanini taarifa ya Mkaguzi mkuu wa serikali,IG (Inspector general) haijapelekwa kwa kamati.

Ni taarifa ya Whistle Blower(WB) anayefanya kazi kazi katika idara ya Intelejensia.
WB alisikia maongezi yaliyomfanya apeleke malalamiko kwa IG kama Whistle Blower.

IG alisema kuna malalamiko kutoka kwa Whistle blower ambayo yamethibitika kwamba ni kweli na kwamba ni ya dharura kupelekwa kwa kamati ya Bunge (House)

DNI alipotakiwa aseme kwanini hakupeleka taarifa akasema ni kutokana na kutoona umuhimu.
Baadaye akasema amepata shinikizo kutoka White House

Hapo ndipo fukunyuku za waandishi zilipoanza na kubaini kuwa, msaada kwa Ukraine kwa milioni takribani 200 uliidhinishwa kwenda Ukraine kukabiliana na Russia mwaka huu.

Trump alizuia pesa hizo zisitolewe siku moja tu baada ya Mueller kutoa taarifa ya Russia.

Imebainika pia kuwa pesa hizo zimeachiwa baada ya kamati ya Bunge kuhoji kuhusu taarifa ya IG ambayo ilitakiwa ifike kwa kamati.

Sakata limeendelea hadi Trump alipokiri kuwa maongezi yake ya simu alishikiza Rais wa Ukraine afanye uchunguzi kuhusu mtoto wa Biden kwa rushwa.

Kumbuka mtoto wa Biden alishasafishwa, lakini Trump anamshinikiza Rais wa Ukraine afanye uchunguzi kwa mtoto huyo.

Inaendelea....
 
Sehemu ya II

Kwahiyo kuna mambo ya kuangalia katika sakata hili ili kujua kwanini kuna mchakato wa Impeachment na kwanini House imeshikilia bango jambo hilo.

1. Trump atakuwa Rais wa 3 baada ya Bill Clinton na Andre Johnson kuwa impeached
Clinton alishtakiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi katika uzinzi kwa ile kesi maarufu- Lewenski. Kesi ya Monical ilianzia hauri jingine hadi ilipotua kwa Lewensiki.Bill alinusurika katika Seneti

2. Johnson alishtakiwa kwa makosa 11, naye pia kunusurika baada ya Seneti kukataa

3. Trump anakabiliwa na chunguzi kadhaa lakini hili linaonekana huenda likawa ni tatizo.
WH inasema itatoa script za maongezi ingawa haijulikani kama itakuwa yote.
Mkuu wa DNI naye kaitwa mbele ya kamati za Bunge kama ilivyo kwa Whistle Blower

4. Kuna uwezekano hakuna kitu kibaya alichofanya Trump, hata hivyo kuna kila sababu ya kuwa na shaka kutokana na mtiririko wa matukio.

a) Trump alizuia msaada ulioidhinishwa na Bunge siku moja baada ya Taarifa ya Mueller
b) Inspector general alipeleka taarifa kwa DNI kuhusu udharura na taarifa hiyo ilitakiwa ifike mbele ya kamati ya Bunge. DNI alikaa kimya na taarifa hiyo hadi ilipovuja? Kwanini?
c) WH imeshinikiza DNI isitoe taarifa hiyo! ikiwa ni maongezi ya kawaida , ni kwanini?
d) Kwanini kuna maelezo tofauti ya Trump kuhusu sakata hili? Kwanza, kakiri alishinikiza Ukraine imchunguze Hunter Biden. Kwanini alitumia mwanasheria binafsi na si kutoka DOJ?

Hayo na mengine yanaongeza shaka kuhusu utata wa suala zima.
Kilichobaki ni kupata nakala halisi ya maongezi, ya DNI na maelezo ya Whistle Blower.

Ikiwa itabainika pasi shaka kwamba Trump alishinikiza kuhusu uchunguzi hapo kuna tatizo.

Itaonekana Trump anatumia madaraka dhidi ya Wapinzani wake kwa kutumia mataifa ya nje.

Hayo yakiendelea wapo watakaojiuliza kwanini Trump anataka uchunguzi dhidi ya Hunter Biden na si Baba yake Joe Biden?

Hunter Biden alikuwa board Member wa kampuni ya Ukraine.
Kinachotakiwa ni kuunganisha rushwa kati ya Hunter Biden na kufukuzwa kwa prosecutor kulikofanywa na Joe Biden.

Kwamba Hunter Biden akionekana na makosa, itaunganishwa kuwa Joe Biden aliyemfukuza prosecutor kumlinda mwanae.

Hiyo itakuwa ni kashfa itakayomsumbua Joe Biden akiwa gombea wa Urais, tishio kwa Trump.

Kwa upande wa Biden, hatua alizochukua zilikuwa za Utawala wa Obama na nchi za Ulaya. Uchunguzi uliofanyika haukubaini lolote isipokuwa kumsafisha Joe Biden.

Mtoto wake Hunter hana uhusiano na rushwa au kufukuzwa kwa prosecutor.

Kazi imebaki kwa Rais Trump. Ikiwa alichokifanya kitakuwa kinyume cha kiapo cha ofisi ''Oath'' kuna tatizo kubwa sana. Impeachment inaweza kuwepo katika House.

Ndani ya Seneti kuna hati hati ! Impeachment inaweza kushindwa hapo, majority ni Republicans

Wasi wasi uliopo ndani ya Trump team ni jinsi hali inavyoweza kubadilika bila kutarajia.

Rais Nixon aliondolewa madarakani na wenzake wa Republicans
Lakini kwa Trump historia ndiyo itakayomuumiza hasa akiwa ni wa 3 kufanyiwa Impeachment

Sakata hili linaendelea kufuatiliwa, hadi hapo transcript na ushahidi wote utakapopatikana ni mapema mno kusema kama mchakato wa impeachment utakuwa na mwelekeo gani.

Kwa upande wa Democrats kuna shinikizo la muda mrefu la impeachment.

Speaker Nancy Pelos amekuwa mgumu kwa kuwa makini sana kwani impeachment ina utaratibu wake ambao ushahidi unatakiwa usiwe na shaka ili umma uwe upande wao.

Kwa bahati mbaya sana shinikizo hasa la vijana wageni katika House halionekani kuzingatia umakini. Wao wanachotaka ni impeachment bila umakini.

Kwa mfano, kwanini waanze mchakato kabla ya transcripts zote hazipjapatikana?

Je, kama hakuna jambo baya, nini itakuwa sababu ya mchakato ukiachilia sababu nyingine ambazo ushahidi wake umekuwa mgumu kupatikana japo upo?

Tunaendelea kufuatiliwa na Leo jioni tutawajulisha nini kinaendelea katika anga za viunga vikubwa vya District of Columbia.

Tusemezane
 
Hivi 'Russia collusion' na 'Obstruction of Justice' zimeishia wapi? Chunguzi za Tax returns na Financial Statement za Trump zimeishia wapi? Madai ya Trump kutajirika kwenye Urais yameishia wapi? Hadi nimesahau zingine!

Sasa hivi ni mazungumzo (call transcript) kati ya Trump na Rais wa Ukraine! Crazy Dems! Si ajabu baadhi ya Dems kusema bila 'impeachment' hawawezi kumshinda Trump. Dems wanatia huruma, ndio maana wanaokota chochote watakachokutana nacho dhidi ya Trump ili mradi gurudumu lao la uchunguzi liendelee kuzunguka.

Whistle-blower:

IG wa Intel community alisema kwenye maelezo yake kuwa kuna viashiria vya kutosha kuwa Whistle-blower ana 'political bias' unaoegemea kwa mpinzani mmoja wa Trump kisiasa. Kwahiyo ngonjera zake haina uzito, waliomtuma hawakujiandaa vizuri.

Case closed.

Call transcript (mazungumzo ya simu) kati ya Trump na Rais wa Ukraine:

Kutokana na uwazi alio nao Trump, WH ilitoa maandishi (transcript) ya mazungumzo yaliyokuwa yanapigiwa kelele na Dems.

Kilichoonekana pengine ni tofauti na matarajio ya Dems, walijua watapata kitu chenye uzito ili wamkaange Trump, lakini imekuwa tofauti.

Ili kesi ya Dems iwe na uzito, ilibidi ionekane kitu kinaitwa 'quid pro quo' yaani 'nipe nikupe', kwamba Trump alizuia msaada wa Marekani wa kijeshi kwa Ukraine hadi Rais wa Ukraine aanzishe uchunguzi dhidi ya Hunter Biden. 'Quid pro quo' haipo kwenye transcript.

Imegundulika, Trump alimzungumzia Biden baada ya Rais ws Ukraine (Zelenskiy) kwanza kuhitaji kukutana na Rudi Giuliani.

Trump pia hakuzungumzia msaada wa kijeshi aliozuia kwa Ukraine katika mazungumzo yake na Rais wa Ukraine.

Mwanzoni katika mazungumzo hayo, Zelenskiy anamshukuru Trump kwa msaada na kusema anafanya maandalizi ya kuangiza vingine vifaa vya kijeshi, hali inayoonyesha hakuwa anafahamu kuwa kuna msaada uliozuiliwa na Marekani.

Case closed.

Trump pia anazungumzia 'server ya DNC' ambapo anasema watu wanasema Ukraine inayo, kwamba angependa Ukraine ichunguze. Hiyo 'server' ya DNC inaaminika kuficha uchafu mwingi wa Dems. Rais wa Ukraine aliahidi kufanya uchunguzi wa wazi.

DOJ walichunguza iwapo Trump alikiuka sheria za fedha za kampeni (campaign finance laws) katika mazungumzo yake na Zelenskiy na kuhitimisha wiki iliyopita kuwa hakukiuka sheria hizo.

Kitendo cha Dems kuokoteza na kutafuta chochote hata cha uongo dhidi ya Trump ili kukidhi matamanio yao ya 'impeachment', ni kuendeleza zilezile siasa za majitaka zisizo na tija yoyote.

Dems wanasababisha 'House' kuonekana kituko, hawana cha maana hadi wanaboa. Juzi Trump alitoa bonge la Speech UN lakini wao siku hiyohiyo wanaongea utumbo wao wa kila siku.

Nina uhakika hata Adam Schiff au Nancy Pelosi wakiulizwa privately/off record, kwamba kwanini Dems wanafanya vituko vya kurukia vitu ili mradi, hawatakuwa na jibu la maana zaidi ya kutaka kufurahisha watu kama muanzisha hii thread. Ila hakuna vya maana kwenye hivi vituko vya Dems.

Huu uzi umepoteza mvuto, ukiachana na 'political bias' na ukosefu wa 'objectivity', huu uzi umekuwa wa kutoa taarifa za tuhuma na chunguzi za Dems zisizokuwa na maana yoyote!
 
...Huu uzi umepoteza mvuto, ukiachana na 'political bias' na ukosefu wa 'objectivity', huu uzi umekuwa wa kutoa taarifa za tuhuma na chunguzi za Dems zisizokuwa na maana yoyote!
Wow, masikini El Jefe, umetokea wapi tena? Tatizo letu kubwa ni Utanzania wetu, tunaangalia kila kitu kwa jicho la Kitanzania, how sad. Marekani ilikuwa hivi hivi zaidi ya miaka 400 iliyopita hadi Wamarekani walipoamua, hapana, we will from now be a republic. Bahati mbaya waliotangulia kujiita Republicans, Trump ameweza kuwatoa kwenye reli lakini je watafanikiwa? Remember...I could stand in the middle of Pennsylvania Ave and shoot somebody in broad daylight and my voters would never abandon me! Nunua pop-corn!
 
YANAYOENDELEA DC
WH imetoa transcript za mangezi kati ya Rais Trump na Zelensky wa Ukraine.
Nyaraka hiyo ambayo sasa inaitwa ''rough'' imetolewa na WH ya Trump.

Pengine kwa kuhofia yajayo WH imetoa baadhi ya sehemu ikidhani zinaweza kusaidia.
Hoja kubwa waliyokuwa nayo ni kitu kijulikanacho kama ''quid pro quo'' yaani nipe nikupe
Yaani walijua kutokuwepo kwa maombi rasmi kutaondoa quid pro quo.

Ukisoma kwa undani, Transcript Trump alimtaka Rais wa Ukraine afanye jambo kwa Joe Biden na mtoto wake, yaani aanzishe uchunguzi utakaomtia Hunter matatani na kisha Joe Biden

Viunga vya DC ni vikubwa, kila linalosemwa linahakikiwa. Kuna nyaraka ya April iliyopatikana.

Imethibitika kuwa Trump na mwanasheria wake Rudy wameshinikiza uchunguzi wa Ukraine.
Katika hilo Rudy kama mwanasheria binafsi amesema alitumwa na State department.

Pompeo anakana kuhusu hilo. Tayari kuna kamati ya Bunge inataka nyaraka za State dept

Nyaraka imemtaja Bill Barr, Attorney General kwamba ashirikiane na Rudy Gullian.

Barr ni yule yule aliyechukua taarifa ya Mueller ya kurasa 400 na kuandika kurasa 4 akiacha mambo mengine katika kumkingia kifua Trump

Uchunguzi wa Ukraine unazidi kupanuka, kuna watu wawili muhimu, SoS Pompeo na Bill Barr.
Kwa namna yoyote kutajwa kwa AG Barr kutamlazimu kutojihusisha na suala hilo''recuse''

Wakati huo huo, ile classified report ya whistle Blower nayo imepatikana.
Haijaeleweka kama ilikuwa kamili au redacted. Walioisoma ni wahusika kisheria na tayari kuna maseneta wawili wa Reublicans wameieleza kama taarifa ya kuudhi ''disturbing'

Kinachofuata ni kufanya declassification ili iweze kuwekwa hadharani ikiwa redacted.

Kwa taarifa ni kuwa whistleblower amelindwa, Trump hamjui kama ni mwanamke au mwanaume

Kitu kimoja muhimu, Inspector general amesema taarifa ya whistle-blower ni ya uhakika na inahitaji udharura. Taarifa ilikuwa declassified na WH ika classify dakika za mwisho.

Tukirudi kwa Inspector general, huyu ameteuliwa na rais Trump kama ilivyo DNI Maguire.

Whistleblowe amekubali kuhojiwa na kamati ya Bunge. Hapo napo tutarajia kusikia ikiwa transcript ilikuwa sahihi, na taarifa yake ya awali iliyotolewa na WH haikunyofolewa.

DNI naye amekubali kufika mbele ya kamati ya Bunge akisisitiza kuwa ikiwa atatakiwa ''kufunga'' mdomo na hatakuwa huru atajiuzulu.

Hili nalo linapeleka mtetemeko WH kwani hakuna anayejua DNI anataka kunena nini.

Kwa siasa za DC klichotokea ni chambo, kwamba kazi ndiyo imeanza.

Kesi ni mbichi na inaelekea itakuwa na mshindo kwa Rais Trump.
Hata Rais Trump ameonekana kupoteza majigambo kwa siku mbili tatu kuchelea taarifa hiyo.

Mwelekeo wa shauri la Ukraine utatoa picha kamili ikifika Ijumaa baada ya kumsikia Maguire wa DNI na Whistle Blower. Hawa ndio wataunga vipande vilivyogizani hadi sasa.

Kwa wanaopata taarifa kutoka tweet za Trump, kesi imeskwisha! na uchunguzi ni kwa Biden.

Tutaendelea kuwajuza siasa za viunga vya District of Columbia

Tusemezane
 
YANAYOENDELEA DC
WH imetoa transcript za mangezi kati ya Rais Trump na Zelensky wa Ukraine.
Nyaraka hiyo ambayo sasa inaitwa ''rough'' imetolewa na WH ya Trump.

Pengine kwa kuhofia yajayo WH imetoa baadhi ya sehemu ikidhani zinaweza kusaidia.
Hoja kubwa waliyokuwa nayo ni kitu kijulikanacho kama ''quid pro quo'' yaani nipe nikupe
Yaani walijua kutokuwepo kwa maombi rasmi kutaondoa quid pro quo.

Ukisoma kwa undani, Transcript Trump alimtaka Rais wa Ukraine afanye jambo kwa Joe Biden na mtoto wake, yaani aanzishe uchunguzi utakaomtia Hunter matatani na kisha Joe Biden

Viunga vya DC ni vikubwa, kila linalosemwa linahakikiwa. Kuna nyaraka ya April iliyopatikana.

Imethibitika kuwa Trump na mwanasheria wake Rudy wameshinikiza uchunguzi wa Ukraine.
Katika hilo Rudy kama mwanasheria binafsi amesema alitumwa na State department.

Pompeo anakana kuhusu hilo. Tayari kuna kamati ya Bunge inataka nyaraka za State dept

Nyaraka imemtaja Bill Barr, Attorney General kwamba ashirikiane na Rudy Gullian.

Barr ni yule yule aliyechukua taarifa ya Mueller ya kurasa 400 na kuandika kurasa 4 akiacha mambo mengine katika kumkingia kifua Trump

Uchunguzi wa Ukraine unazidi kupanuka, kuna watu wawili muhimu, SoS Pompeo na Bill Barr.
Kwa namna yoyote kutajwa kwa AG Barr kutamlazimu kutojihusisha na suala hilo''recuse''

Wakati huo huo, ile classified report ya whistle Blower nayo imepatikana.
Haijaeleweka kama ilikuwa kamili au redacted. Walioisoma ni wahusika kisheria na tayari kuna maseneta wawili wa Reublicans wameieleza kama taarifa ya kuudhi ''disturbing'

Kinachofuata ni kufanya declassification ili iweze kuwekwa hadharani ikiwa redacted.

Kwa taarifa ni kuwa whistleblower amelindwa, Trump hamjui kama ni mwanamke au mwanaume

Kitu kimoja muhimu, Inspector general amesema taarifa ya whistle-blower ni ya uhakika na inahitaji udharura. Taarifa ilikuwa declassified na WH ika classify dakika za mwisho.

Tukirudi kwa Inspector general, huyu ameteuliwa na rais Trump kama ilivyo DNI Maguire.

Whistleblowe amekubali kuhojiwa na kamati ya Bunge. Hapo napo tutarajia kusikia ikiwa transcript ilikuwa sahihi, na taarifa yake ya awali iliyotolewa na WH haikunyofolewa.

DNI naye amekubali kufika mbele ya kamati ya Bunge akisisitiza kuwa ikiwa atatakiwa ''kufunga'' mdomo na hatakuwa huru atajiuzulu.

Hili nalo linapeleka mtetemeko WH kwani hakuna anayejua DNI anataka kunena nini.

Kwa siasa za DC klichotokea ni chambo, kwamba kazi ndiyo imeanza.

Kesi ni mbichi na inaelekea itakuwa na mshindo kwa Rais Trump.
Hata Rais Trump ameonekana kupoteza majigambo kwa siku mbili tatu kuchelea taarifa hiyo.

Mwelekeo wa shauri la Ukraine utatoa picha kamili ikifika Ijumaa baada ya kumsikia Maguire wa DNI na Whistle Blower. Hawa ndio wataunga vipande vilivyogizani hadi sasa.

Kwa wanaopata taarifa kutoka tweet za Trump, kesi imeskwisha! na uchunguzi ni kwa Biden.

Tutaendelea kuwajuza siasa za viunga vya District of Columbia

Tusemezane
Ushaanza kukimbizana na hili nalo! Mbona utachoka mkuu maana kila lisemwalo kwenye liberal media unalichukua unaanza kutoa updates humu, likionekana ni kimeo unaachana nalo unazoa lingine.

Hii ni kwa sababu wewe kama wewe huna mawazo na fikra huru, unaingia kwenye liberal media unaanza kutoa updates wanazotoa wao. Wakiachana na topic fulani na wewe humu unaachana nayo! Wakikaa kimya na wewe humu unakaa kimya!

Nadhani 'uelewa' mkubwa ulio nao kwenye siasa za US ni wa kumeza yanayosemwa kwenye liberal media na kuyaandika humu, nje ya hapo, hamna kitu.

Hapo unasubiri waseme tena halafu uje uendeleze stori humu. Jitahidi uwe 'objective' na usiongozwe na 'bias'.
 
Wow, masikini El Jefe, umetokea wapi tena? Tatizo letu kubwa ni Utanzania wetu, tunaangalia kila kitu kwa jicho la Kitanzania, how sad. Marekani ilikuwa hivi hivi zaidi ya miaka 400 iliyopita hadi Wamarekani walipoamua, hapana, we will from now be a republic. Bahati mbaya waliotangulia kujiita Republicans, Trump ameweza kuwatoa kwenye reli lakini je watafanikiwa? Remember...I could stand in the middle of Pennsylvania Ave and shoot somebody in broad daylight and my voters would never abandon me! Nunua pop-corn!

Kutumia neno 'maskini' katika sentensi yako haikuwa na ulazima wowote, kwa sababu wa kuonewa huruma ni Dems na mashabiki wao kwa vituko vyao.

Nafikiri sio busara kujificha kwenye kichaka cha 'Utanzania wetu' au 'jicho la kitanzania' ili kupinga mawazo tofauti hasa katika masuala haya ya US. Kwanza, unajidhalilisha mwenyewe kama mtanzania, pili, unaweza kuniambia ni sehemu gani nimetumia utaratibu, sheria au kitu chochote cha Kitanzania kuelezea hoja zangu?

Lakini inabidi uelewe kuwa mimi sizolewi na liberal media za US, natafakari nje ya box lao, ndio maana siandiki mapambio yao humu. Kwamba kila wakisema chochote hata kama ni uzushi au uongo au wakidai uchunguzi uchwara niandike humu kama unavyofanya wewe na muanzisha uzi.

Marekani ilikuwa hivi hivi miaka 400 iliyopita? Kwa maana ya kuanzia 1619? Unajumuisha na miaka zaidi ya 168 ya ukoloni? Vituko wanavyovifanya Dems kwa Trump havijawahi kufanywa kwa POTUS yeyote! Muhimu ni kuwa Republicans na wananchi hawayumbishwi na hivi vituko.

Ukisikiliza 'development' ya hiyo quote ya Trump ulioandika hapo utaona ilikuwa purely a 'joke', lakini wewe umeshikilia bango, wakati wamarekani wenye akili zao waliona ni utani na bado wakampa Trump Urais.

Huwa nina-debate na liberals, lakini you guys are so low, mnaimba tu 'impeachment' humu kwa makosa ya kutafuta tokea hii thread ilivyoanzishwa kwa mbwembwe. This is really boring!
 
Kutumia neno 'maskini' katika sentensi yako haikuwa na ulazima wowote, kwa sababu wa kuonewa huruma ni Dems na mashabiki wao kwa vituko vyao.

Nafikiri sio busara kujificha kwenye kichaka cha 'Utanzania wetu' au 'jicho la kitanzania' ili kupinga mawazo tofauti hasa katika masuala haya ya US. Kwanza, unajidhalilisha mwenyewe kama mtanzania, pili, unaweza kuniambia ni sehemu gani nimetumia utaratibu, sheria au kitu chochote cha Kitanzania kuelezea hoja zangu?

Lakini inabidi uelewe kuwa mimi sizolewi na liberal media za US, natafakari nje ya box lao, ndio maana siandiki mapambio yao humu. Kwamba kila wakisema chochote hata kama ni uzushi au uongo au wakidai uchunguzi uchwara niandike humu kama unavyofanya wewe na muanzisha uzi.

Marekani ilikuwa hivi hivi miaka 400 iliyopita? Kwa maana ya kuanzia 1619? Unajumuisha na miaka zaidi ya 168 ya ukoloni? Vituko wanavyovifanya Dems kwa Trump havijawahi kufanywa kwa POTUS yeyote! Muhimu ni kuwa Republicans na wananchi hawayumbishwi na hivi vituko.

Ukisikiliza 'development' ya hiyo quote ya Trump ulioandika hapo utaona ilikuwa purely a 'joke', lakini wewe umeshikilia bango, wakati wamarekani wenye akili zao waliona ni utani na bado wakampa Trump Urais.

Huwa nina-debate na liberals, lakini you guys are so low, mnaimba tu 'impeachment' humu kwa makosa ya kutafuta tokea hii thread ilivyoanzishwa kwa mbwembwe. This is really boring!
Kwa sababu labda hujui umuhimu wa kinachoendelea nchini Marekani, nakupa ushauri tu mdogo; nunua pop-corn, since now it is all system go, just sit down and watch...the genie is outside the bottle! Tick...tack...tick...tack....

Kumbuka: The obligation of the President of the US is to defend the institutions of democracy, to defend the system of checks and balances that the Constitution enshrines and to defend the rule of law...

What was witnessed today was the precursor before the first preliminary official hearing in the impeachment inquiry process and one thing stood out...not one single Republican defended the President's action.

Even the Senate Majority Leader Mitch Mcconnel was dumb-struck...what was unfolding left no room for any doubt as to the nature and significance of the president's action...corrupt abuse of power and coverup, stay tuned!

Contrary to what you may believe you know, the President of the United States of is not above the Law but this one has been acting so since the day he assumed office and now time and tide are finally catching up with him!
 
NDANI YA VIUNGANI DISTRICT OF COLUMBIA
HALI INABANA WH, GOP WATAABIKA KUTETEA YANAYOTOKEA

DNI Maguire amefika mbele ya kamati ya Bunge wiki chache baada ya kuteuliwa (Acting).
Maswali yaliyomkwaza ni iwapo aliongea na Rais Trump kuhusu ripoti ya Whistleblower.

Maguire amasema 'whistleblower'' alifuata taratibu zote katika kufikisha malalamiko yake.

Hata hivyo Maguire alishindwa kutetea hoja ya kwamba, alipopata taarifa ya Inspector general(IG) aliwasiliana na White house na DOJ kwa ushauri.

DOJ inaongozwa na AG Barr aliyesema hakuna jambo la kufanyiwa uchunguzi katika suala hilo

Acting DNI Maguire alishindwa kutetea hoja kwamba, ikiwa AG alitajwa katika transcript na whistleblower na WH ndiyo inayotuhumiwa, ilikuwaje aombe ushauri kwa ''watuhumiw''

Kingine kilichojitokeza ni Republicans kupamba wasifu wa DNI lakini hawakuwa na hoja hata za kubabaisha za kupindisha ukweli uliokuwa mbele yao.

Taarifa zinazidi kupanuka baada ya nakala ya Whistle blower(WB) kupatikana ikiwa redacted tofauti na ile ya jana iliyosomwa na kundi maalumu la Bunge.

Taarifa inaonyesha kuwa kulikuwa na ''rough transcript'' zilizofichwa katika kompyuta maalum inayohifadhi nyeti ''highly classified information''. Transcript ya maongezi ya Rais si sehemu ya.

Kinachoonekana, wasaidizi waliamua kuficha maongezi katika kompyuta hiyo yasiweze kupatikana kwa urahisi na watu wa kawaida.

Hapa inatukumbusha Trump alipomzogoa Hillary Clinton kwa kutumia server nje ya ile ya state department '' what goes around comes around'' na wala si mara moja.

Kuhifadhi taarifa hizo inaonekana kama ''cover up ya abuse of powe''

Kuna ufanano wa cover up ya Richard Nixon na Watergate.
Tofauti ni kwamba ya Richard Nixon ilikuwa local hii ya Trump inahusisha nchi za nje.

Whistle blower anasema yote yalifanywa na watumishi-WH na walijua hakikuwa sahihi.

Suala linaelekea wapi?

Sasa limeondoka katika quid pro quo ambayo ipo kimtindo na kuhusisha mambo mengine.

State dept. itahusika kueleza Rudy Gullian alikuwa na nafasi gani akiwa Rais na mwanasheria binafsi wa Rais

Pili, watu waliohamisha rough transcript kule WH watahojiwa nani aliwaagiza na kwanini?

Tatu, mwanasheria mkuu AG Barr ambaye amekuwa kinga kwa Trump sasa anaelekea kupoteza nguvu hizo. Kitendo cha kutajwa katika transcript kinajenga 'conflict of interest ' na hataweza kusimamia suala hilo ikihitajika DOJ, itabidi aji ''recuse'' kama Session

Wigo wa watu kuanzia WH, State Dept. , DOJ ni mkubwa na kuna uwezekano wapo watakaoamua kuacha ''jahazi na kujitosa'' baharini kwani hali ilivyo si nzuri.

Sakata hili linaweza kufumua mengi, ni zito kwa kuangalia Republicans walivyopigwa butwaa. Katika hali ya kawaida wengi wangejitokeza kufanya ''spinning''

Sakata hili linachukua sura mpya kila uchao, hatujui kesho ina nini.
Tunachojua linaelekea mahali penye tatizo!

Tusemezane
 
Kwa sababu labda hujui umuhimu wa kinachoendelea nchini Marekani, nakupa ushauri tu mdogo; nunua pop-corn, since now it is all system go, just sit down and watch...the genie is outside the bottle! Tick...tack...tick...tack....

Kumbuka: The obligation of the President of the US is to defend the institutions of democracy, to defend the system of checks and balances that the Constitution enshrines and to defend the rule of law...

What was witnessed today was the precursor before the first preliminary official hearing in the impeachment inquiry process and one thing stood out...not one single Republican defended the President's action.

Even the Senate Majority Leader Mitch Mcconnel was dumb-struck...what was unfolding left no room for any doubt as to the nature and significance of the president's action...corrupt abuse of power and coverup, stay tuned!

Contrary to what you may believe you know, the President of the United States of is not above the Law but this one has been acting so since the day he assumed office and now time and tide are finally catching up with him!
There is no official impeachment proceeding to date, partisan House Judiciary committee yapping about it doesn't make it so. Dems need a full House vote for that. Probably they haven't found anything to 'impeach' Trump for!

To wish the Republicans join the 'impeachment' bandwagon is one thing, actually joining is another thing. The Rebublicans questioned the credibility of the 'complaint' relative to the call transcript, they're smart, they know the puppet master. The Senate Majority Leader wasn't 'dump-struck' at any moment, this is his statement:

"It simply confirms that House Democrats' priority is not making life better for the American people - but their nearly three-year-old fixation on impeachment"

This is another sham story and you guys have picked it up and started trending with it, the same way you did with the previous fake stories.

What strikes me the most, is the degree of similarity between the concept of these Democrats' crazy projects and how anyone with an average intelligence can easily controvert them way before they unfold.

'Whistle-blower' report contain second-hand information, which could be very well written by any weak minded liberal. The dems orchestrated this whole 'Ukrainian' thing to lead to a similar endgame after they witnessed their 'Russian' story fell dead under water.

I'm proud that AG Barr saw right through them and decided not pursue the non-credible 'whistle-blower compaint'. House committees have lost their ground and they'll probably try to run with this fabrication too in an attempt to enliven their conspicuous agenda. Once this has been debunked too, it'll vanish without a trail, and you guys won't even discuss it.

I'm delighted though, that all these documents have been released to the American people, and the sentiment have actually improved in favor of Trump.

I think dems should go after Trump with a more 'convincing' story than these fairy tales if they want the Republican suppport in their ulterior motives. Apart from that, it'll just be one phony story after another.
 
There is no official impeachment proceeding to date, partisan House Judiciary committee yapping about it doesn't make it so. Dems need a full House vote for that. Probably they haven't found anything to 'impeach' Trump for!

To wish the Republicans join the 'impeachment' bandwagon is one thing, actually joining is another thing. The Rebublicans questioned the credibility of the 'complaint' relative to the call transcript, they're smart, they know the puppet master. The Senate Majority Leader wasn't 'dump-struck' at any moment, this is his statement:

"It simply confirms that House Democrats' priority is not making life better for the American people - but their nearly three-year-old fixation on impeachment"

This is another sham story and you guys have picked it up and started trending with it, the same way you did with the previous fake stories.

What strikes me the most, is the degree of similarity between the concept of these Democrats' crazy projects and how anyone with an average intelligence can easily controvert them way before they unfold.

'Whistle-blower' report contain second-hand information, which could be very well written by any weak minded liberal. The dems orchestrated this whole 'Ukrainian' thing to lead to a similar endgame after they witnessed their 'Russian' story fell dead under water.

I'm proud that AG Barr saw right through them and decided not pursue the non-credible 'whistle-blower compaint'. House committees have lost their ground and they'll probably try to run with this fabrication too in an attempt to enliven their conspicuous agenda. Once this has been debunked too, it'll vanish without a trail, and you guys won't even discuss it.

I'm delighted though, that all these documents have been released to the American people, and the sentiment have actually improved in favor of Trump.

I think dems should go after Trump with a more 'convincing' story than these fairy tales if they want the Republican suppport in their ulterior motives. Apart from that, it'll just be one phony story after another.
Just like AG William Barr, El Jefe, you have gone rogue. The “rumblings” you have given above is just the kind of talking point that a stooge like Sean Hannity of Fox News would spew out. Incidentally, which is your favourite news outlet, the one that you trust most? Well, let me guess, Fox News. For your information, most of Republican Senators are not commenting on the whistleblower's complaint pretending that they haven't had time to read it, you know why!

“I want to know who’s the person who gave the whistleblower the information because that’s close to a spy. You know what we used to do in the old days when we were smart with spies and treason, right? We used to handle it a little differently than we do now.” That's Donald Trump, the president of the United States of America. Would you say that this sounds more or less like a statement (threat) from the lawless leaders we have in Africa?

And this is the President of USA basically saying in the old days we would have killed the whistleblower. Ring a bell? In the old days a man would be hanged for treason on the spot. Except that in this case the whistleblower didn’t commit treason the President of the USA and his co-conspirators did. If Trump wants to go back to "the old ways" so badly, maybe he should be the first to be held accountable using "the old ways" tactics & punishments.

Of course you, El Jefe, would probably rationalize his statement as a joke, wouldn't you? It is probabaly true that the whistleblower's identity is not known, but the people he reported to as the Law requires are all Trump appointees and all believed the whistleblower's complaint was credible and urgent, right? Do you know what percentage of Trump appointees have fallen out of favor and resigned since he took office? Were they all democrats?

Yeah, I was forgetting one thing...altenative facts! All news outlets are corrupt and peddle fake news except for those that praise and worship him, ring a bell? Do you, El Jefe know what happens to any Republican who disagrees with Trump? Do you know why his last last national security adviser, John Bolton, resigned, oops, was fired? I could go on and on but I have had to learn a few things the hard way...like what is taking place in my own country right now!

This bring us to the United States Constitution and particularly the First Amendment that prevents the government from making laws which respect an establishment of religion, prohibit the free exercise of religion, or abridge the freedom of speech, the freedom of the press, the right to peaceably assemble, or the right to petition the government for redress of grievances.

Dictator's wouldn't happen or survive but for enablers and enablers happen to be just ordinary people like you and me. I am 100% sure that the great people of the United States of America would never, for any reason, sacrifice the First Amendment that was adopted on December 15, 1791, as one of the ten amendments that constitute the Bill of Rights. The coming fight isn't as easy as you are trying to insinuate and my advise to you, relax and enjoy the show.
 
Just like AG William Barr, El Jefe, you have gone rogue. The narrative you have given above is just the kind of talking point that a stooge like Sean Hannity of Fox News would give. Incidentally, which is your favourite news outlet, the one that you trust most? Well, let me guess, Fox News. For your information, most of Republican Senators are not commenting on the whistleblower's complaint pretending that they haven't had time to read it, you know why?

“I want to know who’s the person who gave the whistleblower the information because that’s close to a spy. You know what we used to do in the old days when we were smart with spies and treason, right? We used to handle it a little differently than we do now.” That's Donald Trump, the president of the United States of America. Would you say that this sounds more or less like a statement (threat) from the lawless leaders we have in Africa?

And this is the President of USA basically saying in the old days we would have killed the whistleblower. Ring a bell? In the old days a man would be hanged for treason on the spot. Except that in this case the whistleblower didn’t commit treason the President of the USA and his co-conspirators did. If Trump wants to go back to "the old ways" so badly, maybe he should be the first to be held accountable using "the old ways" tactics & punishments.

Of course you, El Jefe, would probably rationalize his statement as a joke, wouldn't you? It is probabaly true that the whistleblower's identity is not known, but the people he reported to as the Law requires are all Trump appointees and all believed the whistleblower's complaint was credible and urgent, right? Do you know what percentage of Trump appointees have fallen out of favor and resigned since he took office? Were they all democrats?

Yeah, I was forgetting one thing...altenative facts! All news outlets are corrupt and peddle fake news except for those that praise and worship him, ring a bell? Do you, El Jefe know what happens to any Republican who disagrees with Trump? Do you know why his last last national security adviser, John Bolton, resigned, oops, was fired? I could go on and on but I have had to learn a few things the hard way...like what is taking place in my own country right now!

This bring us to the United States Constitution and particularly the First Amendment that prevents the government from making laws which respect an establishment of religion, prohibit the free exercise of religion, or abridge the freedom of speech, the freedom of the press, the right to peaceably assemble, or the right to petition the government for redress of grievances.

Dictator's wouldn't happen or survive but for enablers and enablers happen to be just ordinary people like you and me. I am 100% sure that the great people of the United States of America would never, for any reason, sacrifice the First Amendment that was adopted on December 15, 1791, as one of the ten amendments that constitute the Bill of Rights. The coming fight isn't as easy as you are trying to insinuate and my advise to you, relax and enjoy the show.
To get down to the nitty-gritty, let's take a look at some of the things that have shaped my independent views on these issues:

(1) So you have democrats jumping the gun publicly that there was a quid pro quo during a conversation between Trump and Zelensky and that Zelensky was pressured to investigate the Bidens! It turns out after reading the unredacted full transcript of the call that the whistleblower actually lied. As an objective person I work with facts not opinions of any individual pundit or a news outlet.

This led me to question the credibility of the so called whistleblower. Why would he/she lie?
Now, there is no more talk on the "quid pro quo", the initial allegation, it's dead and gone.

(2) The Dems' paradigm has now shifted to supposedly a new 'smoking gun', that there was a "cover up" by the White House regarding the 'whistleblower complaint'. The acting DNI took responsibility for delaying the submission of the 'complaint' to congress beyond the seven-day period written in the statute, by explicitly stating his reasons.

Through the hearing at HJC, one couldn't help but notice how the Dems wanted a "cover up" headline so hard from the DNI. They were like "Trump must have asked you to delay in order to cover up", "please give us a headline".

Of course the Dems would have loved for the DOJ and FBI to investigate the incident to inflate their story, but the smart AG Barr dismissed it. To the Dems, every person or agency that discredit their sham probes is a Trump stooge. Astounding! Democrats are never the benchmark of integrity, credibility, ethics and goodwill.

(3) Upon learning that there is no "cover up" by the White House regarding the 'complaint', the Dems have yelled for a previous transcript of the call between Trump and Zelensky, which the WH has agreed to release too. "You only need more when what you have is less".


(4) The IG of the Intel Community statements are being used to support the Dems' theory and motives. For instance the word "credible". But one would ask, at the time the IG saw the "whistleblower complaint" had he seen the full transcript of the call in question? No, so why would he criticize it?

It was some kind of a meticulously planned allegation against the President of the United States, and he had to be scrupulous. This is regardless of him being a Trump appointee, and has nothing to do with John Bolton's resignation. So using IGIC's words to build a case against Trump shows nothing but despair.

(5) The alleged whistleblower didn't have direct knowledge of the conversations that largely formed the complaint to the IG. Just second hand information including reports from Washington Post.

The only way this story developed is by having a leaker in the WH, anybody can become indignant because of that including the President of the United States. I don't know what Trump meant in his "spies" statement, but it's clear he didn't mean "killing".

What is unequivocal at this point is that the leaked information was crafted advertently to keep the gas of comic investigations flowing.


To answer your other question, some Senate Republicans decided not to go all out on press on matters of national intelligence, especially before the Senate committees hold their planned closed hearing with the related parties.

What happens to a democrats in congress who support Pres. Trump?
Republicans haven't seen anything tangible from the Dems never ending probes.

All in all, this is simply another episode of another season of a fantasy show produced by the Democrats. I have my movies snacks, popcorn! but the show is really dull, I find it harder to enjoy.
 
To get down to the nitty-gritty, let's take a look at some of the things that have shaped my independent view on these issues:

(1) So you have democrats jumping the gun publicly that there was a quid pro quo during a conversation between Trump and Zelensky and that Zelensky was pressured to investigate the Bidens! It turns out after reading the unredacted full transcript of the call that the whistleblower actually lied. As an objective person I work with facts not opinions of any individual pundit or a news outlet.

This led me to question the credibility of the so called whistleblower. Why would he/she lie?
Now, there is no more talk on the "quid pro quo", the initial allegation, it's dead and gone.

(2) The Dems' paradigm has now shifted to supposedly a new 'smoking gun', that there was a "cover up" by the White House regarding the 'whistleblower complaint'. The acting DNI took responsibility for delaying the submission of the 'complaint' to congress beyond the seven-day period written in the statute, by explicitly stating his reasons.

Through the hearing at HJC, one couldn't help but notice how the Dems wanted a "cover up" headline so hard from the DNI. They were like "Trump must have asked you to delay in order to cover up", "please give us a headline".

Of course the Dems would have loved for the DOJ and FBI to investigate the incident to inflate their story, but the smart AG Barr dismissed it. To the Dems, every person or agency that discredit their sham probes is a Trump stooge. Astounding! Democrats are never the benchmark of integrity, credibility, ethics and goodwill.

(3) Upon learning that there is no "cover up" by the White House regarding the 'complaint', the Dems have yelled for a previous transcript of the call between Trump and Zelensky, which the WH has agreed to release too. "You only need more when what you have is less".


(4) The IG of the Intel Community statements are being used to support the Dems theory and motives. For instance the word "credible". But one would ask, at the time the IG saw the "whistleblower complaint" had he seen the full transcript of the call in question? No, so why would he criticize it?

It was some kind of a meticulously planned allegation against the President of the United States, and he had to be scrupulous. This is regardless of him being a Trump appointee, and has nothing to do with John Bolton's resignation. So using IGIC's words to build a case against Trump shows nothing but despair.

(5) The alleged whistleblower didn't have direct knowledge of the conversations that largely formed the complaint to the IG. Just second hand information including reports from Washington Post.

The only way this story developed is by having a leaker in WH, anybody can become indignant because of that including the President of the United States. I don't know what Trump meant in his "spies" statement, but it's clear he didn't mean "killing".

What is unequivocal at this point is that the leaked information was crafted advertently to keep the gas of comic investigations flowing.


To answer your other question, some Senate Republicans decided not to go all out on press on matters of national intelligence, especially before the Senate committees hold their planned closed hearing with the related parties.

What happens to a democrat in congress who support Pres. Trump?
Republicans haven't seen anything tangible from the Dems never ending probes.

All in all, this simply another episode of another season of a fantasy show produced by Democrats. I have my movies snacks, popcorn, but the how is really dull, I find it to harder enjoy.
Ha ha ha El Jefe, are you for real? You appear to be so out of date buddy. Are you aware for instance that Rudolph W. Giuliani, whose actions as President Trump’s personal lawyer have helped set in motion an impeachment inquiry, abruptly canceled his scheduled paid appearance at a Kremlin-backed conference in Armenia next week? Yes, Rudy Giuliani aka special State Agent aka Trump's Lawyer and of course Putin would be there...

Giuliani’s decision to take part in the conference astounded national security experts. His appearance would have come days after the release of a whistleblower complaint accusing Trump and Giuliani of pressuring Ukrainian officials for damaging information about Democrats. Yeah, chew that! The unfolding scenario has made Washington pasikalike wala kulalika, to borrow a Kiswahili saying!

The shadow knows best...make sure you have your pop-corn ready buddy! It is full steam ahead!

Updates: House subpoenas Pompeo and schedules depositions of five State Department officials...

The chairmen of three powerful House committees subpoenaed Secretary of State Mike Pompeo for documents related to their investigation into President Trump’s controversial call with the leader of Ukraine.

The House panels have also scheduled five depositions beginning next week with State Department officials who would have knowledge of Trump’s engagements with Ukraine (including Rudolph Giuliani?) Who is Giuliani in the State Department anyway?

These are the first concrete steps taken as Democrats seek to build a case for impeachment.

More update:
Kurt D. Volker, the State Department’s special envoy for Ukraine, who got caught in the middle of the pressure campaign by President Trump and his lawyer, Rudolph W. Giuliani, to find damaging information about Democrats, resigned his post on Friday.
 
MZIZIMO NA MVUMO NDANI YA VIUNGA VYA DC
HALI INAZIDI KUDORORA, BAADHI 'WAJITOSA MAJINI''

Habari ya Ukraine kama ilivyokuwa ya Russia ilipokelewa kwa kejeli za ''Fake New''

Hilo linafanyika kuwahakikishia wafuasi mitandaoni na nchi kwamba mambo ni shwari, ni uzushi tu.

Kwa bahati mbaya hali ya viunga vya DC si ya reja reja.

Mtu akikuita 'mwizi' lazima utafakari kabla ya kumdhihaki, kejeli au mtukana.
Mtu huyo anakuwa amejiandaa na hukulisha chambo tu ili ukiingia tofauti abomowe kichwa

Habari ya Ukraine iliitwa Fake, na wageni wa siasa za viungani wanaitikia fake news bila kujua wanazungumzia nini. Ile ''Fake news'' ya Ukraine sasa inatetemesha viunga vya DC

Yote aliyoeleza whistleblower ni kama yalivyo na kuthibitika pasi na shaka.

Kwamba, WH imekiri kuhamisha nyaraka kutoka kompyuta moja hadi nyingine! Ukweli
Kwamba transcript zinaoana na ripoti ya whistleblower! kwa uhakika. n.k n.k.

Kikao cha leo WH kinachomshauri Rais kilifanyika bila kuwepo Lawyer Rudolph Gullian.

Rudy hakuwepo kwa kile kinachoelezwa mchango wake ''mkubwa'' katika kuumua sakata zima.

Wataalam wa WH walinshauri Rais Trump kwamba transcript si nzuri, Rudy akamshauri wafanye pre-preemptive strategy ya kutoa habari mapema ili gumzo liwe juu ya Joe Biden

Katika mkakati huo, Rudy aliitaja State dept akiwemo mjumbe maalumu wa Rais Trump Bw Volker ambaye alishirikiana na Rudy akiwa Ukraine katika kutafuta uchafuzi dhidi ya Biden.

Nyaraka (transcript) pia inamtaja mtu ambaye ni kinga kubwa kwa utawala wa Trump AG Barr mara kadhaa kama mshiriki anayejua nini kinaendelea huko Ukraine na huenda ndiyo maana alifumbia macho suala la whistle blower. Naye inasemwa atahitajika mbele ya kamati

Kamati ya Bunge imemwita Pompeo(SoS) kuhusiana na kutajwa na Rudy, na Volker naye alikuwa aende mbele ya kamati.

Kuchelea hilo jioni hii Volker kaachia ngazi na kujitosa baharini.

Kwa wanaofuatilia, jana tulisema mlolongo wa watu ni mkubwa na taratiiibu kila mmoja ataangali ubawa wake na wengine kulitosa jahazi ili kunusuru nafasi zao. Volker kafungua milango

Kuondoka kwa Volker kunamfanya awe huru na kuepuka kiunzi cha ''executive privilege' mara atakapofika mbele ya kamati ya Bunge.

Wakati huo huo kuna habari zilizoandikwa magazetini zikisema kuwa kompyuta iliyohamishwa ilifanyika hivyo kwa ushauri wa wanasheria. Wanasheria waliona tatizo na transcript za WH.

Inataarifiwa pia kuwa maongezi kati ya Trump na Putin na MBS nayo imelazimika yachimbiwe.
Sababu kubwa ni zile zile kwamba, yapo maneno mazito yanayoweza kumtia Mzee matatani.

Kana kwamba hilo halitoshi, gazeti jingine mashuhiri limeweka wazi maongezi kati ya Trump na balozi wa Russia likimnukuu akisema '' Russia isihofu kuhusu kuingilia uchaguzi kwani Marekani nayo hufanya hivyo kwa nchi nyingine''

Habari hiyo ni mwiba kwa vyombo vya intelejensia na Taifa la Marekani huku Republicans wakionekana kuwa na Rais Trump ingawa taratiibu uchovu dhidi ya mbabe huyo unajidhihiri.

Yote hayo yakisemwa, sasa kuna wafanyakazi wa WH wanaoandamwa kwa kujua hali ilivyo na kusaidia kuficha au kutotoa taarifa.

Ikiwa Pompeo atatoa ushahidi na ikiwa wapo watakaotosa jahazi hali itakuwa mbaya.

Kwasasa watumishi wa WH, DOJ na SoS pamoja na Republicans wanaonekana kuwa kitu kimoja, kusimama na kumtetea Rais Trump hata kama wanajua kinachofanyika si sahihi.

Hata hivyo kundi ni kubwa, na pindi watakapoanza kunyofolewa mmoja mmoja umoja huo utaparaganyika na hapo mengi yatajulikana.

Ni yale yale ya ''Russia'' ambapo lawyer wa Trump Bw Cohen aliapa kuchukua risasi ya kichwa kumlinda Trump.

Ukweli uliposimama alijikuta mwenye Trump akimruka kimanga na sasa anatumikia adhabu gerezani. Kilichofauta baada ya hapo ni umoja kuvurugika, mwaga mboga namwaga ugali!

Hilo litatokea siku chache zijazo na atakayelianzisha ni Rais Trump, atawaruka wenzake.

Kwa sakata hili, kama wapo watakaojitosa baharini kwa msimamo wa liwalo na liwe, hali ya jumba jeupe itakuwa na mtanziko mkubwa ikimwacha mkazi wake katika hali tete! .

Tusemezane
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom