Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,337
- 31,163
- Thread starter
- #961
VIUNGANI DC WIKI HII
RAIS Trump aselelea (Hit rock bottom)
Nyuma ya Pazia anataka mazungumzo na Iran, ngoma nzito
Kama kuna anayemfanya Rais mstaafu Obama aonekane kiongozi bora ni Rais Trump.
Rais Trump aliwahi kumwita Rais Obama ''stupid leader'' na kwamba dunia iliwacheka Wamarekani kwa uongozi wake.
Kama hilo lilikuwa kweli, kwasasa dunia haicheki tena bali imepigwa ganzi, butwaa na kutundawaa
Wiki hii baada ya kuahirisha safari ya Poland kuhudhuria maadhimisho ya vita ya dunia, Rais Trump alionekana akicheza golf huku tishio la dhoruba Dorian likizidi kurindima.
Ni Trump aliyemshambulia sana Obama kwamba anacheza golf kuliko Tiger Woods
Katika miaka 3 ya utawala Trump amecheza golf kumzidi Obama ndani ya miaka 8.
Habari kubwa ni ya kiongozi huyo kutofahamu habari zinazotolewa na serikali yake kuhusu hali ya hewa akiwa pia hajui ramani ya nchi yake na kuwa gumzo la kitaifa na kimataifa.
Trump alidai Dhoruba ya Dorian itaikumba Alabama huku akibadilisha ramani ya mamlaka za hali ya hewa ili kukidhi haja yake na si uhalisia wa kitaaluma.
Tatizo si kufanya makosa bali kuyatetea kwa njia za kitoto chini ya hadhi ya ofisi hiyo kubwa.
Rais ametumia kila aina ya ushawishi kuthibitisha madai yake ya uongo bila mafanikio.
Dhalili anayoipata mbele ya jamii yake ni kubwa na ya kusikitisha kwa namna yoyote ile.
Ukuta
Rais Trump anatumia pesa zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za jeshi na miradi mingine ili kujenga ukuta. Ikumbukwa Rais aliahidi ukuta utalipiwa na Mexico, kwasasa unalipiwa na Wamarekani. Haya tuliwahikuyaeleza na kwamba Trump alikuwa akilaghai wafuasi wake.
Hali ya uchumi
Takwimu zinaonyesha kudorora kwa ajira, mwezi wa 8 ukiwa umetengeneza ajira 130, 000 kati ya hizo 25,000 si za kudumu. Vigezo vingine havina mabadiliko makubwa lakini kwa kulinganisha na muda na hali ya uchumi aliyopokea, namba hiyo ni ndogo sana ukilinganisha na mtangulizi wake Obama. Vita yake ya uchumi haionekani kumsaidia
Trump amemshambulia mkuu wa Bank kuu (Reserve Bank) aliyemtea mwenyewe kwa madai kuwa anaongeza riba na hivyo kuathiri uchumi.
Trump anasema wakati wa Obama viwango havikuongezwa bila kufikiri wakati huo uchumi ulikuwa katika recession na kwamba alikabidhiwa uchumi ulioimarika tofauti na mtangulizi wake.
Meli ya Iran
Zipo taarifa za Afisa wa WH kumshawishi Nahodha wa meli iliyokuwa imeshikiliwa na UK aipeleke Marekani. Kama tulivyowahi kusema, UK ilitumika tu na US kuishikilia meli hiyo.
Nahodha aliahidiwa Pesa na kutukumbusha Trump alivyomsema Obama kupeleka pesa Tehran zilizokuwa mali ya Iran kama sehemu ya deal ya Nyuklia, Trump anafanya kile alichokilaani.
Iran Deal
Nyuma ya pazi taarifa zinaeleza maafisa wa Marekani wana haha kuishawishi Iran irudi katika meza ya majadiliano kuhusu silaha za nyuklia.
Trump alikumbana na wakati mgumu wakati wa G7 alipojaribu kuwashawishi wanachama waungane naye kuhusu Iran huku wakimueleza alijitoa katika deal bila kuwaeleza.
Sasa Trump anarudi kule kule kwa Obama kuhusu Deal
Iran yaahidi kurutubisha Nyuklia
Iran nayo imesema sasa haitatekeleza sehemu kubwa ya Deal na nchi za Ulaya na kuanza kurutubisha mitambo yake ya Nyuklia.
Uamuzi wa Iran ni baada ya kuona udhaifu wa Marekani na kwamba Iran inataka nchi za Ulaya zifanye jambo kurahisha maisha magumu yanayotokana na vikwazo.
Hoja yao ni kuwa ndani ya deal hawaoni matokeo yoyote.
Mpango wa US kuishambulia Iran kwa kushirikiana na Israel unaonekana kukwama.
Tatizo linalojitokeza si nguvu za kijeshi za Iran, bali ushawishi wa Iran katika eneo la mashariki ya kati na kwamba kinachotokea kinaweza kuwa kikubwa zaidi ya kinachoendelea Afghanistan
Deal na Talibani
Serikali ya Trump imekuwa katika mazungumzo na Talibani na imekubaliana nao kuondoa askari wake kwa kiwango kutoka nchi hiyo. Mazungumzo na Talibani hayakuanza leo, Republican na Trump walimkashifu sana Obama alipojaribu kukaa mezani na Telebani.
Leo Republicans na Trump wamerejea kule kule kwa Rais Obama
Kwa hadhi ya jengo jeupe la viungani DC Rais Trump kaselelea chini ya Mwamba(hit rock bottom). Kwa siasa za kimataifa sasa anafuata nyayo za Obama. Kwa hali ya uchumi hofu kubwa ni mdororo mikononi mwake.
Hayo yote yanachigiza sehemu ya jamii kuhoji utayari wake kuongoza Taifa hilo wakitilia mashaka uwezo wake kiakili, lakini pia kumfanya Obama ang'are
Tusemezane
RAIS Trump aselelea (Hit rock bottom)
Nyuma ya Pazia anataka mazungumzo na Iran, ngoma nzito
Kama kuna anayemfanya Rais mstaafu Obama aonekane kiongozi bora ni Rais Trump.
Rais Trump aliwahi kumwita Rais Obama ''stupid leader'' na kwamba dunia iliwacheka Wamarekani kwa uongozi wake.
Kama hilo lilikuwa kweli, kwasasa dunia haicheki tena bali imepigwa ganzi, butwaa na kutundawaa
Wiki hii baada ya kuahirisha safari ya Poland kuhudhuria maadhimisho ya vita ya dunia, Rais Trump alionekana akicheza golf huku tishio la dhoruba Dorian likizidi kurindima.
Ni Trump aliyemshambulia sana Obama kwamba anacheza golf kuliko Tiger Woods
Katika miaka 3 ya utawala Trump amecheza golf kumzidi Obama ndani ya miaka 8.
Habari kubwa ni ya kiongozi huyo kutofahamu habari zinazotolewa na serikali yake kuhusu hali ya hewa akiwa pia hajui ramani ya nchi yake na kuwa gumzo la kitaifa na kimataifa.
Trump alidai Dhoruba ya Dorian itaikumba Alabama huku akibadilisha ramani ya mamlaka za hali ya hewa ili kukidhi haja yake na si uhalisia wa kitaaluma.
Tatizo si kufanya makosa bali kuyatetea kwa njia za kitoto chini ya hadhi ya ofisi hiyo kubwa.
Rais ametumia kila aina ya ushawishi kuthibitisha madai yake ya uongo bila mafanikio.
Dhalili anayoipata mbele ya jamii yake ni kubwa na ya kusikitisha kwa namna yoyote ile.
Ukuta
Rais Trump anatumia pesa zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za jeshi na miradi mingine ili kujenga ukuta. Ikumbukwa Rais aliahidi ukuta utalipiwa na Mexico, kwasasa unalipiwa na Wamarekani. Haya tuliwahikuyaeleza na kwamba Trump alikuwa akilaghai wafuasi wake.
Hali ya uchumi
Takwimu zinaonyesha kudorora kwa ajira, mwezi wa 8 ukiwa umetengeneza ajira 130, 000 kati ya hizo 25,000 si za kudumu. Vigezo vingine havina mabadiliko makubwa lakini kwa kulinganisha na muda na hali ya uchumi aliyopokea, namba hiyo ni ndogo sana ukilinganisha na mtangulizi wake Obama. Vita yake ya uchumi haionekani kumsaidia
Trump amemshambulia mkuu wa Bank kuu (Reserve Bank) aliyemtea mwenyewe kwa madai kuwa anaongeza riba na hivyo kuathiri uchumi.
Trump anasema wakati wa Obama viwango havikuongezwa bila kufikiri wakati huo uchumi ulikuwa katika recession na kwamba alikabidhiwa uchumi ulioimarika tofauti na mtangulizi wake.
Meli ya Iran
Zipo taarifa za Afisa wa WH kumshawishi Nahodha wa meli iliyokuwa imeshikiliwa na UK aipeleke Marekani. Kama tulivyowahi kusema, UK ilitumika tu na US kuishikilia meli hiyo.
Nahodha aliahidiwa Pesa na kutukumbusha Trump alivyomsema Obama kupeleka pesa Tehran zilizokuwa mali ya Iran kama sehemu ya deal ya Nyuklia, Trump anafanya kile alichokilaani.
Iran Deal
Nyuma ya pazi taarifa zinaeleza maafisa wa Marekani wana haha kuishawishi Iran irudi katika meza ya majadiliano kuhusu silaha za nyuklia.
Trump alikumbana na wakati mgumu wakati wa G7 alipojaribu kuwashawishi wanachama waungane naye kuhusu Iran huku wakimueleza alijitoa katika deal bila kuwaeleza.
Sasa Trump anarudi kule kule kwa Obama kuhusu Deal
Iran yaahidi kurutubisha Nyuklia
Iran nayo imesema sasa haitatekeleza sehemu kubwa ya Deal na nchi za Ulaya na kuanza kurutubisha mitambo yake ya Nyuklia.
Uamuzi wa Iran ni baada ya kuona udhaifu wa Marekani na kwamba Iran inataka nchi za Ulaya zifanye jambo kurahisha maisha magumu yanayotokana na vikwazo.
Hoja yao ni kuwa ndani ya deal hawaoni matokeo yoyote.
Mpango wa US kuishambulia Iran kwa kushirikiana na Israel unaonekana kukwama.
Tatizo linalojitokeza si nguvu za kijeshi za Iran, bali ushawishi wa Iran katika eneo la mashariki ya kati na kwamba kinachotokea kinaweza kuwa kikubwa zaidi ya kinachoendelea Afghanistan
Deal na Talibani
Serikali ya Trump imekuwa katika mazungumzo na Talibani na imekubaliana nao kuondoa askari wake kwa kiwango kutoka nchi hiyo. Mazungumzo na Talibani hayakuanza leo, Republican na Trump walimkashifu sana Obama alipojaribu kukaa mezani na Telebani.
Leo Republicans na Trump wamerejea kule kule kwa Rais Obama
Kwa hadhi ya jengo jeupe la viungani DC Rais Trump kaselelea chini ya Mwamba(hit rock bottom). Kwa siasa za kimataifa sasa anafuata nyayo za Obama. Kwa hali ya uchumi hofu kubwa ni mdororo mikononi mwake.
Hayo yote yanachigiza sehemu ya jamii kuhoji utayari wake kuongoza Taifa hilo wakitilia mashaka uwezo wake kiakili, lakini pia kumfanya Obama ang'are
Tusemezane