Duru za Siasa: Awamu ya 5 - Uongozi na Yanayojiri

Dr. Tulia Ackson Mwansasu, ingawa anaitwa daktari wa sheria, liko jambo moja tu la msingi kabisa ambalo hata bila kukanyaga milango ya shule alitakiwa alijue...

Shughuli zote za Mamlaka ya nchi zinatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo vitatu navyo ni;
  1. Serikali...yenye mamlaka ya utendaji ikiongozwa na Rais.
  2. Mahakama...yenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki ikiongozwa na Jaji Mkuu.
  3. Bunge...lenye mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma likiongozwa na Spika.
Mamlaka yote hayo yaliyotajwa yanasimamiwa na Katiba ambayo kwenye utangulizi wake imeandikwa, "Kwa kuwa SISI, Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani..."
katiba-jpg.382896

Hakuna hata sehemu moja inasema, "kwa kuwa mimi Rais nimeamua...", hapana, badala yake Rais kabla ya kuchukua madaraka anatakiwa aape kwa jina la Muumba kuwa atailinda na kuitetea Katiba ya wananchi iliyomweka madarakani. Je Dr. Tulia Ackson iwapo Rais atashindwa kuilinda na kuitetea katiba, amejipangaje?

Swali hili linanisumbua sana si kwa Spika peke yake bali hata kwa wakuu wa mihimili mingine ya mamlaka ya nchi kama Mahakama. Ni wazi Rais Magufuli kashindwa kuheshimu Katiba na kila siku kwa vitendo na matamko anaonekana kama vile yuko juu ya Katiba lakini linalotia hofu zaidi ni swali kwamba imekuwaje wananchi tuko kimya?

Shida kubwa ya nchi zetu hizi inapofika kwa Viongozi kuheshimu KATIBA ya nchi inachukuliwa kuwa ni suala la UTASHI BINAFSI zaidi na sio suala la ULAZIMA au UMUHIMU. Matokeo yake mhimili wa kwanza SERIKALI uko huru kwenda kinyume na katiba uliyoapa kuilinda kutokana na maneno na matendo ya viongozi wake. Na ugonjwa huu umewakumba pia wale wenye wajibu wa kusimamia katiba kwa upande wa mihimili mingine (Bunge & Mahakama) ambao wameshindwa kusimama kwenye nafasi yao pale wanapoona Mhimili wa kwanza unakiuka katiba... hawa kwa namna moja au nyingine wamejiweka kwenye kundi moja lenye jukumu la KUTII mhimili wa SERIKALI.
 
Dr. Tulia Ackson Mwansasu, ingawa anaitwa daktari wa sheria, liko jambo moja tu la msingi kabisa ambalo hata bila kukanyaga milango ya shule alitakiwa alijue...

Shughuli zote za Mamlaka ya nchi zinatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo vitatu navyo ni;
  1. Serikali...yenye mamlaka ya utendaji ikiongozwa na Rais.
  2. Mahakama...yenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki ikiongozwa na Jaji Mkuu.
  3. Bunge...lenye mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma likiongozwa na Spika.
Je Dr. Tulia Ackson iwapo Rais atashindwa kuilinda na kuitetea katiba, amejipangaje?

Swali hili linanisumbua sana si kwa Spika peke yake bali hata kwa wakuu wa mihimili mingine ya mamlaka ya nchi kama Mahakama.

Ni wazi Rais Magufuli kashindwa kuheshimu Katiba na kila siku kwa vitendo na matamko anaonekana kama vile yuko juu ya Katiba lakini linalotia hofu zaidi ni swali kwamba imekuwaje wananchi tuko kimya?
Mkuu Bandiko lako lina hoja nyingi, naomba nipitie moja moja kwa nyakati

1. Tatizo la mihimili mitatu linatokana na ukweli kuwa katiba yetu imetengenezwa katika mfumo ambao mihimili hiyo itategemea Serikali

Ni kwa msingi huo, CCM hawakukubali rasimu ya Warioba.

Walitambua ile nguvu ya serikali inayolinda masilahi yao itakuwa haipo.

Na si katika mihimili hiyo tu bali mamlaka zote zingine

Kwa mfano, tume ya uchaguzi, Takukuru, Polisi, tume ya maadili n.k

Wakati wa awamu ya nne, mfumo wa uchaguzi ulitakiwa uwe wa kieletroniki

Tume ikalalamika haina pesa za kutosha.
Tukaenda katika uchaguzi kibubusa busa katika ili 'mambo' yakae uzuri

Kila agizo la serikali, tume ya uchaguzi ilifuata. Serikali ikisema zoezi litakamilika, tume inasisitiza. Serikali ikisema haiwezekani, tume inasitisha

Tumeona jinsi tume ilivyokuwa inayumbishwa na serikali kila asubuhi na jioni

Utashangaa, tume iliyokuwa haina pesa imerudisha bilioni 12 serikalini badala ya kuimrisha mfumo wa uchaguzi. Hili lilikuwa katika 'kumpendeza'

Ndicho kilichotokea kwa Takukuru, kuna kesi inashughulikia zingine zinaenda bungeni kiaina. Haipo huru, inategemea maagizo, kuna inapowajibika

Ndivyo Bunge lenye dhamana ya kusimamia serikali ikamilishe shughuli kama za elimu kwa ujumla, likijiingiza katika kuchangia madawati

Kuchangia madawati si kazi ya bunge, ni kazi ya bunge kuhakikisha madawati yanapatikana kwa kutumia nyenzo kama bajeti na kamati zao

Ndivyo ilivyokuwa kwa Mahakama ambapo badala ya kuomba fungu kupitia bunge, mahakama ikafikisha maombi kwa Rais na kuahidiwa robo ya makusanyo yatakayotokana na kazi za kisheria zilizosua sua

Mahakama ilipaswa kusisitiza umuhimu wa kuwa na Bajeti yake na kwamba serikali haina chaguo bali kutimiza bajeti iliyotengwa na mhimili wa bunge kwa mhimili wa Mahakama

Lakini pia angalia teuzi za wakuu wa mihimili. Ukiacha Rais anayechaguliwa, Mahakama ni uteuzi,katika hali ya kushangaza mwendo huo umeongeza wigo

Kimsingi ile dhana ya kuwa tuna mihimili 3 kwa sehemu kubwa ni 'theory'

Tuna mhimili mkubwa unaodhibiti mihimili na mamlaka zingine

Sasa swali lako, Dr Tulia amejiandaje katiba ikikukwa?

Well, yeye binafasi ni mteuliwa kabla ya kuwa mchaguliwa wa Naibu spika.

Tayari ana conflict of interest, atafanya nini ni swali linalotegemea 'utashi'

Unapokuwa na conflict of interest, utashi una preclude sheria na taratibu

Na hili la conflict of interest lipo katika mihimili na mamalaka zote

Tutaendelea kwa hoja zingine
 
Shida kubwa ya nchi zetu Viongozi kuheshimu KATIBA, ni suala la UTASHI BINAFSI zaidi na sio suala la ULAZIMA au UMUHIMU. Matokeo yake mhimili wa SERIKALI uko huru kwenda kinyume na katiba uliyoapa kuilinda.

Na ugonjwa huu umewakumba pia wale wenye wajibu wa kusimamia katiba kwa upande wa mihimili mingine (Bunge & Mahakama) ambao wameshindwa kusimama kwenye nafasi yao pale wanapoona Mhimili wa kwanza unakiuka katiba... hawa kwa namna moja au nyingine wamejiweka kwenye kundi moja lenye jukumu la KUTII mhimili wa SERIKALI.
Swali hili linanisumbua sana si kwa Spika peke yake bali hata kwa wakuu wa mihimili mingine ya mamlaka ya nchi kama Mahakama. Ni wazi Rais Magufuli kashindwa kuheshimu Katiba na kila siku kwa vitendo na matamko anaonekana kama vile yuko juu ya Katiba lakini linalotia hofu zaidi ni swali kwamba imekuwaje wananchi tuko kimya?
Tupitie hoja hizo mbili zenye mantiki zinazolingana kwa kuzichangia

Mwalimu ameongelea viongozi na wenye dhamana ya kusimamia katiba kushindwa katika kulisaidia Taifa.
Mag3 anauliza kwanini wananchi wapo kimya hali kama hii inapojitokeza?

Mfumo wetu huko nyuma ulijengwa katika kuamini viongozi ndio wenye dhamana na kauli za mwisho. Ilifika mahali wananchi waliogopa kuwa na nakala ya katiba kama kosa, kama ambavyo Pasi za kusafiria ilikuwa 'privilege' na si haki. Hili lilichangiwa sana na weledi na elimu kwa nyakati hizo

Pia lilichangiwa na utamaduni kuwa, penye sintofahamu serikali husikiliza wananchi wanasema nini na kisha kukaa meza moja kutafuta suluhu

Suala la weledi na elimu halina uzito katika zama hizi tena.
Kilichopo ni kutokubali kuwa utamaduni wa kusikilizwa haufuatwi na uongozi wa nyakati hizi ukilinganisha na zama hizo

Hivyo tatizo la wananchi ni 'legacy' wanaoishi nayo bila kujali mabadiliko ya nyakati na haja ya nyakati tulizo nazo. Je, wana makosa? Linabaki kuwa swali

Hoja ya Mwalimu kuhusu viongozi kuheshimu katiba. Hili ni tatizo la nchi zinazoendelea na imekuwa kama utamaduni wa kudumu katika utawala

Tatizo la nchi hizi ni wananchi kutoweka viongozi kwa dhamira, bali sababu nyingine zisizo na msingi. Vetting ya kupata viongozi ni mbovu sana

Kwavile hawapatikani kwa njia 'sahihi' , kudumu kwao katika utawala kunategemea maguvu. Unapokuwa na maguvu, sheria hukaa pembeni

Lakini pia watawala wametengeneza mfumo unaowafanya viongozi wawe na 'meekly obedience' au submissive kwa watawala. Kwa mfano, angalia katiba yetu ya 1977, viongozi wenye dhamana ya ''checks and balance' ni wateuliwa

Ndiyo maana mabadiliko yatakayoondoa hiyo 'submissive' hayakubaliwi na watawala, Rasimu ya Warioba ni mfano mzuri sana.

Mwalimu amesema, 'ugonjwa wa kusimamia katiba umekumba mihimili mingine kama bunge na mahakama'

Tujadili bandiko linalofuata
 
'GONJWA LA KUSIMAMIA KATIBA'

Mkuu Mwalimu amesema gonjwa hilo limekumba mihimili kama bunge na mahakama. Kwa mtazamo mwingine, gonjwa limeathiri kila sehemu ya jamii

Bunge: Limeporwa 'uhuru' kwasababu kuu mbili
1. Mfumo singiziwa na mabunge ya commonwealth wa caucus za vyama zaidi kuliko masilahi ya Taifa.

In fact mabunge ya C'wealth yanasingiziwa tu.
Uingereza ilipoitisha kura ya maoni, wabunge walikuwa huru si U-vyama.

Hivi nani anaweza kuwa mkatoliki zaidi ya PAPA?

Mfumo wa caucus uliwafunga wabunge-CCM kukataa kiongozi ' aliyeletwa'

2. Bunge hutegemea huruma za mhimili wa serikali.Hizi habari za madawati si kazi yao, lakini watawezaje kulinda masilahi yao iwapo hawakubaliani na waliokamata mpini?

Mahakama
Hili tumelisema mara nyingi. Uongozi wa mahakama unapaswa kupatikana nje ya mifumo mingine. Kwamba, jukumu la uongozi litoke kwa uongozi ili kuiweka mahakaa huru.
Hilo ni pamoja na kuwa na bajeti yake ili kutohemea

Tuliwahi kujadili, viongozi wa mahakama kama majaji wasihusishwe katika shughuli za serikali, mamlaka, idara au mashirika ya umma wakiwa kazini au wakistaafu.
Hili ltawaweka huru ndani na nje ya mahakama always

Makundi ya Jamii

Wasomi: Nao wametambua ukaribu na serikali ni njia ya mkato ya maisha ya sasa na baadaye. Hatusikii wasomi wakizungumzia hoja za jamii wakiogopa mbele ya safari wanaweza kuudhi watwala. Wao 'wataishi vipi'?

Ukimsikia msomi anazungumzia masuala ya kijamii, maisha yake yanategemea usomi na anaamini anaweza kuishi bila kusubiri hisani.
Ni wachache sana, wengi wamebaki kuwa wapiga debe

Watawala wanatambua udhaifu, wapiga debe wanazawadiwa kama si Tume ni bodi memba, au DED, DC n.k.

Hiyo ni njia ya kuwakata makali na kuwazuia wajao kuwa 'kimbelembele'

Inaendelea...
 
Tupitie hoja hizo mbili zenye mantiki zinazolingana kwa kuzichangia

Mwalimu ameongelea viongozi na wenye dhamana ya kusimamia katiba kushindwa katika kulisaidia Taifa.
Mag3 anauliza kwanini wananchi wapo kimya hali kama hii inapojitokeza?

Mfumo wetu huko nyuma ulijengwa katika kuamini viongozi ndio wenye dhamana na kauli za mwisho. Ilifika mahali wananchi waliogopa kuwa na nakala ya katiba kama kosa, kama ambavyo Pasi za kusafiria ilikuwa 'privilege' na si haki. Hili lilichangiwa sana na weledi na elimu kwa nyakati hizo

Pia lilichangiwa na utamaduni kuwa, penye sintofahamu serikali husikiliza wananchi wanasema nini na kisha kukaa meza moja kutafuta suluhu

Suala la weledi na elimu halina uzito katika zama hizi tena.
Kilichopo ni kutokubali kuwa utamaduni wa kusikilizwa haufuatwi na uongozi wa nyakati hizi ukilinganisha na zama hizo

Hivyo tatizo la wananchi ni 'legacy' wanaoishi nayo bila kujali mabadiliko ya nyakati na haja ya nyakati tulizo nazo. Je, wana makosa? Linabaki kuwa swali

Hoja ya Mwalimu kuhusu viongozi kuheshimu katiba. Hili ni tatizo la nchi zinazoendelea na imekuwa kama utamaduni wa kudumu katika utawala

Tatizo la nchi hizi ni wananchi kutoweka viongozi kwa dhamira, bali sababu nyingine zisizo na msingi. Vetting ya kupata viongozi ni mbovu sana

Kwavile hawapatikani kwa njia 'sahihi' , kudumu kwao katika utawala kunategemea maguvu. Unapokuwa na maguvu, sheria hukaa pembeni

Lakini pia watawala wametengeneza mfumo unaowafanya viongozi wawe na 'meek obedience' au submissive kwa watawala. Kwa mfano, angalia katiba yetu ya 1977, viongozi wenye dhamana ya checks and balances ni wateuliwa

Ndiyo maana mabadiliko yatakayoondoa hiyo 'submissive' hayakubaliwi na watawala, Rasimu ya Warioba ni mfano mzuri sana.

Mwalimu amesema, 'ugonjwa wa kusimamia katiba umekumba mihimili mingine kama bunge na mahakama'

Tujadili bandiko linalofuata
Halafu kinacholeta wasi wasi ni hii tetesi...kwamba Spika anatekeleza wajibu wake kwa maelekezo ya Ikulu!

spikatulia-jpg.383399


Kama hii ni kweli, taifa letu linaelekea kubaya.​
 
Makundi ya Jamii

Wanaharakati na taasisi huru
Hizi nazo zinaishi kwa njia zile zile za kisomi. Hivi inakuwaje mkuu wa kitengo cha maadili ya umma, awe 'mfanyakazi' wa mhimili wa serikali?

Huyu anasimamia maadili gani ikiwa yeye ni sehemu ya waajiriwa wa serikali
Tujiulize, mkuu wa kamisheni ya tume ya maadili kwanini ahusike na kazi za Ikulu?

Wanaharakati: Nao wametambua mambo yanaweza kuwa mazuri kama utaungana nao. Wanaona mifano dhahiri. Wanaharakati wamepata ulaji kwa njia mbali mbali, kama si bunge la katiba, basi japo u-afisa tawala

Wamekatwa makali hawana meno, wameacha harakati wengine ni ma-DED, rc, DC n.k. wametulizwa. Waliobaki wanaishi kwa mifano, wanajua one day yes

Inaendelea
 
Viongozi wa Imani

Hili ni kundi linalostajaabisha. Linalohubiri lisichokifanya na kuishi kwa hisani

Lina dhamana kubwa, lakini kwasababu ya 'uluwa' limejiunga na makundi mengine

Mfano, kiongozi mmoja anatafuta suluhu la kwa kulaani kundi moja kwa kauli za maudhi.
Huyu aliwahi kuwa 'mwenyeji' na hivyo anajitahidi kumfurahisha mgeni wake

Kundi linalohusisha mjumuiko wa imani linatafuta suluhu
Kauli walizotoa zinatia shaka kama wanaitenda haki,maadili, uadilifu au njia za suluhu ukiachilia zile za kusoma maandiko matakatifu

Inawezekanaje viongozi wa imani wakazungumzia mikutano/maadamano bila kueleza kwanini imefika hapo?Wanashughulikia dalili za maradhi si kutafuta chanzo

Kwa miezi kadhaa walikuwa na fursa ya kusaidia jamii, walikuwa kimya

Wanaongelea bila kueleza tumefikaje. Wanaelewa, lakini kama wengine ni 'submissive'

Uhalifu, ujambazi na maovu vimetamalaki katika jamii.
Wizi wa mali za umma ambao ni dhuluma kwa walipa kodi umekithiri

Kundi lipo kimya, leo wanaonaje tatizo ambalo kimsingi si kubwa ukilinganisha na changamoto tulizo nazo kama Taifa?Hivi kuna tatizo kubwa zaidi ya umasikini?

Mbona hatusikii kundi hili likiongelea haki za wananchi kuachana na umasikini mmoja mmoja au kama nchi kwa kugawana 'keki sawa'

Ni kundi linalopoteza sifa kwa kasi. Badala ya kusimama haki, maadili na uongofu, limebaki kuwa watazamaji na kuingilia kati pale penye masilahi.

Hivyo unaweza kuona ukubwa wa tatizo tulilo nalo.
Si tatizo la vyama vya siasa pekee, ni tatizo pana lililogusa kila eneo la jamii

Lazima tukae kitako na kujipanga. Tuandike tena utaratibu utakaohakikisha kila mtu, kila kundi na kila mwenye dhamana anawajibika au kuwajibishwa.

Kama hataturaudi mezani kusikiliza wananchi walisema nini kwa tume ya Warioba, tutacheza mduara, ukuti ukuti kila asubuhi, jioni tunakunywa panadol kwa maumivu

Tusemezane
 
Halafu kinacholeta wasi wasi ni hii tetesi...kwamba Spika anatekeleza wajibu wake kwa maelekezo ya Ikulu!
Kama hii ni kweli, taifa letu linaelekea kubaya.​
Tetesi kama hizo iwe kweli au la zinajengwa kwasababu
1. Spika ni mbunge wa kuteuliwa kutoka Ikulu kwa mujibu wa sheria
2. Wabunge wa kuteuliwa waliopewa uwaziri 'wana interest' na serikali. Sawia
3. Mbunge wa kuteuliwa, kawa naibu wa Spika katika chombo cha wawakilishi

Kwa mantiki hii, mawaziri wanaotokana na kuteuliwa wana fulfill interest za serikali kama ilivyokusudiwa.Wabunge wa kuchaguliwa wana fullfill interest za waliowachagua

Kwavile Naibu kateuliwa kwanza kama mbunge , pengine naye ana interest na eneo lake la awali kabla ya kuwa Naibu.Kumbuka ni mbunge wa kuteuliwa ab initio

Kuna conflicts of interest zinazotengeza tetesi za 'kupewa maagizo'

Inapotokea utendaji ukawa wa mashaka, tetesi zinapata nguvu kuliko inavyotarajiwa.

Conflict of interest ni tatizo kubwa na inaonekana mhimili mmoja una overlap!
 
HOFU NA NIDHAMU YA WOGA
MAAMUZI MENGI HAYAZINGATII WELEDI

Tumezungumzia dhana ya hofu na nidhamu.
Tukasema ni rahisi kuacha nidhamu na kuvamia hofu kuliko kinyume chake

Hofu ina tatizo, inavia uwezo wa watu kufikiri, kuamua au kutenda

Watu hujilinda tu, si katika kutanabahi au tafakuri. Ni hatari sana

Mabandiko kabla ya hili tumezungumzia mihimili na jinsi ilivyopoteza nguvu

Tulisema si mihimili,mamlaka huru nazo zimepoteza uhuru.

Mabandiko 168-172 tulizungumzia kuhamia Dodoma na madhara ya uharaka

Again, bila kuzingatia matakwa ya sheria na kuchukua sera kama ndiyo sheria.

Tumesema, wafanyakazi watakabiliana na hali ngumu na uchumi utaathirika

Kutokana na hofu kila mmoja akaanza kufunga virago kuelekea Dodoma

Tunasikia CDA ambao miaka 30 wapo wakitimua wapangaji

Waziri mkuu akiwaanda watumishi kisaikolojia, pengine akiona ukweli ulivyo

Kamati ya bunge imebaini ni mapema mno kwenda Dodoma bila maandalizi

Kubwa ni la Tume ya uchaguzi kupata kiwanja Dodoma na kuwa na Bilioni 12.

Unaweza kuona hofu inavyoondoa vipaumbele na kufunika vitambaa machoni

Tume inachangamoto ya kubadili mfumo uwe wa kisasa 'modern and efficient)

Hatuoni sababu za Tume kukimbilia Dodoma tukijua kazi zake ni 'seasonal'

Haya yanatokana na kile tunachoita hofu inayoondoa weledi
Ofisi ya tume inaweza kubaki Dar si lazima zihamie Dodoma leo hii

Hofu imetanda kiasi wasomi na watumishi hawaelewi maana ya Capital city.

Kwamba, Dar na miji mingine itabaki kuwa commercial cities

Kuwa Capital city hakumaanishi kuhamisha mji, watu au shughuli zote.

Laiti tungeelewa dhana ya Capital City, hii mihemko isingalikuwepo

Tutajadili hili kwa upana

Tusemezane
 
HOFU NA NIDHAMU

KUELEKEA DODOMA

Kabla hatujajadili suala la mji mkuu, ni vema tukapitia hoja za hofu na nidhamu ya woga kwa matukio kadhaa yanayotokea.

Wiki hii mkuu wa bandari aliweka wazi kufungwa kwa bandari kavu
Ni kutokana na kutokuwepo ulazima wa bandari hizo kwa wakti huu

Kauli ilifuatia habari zilizozagaa za kupungua idadi ya mizigo bandarini

Rais aliwahi ema, ni vema mizigo michache inayolipiwa kodi kuliko lundo linalokwepa. Pengine Lundo ndilo lililolazimu uwepo wa bandari kavu

Katika hali ya kushangaza kidogo, mkuu wa bandari ameongea kupitia TV ya TBC akieleza hali ya bandari kuwa nzuri sana.Si suala la bandari kavu tena

Mahojiano hayo'rahisi' yalilenga kusafisha hali ya kukinzana kauli na mkuu.
Kitendo hicho kimeongeza sintofahamu,inaonekana ni 'damage control'

Hapa kuna dalili za hofu. Mkuu analazimika kutoa tatanishi katika wiki moja.

Alichokusudia ni kuweka'hali' sawa si kutokana na uhalisia.

Hofu inazidi nidhamu

Kuhamia Dodoma

Inaendelea...
 
HOFU VS NIDHAMU

Tumezungumzia sana uhamiaji Dodoma.
Kadri muda unavyosonga tuliyoyasema yanazidi kuwa wazi

Waziri ofisi ya waziri mkuu ametangaza kuhamia kwa awamu.
Tulisema kauli za kuhamia siku 30 hazikuwa na uhalisia, ilikuwa hofu

DUWASA wanasema ongezeko la watu 200,000 litaongeza mzigo.
Kwasasa lita 400K za ujazo zinahitaji kwa siku.

Capacity ya mitambo ni 470K L na kwamba miundo mbinu ya mabomba haiwezi kuhimili msukumu katika full capacity.

Waziri na wizara yenye dhamana ilipaswa kutambua hili na kulisema kwanza kabla ya kuanza kufungasha kwa safari isiyo na uhakika. Ni hofu tu !

Kila siku tunajifunza matatizo mapya yanayoweza kutokea kutokana na uamuzi huu ambao 'haupaswi' kushaurika bali kuufuata kwa hofu tu!

Hofu inapotawala, weledi, maarifa na ujuvi vinatoweka. Hofu inapotawala nidhamu inapotea. Matokeo ya hofu ni mazito sana mbele ya safari

Kuhamia Dodoma ilitakiwa iwe porcess katika muda wa mwaka au miwili
Hii si operesheni kwavile inahusu masuala ya kiuchumi, kijamii na miasha

Ilipaswa kutanguliwa na majadiliano, mipango na utekelezaji.

Hili lingetoa fursa kwa watumishi kuamua hatma zao.
Wengine wangeshafanya maaamuzi kustaafu au kuhamia kwa wakati

Kwavile tumechagua hofu dhidi ya nidhamu, lipo kundi litaathirika sana

Lakini, kwanini tuhamishe mji ili kutengeneza Capital city?

Capital city ni nini na inahusu nini? Tutajadili

Tusemezane
 
WIKI HII KATIK MJADALA

Mengi yametokea katika duru za siasa nchini na huenda yakaendelea kwa muda
Ni mchanganyiko wa mambo ambayo kwa namna moja yamekuwa na hisia na changamoto zake

Katika mjadala wa wiki hii ambao utakuwa mrefu tutajadili yafuatayo

Hali ya uvutano wa kisiasa
Tamko la Jeshi la Polisi kuhusu mazoezi ya kawaida
Kauli ya waziri wa zamani, Stephen Wassira
Nini kinaendelea;
-Upinzani
-Ndani ya CUF
-Nini matarajio ya mvutano wa kisiasa kwa pande husika

HALI YA MVUTANO (TENSION)
Tuemiongelea muda mrefu hapa tukisisitiza kuwa hali hiyo haileti utangamano wa kitaifa

Inapoteza fursa za serikali kuendelea kutekeleza agenda zake.
Mathalan, ilikuwa kawaida kusikia Rais akafanya hili au lile hata kama ni kawaida.

Leo kuna suala zito la gesi limeongelewa, hakuna anayefuatilia kwasababu focus ipo katika mvutano wa kisiasa usio na ulazima kusema kwa uchache

Kwa upande wa pili, wapinzani wamendelea na azma ya maandamano kama walivyosema. Hilo nalo linaongeza mvutano kwa upande mwingine

Viongozi wa kidini na wazee wa Taifa hili hawajulikani wanasimama wapi.

Imefika mahali baadhi wakichukua upande na kusahau nafasi zao katika jamii.

Lile ombwe la Wazee linaonekana wazi

JESHI LA POLISI LATOA TAMKO

Pamoja na matamko mengi ya nyuma , jeshi la Polisi limekanusha habari zilizozagaa kuhusu askari wanaoonekana mitaani.

Jeshi limesema shughuli zinazoendelea ni sehemu ya kazi za kawaida

Katika hali iliyopo, ni jambo gumu kueleza kitu tofauti na kinachoonekana.

Tayari kumekuwepo na maonyo kutoka Polisi mengine yakionekana kuelemea

Iwe ni mazoezi ya kawaida au yenye malengo mengine kwa mujibu wa taratibu za jeshi la Polisi, ukweli kuwa wananchi watahusisha na suala la UKUTA hauwezi kukwepeka.

Ni Jeshi hilo limekuwa likisisitiza kuhusu UKUTA na kwa kiasi fulani limeikuza UKUTA bila kutarajia

Inaendelea..
 
KAULI YA WASSIRA

Wassira wa awamu ya nne Mh Wassira amezungumza kuhusu hali iliyopo
Kwa maoni yake Wassira ameeleza kile tunachokiuliza kila siku katika mabandiko haya

''Wassira kama alivyokaririwa alisema mvutano unatokana na 'Lowassa' kwa mtazamo wake
Kwamba ziara za Lowassa za kuwashukuru wapiga kura zitarudisha 'mtazamo' wa uchaguzi

Waziri Wassira anakiri kuwa kwa 'ukaribu' ulivyokuwa, hilo linaweza kuwa na matatizo
Kwamba mgombea huyo alikuwa na kundi kubwa, nyuma yake linaloamini alishinda

Wassira akaendelea kusema huo ni mtazamo wake binafsi, na sasa ni wakati serikali itoke na kusema nini sababu za kupiga mikutano marufuku?''

Kwa mtazamo mwingine, tumehoji mara nyingi miongoni mwa sababu zinazotolewa ipi hasa ndiyo chanzo cha kupiga mikutano marufuku?

Sababu zimekuwa zinabadilika kila mara na kutoka chanzo kimoja hadi kingine kiasi kwamba hakuna mwananchi anayeweza kuelewa kwa urahisi nini tatizo

Katika kuonyesha jinsi suala zima lilivyo na utata, hata wanaojaribu kuliongelea, mara zote wamekimbilia katika hatua ya mwisho tu ya maandamano. Hakuna anayeeleza kwa uyakinifu nini sababu hasa

Serikali inaweza kuwa na sababu za msingi kufanya hivyo, hata hivyo katika hali ya kila siku kuna sababu mpya, hali hiyo inajenga wasi wasi kuhusu sababu hizo na inatia shaka kama kuna sababu na kwanini zinafichwa.

Hapa ndipo mzee Wassira anaposimama, kuwa wananchi waelezwe tu sababu. Wananchi watakuwa na uwezo wa kupima na kufikia suluhisho pengine kutowasikiliza wapinzani kabisa

Kwavile wamechanganyikiwa na hawajui sababu halisi, hilo tu linaongeza mvutano

Tunasisitiza kuwa sisi ni Taifa moja, tunaongea lugha moja na ni wamoja.
Hatuna sababu za kuwaweka wananchi katika hali ya taharuki

Tuna sheria na wanasheria, tuangalie mwongozo wetu tuliojiwekea unasemaje?

Inaendelea..
 
Inaendelea kutoka 194

UPINZANI
Dai kubwa la upinzani ni kuminywa kwa demokrasia kuanzia Bungeni hadi zuio la vyama vya siasa kufanya maikutano.

Ni kuhusu ubabe wanaosema umekithiri, kuvuka na kuvunja haki za katiba

Maadamano ya Sept yana lengo la kupinga wanachokiita udikteta uchwara.

Kinachoanza katika hoja ni ubabe na zuio la mikutano linalopelekea maandamano ya kudai 'haki' wanazosema

Katika hali ya kushangaza Wapinzani wameshindwa kueleza au kueleweka kwa sehemu kubwa, na wameruhusu hoja zao kubadilishwa 'construed'

Hoja yao imebadilishwa kwamba wanapinga hatua anazochukua Magufuli kuhusiana na wizi na Ufisadi, na kwamba wanaadamana kupinga hatua hizo

Kwa average person ambaye weledi unategemea kusikiliza, hoja hiyo inaingia kichwani. Ni watu wenye weledi tu wanaoelewa nini hoja ya wapinzani.

Viongozi wa dini na taasisi za umma kwa kukwepa ukweli, wanabadili hoja kuwataka Wapinzani kusitisha maandamano na si ile ya msingi inayosemwa.

Hili ni kwasababu Wapinzani hawakuchukua muda kulieleza jamii.
Kutangaza UKUTA tu haitoshi kueleweka, na ni kosa la kiufundi.

Mapungufu hayo yanatokana na sababu kadhaa
1. Katika chama kikuu cha upinzani kuna ombwe la uongozi
Katibu mkuu wa CDM ameonekana kupwaya na guwa liability badala ya asset
Hili tumnelizungumzia

2. Mgogoro wa CUF ambao umekuja na kuchukua attention yao

Tujadili Mgogoro katika mpangilio wa #194
 
Inaendelea

MGOGORO WA CUF KATIKA 'MVUTANO'

Mvutano wa kisiasa ukiendelea, CUF wana mkutano mkuu kuchagua mwenyekiti

Katika hali ya kutatanisha, mkutano umevurugika kwa uwepo wa makundi.

Moja likitaka kumchagua mwenyekiti, jingine likitaka Prof Lipumba aendelee

Mgogoro wa CUF ni wa kujitakia, unaotokana na kufanya mambo kienyeji, kutozingatia taratibu na kufanya kazi kwa mazoea.

Ni mgogoro ambao chanzo chake ni cha kipuuzi sana, tuna sababu

1. Kuelekea uchaguzi 2015 Prof Lipumba aliacha ueneyekiti kutokana na tofauti ndani ya UKAWA na kuondoka CUF akiamini halikuwa jambo sahihi.

Msimamo wa Prof hauhojiwi, kwani ni mtazamo wake binafsi

Aliandika Barua ya kujiuzulu kwa katibu mkuu wa CUF Maalim Seif

2. Prof akataka arudi katika nafasi yake kwa madai hakujibiwa barua ya kujiuzulu

Prof Lipumba alikuwa sahihi.
Taratibu za kazi ni kupitia(record) za maandishi. Prof alipoandika Barua alimaanisha hilo

Kuandika barua ya kujiuzulu si kujiuzulu bali nia ya kuonyesha kujiuzulu

Ni hadi pale mhusika atakapojibiwa,suala la kujiuzulu linachukua nafasi
Prof anaposema bado ni mwenyekiti yupo sahihi, hakuwahi kujibiwa

Katibu mkuu alitakiwa kumjibu kwa barua kuweka rekodi si M/kiti wa CUF.
Kutomjibu lilikuwa kosa la kifundi linaloleta mgogoro

Kwa prof Lipumba, akiwa M/Kiti alikuwa na dhamana kubwa.
Kitendo cha kukitosa chama nyakati za uchaguzi ni 'usaliti'

Hilo tu linamuondolewa sifa uenyekiti 'by default'

Mgogoro mzima ni suala la kutofauta taratibu tu na hapa katibu mkuu ni tatizo.

Lipumba naye ni tatizo kwa kuvamia mikutano akiwa hana status ya kuingia vikao.

Alijiuzulu nyadhifa zake zote na anapaswa kuheshimu sheria na taratibu

Prof hakujiuzulu uanachama ana haki ya kugombea

Kama hakukubaliwa kujiuzulu, kuna namna mbili, moja arudishwe katika nafasi yake, au apewe nafasi ya kugombea kama mwanachama na wanachama waamue.

Hili ni suala la taratibu na sheria tu na si visasi, hasira na aina za upuuzi.

Ni mgogoro wa kipuuzi kabisa katika kambi ya upinzani. Kazi kwa mazoea tu

Inaendelea...
 
Sehemu ya mwisho (#194)

MATARAJIO YA MVUTANO UNAOENDELEA
Hali ya mvutano ipo kama inavyoonekana katika habari na matamko

Upande wa Upinzani umesimama katika hoja ya kutumika kwa sheria
Kuachwa waendelee na mikutano kama sheria zinavyosema

Upande wa Serikali, hoja haipo wazi kama alivyosema Mh Wassira

TATIZO: Hata kama ni dogo sana, ukweli unabaki kuwa lipo tatizo

Matamko ya Viongozi wa mikoa na kwingineko yanaeleza hilo
Kauli za Viongozi wa dini na wengine zinaeleza hivyo
Kauli ya Polisi mara kwa mara inaeleza uwepo wa tatizo

Mwaka 2001 ilichukuliwa kirahisi tu kuwa ni baadhi au kundi la watu
Madhara yalikuwa makubwa kwa gharama za maisha ya wananchi

Serikali ikajikuta katika hali ya kujitetea mbele ya uso wa dunia
Tukazalisha Wakimbizi katika nchi inayopokea Wakimbizi

Hakuna aliyeshinda, sote tulishindwa kama nchi na Taifa, tukajitia doa

MSAJILI WA VYAMA
Kaitisha kikao 29/30. Msajili alishatoa kauli kuhusu maandamano na si chanzo cha tatizo. Kwamba haku address tatizo bali kutaka usitishwajwi tu

Hilo lilijenga kutoaminiana kwa mtazamo wa kutokuwa 'impartial'

LHRC(Utawala bora na haki za binadamu)
Waliitisha kikao, wadau wengine hawakuhudhuria bila matokeo chanya

Kikao cha 29/30 kina shaka.Ni dharura, kwanini tarehe zinazokaribia 'tukio'?

Msajili wa vyama katika mazingira yaliyojitokeza alipoteza ile 'trust'.
Busara angeshirikisha makundi mengine muhimu ya kijamii

Msajili na tume ya haki walishindwa,kipi ni tofauti safari hii?

Kikao cha 29/30 kisipotoa ufumbuzi kitakuwa kimechagiza hisia zaidi

Hili ni tatizo, bila kujali ukubwa au udogo wake, ni tatizo.

Linahitaji busara,weledi ujasiri, haki, sheria na kuliangalia Taifa kwanza.

Wadau wote waweke masilahi ya Taifa mbele, watazame nyuma na kujifunza

Tusemezane
 
WIKI HII

Msajili na mkutano wa vyama
Tukio la kusikitisha la shambulio kwa askari Polisi

Msajili wa vyama ameitisha mkutano kama tulivyoeleza bandiko hapo juu

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, msajili alitoa kauli ya kukemea mazoezi ya Polisi yanayoendelea mitaani. Alisema jukumu la mambo ya siasa ni lake

Kauli ya msajili imekuja ikiwa imechelewa sana. Jukumu hilo alitakiwa kulitekeleza kabla na si baada ya malalamiko ya umma, taasisi n.k.

Hata hivyo, msajili hakuchukua jukumu halisi la kutafsiri sheria

Akiwa msajili na Jaji mstaafu alipaswa kuueleza umma kilicho sahihi kwa mujibu wa sheria za usajili wa vyama zinazotokana na sheria za nchi

Mkutano aliotisha unahusisha makundi mengine.
Tulisema, ingalikuwa busara kuhusisha makundi ya watu wenye busara.

Ingawa ni sawa kwa mtazamo wa jukwaa la wanasiasa kuna walakini

Baadhi ya vyama vipo kwa ''masilahi'', na huenda suala zima likajadiliwa kwa muktadha wa 'wengi wanasema' badala ya sheria inasemaje.

Hapo ndipo vyama vinavyopigania haki ya mikutano vinaweza kujikuta katika mtego. Hili si suala la kura, ni suala la kipi ni sahihi kwa mujibu wa sheria

Tunasema hivyo kwa kuzingatia yaliyowahi kutokea huko nyuma

Kwa vyovyote, majibu yanapaswa kuwa katika mfumo wa sheria si mantiki.

Hili lina maana moja, tunaongozwa na sheria wala si busara au hekima.

Busara na hekima ni visaidizi vya sheria lakini haviwezi kuwa juu ya sheria

Mkutano huo usipotoka na jibu,utachagiza tatizo the least to say

Tukio la Polisi

Inaendelea
.
 
Tukio baya la Polisi

Askari 4 wakiwa katika majukumu ya kila siku, waliuawa kwa shambulio
Ni tukio la kusikitisha sana. Tunatoa pole kwa Familia, ndugu na jamaa

Tukio hilo ni mfululizo wa matukio ya kushambulia askari katika vituo vya kazi
Yametokea sehemu nyingi nchini ,na kumlazimu Rais kuliongelea mara nyingi

Rais allihoji, inakuwaje majambazi yanafikia kutwaa silaha za askari

Kinachosikitisha zaidi ni kutokuwa na majibu ya kwanini yanatokea
Uhalifu huo kuna nyakati hauelezeki. Tukio la juzi hakukuwa na uporaji!!!

Kwa hali yoyote huo ni uhalifu hata bila kujua sababu. Ni uhalifu tu.

SURA YA TUKIO
Katika hali nyingine, kutokana na hali ya kisiasa nchini tukio hilo la kusikitisha likageuka kuwa tukio linaloambatana na mambo ya kisiasa. Likawa na sura 2

1. Tukio la uhalifu uliohusisha mauaji
2. Tukio lililohusishwa na mambo ya kisiasa

Tukialiangalia kwa jicho la uhalifu, tumeshasema si la kwanza au la pili
Ni mwendelezo wa uhalifu kutoka kwa wananchi hadi walinzi wa amani
Matukio hayo yamejirudia bila uwepo wa siasa za ukinzani

Tukiliangalia kisiasa, kuna maswali na hoja nyingi za kufikirisha

Chini ya sass 18 , uchunguzi ukiendelea kuwakamata wahalifu mkuu wa operesheni ya mafunzo alitoa kauli kuhusiana na tukio na mikutano ya siasa.

Inaendelea...
 
TUKIO LA POLISI

Kama tulivyoona bila ya uchunguzi wa awali na kina kukamilika, mkuu operesheni alitoa tamko
Moja ilikuwa kupiga marufuku mikutano yote ya ndani na ya nje ya kisiasa

Kamanda akasema, wana taarifa wapo wanasiasa wanaochochea watu kuchukia Polisi
Kwamba, kuna taarifa za bodaboda kutumiwa kuchoma moto maeneo, yakiwemo ya biashara

Wakati huo huo akasema wapo 'wanaoshangilia' tukio nao watachukuliwa hatua

MITANDAONI
Kumekuwa na majadiliano ya tukio kukiwa na mitazamo tofauti.
Wapo wanaoliona ni tatizo la uhalifu, wapo wanaoona ni kutotoa kipaumbele kwa usalama badala ya mambo mengine

VYAMA VYA SIASA
Chadema wameitisha mkutano kutoa kauli juu ya kutohusika kwa UKUTA katika tukio


TATHMINI
Tukio la mauaji ya askari waktimiza majukumu ya ulinzi na usalama ni uhalifu

Kama Taifa, ni jambo la kusitikitisha linaloashiria hali isiyo nzuri kwetu sote kisualama

Hakuna namna tukio linaweza kuzungumzwa kwa lugha nyingine isipokuwa ni baya

Matukio ya namna hii yamejirudia mara kwa mara. Hii si mara moja au ya pili au ya tatu
Je, kuna nini kiasi cha 'intelejensia' ya Polisi kutogundua chanzo cha tatizo kwa uhalisia?

Hakuna sababu ya kuharakisha tamati ya tatizo bila uchunguzi wa kina na mpana.

Yametokea matukio ya Mabomu Arusha katika kanisani Olesaiti na mkutano wa Chadema

Muda wote wananchi waliombwa utulivu vyombo vya umma vikilishughulikia tatizo

Tukio la bomu mkutano wa Chadema lilikuwa na uhusiano moja kwa moja na siasa
Uhusiano ni pale mikutano ya kisiasa iliposhambuliwa

Tukio la kanisani Olesaiti halijulikani lililenga kitu gani. Hadi sasa hakuna anayejua

Matukio ya kituo cha Polisi Mkuranga, Stakishari na kwingineko yakiwemo Tanga hayajulikani chanzo chake kwa mwananchi wa kawaida.

Yote yalitokea wakati hakuna mvutano wa kisiasa

Rais alipohutubia mikutano takribani mitatu alizungumzia matukio hayo kama uhalifu
Akatoa mfano wa nchi ya Rwanda ambako suala la uhalifu limepungua

Kwanini kumekuwa na uharaka wa kuhusisha tukio la juzi na mambo ya kisiasa?

Inaendelea...
 
TATHMINI (ii)
Ingalikuwa tukio moja linaidhinisha marufuku ya shughuli za jamii, lile la Arusha kanisani au mkutano wa Chadema yangelikuwa ya kwanza.

Hata hivyo hakukuwa na marufuku na maisha yaliendelea

Kama tukio hili linahusishwa na siasa, je yale ya nyuma yalitokeaje?

Kamanda anaposema wana taarifa za watu wachochezi, kuna hoja zinajitokeza

Moja ya majukumu ya Polisi ni kuzuia uhalifu. Kwanini wachochezi hawakukamatwa?

Kuzuia mikutano haina tija ikiwa ''wachochezi'' hawafikishwi mbele ya sheria.

Ni vema taarifa ingelitolewa baada ya uchunguzi na ushahidi usio na mashaka
Tukio ima lijulikane ni la kihalifu au kisiasa.

Uchunguzi uwe 'impartial' kutokana na sehemu ya jamii kuonyesha wasi wasi.
Kwamba, mtuhumu hawezi kujichunguza ili kuleta Imani kwa jamii

Kuhusu 'wanaobeza' Polisi kushambuliwa, hapa kuna tatizo

1. Si utamaduni wa Watanzani nyakati za majonzi kuwa katika hali iliyotokea.
Nini kinaendelea?Nini kinachagiza haya.

Je, kuna chuki ya kupandikizwa au kuna chuki inayomea?

a)Chuki inayopandikizwa ni ya kuaminishwa tu.
Katika siasa za vyama vingi, Watanzania wamekomaa kutambua nani anahoja nani anataka kuleta matatizo

b)Chuki inayomea.
Hii haipandikizwi bali hutokea 'naturally' kwamba kuna chuki inayojitokeza ikiwa haina maelezo . Ina mea tu bila kujulikani nini kinaistawisha.

2. Polisi kuwatafuta na kuwachulia hatua 'wabezaji' kwamba tayari jeshi limeshachukua chuki pengi za wachache na kuzifanya ni za sehemu kubwa ya jamii.

kwanini Polisi ilikuze kiasi cha kuonekana ni tatizo?

Kubeza misiba si utamaduni wetu. Pamoja na tofauti za kiitikadi za kisiasa sisi ni wamoja hilo halikubalika tukifahamu walinzi walikuwa ndani ya majukumu yao ya asili

Lakini pia ipo hoja ambayo Jeshi la Polisi ingekuwa busara kuiangalia.
Kwanini kuna chuki dhidi yao kama wanavyosema wenyewe?

Hii ni fursa nzuri si kukamata wanaosema, bali kuwaacha waseme ili kupitia midomo yao Polisi wabaini nini hasa kilicho mioyoni mwa hao wanaosemwa kuwa na chuki.

Kuwakamata haitasaidia Polisi kutambua chanzo halisi na itakuwa kujinyima fursa ya kujifunza mengi yanayotokana na hicho Polisi wanachokiita chuki.

Hili tutalifafanua bandiko linaloendelea..
 
Back
Top Bottom