Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,407
- 31,391
- Thread starter
- #61
VITA YA ISRAEL-HAMAS
Tuliahidi kujadili baadhi ya maswali katika bandiko hapo juu lakini awali ya yote tuangalie yaliyojiri leo
1. Egypt na Jordan Abdulla wamekataa kupokea Wakimbizi wa Palestina katika nchi zao
Rais wa Egypt alisema wakimbizi watashambulia Israel na Israel itajibu kwa kuwashambulia wakiwa Misri. Hataki
Ukweli ni kwamba nchi za Kiarabu hazitaki kuwapokea kwasababu kufanya hivyo kunaipa Israel nafasi ya kuwaondoa katika ardhi yao ya asili. Jordan kwa sasa ina Wakimbizi takribani nusu ya nchi.
Njia rahisi ni kukataa kuwapokea ili Israel ibebe mzigo huo. Japo ni hatua yenye maumivu , kwa muda mrefu ni nzuri
2. Israel ime endelea kuibomoa Gaza kwa makombora , leo imepiga kanisa la Orthodox na kuua watu
Picha za shambulio la jengo moja zimeonyesha maiti 7 za Watoto kupitia Televisheni za Mashariki ya kati
Kushambulia Kanisa kunatoa taswira kwamba Israel ilihusika katika kupiga bomu Hospitali ya Anglican
Pamoja na jitihada zote za vyombo vya magharibi kuweka ''ushahidi' sehemu kubwa ya Dunia imekataa kuwaamini
Taswira ya Israel imezidi ni mbaya kuliko Hamas , ndiyo maana Rais Biden kahutubia na kusema ''maneno'
3. Rais Biden amehutubia Taifa akiomba Bunge liidhinishe pesa kwa ajili ya Ukraine na Israel. Biden amejaribu kuleta ' suluhu' akieleza machungu ya pande zinazohusika. Biden ameitaka Israel ifungue njia za misaada na iache hamaki na makosa na ifuate sheria za kivita. Kauli ya Biden imechukuliwa na vyombo vya habari vya mashariki ya kati kama kukiri kosa la klipua Hospitali.
4. Marekani imedai kuzuia makombora yakitoka Yemen kuelekea Israel.
Ikiwa ni hivyo na si propaganda za vita, makombora hayo ni 'cruise missiles' yanayojiongoza.
Marekani inadai ni ya kundi la 'Huti' linalosaidiwa na Iran. Huenda vita imeingia hatua nyingine na Marekani inaweza kujikuta imeingia, jambo ambao Raia hawataki wakikumbuka ya Afganistan na Iraq
5. Hezbollah wameshambulia kaskazini mwa Israel kwa makombora yenye shabaha.
Wameshambulia miundo mbinu ya mawasiliano na Israel imejibu mashambuli kwa vijiji villivyo karibu.
Mzozo huu wa kaskazini unaonekana kufungua njia nyingine ya vita, Israel haipendi kwani jeshi litasambaa
Wadadisi wanasema hatua ya Hezbollah ni kuiyumbisha Israel katika hatua za kuingia Gaza.
6. Israel yajiandaa kuingia Gaza.
Ni wiki Israel ikijiandaa kuingia Gaza kuwasaka Hamas. Kuna sababu mahususi kwanini Israel imesita sana
Kwanza, kuwanyima 'Hamas' na Wapalestina maji, umeme, matibabu na chakula ili kuwadhoofisha
Pili, kupiga maeneo ya majengo ili kupunguza msongamano na kuepuka vita ya mjini '' Urban war' na vifo vya askari
Tatu, kuna 'mateka' na Israel inataka kuwaokoa lakini inachelea kuingia Gaza watauawa
Nne, Kuna kikosi cha uokoaji kipo kazini kwa mazoezi (simulation) na ili kukipa kikosi muda na nafasi ni lazima hayo matatu juu yafanyike
Tutajadili maswali ya liyotangulia bandiko lijalo
Tuliahidi kujadili baadhi ya maswali katika bandiko hapo juu lakini awali ya yote tuangalie yaliyojiri leo
1. Egypt na Jordan Abdulla wamekataa kupokea Wakimbizi wa Palestina katika nchi zao
Rais wa Egypt alisema wakimbizi watashambulia Israel na Israel itajibu kwa kuwashambulia wakiwa Misri. Hataki
Ukweli ni kwamba nchi za Kiarabu hazitaki kuwapokea kwasababu kufanya hivyo kunaipa Israel nafasi ya kuwaondoa katika ardhi yao ya asili. Jordan kwa sasa ina Wakimbizi takribani nusu ya nchi.
Njia rahisi ni kukataa kuwapokea ili Israel ibebe mzigo huo. Japo ni hatua yenye maumivu , kwa muda mrefu ni nzuri
2. Israel ime endelea kuibomoa Gaza kwa makombora , leo imepiga kanisa la Orthodox na kuua watu
Picha za shambulio la jengo moja zimeonyesha maiti 7 za Watoto kupitia Televisheni za Mashariki ya kati
Kushambulia Kanisa kunatoa taswira kwamba Israel ilihusika katika kupiga bomu Hospitali ya Anglican
Pamoja na jitihada zote za vyombo vya magharibi kuweka ''ushahidi' sehemu kubwa ya Dunia imekataa kuwaamini
Taswira ya Israel imezidi ni mbaya kuliko Hamas , ndiyo maana Rais Biden kahutubia na kusema ''maneno'
3. Rais Biden amehutubia Taifa akiomba Bunge liidhinishe pesa kwa ajili ya Ukraine na Israel. Biden amejaribu kuleta ' suluhu' akieleza machungu ya pande zinazohusika. Biden ameitaka Israel ifungue njia za misaada na iache hamaki na makosa na ifuate sheria za kivita. Kauli ya Biden imechukuliwa na vyombo vya habari vya mashariki ya kati kama kukiri kosa la klipua Hospitali.
4. Marekani imedai kuzuia makombora yakitoka Yemen kuelekea Israel.
Ikiwa ni hivyo na si propaganda za vita, makombora hayo ni 'cruise missiles' yanayojiongoza.
Marekani inadai ni ya kundi la 'Huti' linalosaidiwa na Iran. Huenda vita imeingia hatua nyingine na Marekani inaweza kujikuta imeingia, jambo ambao Raia hawataki wakikumbuka ya Afganistan na Iraq
5. Hezbollah wameshambulia kaskazini mwa Israel kwa makombora yenye shabaha.
Wameshambulia miundo mbinu ya mawasiliano na Israel imejibu mashambuli kwa vijiji villivyo karibu.
Mzozo huu wa kaskazini unaonekana kufungua njia nyingine ya vita, Israel haipendi kwani jeshi litasambaa
Wadadisi wanasema hatua ya Hezbollah ni kuiyumbisha Israel katika hatua za kuingia Gaza.
6. Israel yajiandaa kuingia Gaza.
Ni wiki Israel ikijiandaa kuingia Gaza kuwasaka Hamas. Kuna sababu mahususi kwanini Israel imesita sana
Kwanza, kuwanyima 'Hamas' na Wapalestina maji, umeme, matibabu na chakula ili kuwadhoofisha
Pili, kupiga maeneo ya majengo ili kupunguza msongamano na kuepuka vita ya mjini '' Urban war' na vifo vya askari
Tatu, kuna 'mateka' na Israel inataka kuwaokoa lakini inachelea kuingia Gaza watauawa
Nne, Kuna kikosi cha uokoaji kipo kazini kwa mazoezi (simulation) na ili kukipa kikosi muda na nafasi ni lazima hayo matatu juu yafanyike
Tutajadili maswali ya liyotangulia bandiko lijalo