DUNIANI UTAFITI: Kama unapenda kudanganya umri wako

Salahan

JF-Expert Member
Sep 10, 2014
2,942
3,606
Ni kawaida kwa watu kuficha na wakati mwingine kudanganya umri wao pengine kwa kuhofia kuonekana ama wadogo sana au wakubwa zaidi katika kundi la watu.

Utafiti uliofanywa unadai unaweza kuendelea kuuficha umri wako na kuwadanganya watu kwa sababu itakusaidia kuishi zaidi.

Utafiti uliofanywa unaonesha kuwa watu wanaoamini kuwa ni wadogo kiumri tofauti na kilichopo katika vyeti vyao vya kuzaliwa ni miongoni mwa kundi la watu wenye uwiano mdogo wa kufa ukilinganisha na ama wanaouhisi umri wao au wanaojifaya wakubwa kuliko umri wao .

Utafiti umechapishwa na JAMA INTERNAL MEDICINE ONLINE ambao ulikusanya data kutoka kwa watu 6,489 wenye wastani wa miaka 65.8 ambao wanaelezwa kujihisi watoto wa chini ya umri wa miaka 10.

Kinachofurahisha zaidi ni kuwa watu wengi kwenye utafiti huo hawakuwa na hisia na umri wao halisi ambapo wengi walidai kujihisi kama watoto wa miaka mitatu huku 4.8% walikuwa wanajihisi wakubwa zaidi ya umri wao.
 
Wanataka tudanganye umri ili tusife mapema?

Nachoamini ni kuwa kwasasa tafiti nyingi zinafanyika ili kudhoofisha imani za dini na watu wapotee...

Najua huwezi amini ila chukulia hiyo tafiti inayohamasisha watu kudanganya(kusema uongo),tafiti ya wanawake kunyonywa matiti kuzuia saratani na ile ya kushiriki ngono kunakufanya uwe na kumbukumbu wakati kuna watu wamesahau hadi waliowahi kushiriki nao ngono kwa wingi watu walioshiriki nao ngono.
 
Uzi wako hauna radha

Sent from my itel it1355 using JamiiForums mobile app
He! labda kwa kuwa hakuweka details. Kifupi inahusiana na feelings kama unajiona kijana na utafanya mambo ya ujana utafiti umeonyesha wanaishi zaidi na si lazima kumwambia mtu. Frankly speaking anjion mdogo kuliko umri wangu na watu nikiwatajia umri wangu wengi huwa hawaamini. Utafiti ni wa kweli!
 
Back
Top Bottom