Dunia yashuhudia China ambayo mlango wake umezidi kufunguliwa kwa nje tangu ijiunge na WTO miaka 20 iliyopita

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,006
1,026
Na Fadhili Mpunji

VCG111356270854.jpg

Mwaka huu China inaadhimisha miaka 20 tangu ijiunge na Shirika la Biashara Duniani WTO. Tangu mwaka Novemba 2001 China ilipojiunga na Shirika hilo mjini Doha, uchumi wa China umekuwa kwa kasi na kutoka GDP ya Dola za Kimarekani Trilioni 1.3 ikiwa katika nafasi ya 6 duniani, hadi kufikia dola Trilioni 14 kwa mwaka 2020 na kuwa katika nafasi ya 2 duniani. Lakini mafanikio haya ya China, si kwamba yameinufaisha China peke yake, bali pia yameinufaisha dunia nzima.

China kujiunga na Shirika la Biashara Duniani WTO, ilikuwa ni sehemu ya mpango mkuu wa China wa kutekeleza sera ya mageuzi na kufungua mlango. Lengo kuu la hatua hiyo lilikuwa ni kufungua uchumi wa China na kuufungamanisha uchumi wa dunia, na sasa ni miaka 20 imepita tangu China ijiunge na WTO, ni nini kimebadilika?

Pamoja na kuwa kitakwimu China bado inatajwa kuwa ni nchi inayoendelea, ikiangaliwa kwa vigezo vingi hasa vya kiuchumi, kuna maeneo ambayo China iko mbele zaidi kuliko hata nchi nyingi zilizoendelea. Mbali na kuwa nchi ya pili duniani kwa nguvu ya kiuchumi, China pia ni nchi ya kwanza duniani kwa usafirishaji nje wa bidhaa, ni nchi ya pili kwa uagizaji bidhaa duniani, ni nchi ya nne kwa usafirishaji wa huduma, na ni nchi ya tatu kwa uagizaji wa huduma dunia. Ukiangalia kwa undani takwimu hizo utaona kuwa zote ni matokeo ya juhudi na kuchapa kazi kwa wachina, na ushirikiano wa kibiashara kati ya China na nchi nyingine duniani chini ya utaratibu wa Shirika la Biashara Duniani WTO.

Tangu mwaka 2001 ilipojiunga na WTO, China imebadilisha zaidi ya sheria elfu tatu na sera mbalimbali za uchumi, ili kuruhusu sekta binafsi kutoa mchango katika maendeleo ya uchumi, na kufanya wachina wachangie zaidi kwenye uchumi wa nchi yao kwa nguvu zao na akili zao. Matokeo yake ni kuwa kwa sasa sekta binafsi ni moja ya mchangiaji mkubwa wa mapato ya serikali, mtoaji muhimu wa nafasi za ajira, na ni sekta inayofanya uchumi wa China uwe na uhai zaidi.

Uanachama wa China kwenye Shirika la Biashara Duniani, sio kama tu umeinufaisha China peke yake. Takwimu nyingi zinaonesha kuwa dunia imenufaika sana na uanachama wa China kwa WTO. Kwa sasa China ndio nchi inayoongoza duniani miongoni mwa nchi zinazoendelea kwa kupokea uwekezaji wa moja kwa moja (FDI) kutoka nje. Kwa sasa nchi nyingi kubwa za magharibi zinanufaika na uwekezaji wao nchini China kutokana na soko kubwa, gharama nafuu za uzalishaji, na hata urahisi wa kusafirisha bidhaa hizo kwenda kwenye masoko ya nchi ya tatu.

Kwa nchi zinazoendelea, China imekuwa ni chanzo kikuu cha uwekezaji wa moja kwa moja FDI. Idara ya takwimu ya China imesema hadi kufikia mwishoni mwa mwaka jana, thamani ya jumla ya FDI kutoka China kwenda nje, ilikuwa dola za kimarekani bilioni 153.7, na asilimia 80 ya nchi zote duniani zimepokea uwekezaji wa moja kwa moja kutoka China. Uwekezaji huo unaonekana kwenye sekta za ujenzi, huduma na hata uzalishaji viwandani.

Lakini tukiangalia maisha ya mtu mmoja mmoja duniani, tunaweza kuona kuwa tangu China ianze kusafirisha bidhaa zake kwa wingi katika nchi mbalimbali duniani, tunaona kuwa bidhaa ambazo zamani zilitakiwa kuwa ni adimu, au ambazo zilionekana kuwa ni kwa ajili ya matajiri tu, sasa zimekuwa zinapatikana kwa urahisi, bei nafuu na kwa ubora unaofaa. Kwa hiyo kwa ujumla tunaweza kusema kujiunga kwa China WTO kumekuwa ni jambo lenye manufaa kwa dunia nzima.
 
Nchi yangu Tanzania, duh nakuonea huruma. Mwanamke mrembo uliyejaaliwa kila aina ya tunu ukakosa akili. Wacha tu ziumie sehemu zako za siri
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Kukopi na kupasti huwa inahitaji kipaji pia.

Title ya uzi na maelezo paragraph ya kwanza hayaendani. Umesema kwa miaka 20 tangu China ijiunge na WTO, halafu tena umeandika imejiunga " mwaka Novemba 2021".

Soma tena uzi wako na uuhariri
 
"Tangu mwaka Novemba 2021 China ilipojiunga na Shirika hilo mjini Doha, uchumi wa China umekuwa kwa kasi na kutoka GDP".... SOMA HICHO KIPANDE KIDOGO ULICHOCHAPIA
 
Back
Top Bottom